Nita jitahidi nikisha fanikisha hili swala niulete uzi wa mlolongo mzima ili vijana wengine wanao anza na kutamani kufanya biashara kama hii waweze kua na pa kuanzia. Mambo mengi huwa yanatushinda kuyafanya kwasababu ya kuto kujua pakuanzia na kuogopa mlolongo uliopo kwa kudhania ni mrefu mno...
Shukrani sana, mzigo unafika tani moja kamili, na kwa sasa nimeambiwa inabidi nimpate mtu mwenye leseni ya kununua na kuuza na kusafirisha mazao huyo ndio atanisaidia kupata kibali hicho.
Hahahahaaaa hapana ndugu sipeleki nje ni hapa hapa nchini, ila nimeambiwa nahitaji kibali ili kupita na mzigo getini, shida ni kwamba naanzia wapi kupata kibali na ofisi gani na niwe na nyaraka gani zingine ndio sijui.
Mzigo ni maharagwe na yapo strore. Sasa niko na option mbili niuzie huku huku au nipeleke dar kwasababu yatanilipa zaidi. Sasa kwenye swala la kusafilisha mzigo ndio mgeni kabisa ila nimeambiwa nahitaji kibali ila walio niambia pia hawajui hilo swala la kibali inabidi nianzie wapi niishie wapi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.