Zitto aanika siri nyeti za Mbowe! Adai hatakufa kama Chacha Wangwe...

Status
Not open for further replies.
Zitto hajachelewa kusema ukweli ukizingatia CDM hawapendi kuambiwa ukweli wa udhaifu wao. Kaka Zitto funguka zaidi kuhusu deal la Kinana na Sumaye maana umetuacha njia panda. Pia usisahau lile la NHC na NSSF sisi tunataka kujua ili tuchague pumba na mchele.

Kama unajua Chacha wangwe alichofanyiwa pls tenda Polis ukawape ukweli wote haki ichukue mkondo wake.
Mchuzi wa mbwa unanywewa ukiwa ungali moto, alikuwa wapi siku zote, ni sawa unavamiwa leo na majambazi au vibaka unapiga kimya mpaka unapata fununu ya mwizi wako ndio unakwenda kuripoti
 
Lipumba aliwahi kuandamana na Akachezea kichapo mpk mkono ukaumia.

Mchungaji Mtikila naye pia aliwahi kua na kesi nyingi tu Mahakamani.

Baadhi ya wabunge Wa Cdm na makada Wa Cdm wamewahi kutana na nguvu ya dola na wengine kua na makesi!

ZZK Mbona Mara zote ktk hizo kadhia yeye hayupo na Wala sijapata kusikia ana kesi ya kujibu Zaidi ya hii alofungua mwenyewe? Kwanini Huyu asikumbane na nguvu ya dola Km wapinzani wengine au ana uhusiano gani na dola? Aliwahi tu kupewa adhabu bungeni lkn ktk mambo mengine sijapata kusikia!

Tafakali sn juu ya ZZK!
 
Mkuki kwa nguruwe sio??

Mwenyekiti CHADEMA anatia aibu,aje akanushe tuhuma zake sasa na yeye

Tundu lisu anacheza ngoma ambayo haijui,wanamtanguliza tu kichwa kichwa yeye hajui kama anajidhalilisha!

Ni ujinga mtu mwenye elimu kama ya tundu kupelekwa pelekwa na kujazwa uongo na mbowe...

Mbowe atoke atuachie chama chetu alishashindwa kabla hajaanza

Na Dr Slaa ajiangalie naona anapotea taratibu



Chama chenu wewe na nani? Usione vyaelea vimeundwa.
 
Zito ni nyepesi kwa sasa kutokana na ushauri mbovu na kiburi kisicho na maana. Hana nidhamu! Yawezekanaje uitwe kwenye vikao halali vya chama chako uingie mitini kisha ukiwa mafichoni unatunga uongo eti m/kiti alihongwa! Kwanini hukwenda pale useme hilo kama ndo utetezi wako?
Nilwahi kukuambia humu kuwa unaanzisha hoja ambazo huandai mwisho wake! Ona ya buswagi, hela za uswiss na hili la kutumika linavyokosa kumalizwa na wewe mwanzishaji.
Wanakufukuza uanachama sasa na ubunge ndo basi huoni kuwa umekatwa miguu na kufungwa mdomo wa siasa. Nani atakusikiliza? Labda uwagawie hiyo 3bln.
Pole lakini!! Shule haijakusaidia kuchambua yepi yenye umuhimu wa kesho na si leo!
 
mfa maji haachi kutapatapa

na kelele za chura hazimzuii tembo kunywa maji!
 
Nyinyi Wafuasi wa Mbowe mnashangaza sana kwakweli,Hivi mara hii mshasahau kuwa Zitto alianza kutuhumiwa kwanza na Lissu na yeye ikambidi ajibu mapigo?Nani asiyejua kuwa Mbowe yupo nyuma ya yote haya yanayomtokea Zitto akiwatumia vibaraka wake?Kwahiyo msichukie sana jiandaeni kusikia uozo mwingi kuhusu huyo Mungu wenu na safari asiposimama Mahakamani sijui!

