Ni kweli kwa mambo yalivyoharibika ufisadi kila kona naona kama itakuwa ngumu,nchi ilipofika hapa naona anahitajika rais mkali sana naona kama mpole vile.
Ni kweli gamba ni gamba ila ugumu yanatofautiana kuna gamba la kenge,gamba la mti nk.kwamba El ataweka wapi sura yake je kikwete aliposhindwa na mkapa,pamoja na El waliweka wapi sura zao? mbona ndo hao tunawasikia kila leo.
umenena kweli kwa wale tunaoiombea ccm ipotee kama walivyopotea nzige,ni vema chadema wakageuze namna ya mashambulizi badala ya kuelekeza kwenye ufisadi ,bora wajielekeze kuelezea sera zao,kushambulia ccm badala ya madhaifu ya wagombea mfano kama salim madhaifu yake wengi hatuyajui.
Ni kweli wapiga kura wengi ni wa umri uliousema lakini mbona kuna wabunge wazee sana kama kina Abas Mtenvu, kapuya,sitta,Nkono,nk.wanaendelea kuchaguliwa kwa kura nyingi tena na vijana?.
kwamba watawezaje kumsafisha tayari kateuliwa kwenye kamati kuu hii ndo kumsafisha,kwamba hudhani kama atakubali? kakubali kuwa mjumbe wa kamati kuu tu je urais mzee si zaidi sana.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.