Zitto Kabwe kuwa kiongozi wa Upinzani Bungeni?

Salaam wana JF,
Kwanza napenda kushukuru kwa michango iliyomo humu na inanihusu mimi. Kumekuwa na maneno mengi ya kweli na yasiyo ya kweli kuhusu suala la mimi kugombea nafasi ya Kiongozi wa Upinzani Bungeni. Ninaomba kusema ifuatavyo.
  1. Chama chetu kimepata viti vingi sana vya Bunge mara baada ya uchaguzi wa mwaka huu. Hii ni ishara njema sana kuwa sasa demokrasia nchini itakomaa kutokana na kuwa na Bunge Imara. Idadi kubwa ya wabunge wa upinzani ndani ya Bunge inapunguza nguvu kwa kiasi kikubwa za CCM ndani ya Bunge. Tumejitahidi sana kukifikisha chama chetu mahala hapa. Nawapongeza sana viongozi wa chama chetu kwa mafanikio haya na hasa Mwenyekiti wa Taifa wa chama na Katibu Mkuu wetu ambaye alikuwa mgombea Urais.
  2. Chama chetu kimepata viti vya kuweza kuunda Kambi ya Upinzani Bungeni ama peke yake au kwa kushirikiana na vyama vingine vye wabunge. Kwa vyovyote vile atahitajika Mbunge mmoja wa Upinzani na hususani kutoka CHADEMA ambaye atakuwa KUB. CHADEMA bado haijatangaza utaratibu utakaotumika kupata KUB kutoka miongoni mwa wabunge wake. Nimewajulisha viongozi wangu wa chama kuwa nina nia ya kuomba ridhaa ya chama kuwa KUB. Suala hili linajadiliwa ndani ya chama na mara baada ya taratibu kuwekwa tutajua mwelekeo ni upi.
  3. Nimeomba ridhaa ya chama kuongoza wabunge wenzangu kwa sababu nina uzoefu wa kutosha ndani ya Bunge la Tisa. Tafiti zote zimeonyesha kuwa mimi ni mmoja wa wabunge bora kabisa ndani ya Bunge. Kwa miaka mitano mfululizo nimekuwa polled kama Mbunge Bora kuliko wote. Hii inatokana na michango yangu Bungeni ambayo wananchi wameona kuwa imechangia kwa kiasi kikubwa sana ufanisi ambao wabunge wa CHADEMA wameonyesha. Nimekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma na kuongoza kamati hiyo kwa umakini mkubwa na kurebisha mwenendo wa Mashirika haya. Fanikio langu kubwa sana na la kujivunia ni lile la kuweza kulirejesha Shirika la STAMICO katika Mashirika ya Umma na kurejesha mali zake zote ikiwemop mgodi wa Buhemba. Serikali ilikuwa imeamua kuua STAMICO kabisa! Nimekuwa pia mjumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bunge ambayo mwenyekiti wake ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano. Haya yananipa uzoefu na maarifa ya kuwa Kiongozi bora wa Kambi ya Upinzani Bungeni.
  4. Ninaamini kuwa Wabunge wengi wa CHADEMA wana uwezo wa kushika nafasi kama hii. Sina shaka hata kidogo na uwezo wa waunge 22 wa CHADEMA. Kwa kuwa uongozi ni ushirikiano, ninaamini kuwa nitaweza kuongoza kwa ubora kabisa Kambi hii na kuweka sura chanya ya CHADEMA mbele ya Umma wa Watanzania iwapo chama kikinipa ridhaa.
  5. Humu kwenye jukwaa hili kumekuwa na watu ambao wamekuwa wakitunga uwongo wa dhahiri ili kunichafua mbele ya jamii. Ninawaomba wajue kuwa mimi ni mwadilifu sana. Udhaifu wangu mkubwa ni kupenda kusema ninaloliamini bila woga. Nimekuwa hivyo ndani ya Bunge na nimekuwa hivyo ndai ya chama siku zote. Sura ya kwamba mimi nimenunuliwa na CCM inajengwa makusudi na baadhi ya watu ili kunichafua na kunipunguzia heshima mbele ya jamii. Sura hii hujengwa kila ninapotaka kugombea nafasi ya uongozi na muda huo unapoisha shutuma hizo huisha. Naomba yeyote mwenye ushahidi wa jambo lolote aliweke wazi. Mimi sina V8, magari yangu yote second hand ya kununua kwa watu. Sijawahi kumiliku gari mpya. Mie sina nyumba Kimara (MTAKUMBUKA ILIWAHIWA KUSEMWA KUWA NINAISHI MASAKI..........), ninaishi kwenye nyumba ya kupanga NSSF Tabata na pia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa mzazi mwenzangu ambaye ni Mwalimu pale Chuo Kikuu. Sio vizuri kwa kweli kunizushia uwongo kwa malengo ya kisiasa. Ninastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa UTU wangu. Kuchafuana hakusaidii kujenga nchi hii.
  6. Nina sababu zote na sifa zote za kuwa KUB. Ninasubiri ridhaa ya chama changu na Wabunge wa chama changu. Tuna ajenda moja kubwa, kuhakikisha kuwa Uchaguzi Mkuu ujao unafanyika kwa mujibu wa Katiba Mpya na mfumo mpya wa uchaguzi. Hii ndio kazi ya kwanza ambayo KUB anapaswa kuifanya. Kazi hiyo ninaiweza. Sijawahi kusimamia ajenda ikaishia njiani (mfano sheria mpya ya madini). Iwapo changu kikinipa ridhaa nitatoa uongozi uliotukuka, ee Mungu nisaidie.

