Darasa ni zito kwa kweli maana Mtu mzito anaonyesha upeo mkubwa sana na hata kuweka wazi yale ambayo ni ya ndani sana......kila anapojibu natafuta walau kwenye pengo niongezee lakini nakuta amejitosheleza.
Naam hii ni hatari sana japokuwa mtu akimudu huonekana shujaa lakini risk ni kubwa mno, utibabu huu mara nyingi wakati wa kukabidhiwa mkoba unafichiwa tunguri kwanza na ukihangaika na kujua ilipo......huonekana tayari umewiva.
Nipo mkuu na naona umahiri mkubwa ulionao ndani ya sayansi hii nyeusi, unajibu maswali ya kila namna tena kwa ustadi mkubwa kiasi cha kutosha kabisa, nipo na nitaweka neno wala usitie shaka
Hakika mkuu......hii imerahisisha kazi zaidi na mimi nimekaa kitako kuweza kufuatilia mambo yetu, furaha yangu ni kuona kuna majibu na maswali yenye staha na hakuna malumbano.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.