Pengo
JF-Expert Member
- Oct 15, 2009
- 579
- 10
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Zuberi Kabwe amejipanga kikamilifu kulitetea jimbo lake la Kigoma Kaskazini na kurudi bungeni kwa kuweka program ya michango mitandaoni.
Kwa mujibu matangazo aliyoyaweka kwenye ukurasa wake wa Facebook, Zitto ametoa nambari mbalimbali za akaunti na kuwataka Watanzania wanaomuunga mkono, wamchangie fedha ili kutunisha mfuko wake wa kampeni.
Katika maelezo yake, Zitto amewataka Watanzania wenye ni maendeleo ya demokrasia kumchangia ili aweze kurudi bungeni.
Tayari nimekabidhi fomu zangu kwa ajili ya kugombea ubunge Jimbo la Kigoma Kaskazini ili kuwatumikia tena wananchi wa Kigoma Kaskazini na Tanzania kwa jumla. Mimi nipo tayari, ilisema taarifa ya Zitto Mtandaoni.
Katika maelezo yake, Zitto alizitaja nambari za akaunti benki ya CRDB, 01J2082022500 ZITTO KABWE ZUBERI na NMB, 2012510971 KABWE ZUBERI ZITTO.
Gazeti hili lilipowasiliana na Zitto wikiendi iliyopita alisema: Nimeita michango mitandaoni kwa sababu naamini wengi wangependa kunichangia ili kukuza demokrasia. Wadau wanaweza kunipata kwa namba 0756-809535 na wakiweza wanitumie kwa M-Pesa.
Chanzo:-Global Publishers
Kwa mujibu matangazo aliyoyaweka kwenye ukurasa wake wa Facebook, Zitto ametoa nambari mbalimbali za akaunti na kuwataka Watanzania wanaomuunga mkono, wamchangie fedha ili kutunisha mfuko wake wa kampeni.
Katika maelezo yake, Zitto amewataka Watanzania wenye ni maendeleo ya demokrasia kumchangia ili aweze kurudi bungeni.
Tayari nimekabidhi fomu zangu kwa ajili ya kugombea ubunge Jimbo la Kigoma Kaskazini ili kuwatumikia tena wananchi wa Kigoma Kaskazini na Tanzania kwa jumla. Mimi nipo tayari, ilisema taarifa ya Zitto Mtandaoni.
Katika maelezo yake, Zitto alizitaja nambari za akaunti benki ya CRDB, 01J2082022500 ZITTO KABWE ZUBERI na NMB, 2012510971 KABWE ZUBERI ZITTO.
Gazeti hili lilipowasiliana na Zitto wikiendi iliyopita alisema: Nimeita michango mitandaoni kwa sababu naamini wengi wangependa kunichangia ili kukuza demokrasia. Wadau wanaweza kunipata kwa namba 0756-809535 na wakiweza wanitumie kwa M-Pesa.
Chanzo:-Global Publishers