Kaka Zitto, Umesomeka, jambo la msingi unalotakiwa kujifunza kwa wana JF ni kuwa wao pia wanaruhusiwa kutoa mawazo na dukuduku zao. lengo likiwa moja tu kujenga chama chetu, kama ulivyoeleza vizuri, hatutegemei kuanzishwa kwa ajenda za kuvunja umoja wa chama ambao pia wewe ni mdau mkuu. nikupongeze kwa kueleza vizuri na nikuombe uwe tayari kwa majibu yoyote yatakayotolewa na chama. uwezo wako tunaufahamu na kuuamini lakini pia mawazo ya mashaka hatuwezi kuyazuia. please prove us wrong by doing the right things
 
Zitto you cant fool us any more. Mambo ya kutaka ushahidi hata mafisadi walitaka ushahidi. Tabia yako imebadilika sana baada ya kupata umaarufu. Maneno na vitendo vyako vinatuonyesha kuwa we sasa ni vuguvugu. Si moto wala baridi. Demokrasia haina maana kubehave unwisely. Bila hata ya huo ushahidi mimi mmojawapo sikuamini tena
 
naunga hoja,

mh.Zitto hili liko nje ya hoja yetu, lakini ningependa kujua
1.hatua ambayo chama chetu kimechukua kwa majimbo ambayo yanamigogoro ya uchakachuaji wa kura.
2.nini uamuzi wa chama juu ya uchakachuaji uliyofanywa na nec juu ya kura za urais?
 
