Zanzibar: Yaliyojiri kwenye ziara ya Rais Magufuli kisiwani Pemba - Sept 2016: Ampongeza Jecha kusimamia uchaguzi vizuri

Mondoros

JF-Expert Member
Aug 29, 2015
629
472


IMG-20160902-WA0058.jpg
IMG-20160902-WA0057.jpg

Anaeongea kwa sasa ni Rais John Magufuli baada ya kukaribishwa na Rais wa Zanzibar, Dk. Shein na anazungumzia amani. Anasema mtu hawezi kuja kuwekeza Pemba wakati watu hawasalimiani, anasema mume na mke wakiwa hawaelewani kwa sababu ya vyama vya siasa hajui usiku wanalalaje. Amesema anajua vijana wengi hawana ajira Pemba, watapata ajira endapo wawekezaji watakuja kujenga sehemu ambayo ina amani.

Magufuli: Uchaguzi umeshakwisha na utakuja tena 2020, huo ndio ukweli na msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Uchaguzi umekwisha mimi nikachaguliwa kuwa Rais na naitwa John Pome Magufuli na nimefunga Makufuli yote na funguo nimeshatupa.

Nataka niseme Mhe Dk Shein, wewe ndie Rais na inawezekana umekuwa mpole kidogo, huo upole weka pembeni, unasapoti yangu yote, atakaekuchezea chezea niambie hata kwa kuninong'oneza.

Tushirikiane kwa nguvu zote, wanaojaribu kuchezea amani yetu, mimi niliwahi kwenda Libya, mojawapo ya nchi za Afrika zilizokuwa na raha ni mojawapo. Pakajitokeza watu wachache kwa kuahidiwa ahadi za uongo, Libya leo siyo mahali panapokalika, watu wanamwaga damu kila siku, watu walichezea amani, hata amani inalevya.

Rwanda wakati wa genocide walikufa watu wanaokaribia milioni moja, mmenichagua kuwa Rais wenu, nna wajibu wa kuwaeleza ukweli, wanaofanya chokochoko tunawajua wengine, wafatilieni wote wanaochomachoma washughulikiwe wote bila huruma. Mna bahati mna Rais mpole sana na hata sura yake nzuri tu na ni Rais alietoka Pemba, ni kitu gani kinatusumbua.

Mimi nilifanya nae kazi nikiwa naibu waziri na waziri, ninamfajhamu Dk Shein, mpeni ushirikiano. Kuna mtu alijifungia kwenye chumba alafu akasema ametoka Ulaya, msikubali kudanganywa, hivi karibuni alinunua Meli na zinafanya kazi, kuna maeneo mengi yamepelekwa maji na umeme, watu hamtaki kuyaona haya. Palikuwa na Prof Mbarawa hapa mkamkataa jimbo la mkoani(Mkanyageni) mkamkanyagia hukohuko, mimi nnafahamu umuhimu wake na nikachukua wizara tatu nikaziunganisha zote nikampa mtu aliekanyagwa huku.

Mpeni ushirikiano Dk Shein, imebaki miaka minne tu na kitu na kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar hiki ndio kipindi chake cha mwisho. Nawaomba wananchi tujenge umoja wetu. Tukienda kwa umoja wetu tutafanikiwa, tunataka tuimarishe uvuvi, mazao na serikali iliongeza hela kununua karafuu japo pato lake limeanza kushuka, tunataka tujenge hii nchi. Katika kipindi kifupi Pemba itakuwa kama Ulaya na wanaoharibu Pemba ni watu wachache sana.

Wengine wanasema uchaguzi utarudiwa, kwa kawaida ndoto huwa ni usiku lakini hizo ni ndoto za usiku, lakini ukimkuta mtu anaota mchana, huyo anatafuta ukichaa. Nampongeza sana nh Jecha kwa kusimamia uchaguzi na umeenda vizruri sana na kama kuna tuzo mheshimiwa Shein utatoa, Jecha umpe hizo tuzo. Napongeza sana vyombo vya ulinzi, mmefanya kazi nzuri sana, mmesimamia amani ya Tanzania kwa uzalendo mkubwa sana.

