Wakati wa chaguzi za 2019 na 2020, watu walikuwa wanasema ya moyoni kutokana na matendo ya chaguzi. Baada ya muda, baadhi walianza kuropoka yaliyofanyika sirini, mmoja baada ya mwingine.
Mkuu Lusungu, kwa heshima na taadhima, ni sahihi kwako kuona Wanachama wa CCM hapa JF wakimpigia chapuo Mbowe?!!!
Huoni kwamba kuna kitu hakipo sawa?
Busara yangu inaniongoza siku zote mpinzani wako akikusifia, ujue kuna mahali umekosea na ni kwa faida yake siku zote.
Nyakati nyingine, tuache Demokrasia ishike hatamu. Kwa nini Mtu aonekane kufika bei kwa kutia nia ya kugombea nafasi ya M/Kiti kipindi cha kuelekea kwenye Uchaguzi?!!!
Hapa, umeanza kuongea point na kuona shida Iko wapi badala ya kumshambulia Mleta Hoja ambaye amejenga Hoja yake kupitia taarifa zinazopatikana MCT na amelisema hili tangu mwanzo na mara kwa mara.
Shida kubwa, ni watu kuhemka kisa tuu anayeongelewa ni Prof aliyependekezwa kuiwakikisha Nchi...
Nami naungana naye ya kwamba, kwa mujibu wa taarifa na CV zilizoletwa humu, Prof siyo Daktari Mbobezi wa Magonjwa ya Moyo wala kitu chochote kwa sababu anakosa sifa za kuwa Mbobezi. Labda kama kuna taarifa (CV) nyingine mbali na hizi zilizoletwa hapa.
Mkuu, acha kisirani. Ni vizuri ukajikita katika kuonyesha Ubobezi wa Prof kwenye Magonjwa ya Moyo kuliko kumshambulia mtoa mada.
Hata hivyo, binafsi nampongeza sana Marehemu Dkt. Ndugulile kwa kuwa Game Changer kiasi kwamba sasa, kila Daktari ameona fursa ya WHO. Najiuliza, walikuwa wapi kabla?!!!
Binafsi, nimekuwa nikimtambua kama Daktari Bingwa/Mbobezi wa Moyo. Na wengi wanamtambua hivyo na ndiyo maana, wengi wamehamaki na Hoja iliyoletwa, kwamba, Prof siyo Daktari Bingwa wa Moyo.
Asante sana kwa ufafanuzi. Namna hii, tutafika nchi ya ahadi tukiwa na afya zetu zote kabisa.
Kwenye CV za Prof zilizoletwa JF, zinaonyesha amesoma MSc (Tropical Health) ambayo anasoma mtu yeyote na kwamba hajasoma MMED (Internal Medicine) inayompa sifa ya kuwa Daktari Mbobezi wa Magonjwa ya...
Hakuna mahali anaruka viunzi. Hoja hujibiwa kwa Hoja, na siyo vinginevyo. Kwenye hili, Mleta mada Hoja zake zinaeleweka kwa nini anasema Prof siyo Daktari Mbobezi wa Magonjwa ya Moyo. Shida, wewe na wengine, tumehamaki na kumshambulia Mleta Uzi badala ya kujibu Hoja zake kwa Hoja.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.