Yupo wapi Prof. Ludigo?

MdengestanfromCuba

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
572
573
Jamani huyu mtu wasanii wakongwe kwenye game nasikia wanamtaja sana, mfano kina Joh Makini, RIP Ngwea. Kwa mwenye kujua huyu mtu alikua ni nani, anafanya nini, na kwa sasa yuko wapi naomba mnijuze wadau!
 
Profesa Ludigo ni miongoni mwa watayarishaji wazuri wa muziki wa Hip Hop na Bongo Fleva hapa nchini Tanzania, kazi nyingi nyingi za wasanii mwishoni mwa miaka ya 90 zilikua na mikono yake!

Aliganya kazi na P-Funk Majani ndani ya Bongo Record na Master Jay katika studio za Mj Records.

Asilimia 70 ya wasanii waliowika miaka ya 1990's mpaka miaka ya 2005 walifanya nae kazi, ndio maana wanamkumbuka sana, kwani kwa kiasi kikubwa alichangia mafanikio yao.
 
Baraka F.K,

Alipiga mikono mingi sana MJ na Bongo Records ila credits nyingi zilikuwa zinaenda kwa Master Jay na Majani coz ndo wamiliki wa Studio. Moja kati ya beat aliyoigonga nikaikubali ni HAO ya Joh Makini
 
Hapana Mkuu, hiyo ni nickname yake. Huyu jamaa ni mmoja kati ya "unsung heroes" wa bongo flava. Kuna ngoma nyingi zilizo-hit alitengeneza huyu jamaa lakini watu hawamjui, baadhi yake ni Mi Mmasai wa Mr Ebbo, Mikasi wa Ngwea, Akwelina wa OCG na Juma Nature na nyingine.

basi jamaa ni noma
 
Hapana Mkuu, hiyo ni nickname yake. Huyu jamaa ni mmoja kati ya "unsung heroes" wa bongo flava. Kuna ngoma nyingi zilizo-hit alitengeneza huyu jamaa lakini watu hawamjui, baadhi yake ni Mi Mmasai wa Mr Ebbo, Mikasi wa Ngwea, Akwelina wa OCG na Juma Nature na nyingine.

Kwa sasa yupo wapi?? Na anafanya nini maana kama katulia fulani hivi!!
 
Hapana Mkuu, hiyo ni nickname yake. Huyu jamaa ni mmoja kati ya "unsung heroes" wa bongo flava. Kuna ngoma nyingi zilizo-hit alitengeneza huyu jamaa lakini watu hawamjui, baadhi yake ni Mi Mmasai wa Mr Ebbo, Mikasi wa Ngwea, Akwelina wa OCG na Juma Nature na nyingine.

Daaah! Umenenaa hapo OCG mselaa alikua kichwa kizurii katika uandishii ila kwa sasa sijui yuko wapii tenaa!
 
Jamaa alikaa sana mtoni, then akarudi bongo miaka ya katikati ya 90. Album zote za mwanzo za Hardblasters na Prof Jay kuazina chemsha bongo mpaka mamsap jamaa ndio alikuwa nyuma ya scene. usela mwingi sana mwanangu huyu, na kilaji kingi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom