Mjanja M1
JF-Expert Member
- Oct 7, 2018
- 3,697
- 12,445
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ametangaza rasmi nia yake ya kugombea Ubunge Jimbo la Kigoma Mjini katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 huku akisisitiza kuwa kwa vyovyote vile anataka kurudi Bungeni kwasababu anaamini miaka mitano hii Bunge limerudi nyuma kwa sababu ya kutokuwepo kwa Wabunge wa upinzani.
“Nagombea Ubunge, kuhusu Vijana sijawazuia kugombea, mwaka 2020 nilienda kwenye kura za maoni na Abdul Nondo kwahiyo 2025 anaweza kugombea pia, Chama chetu ni cha kidemokrasia mno yaani mambo yanayofanyika ACT huyaoni kwenye Vyama vingine, siamini kama kuna Chama kingine ambacho Kiongozi wake wa Kitaifa anagombea kwenye Jimbo Mwanachama yoyote tu anaweza akatokea akaenda kugombea”
“Mwaka 2020 nimeenda kwenye kura za maoni na Mdogo wangu Abdul, mwaka 2025 akitaka atakuja kwenye kura za maoni na Wajumbe wakimchagua yeye atakuwa Mgombea na nitatembea kumuunga mkono na wakiona niendelee kwasababu Mimi kwa vyovyote nataka nirudi Bungeni kwasababu naamini miaka hii mitano ambayo hatupo Bunge limerudi nyuma kwahiyo tungependa kurejesha la kabla ya mwaka 2015” — Zitto
Credit-MillardAyo
“Nagombea Ubunge, kuhusu Vijana sijawazuia kugombea, mwaka 2020 nilienda kwenye kura za maoni na Abdul Nondo kwahiyo 2025 anaweza kugombea pia, Chama chetu ni cha kidemokrasia mno yaani mambo yanayofanyika ACT huyaoni kwenye Vyama vingine, siamini kama kuna Chama kingine ambacho Kiongozi wake wa Kitaifa anagombea kwenye Jimbo Mwanachama yoyote tu anaweza akatokea akaenda kugombea”
“Mwaka 2020 nimeenda kwenye kura za maoni na Mdogo wangu Abdul, mwaka 2025 akitaka atakuja kwenye kura za maoni na Wajumbe wakimchagua yeye atakuwa Mgombea na nitatembea kumuunga mkono na wakiona niendelee kwasababu Mimi kwa vyovyote nataka nirudi Bungeni kwasababu naamini miaka hii mitano ambayo hatupo Bunge limerudi nyuma kwahiyo tungependa kurejesha la kabla ya mwaka 2015” — Zitto
Credit-MillardAyo