Uozo wa kutungwa na Zitto nao ni uozo?.
 
siasa mbaya aisee, hawa jamaa huwa wanahutubia mishipa imewatoka,oh tunataka kuwakomboa watz,mara oh kamanda wa anga na watu tunawaamini, kumbe wanapokea mihela kibao nyuma ya pazia

Toka lini mgacha akawa mkombozi?chezeya mbesa weye
 
AMA KWELI FADHILI MBUZI UTAMLA NYAMA.............

Nampa pole sana Mh Freeman Mbowe, mwenyekiti wa Chadema Taifa kwa kutukanwa na kukosewa adabu na kijana mdogo, Msaliti Zitto Kabwe, ambaye leo mafanikio yake yametokana na yeye Mh Mbowe, lakini kasahau na kaamua kukutuna ati wewe ndo kamati kuu!

vile vile nimpe pole Mh Tundu Lissu Mbunge wa Singida mashariki na Mwanasheria wa chama, kwa kuitwa Kifaranga na huyu kijana ----- asiye na Adabu, we mpuuuze kwani leo amewadhihirishia watanzania kuwa hafai hata kuwa Balozi wa nyumba kumi......

Zitto Z Kabwe mpaka sasa hujakanusha tuhuma za kweli kabisa kwamba ulihongwa Magari mawili na Mh mkono iliusimsimamishe mgombea Msoma Vijijini, badala yake uliishia kujitoa ufahamu na kuwatukana Viongozi mtandaoni kuonyesha ulivyofilisika mawazo kama si kufilisika hoja!

Zitto Kabwe amejitoa ufahamu na kudai eti mtu asiyemuheshimu mke wake aliyewazalia watoto wake hawezi kumfundisha mtu maadili.......
Zitto, kabla ujanyoosha kidole kwa mwenzako embu jaribu kujitazama wewe mpaka leo una umri miaka 37 umeshindwa kuoa, na kinacho kusumbua ni uzinzi, embu kumbuka April tukio la aibu ulilolifanya pale Mount Meru Arusha, baada ya kunywa KONYAGI, mbona sisi hatusemi..........

Si jambo jema kujadili misha ya Binafsi ya Kiongozi, kwani hakuna aliye mkamilifu Chini ya Jua.......

SI VEMA MAAMUZI YA KAMATI KUU KUMBEBESHA MH MBOWE NA LISSU PEKE YAO..

jee wewe unatofauti gani, hiyo ya konyagi imeletwa na nini kama sio mnafiki nawe.

Zito anastahili kujibu la magari, lakini na mbowe nae anastahili kujibu tuhuma zilizoletwa na zitto. Ndugu kama una nia ya kumkandamiza zitto, kwa niaba yako ya kuwatetea mbowe na tundu, basi hustahili kuwa mtoa haki, bali unakuwa mpambe.

Mbona Tundu alipomshtumu zitto kuhusu magari, mlinyamaza kimya hamkusema tundu hana busara. Hizi siasa za kupendeleana ndizo zinazo ifilisi CDM.

La Kujiuliza hapa wale wapambe wa Slaa mbona wamekaa kimya, au wanafurahia vita za kuchafuana kati ya mbowe na zitto , maana hiyo sarakasi inampa upenyo mkubwa kiondozi wao Slaa kushika usukani wa chama, na kuhamishia mamlaka karatu... Hiyo itakuwa safi sana.
 
Nasubiri kauli rasmi ya Mbowe,bado cjaamiini ma gazeti ambayo zzk na Dr Mkumbo ni waandishi wa makala
 
Pamoja na kwamba natamani dogo apewe one more chance lakini naungana na wewe alikuwa wapi siku zote kusema hayo aliyosema kama ni kweli maana mnapokuwa marafiki mlivumiliana kwenye madhaifu flani flani lakini once mkitofautiana tu mnaanza kuibua yale yote yaliyojificha kipindi kile mlipokuwa mpo vizuri, sidhani kama ni utamaduni mzuri huu kama mlivumiliana siku za nyuma basi ni busara kuendelea kuvumiliana pindi mnapotofautiana

Mkuu kuvumiliana kupi unakozungumzia!Mbona wao walishindwa kumvumilia udhaifu wake wakapanga kumtimua?Tujaribu kubalance mahaba jamani.
 
