Zaidi ya Wafanyakazi 400 wa SGR - Dodoma wafanya mgomo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,988

Zaidi ya Wafanyakazi 400 wanaoshiriki katika ujenzi wa Mradi wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge Railway – SGR) Awamu ya 2 (Lot 2) kipande cha Morogoro - Makutupora chenye urefu wa Kilometa 422 wameshiriki mgomo kwa kile kinachodaiwa kutoafikiana na uongozi wa Mkandarasi Mkuu Yapi Merkezi kuhusu suala la malipo na muda wa kufanya kazi.

Taarifa kutoka Dodoma zinaeleza kuwa kwa siku kadhaa kumekuwa na mvutano kati ya uongozi wa Yapi na Wafanyakazi hao kuhusu malipo na muda wa kufanya kazi.

Inaelezwa kuwa Mkandarasi alitoa tangazo la kupunguza muda wa kufanya kazi, kutoka saa kumi na kuwa saa nane uamuzi ambao uliendana na kupunguza malipo ya Wafanyakazi hao.

Yapi kazi.jpg



e97b4ad0-2796-49ab-804c-437f99d08549 (1).jpeg

f5b27c6f-d4db-4375-ad73-c3e5cfb6115d.jpeg

75031aaa-eee0-490e-8704-60b7d97826b1.jpeg

Maamuzi hayo hayakukubaliwa na Wafanyakazi wengi ambao baadhi yao wanataka malipo yarejeshwe kama awali na wengine wanataka walipwe stahiki zao waondoke kazini kwa kuwa pia wanadai hawajaingiziwa malipo yao ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa miezi kadhaa.

Uongozi wa Yapi haujajitokeza kujibu madai hayo ya Wafanyakazi ambao kuanzia asubuhi ya leo Novemba 8, 2023 walifika katika ofisi za Yapi na kutaka kikao.

Pia soma

- (Video) Raia wa Uturuki wanaojenga Reli ya SGR waendeleza mgomo, wakidai mishahara, waomba msaada kwa Rais Samia

- Mkandarasi Yapı Merkezi anayejenga Reli ya SGR atoa ufafanuzi taarifa za kushindwa kuwalipa wafanyakazi wake raia wa Uturuki
 
Mwenndazake kamuacha mtu asiyejali wala kuweka nguvu katika utekelezaji
 
Huu mradi kwa asilimia kubwa umeshafeli kuendelea huko lot3&4 mambo ni hayo hayo, na tetesi ni kwamba waturuki hawana pesa za kuendesha huu mradi kwa sasa mpaka wapewe asilimia kadhaa tena na serikali.

Mradi unaenda kufa huu yapi wanao ndoa wafanyakazi wao wa kituruki kila wiki.
 
Zaidi ya Wafanyakazi 400 wanaoshiriki katika ujenzi wa Mradi wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge Railway – SGR) Awamu ya 2 (Lot 2) kipande cha Morogoro - Makutupora chenye urefu wa Kilometa 422 wameshiriki mgomo kwa kile kinachodaiwa kutoafikiana na uongozi wa Mkandarasi Mkuu Yapi Merkezi kuhusu suala la malipo na muda wa kufanya kazi.

Taarifa kutoka Dodoma zinaeleza kuwa kwa siku kadhaa kumekuwa na mvutano kati ya uongozi wa Yapi na Wafanyakazi hao kuhusu malipo na muda wa kufanya kazi.

Inaelezwa kuwa Mkandarasi alitoa tangazo la kupunguza muda wa kufanya kazi, kutoka saa kumi na kuwa saa nane uamuzi ambao uliendana na kupunguza malipo ya Wafanyakazi hao.

Maamuzi hayo hayakukubaliwa na Wafanyakazi wengi ambao baadhi yao wanataka malipo yarejeshwe kama awali na wengine wanataka walipwe stahiki zao waondoke kazini kwa kuwa pia wanadai hawajaingiziwa malipo yao ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa miezi kadhaa.

Uongozi wa Yapi haujajitokeza kujibu madai hayo ya Wafanyakazi ambao kuanzia asubuhi ya leo Novemba 8, 2023 walifika katika ofisi za Yapi na kutaka kikao.

Pia soma

- (Video) Raia wa Uturuki wanaojenga Reli ya SGR waendeleza mgomo, wakidai mishahara, waomba msaada kwa Rais Samia

- Mkandarasi Yapı Merkezi anayejenga Reli ya SGR atoa ufafanuzi taarifa za kushindwa kuwalipa wafanyakazi wake raia wa Uturuki
Akina Kadogosa wakamatwe,huyu mkandarasi hana uwezo wa kifedha na management

Kwa nini asipokonywe vipande vilivyosalia maana atatuchelewesha sana.
 
We HR was kibongo mwenye roho mbaya hapo makutupora ulininyima nafasi kisa sina20% ........bado nasoma novena tutaelewana tu
 
Mwenndazake kamuacha mtu asiyejali wala kuweka nguvu katika utekelezaji
Toa upumbavu huyo Mwendazake wako na Kadogosa ndio wa Kukamatwa Kwa kuleta mkandarasi njaa Ili wao wapige Cha Juu.

Mambo ya management ya mkandarasi Serikali inahusikaje?
 
Huu mradi kwa asilimia kubwa umeshafeli kuendelea huko lot3&4 mambo ni hayo hayo, na tetesi ni kwamba waturuki hawana pesa za kuendesha huu mradi kwa sasa mpaka wapewe asilimia kadhaa tena na serikali.

Mradi unaenda kufa huu yapi wanao ndoa wafanyakazi wao wa kituruki kila wiki.
Kadogosa Akamatwa harafu mkandarasi avunjiwe mkataba tuwape Wachina,huyu ana njaa hatomaliza hiyo kazi.
 
Wafanyakazi wa SGR DODOMA leo hii wamegoma kufanya kazi wakidai kufutiwa masaa 10 nakuwekewa masaa 8 ya kazi nijambo ambalo linawaumiza sana.

Kwakweli Hawa jamaa walifikia pabaya sasa kwamba kutoa masaa 10 mpaka masaa 8 nijambo limewafedhehesha snaa ndugu zetu wanaofanya kazi katika mradi wa SGR wakidai NSSF zao kuanzia January mpaka sasa hazijawekwa sio sawa aise ebu tusaidiane kutafakari hili jambo unafanya kazi mda mrefu kazi ngumu huoni mafao yakiingizwa kwenye account ni kitu kinachosha moyo.

Muafaka uliochukuliwa na viongoz wa mradi ifikapo tarehe 15 kuingiza pesa za Mafao (kiinua mgongo) kwenye account za wafanyakazi wa SGR DODOMA.

Je, Zitawekwa?

IMG20231108121855.jpg
 
Tutafute pesa kwa kweli, mfanyakazi analazimisha kufanya kazi masaa mengi daah
Inasikitisha. Sarakasi kibao kwenye mradi. Pesa inatafutwa hakuna kupumzika.

Nilisoma sehemu miaka hiyo kwamba, shirika la kazi duniani (ILO) lilipendekeza saa za binadamu kufanya kazi halafu apumzike ni saa nane, ambazo ndio hutekelezwa pia na serikali ya Tanzania.

Kwa upande wa wafanyakazi wa SGR wao wanataka saa kumi labda kwa sababu wakifanya kazi saa nyingi ndio angalau pesa zinaongezeka ili waendelee kuishi, tofauti na saa nane ambapo hela zinapungua.

Je, hizo kazi za kufanya kwa saa kumi zipo lakini huko kwenye mradi?
 
Back
Top Bottom