Salaam wana JF,
Kwanza napenda kushukuru kwa michango iliyomo humu na inanihusu mimi. Kumekuwa na maneno mengi ya kweli na yasiyo ya kweli kuhusu suala la mimi kugombea nafasi ya Kiongozi wa Upinzani Bungeni. Ninaomba kusema ifuatavyo.
  1. Chama chetu kimepata viti vingi sana vya Bunge mara baada ya uchaguzi wa mwaka huu. Hii ni ishara njema sana kuwa sasa demokrasia nchini itakomaa kutokana na kuwa na Bunge Imara. Idadi kubwa ya wabunge wa upinzani ndani ya Bunge inapunguza nguvu kwa kiasi kikubwa za CCM ndani ya Bunge. Tumejitahidi sana kukifikisha chama chetu mahala hapa. Nawapongeza sana viongozi wa chama chetu kwa mafanikio haya na hasa Mwenyekiti wa Taifa wa chama na Katibu Mkuu wetu ambaye alikuwa mgombea Urais.
  2. Chama chetu kimepata viti vya kuweza kuunda Kambi ya Upinzani Bungeni ama peke yake au kwa kushirikiana na vyama vingine vye wabunge. Kwa vyovyote vile atahitajika Mbunge mmoja wa Upinzani na hususani kutoka CHADEMA ambaye atakuwa KUB. CHADEMA bado haijatangaza utaratibu utakaotumika kupata KUB kutoka miongoni mwa wabunge wake. Nimewajulisha viongozi wangu wa chama kuwa nina nia ya kuomba ridhaa ya chama kuwa KUB. Suala hili linajadiliwa ndani ya chama na mara baada ya taratibu kuwekwa tutajua mwelekeo ni upi.
  3. Nimeomba ridhaa ya chama kuongoza wabunge wenzangu kwa sababu nina uzoefu wa kutosha ndani ya Bunge la Tisa. Tafiti zote zimeonyesha kuwa mimi ni mmoja wa wabunge bora kabisa ndani ya Bunge. Kwa miaka mitano mfululizo nimekuwa polled kama Mbunge Bora kuliko wote. Hii inatokana na michango yangu Bungeni ambayo wananchi wameona kuwa imechangia kwa kiasi kikubwa sana ufanisi ambao wabunge wa CHADEMA wameonyesha. Nimekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma na kuongoza kamati hiyo kwa umakini mkubwa na kurebisha mwenendo wa Mashirika haya. Fanikio langu kubwa sana na la kujivunia ni lile la kuweza kulirejesha Shirika la STAMICO katika Mashirika ya Umma na kurejesha mali zake zote ikiwemop mgodi wa Buhemba. Serikali ilikuwa imeamua kuua STAMICO kabisa! Nimekuwa pia mjumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bunge ambayo mwenyekiti wake ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano. Haya yananipa uzoefu na maarifa ya kuwa Kiongozi bora wa Kambi ya Upinzani Bungeni.
  4. Ninaamini kuwa Wabunge wengi wa CHADEMA wana uwezo wa kushika nafasi kama hii. Sina shaka hata kidogo na uwezo wa waunge 22 wa CHADEMA. Kwa kuwa uongozi ni ushirikiano, ninaamini kuwa nitaweza kuongoza kwa ubora kabisa Kambi hii na kuweka sura chanya ya CHADEMA mbele ya Umma wa Watanzania iwapo chama kikinipa ridhaa.
  5. Humu kwenye jukwaa hili kumekuwa na watu ambao wamekuwa wakitunga uwongo wa dhahiri ili kunichafua mbele ya jamii. Ninawaomba wajue kuwa mimi ni mwadilifu sana. Udhaifu wangu mkubwa ni kupenda kusema ninaloliamini bila woga. Nimekuwa hivyo ndani ya Bunge na nimekuwa hivyo ndai ya chama siku zote. Sura ya kwamba mimi nimenunuliwa na CCM inajengwa makusudi na baadhi ya watu ili kunichafua na kunipunguzia heshima mbele ya jamii. Sura hii hujengwa kila ninapotaka kugombea nafasi ya uongozi na muda huo unapoisha shutuma hizo huisha. Naomba yeyote mwenye ushahidi wa jambo lolote aliweke wazi. Mimi sina V8, magari yangu yote second hand ya kununua kwa watu. Sijawahi kumiliku gari mpya. Mie sina nyumba Kimara (MTAKUMBUKA ILIWAHIWA KUSEMWA KUWA NINAISHI MASAKI..........), ninaishi kwenye nyumba ya kupanga NSSF Tabata na pia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa mzazi mwenzangu ambaye ni Mwalimu pale Chuo Kikuu. Sio vizuri kwa kweli kunizushia uwongo kwa malengo ya kisiasa. Ninastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa UTU wangu. Kuchafuana hakusaidii kujenga nchi hii.
  6. Nina sababu zote na sifa zote za kuwa KUB. Ninasubiri ridhaa ya chama changu na Wabunge wa chama changu. Tuna ajenda moja kubwa, kuhakikisha kuwa Uchaguzi Mkuu ujao unafanyika kwa mujibu wa Katiba Mpya na mfumo mpya wa uchaguzi. Hii ndio kazi ya kwanza ambayo KUB anapaswa kuifanya. Kazi hiyo ninaiweza. Sijawahi kusimamia ajenda ikaishia njiani (mfano sheria mpya ya madini). Iwapo changu kikinipa ridhaa nitatoa uongozi uliotukuka, ee Mungu nisaidie.

Heshima kwako Zitto,

Mkuu kama umeomba ridhaa ya chama chako kwanini unaanza kampeni nje ya chama.Matangazo face book & JF ya nini ?.Nadhani umetumia njia sahihi kuomba nafasi hiyo muhimu tatizo langu ni jambo lenyewe kuwa public ukiikosa yatakuwepo malalamiko mengi yasiyo na msingi.
 
Heshima kwako Zitto,

Mkuu kama umeomba ridhaa ya chama chako kwanini unaanza kampeni nje ya chama.Matangazo face book & JF ya nini ?.Nadhani umetumia njia sahihi kuomba nafasi hiyo muhimu tatizo langu ni jambo lenyewe kuwa public ukiikosa yatakuwepo malalamiko mengi yasiyo na msingi.
Wise advice.
 
Kila la kheri ndugu Zitto. Natumai utashirikiana vyema na sisi wana CCM katika kuijenga vyema nchi yetu ili watoto na wajukuu wetu waishi maisha bora zaidi.
 
Heshima kwako Zitto,

Mkuu kama umeomba ridhaa ya chama chako kwanini unaanza kampeni nje ya chama.Matangazo face book & JF ya nini ?.Nadhani umetumia njia sahihi kuomba nafasi hiyo muhimu tatizo langu ni jambo lenyewe kuwa public ukiikosa yatakuwepo malalamiko mengi yasiyo na msingi.

Kwa nini mnapenda mambo ya kuficha. Ndugu Zitto keshasema kuwa haoni tatizo katika kutoa maoni yake hadharani. Mbona watu mnaogopa demokrasia????? woga huu utaisha lini ndani ya mioyo ya watanzania???

Achana na nidhamu ya woga???
 
Kuna mifumo miwili inayoweza kutumika kupata kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni. Mfumo wa kwanza ni ule wa Uingereza, ambapo kiongozi wa chama anakuwa moja kwa moja ni kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni na waziri mkuu mtarajiwa. Kwa kufuata mfumo huu ina maana kuwa M/Kiti wa CHADEMA moja kwa moja anakuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni na by extension anaweza kuwa ndio mgombea wa kiti cha urais katika chaguzi zijazo. Uzuri wa mfumo huu ni kwamba una-consolidate madaraka na mamlaka ya uongozi wa chama ndani na nje ya bunge. Ubaya au udhaifu wa mfumo huu ni katika maeneo mawili. Mosi, itakuwa vigumu kwa chama kuwaajibisha wabunge kwa sababu tayari M/Kiti wake ni kiongozi wa bunge. Vilevile ni vigumu sana kwa chama kuwaagiziza wabunge kutekeleza jambo fulani bungeni-kuna hatari ya wabunge kuwa wanatoa maelekezo kwa chama. Pili, mfumo huu unaenda kinyume na dhana ya CHADEMA ya kupinga kurundika madaraka kwa mtu mmoja. Kumbuka malengo mojawapo ya CHADEMA ni kumpunguzia Rais madaraka makubwa aliyo nayo.

Mfumo wa pili ni ule wa Amerika. Msingi wa demokrasia ya Amerika ni mgawanyo wa madaraka (separation of power). Wamerika hawapendi mtu mmoja arundikiwa madaraka. Kwa hiyo wao Kiongozi wa Chama sio lazima awe Kiongozi wa Kambi ya upinzani bungeni, na kwa kweli siye. Ndio maana unaona leo aliyekuwa Spika wa Beraza la Wawakilishi Nancy Pelosi ndio anayegombea Minority Leadership. Wanachofanya wao ni kwa mbunge yeyote anayetaka kuwa kiongozi wao bungeni kugombea na wabunge wanamchagua mojawapo. Ni nafasi yenye ushindani mkubwa sana ndani ya wabunge wa Democrats au Republicans. Kama CHADEMA wataamua kutumia mfumo huu ina maana kwamba wabunge watakuwa huru kugombea nafasi ya kiongozi wa upinzani na wabunge wenzao kumchagua mojawapo.

