Zitto awazindua Wasanii: 153 wameshasaini kuvunja mkataba

Wakati wanaingia mikataba, wameingia kimya kimya na kila mtu kivyake....mbona wanataka kutoka kwa kelele na kama kundi? Hii press release ina nguvu gani ya kisheria hasa ukizingatia uwepo wa mikataba...isije ikawa ni kupoteza muda na rasilimali (hasa kama watakubali kutumika kwa manufaa ya wanasiasa bila kuwa makini na kuwa na uhakika wa kile wanachikipigania).

Mikataba yao inasemaje kuhusiana na kuvunja/kuvunjika? Kwa kuwa muziki ni biashara, je suala hili wanamuziki linaendana vipi na sheria ya ushindani wa kibiashara (The Fair Competition Act, 2003)? Ni vema wasanii wakawa makini katika masuala haya yahusuyo mikataba ambayo inaweza ku-back fire kwa individual musicians na sio kwa group (maana sio group la hao wanamuziki 153 lilioingia mkataba na makampuni ya simu)

Well said. Wasijekuwa wamekurupuka kuvunja mkataba na makampuni ya simu bila kuzingatia legal issues zinawabanaje kwenye huo mkataba wa kinyonyaji. Kuingia mkataba ni kitu kimoja na kuvunja mkataba ni kitu kingine, one party must suffer the consequences of breaching the contract, in our case, the artists.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Zitto amehusika sana kuwashtua wasanii kwa jinsi wanavyoibiwa mapato ya kazi zao, nafkiri wote tuliskia hotuba yake bungeni. Makampuni ya simu hayakaa kimya, tusubiri tuone kitakachofuata.

Kama hawajawahi kumpatia rushwa hawatakuwa na chakumfanya bwana!!!! Yaani kuwaamsha wasanii juu ya haki yao ndiyo wamlipizie kisasi?? HAYA NGOJA TUONE BASI
 
kama kawa,kazi ya mbunge ni kuwatetea na kuwafumbua macho wanyonge,kampuni hazina cha kufanya ila kukaa na wasnii upya!
 
kwani wasanii wa nyimbo za dini nao wanataka haki gani wakati ring tone zinaeneza ujumbe wa neno la mungu? kwa maoni yangu muziki wa dini ni sadaka na si biashara ,kwahiyo kuwazuia makampuni ya simu ni sawa na kuweka makwazo kwa neno la mungu!

Kama ni sadaka basi na hata hayo makampuni ya simu yasiuze ili kila mpenda gospel ajiunge pasipo kudaiwa pesa.
 
kuna kampuni ya mhindi iko pale shopers plaza ndo inawasinisha mikataba wasanii kwa kifupi watakua wanaliwa na huyo mhindi ye ndo anadeal na mitandao ya simu nafkiri hakuna mkataba wa moja kwa moja wa kampuni ya simu na msanii
 
aliye piga kazi ni kamanda mbilinyi aka sugu zito alikuwepo inakalibia miaka 8 na habali hii haikuwepo leo kaingia sugu kwa miaka 2 tu vitu vinaongeleka sasa hongera sugu
 
kwani wasanii wa nyimbo za dini nao wanataka haki gani wakati ring tone zinaeneza ujumbe wa neno la mungu? kwa maoni yangu muziki wa dini ni sadaka na si biashara ,kwahiyo kuwazuia makampuni ya simu ni sawa na kuweka makwazo kwa neno la mungu!

Kumbuka kuwa huwo wimbo hautolewi bure. Anayeuweka kwenye simu anaulipia. Na asilimia kubwa ya hizo fedha zinaenda kwa makampuni ya simu na sio kwa mwimbaji au mwenezaji wa neno la mungu. Hivyo ni bora makampuni ya simu yasiwe yanatoza hela kwa kueneza neno la mungu iwe sadaka kweli au hiyo hela kwa kiasi kikubwa itumike kuendeleza neno la mungu kwa kumwezesha mtungaji atoe nyimbo nyingine nk. nk.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom