Zitto na pesa za sensa ya watu

peas hizo wazipeleke wanakoita kilimo kwanza mbona wakulima wanalia na mazao bei chini,watumie hizo mill 300 kuongeza thamani ya mazao ya wakulima. hiyo ni rushwa wanataka kuwatengenzea skendo wabunge w upinzani hasa cdm na kuua issue ya pm
 
mwambieni kwanza atueleze amepataje utajiri wote huo alionao? pengine ndiyo maana hataki posho maana ameishashiba
 
Bunge linalohonga wabunge wake. Spika kwa hili naye aondoke. Kama takrima ilivyokuwa, ilipambwa vizuri kuwa ni "african hospitality" kumbe rushwa. Ndio maana miaka hamsini lakini nchi inarudi nyuma.rushwaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa mpaka mjengoni
 
mwambieni kwanza atueleze amepataje utajiri wote huo alionao? pengine ndiyo maana hataki posho maana ameishashiba

Tafuta kidume kifanye Doria kichwani kwako unaweza kujitambua siku nyingine, kama ishu ni utajiri mbona watu kama Mohamed Dewji,Lowassa,Nimrod Mkono,Aboud,Shabiby wanazifakamia posho,we umesahau Pinda alisain Posho feki ya jairo ya 280,000??? Zitto ni zaid ya mbunge but ntaendelea kumwita mbunge as sina jina la kumtofautisha na wabunge kama kina makamba,lusinde n.k
 
Neema Kishebuka, Dsm

Kamati kuu ya chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) iumewataka wabunge wa chama hicho kurudisha pesa zilizowekwa katika account za wabunge kwa ajili ya kuhamasisha zoezi la kuhesabu watu linalotarajiwa kufanyika nchini kote Agost 25 mwaka huu.

Kamati hiyo iliyokutana jijini hapa imetoa maagizo hayo na kuwataka wabunge wake kuzirudisha fedha hizo kwa katibu wabunge wake baada ya kuzipitia akount zao na kubaini kuwepo kwa pesa hizo kiasi cha shilingi milioni moja kwa kila mbunge zilizowekwa katika akaunti zao.

Kamati hiyo imesema kuwa si halali wabunge hao kupokea pesa hizo kwa kuwa ni wajibu wao kuhamasisha zooezi la sensa katika maeneo hayo.

Imeelezwa kuwa ni wajibu wa wabunge kushughulikia masuala ya kiserikali kama ya sensa ya watu na makazi hivyo kupokea pesa Hizo ni sawa na rushwa kwani ni wajibu wao.

Hata hivyo wabunge hao wamekanusha kupata taarifa ya kuingiziwa pesa Hizo na ofisi ya Bunge na kuahidi kuzinagalia akaunti hizo na endapo watakuta pesa zimeingizwa watazirudisha kama kamati kuu ilivyoagiza.

Kwa upande wake naibu katibu mkuu wa CHADEMA Zitto Kabwe, aliwaasa wabunge wa CHADEMA kuwa makini na pesa zinazotolewa na serikali kwa ajili ya utekelezaji wa masuala ambayo tayari ni wajibu wa wabunge wa Bunge hilo lililo chini ya Ana Makinda.

"Hii ni rushwa ya wazi ndugu zangu, mimi nimeambuwa na katibu wa Bunge kuwa amewaingizia milioni moja kila mbunge sasa ni wajibu wetu kurudisha pesa hizo kwakuwa ni wajibu wetu kufanya kazi za kijamii'' alisema Zitto.
Nasikia kulengwalengwa na machozi....... watoto wetu mtarithi nini kwa spidi hii ya mama-Myarukolo
 
AMA KWELI, NGOJA TUONE MWISHO WAKE ! Kwa madaktari - hatuna pesa, hizi zinatoka wapi ?
 
kazi ipo!
wabunge sijui miatatu na ngapi mara milioni moja!! vijichenji ambavyo vingeliweza alau kutosha kujenga kijizahanati na kijishule cha chekechea watoto wetu wakapata chanjo za polio na kuchangamsha akili zinatapanywa!
ama kweli kufa kwa mdomo mate kutawanyika!
nchi imeoza imebakiza kunuka tu
Nadhani ni 350+ (nimechukua %20 ya kura 70x5 zilizotakiwa kumuondosha WM), hii ni kusema zaidi ya Shs. 350, 000,000. Tunaelekea wapi. Hawa wamekaa kama watoto wadogo, wakikatazwa mavi wanachezea mkojo.
 
Back
Top Bottom