Imany John
JF-Expert Member
- Jul 30, 2011
- 2,930
- 1,165
Habari wana Jf!
Kwa habari za kutoka kwa chanzo cha habar ndani ya CHADEMA huko arumeru ni kwamba mgombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA Joshua Nassary amesema kwamba amesikitishwa sana na kauli ya zitto kutangaza nia ya kugombea urais kwan kauli hiyo haijaja muda muafaka na inachochea makundi ndani ya chama pia na kuvunja nguvu ya wapiganaji huko arumeru. Pia ijapokuwa ni haki yake kikatiba lakini haikuwa ni muda muafaka kwa sasa.
My take
zitto pamojaa na vijana wako wakina benard sanane acheni hila na chuki zenu kwani mnazidi kujiondolea imani kwenye chama, pia jueni kwamba 'this time tommorow' msilete upinzani ndani ya upinzani. kwani david kafulila aliwahi kusema kwamba" UONGOZI BILA DEMOKRASIA NI UDIKTETA LAKINI DEMOKRASIA BILA NIDHAMU NI FUJO"
Hata hivyo Zitto mwenyewe
amekanusha kuhusika na
waraka huo na amesema
mchezo huo ni mchezo wa
siasa chafu kupitia makaratasi. Alisema chama hicho kiko
imara na viongozi wote wako
bega kwa bega kuhakikisha
kuwa Nasari anashinda
ubunge wa jimbo hilo. Alisema kinachojaribu
kuenezwa ni uongo wa
kipuuzi unaopaswa
kudharauliwa na kila mwenye
akili timamu, na hakuna
kiongozi makini wa CHADEMA anayeweza kuwaza na
kuandika upuuzi huo. Huo ni upuuzi, wapiganaji
wako mstari wa mbele;
hatuwezi kuanza kuwavuruga
hata kidogo, wala
kuwakatisha tamaa hapa ni
kuungana tu, tena tunapenda CCM ijue kuwa tumeungana
kwa dhati na tuko pamoja
kuhakikisha mgombea wetu
anashinda jimboni. Hatuwezi
kusumbuliwa na mchezo
mchafu, tunatumaini wananchi watatuchagua kwa
hoja zetu na sera. Hizo ni dalili za mfa maji
CCM sasa wanatapatapa sana,
tunajua mpaka sasa hali yao ni
mbaya sana, hawatafanikiwa
kwa siasa chafu hizo,
tumeungana kikwelikweli; kwanza hizo wanazosambaza
si hoja ambazo watu wa
Arumeru Mashariki wanataka
kujua au kusikia. Kwa watu
wa Arumeru Mashariki hoja za
msingi ni juu ya maji yao, afya yao, elimu yao, ajira kwa
vijana na hizo ndizo CHADEMA
tunazungumzia si kufanya
propaganda, alisema Zitto.
Chanzo:TANZANIA DAIMA LA JANA.