Haya mambo yameelezwa vizuri tu kwenye biblia lakini watu wanayapindisha kwa maslahi yao na kwa sababu waumini wengi hawasomi biblia basi wanatapeliwa kirahisi sana
Uko serious kabisa na ulichoandika? Mtume Paulo alifanya kazi kubwa mno kueneza injili lakini alifanya kazi ya kushona mahema kupata hela ya mahitaji yake. Nani kati ya hawa wa leo wenye kupiga makelele ya kutaka kuhudumiwa kwa sadaka ana viwango vya mtume Paulo? Wanakaa tu mijini hawahangaiki...
Zaka haikuwa pesa na jinsi ilivyokuwa inatumika kuna mtu ameshaandika humu labda urudie tena kusoma
Ukitaka uelewa mzuri wa maandiko yasome kwenye original tongues ( lugha mama). Hizi tafsiri nyingi ziko kimaslahi ya hao wanaotafsiri. Biblia iliandikwa kwa Kiebrania, Kiaramayo na Kigiriki...
Hubirini ukweli kwanza. Hayo mengine Mungu atawapa. You are too anxious about money na mmeacha kufundisha mafundisho mengine na kuwaacha waumini wakiwa mbumbumbu kabisa. Hawajui hata historia ya kanisa wala doctrine of faith. Kazi yenu kuhubiri kutoa tu na miujiza ya uongo.
Mbona hamtilii mkazi kuokoa roho za watu? Ni kwa sababu hazina faida binafsi kwenu. Yesu alikuja kutafuta roho za watu ila ninyi mnakuja kutafuta pesa.
Wewe ni mlawi asiyekuwa na urithi wa ardhi kwenye kabila 12 za Israel? Tutoe pesa zetu kuwategemeza watu wenye majumba, mashamba na biashara? Which biblical principle is that?
Umenena vema. Hawa ni waganga njaa tu. Ingekuwa hizo pesa zinaenda kwa Mungu moja kwa moja wasingetokwa povu kukazania sadaka. Ni kwa sababu zinajaza mifuko yao.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.