Tatizo letu bado tumelewa siasa za umwinyi na uCCM. Tunaona kushindana ni jambo la hatari kwa chama. Kwa nini kushindana lionekana jambo la hatari na sio la kukuza demokrasiandani ya chama? Kuna ubaya gani kwa wanaotaka nafasi ya uongozi wa wabunge wapinzani kugombea na wenzao kuwachagua? Mambo ya kukwepa kushindana katika ngazi ya chama ndio yanayoletekeza uchakajuaji hata katika ngazi ya Taifa. Ni muhimu tukazoea siasa za ushindani ndani na nje ya vyama kwa sababu ndio msingi wa mfumo wa demokrasia ambao tumeamua kuufuata.
Kwa maoni yangu ni kwamba sifa moja muhimu sana kwa mtu atakayechaguliwa kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni awe ni mwenye uwezo wa kuwaunganisha wapinzani wengine katika bunge. Ni muhimu sana wapinzani wafanye kazi kama timu moja. Itakuwa ni balaa kama tutapata kiongozi ambaye yeye ana deal na wabunge wake tu na kuwatenga wengine. Ushirikiano bungeni uwe ni mwanzo wa ushirikiano mpana tunapojiandaa kwa uchaguzi wa 2015.

Mwisho, jambo la mtu kujitokeza mapema sio jambo la kulaaniwa. Ni jambo zuri na la kupongezwa. Kama unataka unasema sio unavizia au unataka watu wengine wakusemee. Tuna wabunge mahiri sana wa kambi ya upinzani na ninaamini jambo la nani awe kiongozi wao halitawayumbisha hata kidogo.

Sasa Chadema mfumo wao ni upi? Maanake wewe ndio consultant wao, possibly wamekwisha ku-consult. Zitto hafai kwa sababu alikubali kuingia kwenye tume ya JK ya madini na kutaka kununua mitambo chakavu ya Dowans kinyume na sheria ya manunuzi ya umma na kudai bila kufanya hivyo nchi itaingia gizani. Hivi muda huo wa kuingia gizani bado? Dowans imezaliwa na Richmond halafu Serikali inunue mitambo yake sio mwendelezo wa ufisadi wa Richmond huo?

Tunataka mtu kama Hamad Rashid aliyemtoa kamasi na chozi bwana Pinda.

Suala la tume ya madini alitakiwa kuisubiri ripoti na kuikosoa na sio kuingia huko, hivi tutajuaje kama maamuzi aliyapinga au hakuyapinga? Maamuzi ya tume hiyo yalikuwa yanapitishwa vipi?
 
Heshima kwako Zitto,

Mkuu kama umeomba ridhaa ya chama chako kwanini unaanza kampeni nje ya chama.Matangazo face book & JF ya nini ?.Nadhani umetumia njia sahihi kuomba nafasi hiyo muhimu tatizo langu ni jambo lenyewe kuwa public ukiikosa yatakuwepo malalamiko mengi yasiyo na msingi.
Wakuu zangu jamani mweee.. mbona Mama Anna Kilango,Chenge na wengine wamechukua fomu za kugombea Uspika na hakuna mtu alokuja hapa na kusema wao ni watu wa aina gani?..
Hivi huyu Zitto kweli kawafanyia kipi kibaya zaidi ambacho mnakosa hata heshima kwake....Na hakika mnatisha sana kuona jinsi mnavyoweza kuchonganisha watu ndani ya chama kwa sababu tu mtu huyo anapingana na Mbowe. Yalitokea kwa Chacha sasa mnaanza kumfuata Zitto hali mkijua wazi kwamba chokochoko kama hizi hazina faida isipokuwa kukibomoa chama. Na hakika mnazidi kuwafanya watu waamini yasiyokuwepo...

