Unabahati nami niko katika kozi ya kujifunza kuwa na uso wa mbuzi. Mungu anisaidie tu kwa kweli maana moja ya udhaifu nilionao siwezi mnyima msaada mwenye uhitaji kama ninacho hata kama mwenyewe hakinitoshi. Jamaa kanifanya nisiwe na rafiki wa jirani hivyo kila mtu namchukulia sawa na mwingine.
Kaka hujui tu. Sidhani kama kuna ambaye anaweza chomwa na mwiba mguuni na asiwe na mpango wa kuutoa ili atembee kwa amani. Omba lisikukute kwani litakufanya usiwe na rafiki wakati marafiki ndio mtaji wa muingiliano katika jamii
Kiwanja kimoja documents zote ziko sawa na ninazo ila cha pili ndiyo kaziyumbisha kwa nia ovu. Ila vyote viwili kavishikiria. Kuhusu mtaji nilifanya kila kitu na uzuri nilimuandikia chq. Nikamwambia mpaka atimize masharti ya document ndipo nitaruhusu benki imlipe na alifanya kama ninavyotaka...
Hamna tatizo alikuwa anajaribu kuniambia kuwa maelezo marefu mno ila kwa bahati mbaya nimejaribu kufupisha sana kwani sio rahisi sana kuandika historia ya mateso ya miaka zaidi ya saba kwa maelezo mafupi. Naomba anisamehe ila ushauri wake ungeweza nifaa endapo angepata wasaa wa kusoma.
Dah! Napokea ushauri wako. Ila ni sawa na kuwa chini ya ulinzi na adui kuruhusu mbwa ale nyama inayoonekana kny jereha la kidonda mguuni mwako. Maumivu makali ila huoni njia rahisi ya kukwepa mateso.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.