Black Sniper
JF-Expert Member
- Dec 10, 2013
- 29,000
- 46,980
HaswaIlikua hii hapa. Yawezeka inabadrika kama kinyonga.View attachment 2384792
Bora umeileta na hii ndio ndinga langu siku zijazo
Sio mbali kustaafu kwangu
HaswaIlikua hii hapa. Yawezeka inabadrika kama kinyonga.View attachment 2384792
Hahahaha...sasa wewe watakudaka halafu watashikilia kiinua mgongo..chako...🤣🤣🤣Haswa
Bora umeileta na hii ndio ndinga langu siku zijazo
Sio mbali kustaafu kwangu
Ntakufaaa nifufuke tena kwa mshtukoHahahaha...sasa wewe watakudaka halafu watashikilia kiinua mgongo..chako...
Pension schemes za bongo hizi wanazokulioa 33% halafu 66% wanakupa kwa style ya pension? Ni bora ukatengeneza michongo mingine ya mipunga uvute hiko chuma maana hapo kwa haraka haraka si chini ya 600m utahitaji kuilaza halafu umepaki zako mtoto anakuja kuichuna rangi na kisoda...🤣🤣🤣Ntakufaaa nifufuke tena kwa mshtuko
Mkuu usiseme hivyo basi
Maana jana pension schemes karibu zi collapse ila tumeponea chuchupu
Hi Nchi ya hovyo sanaBongo kuna upumbavu sana.....ndio maana majitu ni masikini ya kutupwa...hivi kodi yote hiyo kweli duh!
Mkuu ya huko wala nisingeisubiri hata kama mfanyakazi wa serikaliPension schemes za bongo hizi wanazokulioa 33% halafu 66% wanakupa kwa style ya pension? Ni bora ukatengeneza michongo mingine ya mipunga uvute hiko chuma maana hapo kwa haraka haraka si chini ya 600m utahitaji kuilaza halafu umepaki zako mtoto anakuja kuichuna rangi na kisoda...
Kama ya mtoto wa bakhresa.Ilikua hii hapa. Yawezeka inabadrika kama kinyonga.View attachment 2384792
Hakutoa fedha bali aliwadhamini kwa mali kauli.Huyu mbunge Baba yake alikuwa ni mtu na nusu, Mzee Turky ndio alitowa pesa akiwa bungeni Dodoma Lisu akodiwe ndege kuwahishwa Nairobi, huyu mtoto Sasa figisu za Ccm wenzake hazijui hata hivyo alipe kodi, ameachiwa utajiri mkubwa sana zikiwemo boti za kisiasa za Dar Zanzibar.
Na hicho sasa cha kulipa gharama za ndege iliyombeba Lissu kwenda Nairobi, alandamwa mpaka umauti ukamfika.Huyu mbunge Baba yake alikuwa ni mtu na nusu, Mzee Turky ndio alitowa pesa akiwa bungeni Dodoma Lisu akodiwe ndege kuwahishwa Nairobi, huyu mtoto Sasa figisu za Ccm wenzake hazijui hata hivyo alipe kodi, ameachiwa utajiri mkubwa sana zikiwemo boti za kisiasa za Dar Zanzibar.
Sasa kiko wapi? Na ushetani wake wote wajuaji wamemtanguliza kuzimu na Sasa anatandikwa mijeledi tu na kutupwa motoni.Na hicho sasa cha kulipa gharama za ndege iliyombeba Lissu kwenda Nairobi, alandamwa mpaka umauti ukamfika.
Magufuli alikuwa ni SHETANI mwenye jicho Moja na pembe kichwani
Tshs 498,462,891 ndo ilete kodi 308,500,000? Mbona kama kuna kitu sikielewi hapa?Baada ya awali kuelezwa kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ipo mbioni kuuza mali za Mbunge Toufky Turky ambaye ni Mfanyabiashara aliyedaiwa kushindwa kulipa ushuru wa Gari aina ya Marcedes Benz G Wagon aliloliingiza Nchini Januari 2022, fafanuzi umetolewa.
Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya amenukuliwa na Clouds FM kuwa tayari deni hilo limekamilishwa kulipwa huku akitolea ufafanuzi kilichotokea.
Zanzibar waelezea
Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar, Juma Mwenda amesema “Kampuni yake (Mbunge Turky) ilikuwa inadaiwa hiyo kodi, alitegemea apate msamaha lakini hakuupata, msamaha alioomba upo chini ya mamlaka ya Waziri.
“Gari hilo (Marcedes Benz G Wago) lililetwa na kwa matumizi ya Kampuni na si matumizi ya Mbunge na ndiyo lilikuwa likiombewa msamaha, lingekuja kwa jina la Mbunge kuna taratibu zake za msamaha ambazo angezitumia kwa ajili ya msamaha.”
Kuhusu tofauti ya kodi ya Bara na Zanzibar, amesema Mwenda amesema “Tofauti ipo lakini huwa ni kwa magari yaliyotumika, hili linalohusika hapa ni jipya, lilikuja likiwa jipya, hivyo lilitaiwa kulipiwa ushuru sambamba na ule unaolipwa Tanzania Bara.
“Utaratibu ulivyo ni kuwa endapo kutakuwa na kodi inadaiwana na haijalipwa mali ya mhusika inaweza kukamatwa na kupigwa mnada.
Kuhusu mali za Mbunge kupigwa mnada
“Hivyo, mali za hiyo kampuni ya Mbunge hazikuwa zimepigwa mnada, lakini hiyo ni option ambayo ingefikiwa ikiwa kodi isingelipwa.”
Kuhusu madai kuwa gari hilo limetangazwa kupigwa mnada, amesema “Kama kuna mazingira ya mlipa kodi ameomba kulipa kidogo kidogo hayo yanaheshimiwa na anapewa nafasi hiyo.
“Wanaoamua kuhusu msamaha ni Waziri wa Fedha kwa kufuata ushauri wa taasisi inayosimamia uwekezaji, baada ya hapo mamlaka ya mapato inapewa maagizo ya utekelezaji.”
Waziri afafanua
Akizungumzia sakata hilo, Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya akasema “Utaratibu ambao umetumika kuleta hilo gari ni za uwekezaji wakati wa ujenzi, mfano linaweza kutumika kurahisha ujenzi.
“Wakati hilo gari limekuja mradi ulikuwa umeshakamilika, hivyo mwanzoni Sheria zikawa haziruhusu kwa kuwa muda ulikuwa umeshapita.
“Hapa Zanzibar ukiingiza gari kwa matumizi yako ya kawaida, utaratibu upo wa kulifanyia tathmini ili kuendana na mazingira ya Zanzibar, kama tunavyojua uchumi wa hapa ni tofauti, lengo ni kuwawezesha Wananchi kujikimu na kununua magari.
“Ndio maana (Mbunge) alipofanyiwa tathimini ikaja ile ambayo aliambiwa.”
Alipoulizwa suala la Mbunge Turky kulipa kodi kidogokidogo, kwanza alipongeza uwekezaji wa Turky katika kiwanda cha mifuko na akajibu kwa ujumbe wa maandishi kuwa tayari Mbunge huyo ameshakamilisha kulipa.
Thamani ya gari
Gari hilo lenye thamani ya Dola za Marekani 214,668.71 (Tsh. 498,462,891), liliingizwa kupitia bandari ya Malindi na kampuni ya uwakala wa mizigo ya Kimataifa HT Motors Group LTD (UK) kwa kushirikiana na kampuni ya uwakala wa mizigo ya ZARA Freight Forwaders ya Malindi, Zanzibar.
Chanzo: Clouds FM
Pia soma: TRA yaendelea kumkaba koo Toufiq Salum Turky kodi ya gari milioni 308.5
Ndio sababu magari mapya na mazuri yananunuliwa na serikali tu.Tshs 498,462,891 ndo ilete kodi 308,500,000? Mbona kama kuna kitu sikielewi hapa?
Hii nchi inanyonga sana uchumi wa raia wake. Jasho la mtu lakini serikali INAKWAPUA zaidi ya 40% ya jasho hilo.
Ndo maana CCM haitoki madarakani kwa sababu viongozi wake wanaficha siri kubwa ya unyonyaji wanaoufanya kupitia sheria walizozipitisha wao
Hiyo Kodi ni almost 62% 🙄Tshs 498,462,891 ndo ilete kodi 308,500,000? Mbona kama kuna kitu sikielewi hapa?
Hii nchi inanyonga sana uchumi wa raia wake. Jasho la mtu lakini serikali INAKWAPUA zaidi ya 40% ya jasho hilo
Na walitaka kukamata na kuuza mali zake.Hiyo Kodi ni almost 62% 🙄
Kodi TZ ni sawa na lile onyo la Mmakonde "uchiteme, uchimung'unye, wala uchimeche. Uchitema nchale, uchumungunya nchale, na uchimecha nchale". Ukileta mpya kodi juu. Ukileta nzee unalipa kodi za kawaida za thamani ya gari na unaongezewa kodi nyingine ya uchakavu. Hakwepi ntu hapo.Mkuu ya huko wala nisingeisubiri hata kama mfanyakazi wa serikali
Mimi niko nje na muanguko huo ni uk
Haha eti aichune na kisoda
Tena sio mtoto bali jitu zima kwa husda
Hilo ndinga la 2022 iliyotembea 1000km ni $800,000 ila mimi ntachukua la miaka 15 nyuma mzee
Sio mbaya na haikanyagi huko
Full of doubtsWaziri alionesha msimamo mzuri sana kwenye hili suala, hasa kwenye sababu alizotoa za kukataa msamaha wa kodi ulioombwa na huyo mbunge, nampongeza.
Naamini maelezo aliyotoa waziri ni sahihi na hapakuwepo na kimemo toka juu kumtaka afanye hivyo, hili taifa lazima liende na standard ya aina hii, tuache kujuana na kuishi kwa mazoea ya masikini pekee ndio wakulipa kodi
Tatizo hakuna ajira za kuingiza kipato na kodi serikaliniKodi TZ ni sawa na lile onyo la Mmakonde "uchiteme, uchimung'unye, wala uchimeche. Uchitema nchale, uchumungunya nchale, na uchimecha nchale". Ukileta mpya kodi juu. Ukileta nzee unalipa kodi za kawaida za thamani ya gari na unaongezewa kodi nyingine ya uchakavu. Hakwepi ntu hapo.