Hazikutumika kwa kuwa Yanga walikuwa na 'kichaka' kizuri cha kujifichia.....ambapo kulikuwa na mkanganyiko wa muda wa mechi uliosababishwa na mamlaka husika. Kama unakumbuka timu zote ziliingia uwanjani ila muda tofauti. Tarehe 3 Julai habari itakuwa tofauti.
Umetumia muda mrefu kueleza impossible scenario. Yanga kuingiza timu tarehe 3 au kutoingiza timu hakufanyi Simba asitimize mechi 34. Mechi ikipangwa na mamlaka husika na na mojawapo ya timu isitokee, mbali na hatua nyinginezo, timu iliyofika inapewa ushindi wa alama za mezani kwa kufuata kanuni...
Timu ilicheza vizuri kiasi hadi dkk ya 70 hivi ikaanza kupoteana. Mkude alikuwa na kiwango bora lakini ameharibu sana kwa kulazimisha kupewa kadi bila sababu za msingi. Ameigharimu sana timu na anapaswa kuwajibishwa. Refa hakuwa kwenye kiwango kizuri anapaniki pasipo na sababu na pia kupanikisha...
Ungekuwa mfuatiliaji mzuri ungejuwa kuwa Eddo Kumwembe ameshawahi kwenda Morocco kwa ajili ya Msuva na akawa na mfululizo wa makala karibu wiki nzima. Sio kwamba Msuva hajaandikwa, kaandikwa kwa kiwango kilichostahili hasa kwa sababu kwa vyovyote vile asingeweza kuwa promoted kuliko Mbwana...
Yanga wakubali kubadilika, na kusema kweli wameshachelewa sana, wasiendelee kuchelewa.Tumekuwa tukisema haya kwa karibu 5 years now lakini watu wanajifichia kwenye historia za miaka ya kugombania uhuru. Dunia imebadilika!!!
Gharama za uendeshaji timu ni kubwa sana, huu sio wakati wa kusajili...
Mechi ya 3-3 haiwezi kusahaulika kwa muda mrefu. Haikuwa mechi yenye msisimko sana nje ya uwanja lakini uwanjani ilikuwa ni burudani mwanzo mwisho. Hakuna dkk ya mchezo ambayo haikuwa na maana.
Yanga iliperform kwa kiwango cha juu sana katika kipindi cha kwanza huku Simba ikionekana kuzidiwa...
Anayeidharau ligi ya Sudan atakuwa hajui anachokizungumza.
Kwa taarifa yako, sio rahisi kumchukua mchezaji kutoka Sudan kwa timu kama Al Hilal na El Meriekh.
Tena hata hivyo Simba wamefanya usajili wa watu wengi, kwa timu waliyokuwa nayo msimu uliopita, walitakuwa kuongeza vichwa 3 tu kutoka...
Simba wako kwenye uelekeo sahihi kama ilivyo sehemu kubwa ya dunia. Mambo ya ufadhili, udhamini sijui fadhila hayana nafasi. Timu zetu zimekuwa huko miaka nenda miaka rudi, sasa hivi ni uwekezaji tu, na pawepo bodi ya wakurugenzi washughulikie timu kibiashara.
Habari kubwa ni UWEKEZAJI, kila...
Wachezaji wetu huwa wanaishiwa maarifa wanapofanyiwa pressing kali hasa kwenye eneo la kiungo. Hata Ajibu na Mkude wangekuwepo bado tunashida kama nchi. Ni Samatta pekee na labda Erastho Nyoni ndio wanaweza kutuliza mpira na kuulinda hata wakiwa wanakabwa na watu 2 hadi 3!!
Himid anaweza kukaba...
Nina maoni tofauti. Mimi binafsi siridhishwi na style na personality ya Amunike. Lakini hii haininyimi nafasi ya kuona ubora na uzuri wa kitu anachokifanya na timu inavyocheza.
Kwanza timu imecheza kwa mfumo mzuri unaoeleweka. Wamekaba vizuri hasa kuzuia krosi za Wamisri japo walifanikiwa...
Akina Kilomoni wapo wengi lakini wamejaa hofu inayoletwa na mabadiliko. Mabadiliko yoyote yanakuja na vitu vingi na yanapokelewa tofauti tofauti. Kuna kundi huwa linakinzana na mabadiliko kwa sababu wanazozijua au wasizozijua.
Vyovyote iwavyo Simba hakuna kurudi nyuma. Ni gia ya mbele tu, huko...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.