Maamuzi ya Zitto kuuhusiana na Dowans hata Dr.Slaa mwenyewe alikuwa akim support Zitto, nakumbuka alikuja hapa kijiweni na kutuambia tusichukue hukumu mapema kwani hata yeye alikubaliana na mawazo ya mabaraza mawili kukutana kufikia Uamuzi pasipo kutoa msimamo wa chama kuhusiana na swala la mitambo ya Dowans. hakuna kiongozi hata mmoja toka Chadema aliyeweza kutueleza msimamo wa chama kuhusiana na swala hilo wakati mgogoro ule ukiendelea, hivyo kusema haya yalikuwa mawazo ya Zitto bado tunamtungia kwani hatujui chama kililkuwa na msimamo gani ila sote tunafahamu JF ilikuwa na msimamo gani...

Yes, Zitto amewahi kufanya makosa huko nyuma kinyume cha tulivyotarajia, lakini Zitto kugombea Uenyekiti wa chama halikuwa kosa hata kidogo tena ilikuwa sifa kwa chama kuonyesha demokrasia inavyotumika ndani ya Chadema.

Zitto kugombea Uongozi wa Upinzani hauna makosa hata kidogo kwa sababu demokrasia ni pamoja na kuchagua, na hofu yenu kubwa ni kwamba Zitto anaweza kushinda, hakuna lolote zaidi ya hofu. haya maneno ya dhihaka ndiyo waliyotumia CCM kumdhihaki Dr.Slaa ktk uchaguzi na nyote humu hamkupenda kuyasikia hata kama kulikuwepo na dalili za ukweli lakini mlidai ushahidi. Ni chuki ile ile iliyotumika kumkosoa Dr.Slaa kila siku ya Mungu ndiyo inatumika hapa kumkosoa Zitto ili hali yeye amekuwa mwiba kwenu..

Mimi nasema hivi, mara zote swala la Uchaguzi wa kiongozi wa Upinzani ni swala la kikatiba, mfumo na uundwaji wake unatakiwa kuwa ndani ya katiba kama zilivyo nafasi nyinginezo kwa hiyo kukilaumu chama Chadema kwa kutokuwa na mfumo tayari ni kutafuta mchawi wakati mchawi wetu ni Katiba yenyewe. Mbona nafasi nyingine zooote zinajieleza wazi iweje hii iwe ya kutungwa na chama kinachochukua nafasi ya pili..Kwa hiyo kesho kikiingia chama kingine kinaweza chagua kivyake vile vile hata kumweka mtu wa CCM ikiwa watapenda au sio?.


Hatuwezi fuata utaratibu wa Marekani au UK kwa sababu Marekani Upinzani ni chama kimoja wakati Tanzania tuna vyama zaidi ya vinane. Kwa hiyo mgombea wa kiti hiki anatakiwa akubalike ili kuunda nguvu moja ya Upinzani bungeni na sio kuwakilisha mawazo ya Chadema zaidi ya vyama vinginevyo. Tatizo la kufikiria kwamba pale bungeni anatakiwa kiongozi wa kuwakilisha zaidi Chadema kutawafanya wabunge wa vyama vingine kutofautiana na Chadema, hivyo kuwaunga mkono CCM na kupoteza zaidi nguvu ya Upinzani. Kinachotakiwa ni ushirikiano wa wabunge wa vyama vya Upinzani dhidi ya CCM kwa manufaa ya ya wananchi na sii ya Chadema. Kwa hiyo tuwe makini sana na vitu tunavyo kiombea chama hiki kwani tunaweza kabisa kubomoa hata kidogo kilichokwisha jengwa..
 
