Wewe jamaa unatia aibu na unatia huruma sana...unajivunia kuwa na vyuo vinavyofundisha mafundisho ya wanadamu badala ya kufundisha neno la Mungu. Yesu alisema "...nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.
Ndugu yangu, hivyo vyuo ningeviona vya maana kama...
Hayo ni maswali ya kitoto, eti Mungu atamwombeaje mtu aliyemwuumba? Mbona hushangai Mungu atamfiaje mtu aliyemwuumba?
Soma Waebrania 7: 25 Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.
Soma pia 1Yonana 2:1 Watoto wangu wadogo...
Ndugu nakushukuru kwa kuniita taahira...lakini unapaswa ujue hilo fungu linahusu mji mpya wa Yerusalemu na si mbinguni. Katika Yerusalemu mpya hapatakuwa na hekalu lakini kwa sasa mbinguni kuna hekalu kama fungu la Ufunuo 11;19 linavyosema. Soma pia kitabu cha waabrania kinaelezea vizuri hekalu...
Ufunuo 11:19 Kisha Hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana ndani ya hekalu lake. Kukawa na umeme, na sauti, na radi, na tetemeko la nchi, na mvua ya mawe nyingi sana.
Waebrania 9: 24.
Kwa sababu Kristo hakuingia katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu; wala si kwamba ajitoe mara nyingi, kama vile kuhani mkuu aingiavyo katika patakatifu kila mwaka kwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.