Yondo Kusala Denise (Yondo Sister) JamiiForums tunakupa heshima zako na tunauthamini mchango wako, hatuna tuzo, ila tuna uzi wako.

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,894
155,913
1690698964797.png


Yondo Kusala Denise (amezaliwa tar. 1 Januari 1958) ambaye anajulikana zaidi kwa jina la kisanii kama Yondo Sister, ni msanii wa Kikongo. Wengi humwita "Malkia wa Soukous", "Tina Turner" wa muziki wa dansi barani Afrika. Yondo Sister amepata kuwa mwimbaji mkuu katika bendi ya Soukous Stars kwa miaka kadhaa kabla ya kwenda kufanyakazi kama msanii wa kujitegemea. Uwezo wake wa kuimba iliibuliwa na Lutu Mabangu wakati huo Yondo akiwa kama mnenguaji wa Tabu Ley katika bendi yake ya Rocherettes. Yondo muziki uko katika damu, mzee wake alikuwa akipiga muziki kwa kujifurahisha tu, humo kukajengeka ujasiri wa kutoogopa hadhira. Na mara kadhaa alishiriki katika dansi, polepole na kuja kuwa mwanamuziki kamili na kutoa albamu ya kwanza mwaka 1991.

Yondo Sister amepata kutoa album 6 kwenye studio za Air B. Mas Production na Melodie, T.J.R. Music na zote zilikuwa moto mkali. Album hizo ni:-

FBI (2001)
Agenda (2002)
Dernière Minute(1995)
Deviation (1994)
Bazo (1991)
Planete (1990)
1690699002986.png

Yondo Sister bado yuko hai nchini kwao Congo DRC akiendelea na shughuli za muziki.

Mungu amjalie umri mrefu wenye afya njema, furaha, amani ya moyo, ma mafanikio ya kila aina na ya kila rangi.

Mshana Jr , Pascal Mayalla, Elli
 
View attachment 2702740

Yondo Kusala Denise (amezaliwa tar. 1 Januari 1958) ambaye anajulikana zaidi kwa jina la kisanii kama Yondo Sister, ni msanii wa Kikongo. Wengi humwita "Malkia wa Soukous", "Tina Turner" wa muziki wa dansi barani Afrika. Yondo Sister amepata kuwa mwimbaji mkuu katika bendi ya Soukous Stars kwa miaka kadhaa kabla ya kwenda kufanyakazi kama msanii wa kujitegemea. Uwezo wake wa kuimba iliibuliwa na Lutu Mabangu wakati huo Yondo akiwa kama mnenguaji wa Tabu Ley katika bendi yake ya Rocherettes. Yondo muziki uko katika damu, mzee wake alikuwa akipiga muziki kwa kujifurahisha tu, humo kukajengeka ujasiri wa kutoogopa hadhira. Na mara kadhaa alishiriki katika dansi, polepole na kuja kuwa mwanamuziki kamili na kutoa albamu ya kwanza mwaka 1991.

Yondo Sister amepata kutoa album 6 kwenye studio za Air B. Mas Production na Melodie, T.J.R. Music na zote zilikuwa moto mkali. Album hizo ni:-

FBI (2001)
Agenda (2002)
Dernière Minute(1995)
Deviation (1999)
Bazo (1991)
Planete (1999)
View attachment 2702741
Yondo Sister bado yuko hai nchini kwao Congo DRC akiendelea na shughuli za muziki.

Mungu amjalie umri mrefu wenye afya njema, furaha, amani ya moyo, ma mafanikio ya kila aina na ya kila rangi.

Mshana Jr , Pascal Mayalla, Elli
Asante sana Buji... Hawa ndio wanamuziki wa ujana wetu.. Huyu mwanadada alitusababishia sana ndoto nyevu na wimbo wake wa Mbuta mutu


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu mwanadada alitusababishia sana ndoto nyevu
Aiseee hatari sana enzi zile. Nakumbuka those days back, ninasoma Mbeya, nimekata tiketi ya kwenda Mwanza, basi la Subira la kanisa Katoliki Mbeya.

Lami enzi hizo inaishia Isanga, haifiki hata Kawetere. Barabara vumbi balaa, yaanibukiiangalia barabara unaiona iko very smooth, ukiingiza mguu ni vumbi tupu, hadi pajani ndipo uikute sakafu ya barabara.


