Hapo ndio ujue babu zetu hawakukosea waliposema "hasira hasara". Sawa alikuwa ana hasira na hasara ya hasira zake zimeonekana, alipanda tena jukwaani kutengua kauli? Wafuasi wameelewa kuwa ilikuwa ni hasira na ameichukuliaje hasara aliyosababisha?
Sio kweli, usikurupuke uliza ueleweshwe na kuna mtu aliuliza humu na amejibiwa kwa usahihi. Unapoikuta mada ilishaanza kujadiliwa, ni vyema ukaanzia mwanzo ili uelewe azidi.
Sidhani kama mleta mada haelewi hili ila inastaajabisha Askofu Pengo anapowasemea maaskofu wengine. Yeye akitoa maoni yake, hakuna Askofu anayesisitiza chochote katika maoni hayo hata kama ni tofauti na mtazamo wake ila wenzake wakitoa maoni ambayo ni tofauti na ya kwake yeye anasisitiza kuwa...
Hata mimi ni kardinari wangu lakini sikubaliani naye katika haya.
Watanzania wenzangu, uzalendo si kushabikia au kutetea vyama bali kushabikia na kutetea taifa.
Mamlaka husika inatakiwa kutoa majibu ya huu utekaji wa mara kwa mara. Hivi kweli watanzania tumefika mahali haya mambo yanatokea halafu wafia vyama wanashutumiana mitandaoni bila mamlaka husika kutolea maelezo na watu kuchukuliwa hatua za kisheria? Halafu bado mnataka watanzania tuwe na imani...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.