Ni sahihi kabisa nakubaliana na unalolisema Sisi huku kilindi tunateseka Sana na huyu bwana ambaye kwa sifa zake hata ujumbe WA nyumba kumi hawezi kuongoza
Ni nafuu angekuwa tu mpigaji lakini amevuka mipaka kwa kulewa madaraka amekuwa mnyanyasaji sana , vitendo anavyofanya kwa wakulima wa huku ni vya kiuonevu , huyu bwana tunajipanga kufanya maandamano kwenda ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Tanga na mabango
Niliyoyasema hapo ni machache ana madudu mengi ameyafanya ila watu hawana pa kusemea ukizingatia na mazingira ya hii WILAYA yetu huku bado hakuna maendeleo na uhaba wa waandishi wa habari . Mimi ni mzawa wa huku nimezaliwa huku nimekulia huku mpaka utu uzima wangu, hakuna mkuu wa wilaya amewahi...
Rais wangu nakusalim kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mimi raia wako Rashidi Jumaa kutokea Tanga wilaya ya Kilindi ni mzawa wa huku
Sauti ya mnyonge huwa haisikiki kwa urahisi, nimeona nilitoe dukuduku langu humu kwenye mitandao ya kijamii kutokana na kero tuliyokuwa nayo na huyu...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.