Basi kuanzia Mbeya hadi Tabora tulipigiwa kanda moja tu, YONDO SISTER album Deviation.

Hakika ni miongoni mwa siku zangu bora kabisa za kukumbukwa. Ilikuwa September mwaka 1994.
 
Aiseee hatari sana enzi zile. Nakumbuka those days back, ninasoma Mbeya, nimekata tiketi ya kwenda Mwanza, basi la Subira la kanisa Katoliki Mbeya.

Lami enzi hizo inaishia Isanga, haifiki hata Kawetere. Barabara vumbi balaa, yaanibukiiangalia barabara unaiona iko very smooth, ukiingiza mguu ni vumbi tupu, hadi pajani ndipo uikute sakafu ya barabara.


Basi kuanzia Mbeya hadi Tabora tulipigiwa kanda moja tu, YONDO SISTER album Deviation.

Hakika ni miongoni mwa siku zangu bora kabisa za kukumbukwa. Ilikuwa September mwaka 1994.
Unajikuta umekariri nyimbo kulingana na mpangilio uliokuwepo kwenye kaseti
Yani ukitoka wimbo huu... unafwata huu

Hatari sana.

Sisi kijijini kwetu zilikuwa zikipigwa kwenye klabu za pombe... kanda inapigwa mfululizo inachoka mpaka inaanza kuongea kichina(fast forward) inafika wakati unakuwa huelewi hata kinachoimbwa
 
Welldone mkuu mtoa hoja,umenikumbusha mengi sana, baada ya kitabu cha pale Mkwawa CNE kuzingua, unaambaa na ilala, mwembe togwa mara ndani ya stendi kubwa ya mabus iringa, unajisogeza karibu na kwa Mbata music studio, unasikiliza hizi nyimbo hadi machozi yanakutoka, then back shaaban Robert west kuendelea na maisha, pale Radio one (sio uchafu wa sasa)kulikua na kipindi cha nani zaidi, mapambano mawili yaliifanya Dar isimame, Yondo sister vs Mbilia Bel na kubwa lao SIKINDE vs MSONDO (hili pressure ilikua kubwa kwa producer wa kipindi ,ikabidi lirudiwe!!),yeah nchi wakati ina heshima na adabu, police na tiss Wali EARN RESPECT, sio kulazimisha heshima
 
Unajikuta umekariri nyimbo kulingana na mpangilio uliokuwepo kwenye kaseti
Yani ukitoka wimbo huu... unafwata huu

Hatari sana.

Sisi kijijini kwetu zilikuwa zikipigwa kwenye klabu za pombe... kanda inapigwa mfululizo inachoka mpaka inaanza kuongea kichina(fast forward) inafika wakati unakuwa huelewi hata kinachoimbwa
Hahah hahha fast forward ilikuwa noma, radio Lasonic
 
Unajikuta umekariri nyimbo kulingana na mpangilio uliokuwepo kwenye kaseti
Yani ukitoka wimbo huu... unafwata huu

Hatari sana.

Sisi kijijini kwetu zilikuwa zikipigwa kwenye klabu za pombe... kanda inapigwa mfululizo inachoka mpaka inaanza kuongea kichina(fast forward) inafika wakati unakuwa huelewi hata kinachoimbwa
Hii ndio Lasonic yenyewe.
1690700970514.png
 
Asante sana Buji... Hawa ndio wanamuziki wa ujana wetu.. Huyu mwanadada alitusababishia sana ndoto nyevu na wimbo wake wa Mbuta mutu


Sent using Jamii Forums mobile app
Kipindi sisi tunachipukia chipukia tulikuwa tunawanyemelea baba zetu wadogo na mashangazi zetu wakiwadisko huyu nyimbo zake usipoweka disko halinogi kabisa
 
Lasonic wanijumbusha mbali sana, siku ukiona mzee amerudi na battery zile za size "A" kama nane hivi unajua kabisa siku hiyo ni mziki tu, battery cheap zilikuwa BELL zile kanda tatu tu ziko chali, kiboko ilikuwa ni NATION ambazo sasahivi zinaitwa PANASONIC
 
Back
Top Bottom