Zaidi ya madereva 300,000 wabadilisha leseni

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
Mpinga(25).jpg

Kamanda wa Kikosi cha usalama Barabarani nchini, Mohamed Mpinga


Madereva zaidi ya 357,552 wamebadilisha leseni zao za zamani na kupata mpya tangu zoezi hilo lilipoanza Oktoba mwaka 2010.
Akizungumza na NIPASHE ofisini kwake Jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Kamanda wa Kikosi cha usalama Barabarani nchini, Mohamed Mpinga, alisema zoezi hilo linaenda vizuri kwa kuwa waliobadilisha leseni ni nusu ya lengo.
"Hadi sasa madereva wapatao 357,552 wamebadilisha leseni zao na hili zoezi linaenda vizuri tangu lilipoanza oktoba 2010," alisema Mpinga.
Alisema zoezi hilo limeenda vizuri baada ya operesheni waliyoifanya januari mwaka huu kwa madereva wa mabasi yanayobeba abiria wengi wao wameitikia wito na kwenda kusoma ili waweze kupata leseni daraja C.
Alisema kwa kipindi cha wiki tatu zilizopita kulikuwepo na msongamano katika vituo vya kukatia kwa kuwa mtandao ulikuwa chini ikawalazimu kuagiza wataalamu kutoka Israel kutatua tatizo hilo na kwa sasa zoezi linaendelea kwa kasi.
Mpinga alitoa wito kwa madereva ambao hawajabadilisha leseni zao wafanye haraka kufanya hivyo hasa kwa wale wa daraja C kwa kuwa wasipofanya hivyo watakakosa sifa za udereva kuendesha magari ya abiria.



CHANZO: NIPASHE
 
Yaani muda woote huo tangu waanzishe huu utaratibu ni watu laki tatu na tu!
Jamani Bongo kweli waachie wabongo wenyewe hakuna kitu kinafanyika na kufanikiwa
 
Back
Top Bottom