SPIKA-CHENGE
RAISI-JAKAYA
KIONGOZI WA UPINZANI BUNGENI-ZITTO


niborani hame nchi sasa nimechoka na naumia na sina la kufanya ni sawa na keshi la kivita likiniteketeza huku nikiwa nimefungwa kamba mikononi na miguuni na nimezibwa mdomo na matambara na sioni sbb ya damu imeziba macho

Nalililia nchiyangu.. sipaswi kuumia hivi katika nchi niliozaliwa mimi.. naumia
 
pole sana wana JF wengi tu tunaumia nivile tu tumekosa la kufanya laki ipo siku,

nec ya uchakachuaji inaumiza sana
 
Kuweni wawazi mnapotoa mawzo yenu,kuna kitu mnakificha huu si wakati wakuficha ficha nyinyi vipi sio wakweli kabisa? Nyinyi humu JF wengi wenu mmeenda shule lakini inaonekana uelewa wenu ni mdogo sana! lakini ndo watanganyika wengi mlivo ni watu wa mihemko(emotional) tazameni us election 2008 walivojuu katika maoni yao baadhi ya wamerekani walikuwa wakisema wazi kabisa kuwa hawamtaki Obama kwa sababu ni muislaam na wengine wakisema ni muafrika na mawazo yao yaliheshimiwa na ikawa ni njia moja ya kuondoa ubaguzi na other descriminations.na tokea wakati huo wayahudi wa usa walikuwa wakisema kama obama ni one term president na muelekeo ndio huo kutokana na matokeo ya midle term election.unajua kutoa mawazo kwa uhuru zaidi bila ya kuficha ni njia moja ambayo watanzania itawasaidia katika kutatua matatizo yao ya kibaguzi,mfano mimi pamoja na sababu nyingi nilizonazo za kutokumchagua Dr.Slaa moja ni Mkristo( KAFIRI),kuweni wawazi semeni hatumtaki zitto kwa sababu ni muislaam,najua kwa mawazo yenu mafupi mushaaccount,RAISI MUISLAAM,M/R MUISLAAM,,,,,BSI na kiongozi wa upinzani awe muislaam,.. ACHENI MAWAZO FINYU AYO APEWE MWENYE UWEZO AMBAYE BILA SHAKA KWA SASA CHADEMA NI ZITTO,ACHENI UDINI...!!!MBOWE NA TUNDU LISU hawana hata tonation ya kuongea ni watu wa mihemkwo tu kama wakina Kilango.......na Nkya.
 
Mh. Zitto;

Nimekusoma kwa makini sana na hoja zako zote ni za msingi na zinatoa majibu kwa wale wanaoeneza propaganda dhidi yako.

Bahati mbaya siasa zetu za TZ na JF zinahitaji burden ya proof iwe kwa mtuhumiwa si anayetuhumu, unless kama suaala likienda mahakamani.

Ninachofahamu, wewe ni kijana mwenye vision kubwa sana na nchi hii. which is good. Shida kubwa iliyopo kwa Watanzania wengi na hata ndani ya chama chako ni kwenda na kasi yako. (Bado Watanzania hatujaamka. fikiria turn out ya voters only 42% baada ya kampeni ya media ya karibu miezi 6).

katika hali kama hii, si wazo baya ku-slow down pale ambapo wengi hawaendi kwa speed yako.

Ninachofahamu mimi, ili uwe kiongozi mzuri na kutimiza ndoto zako za kuwa Rais, unahitaji watu wengi wakuunge mkono ndani na nje ya chama chako. Jijengenezee marafiki wengi kuliko maadui. Kama hawataki kukupa nafasi, work and make a difference from where you are. Kizuri hakifichiki. Wakikuzibia njia watu watakuibua wenyewe. Iga mfano wa Dr. Slaa. Hakuomba kugombea Urais, aliombwa. As a result ameleta impact kubwa sana katika uchaguzi wa mwaka huu kwa kuleta upinzani mkali kwa JK na hata kuzalisha wabunge zaidi.

You know more about Mwalimu Nyerere . . . . mbinu zake nyingi na mikakati yake bado viko valid.

Huu ni ushauri wangu tu wa kiungwana. You may take it, or leave it.

Good luck Mkuu!
 
Mi wakubwa Zitto si mwamini kabisa yeye mwenyewe anajua ni wapi alikosea.
HELA HAIWEZI KUNUNUA UTU WA MTANZANIA.........muulizeni katika miaka yake ya ubunge ni ishu gani aliitetea bungeni ikawa imempa jina kuliko zote? na je hiyo ishu hatima yake iliishia wapi??
 
Back
Top Bottom