MOSES MACHALI.
"Hayo hapo chini ndiyo maneno aliyoyasema kupitia mtandao wa kijamii, jisomee ujue anachokisema na majibu ujipe mwenyewe>>>>"

Moses Machali
Kuna watu wanazungumzia nidhamu na kwamba ili mtu uweze kufanikiwa maisha ni lazima uwe na nidhamu. Nami nakubaliana na kauli hiyo, lakini tunapaswa kujiuliza ni nidhamu ya aina gani?

Inawezekana mtu akasema ZITTO hana nidhamu kwa chama chake lakini ikawa ni kinyume chake. Hii ni kwa sababu hana nguvu za kufanya maamuzi ndani ya chama na kwa hiyo akawa anatakiwa kutii mambo ambayo yako kinyume cha utaratibu wa chama chake lakini kwa kuwa yanatolewa na kusimamiwa na watu wenye nguvu basi akipinga anaonekana hana nidhamu. Binafsi niseme moja tu kwamba, wakati mwingine sisi wanasiasa tunakurupuka na kukosea.

Katika sakata la zitto na CDM nadhani pande zote zinaweza kuwa na makosa kwa kuwa hadi mambo yamefikia hapo yalipofika ni kwa sababu kumekosekana collective responsibilty na imekosekana pia nidhamu ya kiuongozi inavyoonekana kwa kuwa hata akina Mbowe; Dr. SLAA na wengine siyo malaika wakati mwingine nao hukosea tena sana.

Na kwa hiyo napingana na wale wote wanaosema mkosefu ni Zitto tu la hasha ni uonevu kwa upande mmoja.

Lakini pia napingana na wale wote wanaosema Zitto anaonewa tu la hasha inawezekana kweli kukawa kuna makosa tofauti na historia tunayoifahamu wachache. Ngoja niwakumbushe kidogo wana jamvi: Mwaka 2009 wakati wa uchaguzi ndani ya CDM uliibuka mgogoro kati kundi la Mbowe na kundi la Zitto ambapo wazee wa chama wakamtaka Zitto aache kugombea uenyekiti wa chama kwa kuwa yeye ni kijana bado ana muda mwingi na kwamba anaweza kugombea wakati mwingine na kwa hiyo amwachie mbowe kwanza akiongoze chama.

Finally Zitto alijiondoa kwa shingo upande yaani pasipo kupenda na wafuasi wengine wa Zitto wakakutana na majanga mazito ndani ya CDM na wakaamua kuondoka CDM wakaitwa majina ya kwamba wao ni sisimizi nk; wakati mwingine wakaitwa Wasaliti na watu wenye njaa nk. Waliopatwa na kadhia hiyo baadhi ni hawa wafuatao: mhe. david KAFULILA(MB), MARTINE DANDA kutoka Iringa.

Wengine ni akina Mhe. Mkosamali(mb) pamoja nami Machali(mb) na baadaye kabisa waliondoka akina Mama Msole nwengineo. Wapo wadau wasemao kwamba huenda mgogoro uliopo hivi sasa unatokana na kile kilichotokea 2009 kwa kuwa CDM walipaswa kufanya uchaguzi lakini wakaahirisha kwa kile kinachosema kwamba watamwambia nini Mhe. Zitto mwaka huu katika kugombea Uenyekiti wa chama kama ilivyo dhamira yake ya siku nyingi ya kukiongoza CDM.

INASEMEKANA kwamba baadhi ya viongozi wa CDM wenye nguvu ndani ya chama wametafakari ni namna gani Zitto hapenyi katika kinyanganyiro cha uchaguzi ikaonekana ni ngumu sana na kwamba inabidi kuangalia namna ya kufanya na huenda ndiyo haya tunayoyaona sasa. Aidha Ikumbukwe kuwa kuna nyakati vyombo vya habari vilimnukuu Mhe. Mbowe akisema kwamba Dr. Slaa ndiye atakaechukua fomu za kugombea Urais na kwamba yeye hatagombea tena(Mbowe), Lakini Zitto amekuwa akitangaza nia ya kugombea Urais anakutana na vikwazo au mikwara mingi kutoka kwa baadhi ya viongozi na wanachama wa CDM. Na baadhi ya vyombo vya habari vilipata kumnukuu Mzee Mtei akimshauri Mhe. Zitto kuachana na masuala ya kutangaza nia ya kuombea urais kwamba ni kusababisha fujo au vurugu ndani ya CDM na kwamba atulie hadi wakati ukifika.

Tujiulize mimi na wewe, inakuaje Zitto akitangaza nia iwe kosa lakini Mbowe akitangaza nia iwe ni sawa wakati kwa mujibu wa katiba ya CDM kuna mamlaka inayotakiwa kumtangaza mgombea urais ni nani lakini pia sidhani kama kuna mahala katiba ya CDM inakataza Mwanachama wake kutangaza nia ya kugombea nafasi fulani kama vile urais.

Kama kuna kipengele hicho CDM wanapaswa kukionesha ili kuondoa mashaka yaliyopo juu ya kwamba wanamuonea Mhe. Zitto. Hata hivyo wapo wanachama wengi wametangaza nia kugombea Ubunge ndani ya CDM mwaka 2015 kama ilivyokuwa kwetu sisi kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010; tulitangaza nia sana tu; wote akina Wenje, akina HAINESS KIWIA na wengine na hawakuelezwa kwamba wanaleta fujo ndani ya CDM.

Ndugu zangu ndiyo maana ninakuwa na mashaka wakati mwingine kwa kusema kwamba huenda kweli Mhe. Zitto akawa anaonewa kama anavyosema, mtazamo huu unatokana na records hizo za nyuma. CDM wajitokeze kufafanua hoja hizo ili nasi makomredi wao kimkakakti tuweze ku clear dout. Inawezekana baadhi wakaja na maneno maneno yaliyozoeleka kwamba nimetumwa na Zitto nk.
La hasha ni utashi wangu tu kutokana na uzoefu wangu katika siasa za CDM na sasa niko NCCR-Mageuzi. Uzoefu wangu usibezwe kwa kuwa ninayo
Email This
BlogThis!
Share to Twitter
Share to Facebook
at 1/05/2014 03:10:00 AM
 
We kweli muathirika hivi unafikiri mbowe ni sawa na papuchi mwenzio zito? Nani anamda wa kujitu hekaya kama hizi?yaani zitto anatabia kama za watoto ukimuudhi anaaza kudai alicho kupa, huo ni utoto na umama wa huyo mwenzenu,,na ccm mlivo majinga ya kufikiri utakuta mnaona kama hii bonge ya hoja!wakati wenzenu wanajua ni mafa maji tu huyo anatapatapa

acha jazba kamanda jibu hoja - ishu ni kwamba ni kweli mbowe alipokea hiyo 'mizigo' au hakupokea?!
kwa hiyo kwa mbowe ni hekaya ila kwa zito........................
ama kweli mkuki ni kwa nguruwe tu, ila kwa binadamu mchungu!
 
Naona wengine mmeishiwa nguvu kabisa mmebakia kulia na kusaga meno tuh,

ZUBERI KABWE KIBOKO YAO,A.K.A GOGO LA UDII,,MZEE WA LEKATUTIGITEE,,,

WASALIMIEN TENGERU KWA LILE ZEE LENYE MAKENGEZA

kuna watz mandondocha kweli , hivi mtu na akili yako unapost huu uharo.Pengine huna hata nyumba,huna kitanda ,unalala kitanda kimoja na wadogo zako! ukipewa 1,000,000 unasema ni 10,000,000.Kuna watu wanakera sana fanyeni kazi acha kushabikia ujinga.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom