Zanzibar: Waziri wa Fedha aelezea sakata la Mbunge Toufky Turky, asema amekamilisha kulipa ushuru wa Marcedes Benz G Wagon, ampongeza

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
424
1,051
774ab020-fbf1-425a-bf3f-f36dc7eefe9d.jpg
Baada ya awali kuelezwa kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ipo mbioni kuuza mali za Mbunge Toufky Turky ambaye ni Mfanyabiashara aliyedaiwa kushindwa kulipa ushuru wa Gari aina ya Marcedes Benz G Wagon aliloliingiza Nchini Januari 2022, fafanuzi umetolewa.

Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya amenukuliwa na Clouds FM kuwa tayari deni hilo limekamilishwa kulipwa huku akitolea ufafanuzi kilichotokea.

Zanzibar waelezea
Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar, Juma Mwenda amesema “Kampuni yake (Mbunge Turky) ilikuwa inadaiwa hiyo kodi, alitegemea apate msamaha lakini hakuupata, msamaha alioomba upo chini ya mamlaka ya Waziri.

“Gari hilo (Marcedes Benz G Wago) lililetwa na kwa matumizi ya Kampuni na si matumizi ya Mbunge na ndiyo lilikuwa likiombewa msamaha, lingekuja kwa jina la Mbunge kuna taratibu zake za msamaha ambazo angezitumia kwa ajili ya msamaha.”

Kuhusu tofauti ya kodi ya Bara na Zanzibar, amesema Mwenda amesema “Tofauti ipo lakini huwa ni kwa magari yaliyotumika, hili linalohusika hapa ni jipya, lilikuja likiwa jipya, hivyo lilitaiwa kulipiwa ushuru sambamba na ule unaolipwa Tanzania Bara.

“Utaratibu ulivyo ni kuwa endapo kutakuwa na kodi inadaiwana na haijalipwa mali ya mhusika inaweza kukamatwa na kupigwa mnada.

Kuhusu mali za Mbunge kupigwa mnada
“Hivyo, mali za hiyo kampuni ya Mbunge hazikuwa zimepigwa mnada, lakini hiyo ni option ambayo ingefikiwa ikiwa kodi isingelipwa.”

Kuhusu madai kuwa gari hilo limetangazwa kupigwa mnada, amesema “Kama kuna mazingira ya mlipa kodi ameomba kulipa kidogo kidogo hayo yanaheshimiwa na anapewa nafasi hiyo.

“Wanaoamua kuhusu msamaha ni Waziri wa Fedha kwa kufuata ushauri wa taasisi inayosimamia uwekezaji, baada ya hapo mamlaka ya mapato inapewa maagizo ya utekelezaji.”

Waziri afafanua
Akizungumzia sakata hilo, Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya akasema “Utaratibu ambao umetumika kuleta hilo gari ni za uwekezaji wakati wa ujenzi, mfano linaweza kutumika kurahisha ujenzi.

“Wakati hilo gari limekuja mradi ulikuwa umeshakamilika, hivyo mwanzoni Sheria zikawa haziruhusu kwa kuwa muda ulikuwa umeshapita.

“Hapa Zanzibar ukiingiza gari kwa matumizi yako ya kawaida, utaratibu upo wa kulifanyia tathmini ili kuendana na mazingira ya Zanzibar, kama tunavyojua uchumi wa hapa ni tofauti, lengo ni kuwawezesha Wananchi kujikimu na kununua magari.

“Ndio maana (Mbunge) alipofanyiwa tathimini ikaja ile ambayo aliambiwa.”

Alipoulizwa suala la Mbunge Turky kulipa kodi kidogokidogo, kwanza alipongeza uwekezaji wa Turky katika kiwanda cha mifuko na akajibu kwa ujumbe wa maandishi kuwa tayari Mbunge huyo ameshakamilisha kulipa.

Thamani ya gari
Gari hilo lenye thamani ya Dola za Marekani 214,668.71 (Tsh. 498,462,891), liliingizwa kupitia bandari ya Malindi na kampuni ya uwakala wa mizigo ya Kimataifa HT Motors Group LTD (UK) kwa kushirikiana na kampuni ya uwakala wa mizigo ya ZARA Freight Forwaders ya Malindi, Zanzibar.

Chanzo: Clouds FM

Pia soma: TRA yaendelea kumkaba koo Toufiq Salum Turky kodi ya gari milioni 308.5
 
Huyu mbunge Baba yake alikuwa ni mtu na nusu, Mzee Turky ndio alitowa pesa akiwa bungeni Dodoma Lisu akodiwe ndege kuwahishwa Nairobi, huyu mtoto Sasa figisu za Ccm wenzake hazijui hata hivyo alipe kodi, ameachiwa utajiri mkubwa sana zikiwemo boti za kisiasa za Dar Zanzibar.
 
Baada ya awali kuelezwa kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ipo mbioni kuuza mali za Mbunge Toufky Turky ambaye ni Mfanyabiashara aliyedaiwa kushindwa kulipa ushuru wa Gari aina ya Marcedes Benz G Wagon aliloliingiza Nchini Januari 2022, fafanuzi umetolewa.

Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya amenukuliwa na Clouds FM kuwa tayari deni hilo limekamilishwa kulipwa huku akitolea ufafanuzi kilichotokea.

Zanzibar waelezea
Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar, Juma Mwenda amesema “Kampuni yake (Mbunge Turky) ilikuwa inadaiwa hiyo kodi, alitegemea apate msamaha lakini hakuupata, msamaha alioomba upo chini ya mamlaka ya Waziri.

“Gari hilo (Marcedes Benz G Wago) lililetwa na kwa matumizi ya Kampuni na si matumizi ya Mbunge na ndiyo lilikuwa likiombewa msamaha, lingekuja kwa jina la Mbunge kuna taratibu zake za msamaha ambazo angezitumia kwa ajili ya msamaha.”

Kuhusu tofauti ya kodi ya Bara na Zanzibar, amesema Mwenda amesema “Tofauti ipo lakini huwa ni kwa magari yaliyotumika, hili linalohusika hapa ni jipya, lilikuja likiwa jipya, hivyo lilitaiwa kulipiwa ushuru sambamba na ule unaolipwa Tanzania Bara.

“Utaratibu ulivyo ni kuwa endapo kutakuwa na kodi inadaiwana na haijalipwa mali ya mhusika inaweza kukamatwa na kupigwa mnada.

Kuhusu mali za Mbunge kupigwa mnada
“Hivyo, mali za hiyo kampuni ya Mbunge hazikuwa zimepigwa mnada, lakini hiyo ni option ambayo ingefikiwa ikiwa kodi isingelipwa.”

Kuhusu madai kuwa gari hilo limetangazwa kupigwa mnada, amesema “Kama kuna mazingira ya mlipa kodi ameomba kulipa kidogo kidogo hayo yanaheshimiwa na anapewa nafasi hiyo.

“Wanaoamua kuhusu msamaha ni Waziri wa Fedha kwa kufuata ushauri wa taasisi inayosimamia uwekezaji, baada ya hapo mamlaka ya mapato inapewa maagizo ya utekelezaji.”

Waziri afafanua
Akizungumzia sakata hilo, Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya akasema “Utaratibu ambao umetumika kuleta hilo gari ni za uwekezaji wakati wa ujenzi, mfano linaweza kutumika kurahisha ujenzi.

“Wakati hilo gari limekuja mradi ulikuwa umeshakamilika, hivyo mwanzoni Sheria zikawa haziruhusu kwa kuwa muda ulikuwa umeshapita.

“Hapa Zanzibar ukiingiza gari kwa matumizi yako ya kawaida, utaratibu upo wa kulifanyia tathmini ili kuendana na mazingira ya Zanzibar, kama tunavyojua uchumi wa hapa ni tofauti, lengo ni kuwawezesha Wananchi kujikimu na kununua magari.

“Ndio maana (Mbunge) alipofanyiwa tathimini ikaja ile ambayo aliambiwa.”

Alipoulizwa suala la Mbunge Turky kulipa kodi kidogokidogo, kwanza alipongeza uwekezaji wa Turky katika kiwanda cha mifuko na akajibu kwa ujumbe wa maandishi kuwa tayari Mbunge huyo ameshakamilisha kulipa.

Thamani ya gari
Gari hilo lenye thamani ya Dola za Marekani 214,668.71 (Tsh. Milioni 498,462,891), liliingizwa kupitia bandari ya Malindi na kampuni ya uwakala wa mizigo ya Kimataifa HT Motors Group LTD (UK) kwa kushirikiana na kampuni ya uwakala wa mizigo ya ZARA Freight Forwaders ya Malindi, Zanzibar.

Chanzo: Clouds FM

Pia soma: TRA yaendelea kumkaba koo Toufiq Salum Turky kodi ya gari milioni 308.5
Wizi mtupu,thamani ya gari mil.500, kodi mil.300,

Tengenezeni Basi hapa nchini muuze mpate faida Mara dufu
 
Baada ya awali kuelezwa kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ipo mbioni kuuza mali za Mbunge Toufky Turky ambaye ni Mfanyabiashara aliyedaiwa kushindwa kulipa ushuru wa Gari aina ya Marcedes Benz G Wagon aliloliingiza Nchini Januari 2022, fafanuzi umetolewa.

Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya amenukuliwa na Clouds FM kuwa tayari deni hilo limekamilishwa kulipwa huku akitolea ufafanuzi kilichotokea.