=====

Rais John Magufuli atua Pemba muda mfupi uliopita akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli baada ya mapokezi yaliyombatana na kikundi cha ngoma, ameenda kuzulu kaburi la aliyekuwa Makamu wa Rais, Dk Omary Ali Juma. Baadaye saa tisa alasiri atafanya mkutano wa hadhara katika uwanja wa Gombani ya Kale, Pemba.

==========

Habari zaidi...

Septemba 2, 2016, Rais John Magufuli amefanya ziara ya kikazi ya siku mbili visiwani Zanzibar, baada ya kukaribishwa na Rais wa Zanzibar, Dk. Shein na akazungumzia amani. Amesema mtu hawezi kuja kuwekeza Pemba wakati watu hawasalimiani, anasema mume na mke wakiwa hawaelewani kwa sababu ya vyama vya siasa hajui usiku wanalalaje. Amesema anajua vijana wengi hawana ajira Pemba, watapata ajira endapo wawekezaji watakuja kujenga sehemu ambayo ina amani.

Magufuli: Uchaguzi umeshakwisha na utakuja tena 2020, huo ndio ukweli na msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Uchaguzi umekwisha mimi nikachaguliwa kuwa Rais na naitwa John Pome Magufuli na nimefunga Makufuli yote na funguo nimeshatupa.

Nataka niseme Mhe Dk Shein, wewe ndie Rais na inawezekana umekuwa mpole kidogo, huo upole weka pembeni, unasapoti yangu yote, atakaekuchezea chezea niambie hata kwa kuninong’oneza.

Tushirikiane kwa nguvu zote, wanaojaribu kuchezea amani yetu, mimi niliwahi kwenda Libya, mojawapo ya nchi za Afrika zilizokuwa na raha ni mojawapo. Pakajitokeza watu wachache kwa kuahidiwa ahadi za uongo, Libya leo siyo mahali panapokalika, watu wanamwaga damu kila siku, watu walichezea amani, hata amani inalevya.

Rwanda wakati wa genocide walikufa watu wanaokaribia milioni moja, mmenichagua kuwa Rais wenu, nna wajibu wa kuwaeleza ukweli, wanaofanya chokochoko tunawajua wengine, wafatilieni wote wanaochomachoma washughulikiwe wote bila huruma. Mna bahati mna Rais mpole sana na hata sura yake nzuri tu na ni Rais alietoka Pemba, ni kitu gani kinatusumbua.

Mimi nilifanya nae kazi nikiwa naibu waziri na waziri, ninamfajhamu Dk Shein, mpeni ushirikiano. Kuna mtu alijifungia kwenye chumba alafu akasema ametoka Ulaya, msikubali kudanganywa, hivi karibuni alinunua Meli na zinafanya kazi, kuna maeneo mengi yamepelekwa maji na umeme, watu hamtaki kuyaona haya. Palikuwa na Prof Mbarawa hapa mkamkataa jimbo la mkoani (Mkanyageni) mkamkanyagia hukohuko, mimi nnafahamu umuhimu wake na nikachukua wizara tatu nikaziunganisha zote nikampa mtu aliekanyagwa huku.

Mpeni ushirikiano Dk Shein, imebaki miaka minne tu na kitu na kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar hiki ndio kipindi chake cha mwisho. Nawaomba wananchi tujenge umoja wetu. Tukienda kwa umoja wetu tutafanikiwa, tunataka tuimarishe uvuvi, mazao na serikali iliongeza hela kununua karafuu japo pato lake limeanza kushuka, tunataka tujenge hii nchi. Katika kipindi kifupi Pemba itakuwa kama Ulaya na wanaoharibu Pemba ni watu wachache sana.

Wengine wanasema uchaguzi utarudiwa, kwa kawaida ndoto huwa ni usiku lakini hizo ni ndoto za usiku, lakini ukimkuta mtu anaota mchana, huyo anatafuta ukichaa. Nampongeza sana Mh. Jecha kwa kusimamia uchaguzi na umeenda vizuri sana na kama kuna tuzo mheshimiwa Shein utatoa, Jecha umpe hizo tuzo. Napongeza sana vyombo vya ulinzi, mmefanya kazi nzuri sana, mmesimamia amani ya Tanzania kwa uzalendo mkubwa sana.

“Dokta Shein una support yangu yote, ukiona umemshindwa mtu, nambie mimi uone kama itapita hata dk 5”
“Wakati tukinadi kwenye kampeni mimi na Shein, tulisema tunataka Tanzania yenye viwanda”
“Hawezi mtu kuja kujenga kiwanda kama kuna vurugu, watu hawasalimiani, hamna amani.”

“Vijana wa Pemba hawana ajira kama walivyo vijana wa bara, kwa hiyo vijana lazima tuwe wa mbele kujenga amani.”
“Na mimi nataka nikwambie Dk. Shein, wewe ndiyo Rais, na naona umekuwa mpole sana,
“Upole uweke pembeni, uwe mkali kidogo, usikubali kuchezewa na mtu,

“Libya ilikuwa nchi ya amani, wakatumiwa watu wachache kwa ahadi za uongo, sasa Libya hakukaliki, watu wanakimbia…”
“Libya watu wanamwaga damu kila siku, kwa sababu watu walichezea amani.”

Mna bahati ndugu zangu, mna rais mpole sana , hata sura yake nzuri tu, Lakini pia ametoka Pemba, mnataka nini!? Mnataka malaika aje aongoze!?


Alisema rais Magufuli.

======

Habari kutoka Gazeti la Jambo leo

Jambo leo Liliandika:


RAIS John Magufuli ameonekana kuteswa na kusikitishwa na kitendo cha Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, kumnyima mkono Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein alipomsalimia wakati wa maziko ya Rais wa Awamu ya Pili Zanzibar, Aboud Jumbe Mwinyi.

Masikitiko hayo aliyatoa jana wakati akihutubia kwenye mkutano wa hadhara wa kushukuru wananchi wa Zanzibar kwa kumchagua kuwa Rais wa Tanzania, katika viwanja vya Demokrasia Unguja, ambako alitumia muda mrefu kufafanua kuhusu mkono huo kwa kauli tofauti tofauti.

Alisema Dk Shein kwa upendo na moyo wake wa huruma, aliamua kumpa mkono mtu fulani (Maalim Seif), lakini cha kushangaza alikataa kupokea mkono na kibaya zaidi ilikuwa msibani.

“Juzi wote tumeshuhudia msibani na Watanzania wameona kwenye picha, Dk Shein kwa unyenyekevu alimsalimu mtu fulani, lakini akakataa. Mkono huo huo ambao ameukataa, ndio Rais Shein anautumia kusaini fedha za safari na matibabu.

“Kweli una moyo wa upendo, natamani ningekuwa na hata robo maana mimi nisingeweza kutumia mkono wangu kumsainia mtu akatibiwe, wakati mkono huo huo aliukataa,” alisema Dk.Magufuli.

Dk Magufuli alisema pamoja na mambo mengine, bado anampongeza Rais Shein kwa upole, ukarimu na uungwana kwani licha ya kupata asilimia 92 ya kura zote, ameingiza wapinzani kwenye serikali yake.

‘Hataki’ wapinzani
Alisema yeye hawezi kumuingiza mpinzani kwenye Serikali yake kama alivyofanya Dk Shein na kufafanua kuwa ndani ya Serikali yake, hatakuwa tayari kumuingiza mpinzani afanye naye kazi.

“Rais Shein muombe Mungu akupe hata robo ya mawazo yangu. Natamani niwe na moyo wa aina yako lakini siwezi maana kama mimi ningekuwa nimekataliwa mkono, tena msibani, nisingesaini hata kidogo fedha kwa ajili ya huyo mtu.

“Jana (juzi) nikiwa Pemba nilikuomba uongeze ukali hata kidogo. Kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 uchaguzi umekwisha na hautarudiwa tena ila uchaguzi mwingine ni mwaka 2020. Kwa sasa ni muda wa kufanya kazi tu,” alisisitiza Dk. Magufuli.

Alisema anafahamu kuwa Zanzibar kuna tatizo la maji lakini tayari kuna fedha Sh bilioni 200 zimetengwa kwa ajili hiyo, ambapo alirudia kuwa hata kama kuna watu wanamnyima mikono, aendelee na jukumu la kuhakikisha wananchi wanapata maji.

Magufuli alisema lazima watu watambue walikotoka, walipo na wanakokwenda kwa kuwa sasa Zanzibar ni tofauti na ile ya zamani.

Alikumbusha alipokuwa Waziri wa Ujenzi, kwamba alisimamia upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Zanzibar na anakumbuka hiyo ilikuwa ni kwenye utawala wa Awamu ya Tatu chini ya mzee Benjamin Mkapa.

Alielezea kushangaa kuona mtu anatoka Zanzibar na kwenda kuwaambia wageni wasije Zanzibar, lakini cha kufurahisha wamempuuza na wageni wameendelea kuja maana kuna usemi unaosema kuwa mgeni njoo mwenyeji apone.

*Kufuga ndevu

Magufuli alisema katika maisha yake hakuwahi kufikiria kuwa Rais, maana alitambua kuwa vyeo vinaletwa na Mungu na kama Mungu amesema hapana ni hapana tu, hata kama unafuga ndevu namna gani kama Mungu amekataa huwezi kuwa Rais.

“Rais Shein ana moyo wa upendo kwa watu wote lazima aachwe afanye kazi yake maana Wazanzibari wameamua ndio awe Rais,” alisema na kuongeza kuwa wakati Rais Shein anafanya mambo yote kwa ajili ya Zanzibar, anatokea mtu anamnyima mkono mbele ya waombolezaji waliopo msibani.

Alifafanua kuwa hakuna kitabu chochote au dini yoyote duniani kinachofundisha chuki badala yake pale watu wanapokoseana, basi wasameheane.

“Lakini hata kwenye msiba uuuwiii,” alisisitiza Rais Magufuli na kuongeza anatamani kuona nchi inakuwa ya viwanda ili watu wengi wapate ajira kwani hakuna mtu anayekula chama cha siasa.

Aliomba wananchi wa Zanzibar wadumishe umoja na mshikamano na kuweka chuki pembeni, kwani ni jambo baya kuona kuna watu wanafanya kazi ya kufarakanisha watu.

“Mnamkuta mtu na dada yake mmoja CUF na mwingine CCM wewe unamfarakanisha. Unakuta mtu na mkewe mmoja CUF na mwingine CCM unawafarakanisha mpaka wanashindwa kulala chumba kimoja, huu ni sawa na ushetani,” alisema.

*Fyoko fyoko

Wakati huohuo Rais Magufuli ameonya kuwa katika utawala wake, amani ataipa kipaumbele na yeyote atakayeleta fyokofyoko itamrudia mwenyewe.

Alisema msimamo wake hautabadilika na anayetaka kuvuruga amani atamshughulikia kwani hatamuachia iwe mchana au usiku, iwe asubuhi au jioni na hata akiwa kitandani, atakayejaribu kuleta chokochoko lazima atamshughulikia.

Magufuli alisema amekwenda Zanzibar kwa dhamira ya kuwaeleza wazi kuwa katika urais wake, amani itakuwa kitu cha kwanza ndio maana aliwahi kusema Dar es Salaam atakayeleta fyoko fyoko, atakiona cha mtema kuni.

Alisisitiza kuwa msimamo wake wa pili ni kudumisha Muungano uliopo kati ya Tanzania Bara na Zanzibar kwa kuulinda kwa nguvu zake zote.

Kipaumbele chake cha tatu, alisema ni kuleta maendeleo ya wananchi wote bila kujali vyama vyao. “Iwe CCM, iwe CUF, iwe Chadema na hata wasio na vyama wote nitahakikisha naleta maendeleo yao,” alisema.

*Dk Shein

Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Rais Magufuli, Dk Shein alisema vyama vya upinzani vitaiona Serikali ya Zanzibar kama ilivyo, kwa kuwa kwa kutumia utaratibu wa kidemokrasia CCM hawang’ooki kwani kila uchaguzi watashinda na kuwagaragaza.

“Baada ya uchaguzi zikatoka kauli kwamba utarudiwa tena, masikini roho zao, nami huwa nawauliza utarudiwa kwa Katiba gani, na kwa sheria gani? Maana chini ya Tume ya Uchaguzi ya Mwenyekiti Salimu Jecha, uchaguzi umemalizika.

“Sheria na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ndio iliyotoa mamlaka kwa Tume ya Uchaguzi kuendesha uchaguzi wa rais, wabunge, madiwani na wawakilishi. Ni katiba ya Zanzibar hakuna katiba nyingine duniani inayoweza kuitisha uchaguzi tena, hizi ni hadithi ziacheni mitaani, ukweli tutakutana mwaka 2020 wakati wa Uchaguzi Mkuu,” alisema.

Alisema hakutakuwa na Serikali ya mpito Zanzibar na wanaosema hivyo wanajidanganya kwani hakuna sababu ya kuwa na serikali ya aina hiyo, kwa sababu Serikali imeshakuwa madarakani.

*Mafuta na gesi

Kuhusu mafuta na gesi Zanzibar, alisema limepatiwa ufumbuzi wa kudumu kwa kushirikiana na Rais mstaafu Jakaya Kikwete, ambapo walitunga Sheria ya Mafuta na Gesi na kwa sheria hiyo, Zanzibar ilipewa mamlaka ya kutunga sheria yake ya mafuta na gesi na imeshapelekwa kwenye Baraza la Wawakilishi na kikao kijacho cha Septemba 26, itasomwa tena.

“Baraza wakiipitisha wataileta kwangu, nitasaini na kuwa sheria na kuanza kutumika, baada ya hapo tutaanza kuita wawekezaji na Zanzibar itaanza kupiga hatua kwa kuwa tuna mambo mazuri ya mafuta na gesi,” alisema.

Alisema atashirikiana na Rais Magufuli kutekeleza sheria hiyo, pamoja na kuiwezesha Zanzibar kukuwa kiviwanda hasa vya samaki.

Aliongeza kuwa Zanzibar imeendelea kukusanya kodi ipasavyo, kwani hivi sasa mapato yameongezeka kwa kiasi kikubwa. Alitoa mfano wa 2011 walipokuwa wakikusanya Sh bilioni 13 kwa mwezi, wakati sasa wanakusanya Sh bilioni 52.

“Pesa hazitutoshi lakini tunazo, tumewalipa wastaafu takribani Sh bilioni 16, tunatoa mishahara kwa wakati na utalii umetuingizia fedha za kigeni kwa zaidi ya asilimia 80,” alisema.
 
Rais John Magufuli atua Pemba muda mfupi uliopita akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli baada ya mapokezi yaliyombatana na kikundi cha ngoma, ameenda kuzulu kaburi la aliyekuwa Makamu wa Rais, Dk Omary Ali Juma. Baadaye saa tisa alasiri atafanya mkutano wa hadhara katika uwanja wa Gombani ya Kale, Pemba. Picha na Ikulu

Usipoyaalika "makolokolo" ya huko Lumumba kuja kupanga foleni hapa,Uzi huu unaweza kupatwa na jua kiasi cha kuufanya usionekane na kusababisha ukose wachangiaji.Watu walishachoka kusikia hotuba zisizo na "uti wa mgongo" zinazofuatwa na masahihisho baada ya kutolewa majukwaani.
 
Big-up! Katumia usafiri wa national flag carrier, naona ATCL ikirudi katika nafasi yake.
Itakuwa 'kalazimika' kutumia hii ili kujibu hoja za Kitwanga... Si unajua zile Jet zinahitaji long runway ili ziweze kutua wakati hizi za mapanga boi zinahitaji kiwanja kifupi tuu...
 
Big-up! Katumia usafiri wa national flag carrier, naona ATCL ikirudi katika nafasi yake.

Naona anatumia Air Tanzania aka Pangaboy
Usikute ile ndege ya Jk ameshaipiga mnada. Maana jamaa kwa kubana matumizi namsifu

Nadhani kaitumia hiyo pangaboi kwasababu ndege ya rais (G550) haiwezi kutua pemba...uwanja mdogo. unless uwanja wa pemba umepanuliwa siku hizi basi atakua ameamua kuwapa ATC promo tu
 
Back
Top Bottom