Zanzibar waelezea
Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar, Juma Mwenda amesema “Kampuni yake (Mbunge Turky) ilikuwa inadaiwa hiyo kodi, alitegemea apate msamaha lakini hakuupata, msamaha alioomba upo chini ya mamlaka ya Waziri.

“Gari hilo (Marcedes Benz G Wago) lililetwa na kwa matumizi ya Kampuni na si matumizi ya Mbunge na ndiyo lilikuwa likiombewa msamaha, lingekuja kwa jina la Mbunge kuna taratibu zake za msamaha ambazo angezitumia kwa ajili ya msamaha.”

Kuhusu tofauti ya kodi ya Bara na Zanzibar, amesema Mwenda amesema “Tofauti ipo lakini huwa ni kwa magari yaliyotumika, hili linalohusika hapa ni jipya, lilikuja likiwa jipya, hivyo lilitaiwa kulipiwa ushuru sambamba na ule unaolipwa Tanzania Bara.

“Utaratibu ulivyo ni kuwa endapo kutakuwa na kodi inadaiwana na haijalipwa mali ya mhusika inaweza kukamatwa na kupigwa mnada.

Kuhusu mali za Mbunge kupigwa mnada
“Hivyo, mali za hiyo kampuni ya Mbunge hazikuwa zimepigwa mnada, lakini hiyo ni option ambayo ingefikiwa ikiwa kodi isingelipwa.”

Kuhusu madai kuwa gari hilo limetangazwa kupigwa mnada, amesema “Kama kuna mazingira ya mlipa kodi ameomba kulipa kidogo kidogo hayo yanaheshimiwa na anapewa nafasi hiyo.

“Wanaoamua kuhusu msamaha ni Waziri wa Fedha kwa kufuata ushauri wa taasisi inayosimamia uwekezaji, baada ya hapo mamlaka ya mapato inapewa maagizo ya utekelezaji.”

Waziri afafanua
Akizungumzia sakata hilo, Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya akasema “Utaratibu ambao umetumika kuleta hilo gari ni za uwekezaji wakati wa ujenzi, mfano linaweza kutumika kurahisha ujenzi.

“Wakati hilo gari limekuja mradi ulikuwa umeshakamilika, hivyo mwanzoni Sheria zikawa haziruhusu kwa kuwa muda ulikuwa umeshapita.

“Hapa Zanzibar ukiingiza gari kwa matumizi yako ya kawaida, utaratibu upo wa kulifanyia tathmini ili kuendana na mazingira ya Zanzibar, kama tunavyojua uchumi wa hapa ni tofauti, lengo ni kuwawezesha Wananchi kujikimu na kununua magari.

“Ndio maana (Mbunge) alipofanyiwa tathimini ikaja ile ambayo aliambiwa.”

Alipoulizwa suala la Mbunge Turky kulipa kodi kidogokidogo, kwanza alipongeza uwekezaji wa Turky katika kiwanda cha mifuko na akajibu kwa ujumbe wa maandishi kuwa tayari Mbunge huyo ameshakamilisha kulipa.

Thamani ya gari
Gari hilo lenye thamani ya Dola za Marekani 214,668.71 (Tsh. Milioni 498,462,891), liliingizwa kupitia bandari ya Malindi na kampuni ya uwakala wa mizigo ya Kimataifa HT Motors Group LTD (UK) kwa kushirikiana na kampuni ya uwakala wa mizigo ya ZARA Freight Forwaders ya Malindi, Zanzibar.

Chanzo: Clouds FM

Pia soma: TRA yaendelea kumkaba koo Toufiq Salum Turky kodi ya gari milioni 308.5
nchi ngum hii
 
Waziri alionesha msimamo mzuri sana kwenye hili suala, hasa kwenye sababu alizotoa za kukataa msamaha wa kodi ulioombwa na huyo mbunge, nampongeza.

Naamini maelezo aliyotoa waziri ni sahihi na hapakuwepo na kimemo toka juu kumtaka afanye hivyo, hili taifa lazima liende na standard ya aina hii, tuache kujuana na kuishi kwa mazoea ya masikini pekee ndio wakulipa kodi
 
Huyu mbunge Baba yake alikuwa ni mtu na nusu, Mzee Turky ndio alitowa pesa akiwa bungeni Dodoma Lisu akodiwe ndege kuwahishwa Nairobi, huyu mtoto Sasa figisu za Ccm wenzake hazijui hata hivyo alipe kodi, ameachiwa utajiri mkubwa sana zikiwemo boti za kisiasa za Dar Zanzibar.
Mungu anaona kila kitu !! Iko siku wenye visasi wataanza kuhukumiwa hapa hapa Duniani kwanza. !! Karma!!
 
Back
Top Bottom