Yanayoendelea ndani ya uongozi wa CCM na serikali yanatafakarisha

Steven Joel Ntamusano

JF-Expert Member
Jun 17, 2023
3,013
2,044
Kuna siasa za majibizano zinaendelea ndani ya uongozi wa juu kabisa wa CCM na serikali kuu. Mheshimiwa Nchimbi haonekani kufurahishwa na hulka za kikazi za RC wa Arusha na hakai na kitu moyoni mwake, anaweka wazi kabisa kutofurahishwa na kauli pamoja na tabia za Paul Makonda.

Wakati Makonda akifanya kazi nzuri mkoa wa Dar Mheshimiwa Nchimbi alikuwa nje ya nchi akifanya shughuli za ubalozi, Samia alikuwa msaidizi wa moja kwa moja hayati JPM hivyo anamfahamu vyema Makonda.

Naamini Samia anawavuta vijana wa hayati JPM karibu yake wakiwa na uwezo wa kujilipua na hawana aibu kabisa wakiwa kazini. Ni utamaduni mpya wa hayati ambao kwa serikali ya Samia ni wa kawaida kabisa.

Hata kutolewa kwake nafasi ya uenezi ni kwa shinikisho la wakubwa ndani ya CCM wakongwe hawaonekani kufurahishwa na hulka za vijana wa kisasa kina Makonda na wenzake wote wa rika lake na Nchimbi anawakilisha siasa za umri fulani wenye kuheshimu busara na hekima kabla ya kutoa hotuba na baada ya hapo.

Kitendo cha Rais Samia kufurahia namna Makonda alivyokipeleka mchakamchaka chama katika kipindi cha muda mfupi ni ushahidi wa uwepo wa sintofahamu ya chini kwa chini katika uongozi wa juu wa serikali na CCM.

Nchimbi akiwa katibu mkuu wa CCM anapopingana katika hotuba na bosi wake Samia juu ya hulka za kikazi za Makonda sio suala lenye afya nzuri ya kisiasa kwa maana ya muelekeo mzima wa serikali. Nchimbi hana la kufanya vinginevyo Makonda angeondolewa kabisa kutoka kwenye serikali na kurudi mtaani.

Na mpaka muda huu Mzee Kikwete bado ana nguvu ndani ya serikali na anaonekana ni mtu mwenye kupenda sana kuwa karibu na kila kinachoendelea, kule kuombwa kushauri na kutumwa kwenye mikutano mikubwa huko ughaibuni ni ushahidi wa kuhitajika kama mshauri wa masuala nyeti na yenye kuhitaji uzoefu.

Anatumia huko kuhitajika kwake kama tiketi ya kuingiza ushauri wake katika shughuli za kila siku, ni hapa tunapoona namna ambavyo Rais aliyepo madarakani anavyokwazwa na mstaafu anayekuwa nje ya ofisi. Sioni namna yoyote ambayo Nchimbi anakuwa na uhuru wa kufanya kazi pasipo maamuzi yake kutokuwa na chembechembe za hisia za Jakaya Kikwete.

Maamuzi ni yake kumhusu Makonda, Sabaya na Biteko ambao ni masalia halisi ya Bosi wake wa zamani hayati JPM, aendelee kuwa karibu nao kikazi akiwa anaujua uwezo wao au aachane nao kwani Mstaafu Kikwete na kund lake kubwa hawapendi hulka zao za kikazi.

Kinachofikirisha ni ukweli kwamba Kikwete akiwa Rais hakuingiliwa kwa namna yoyote ile na Hayati Mkapa, haonekani kuondoka kabisa kwenye duru za kisiasa akihitajika kwa uzoefu wa ushauri wake na wakati huo huo akiwa na hulka ya kupenda kuhusika kwenye mengi zaidi ya ustaafu wake.
 
Kwani Rais angewaweka pembeni hao Vijana wa Mwendazake Kuna shida gani?

Kiufupi Kuna Kambi 2 hapa ya Walinda Ligacy(Sukima Gang) na wale wanaotaka Kufuata baada ya Samia (Msoga Gang).

Kwa Samia hana Kambi labda watu binafsi wanaomkubali kama kina Jokate and the likes.

So Kwa Mama nadhani Yuko sawa Wacha waparuane madam hakuna Kambi inatoshia nafasi yake 2025.

Walijaribh ila Wameshindwa so wanajipanga Kwa 2030.
 
Kwani Rais angewaweka pembeni hao Vijana wa Mwendazake Kuna shida gani?

Kiufupi Kuna Kambi 2 hapa ya Walinda Ligacy(Sukima Gang) na wale wanaotaka Kufuata baada ya Samia (Msoga Gang).

Kwa Samia hana Kambi labda watu binafsi wanaomkubali kama kina Jokate and the likes.

So Kwa Mama nadhani Yuko sawa Wacha waparuane madam hakuna Kambi inatoshia nafasi yake 2025.

Walijaribh ila Wameshindwa so wanajipanga Kwa 2030.
Simuoni JK akiwa amepunguza mahaba yake kwa kina Makamba zaidi zaidi namuona akiwa huru ndani ya Chama.

Wastaafu waliomtangulia wameshaaga dunia hivyo yeye ndiye mkongwe wa CCM tofauti na siku za nyuma walipokuwepo kina RIP Mkapa, Mwinyi wakongwe waliomtangulia na kuwa na uwezo wa kumkosoa hadharani muda wowote.

Samia anapowavuta hao kina Sabaya, Biteko na Makonda anatengeneza kambi yake mwenyewe kwa ajili ya 2025, hivyo unapoona Nchimbi anamkosoa hadharani Makonda anakuwa akifikisha ujumbe kwa Samia kwamba mambo sio rahisi kihivyo kama anavyodhania.

Lakini Mungu anaipenda sana Tanzania, hii ni nchi iliyowekwa chini ya usimamizi wa nguvu za Mungu siku ya tarehe 8 Desemba 1961 kina Makamba na wengine wenye sifa za upigaji wasahau kabisa kuja kuwa warithi wa Samia atakapostaafu.
 
Kwani Rais angewaweka pembeni hao Vijana wa Mwendazake Kuna shida gani?

Kiufupi Kuna Kambi 2 hapa ya Walinda Ligacy(Sukima Gang) na wale wanaotaka Kufuata baada ya Samia (Msoga Gang).

Kwa Samia hana Kambi labda watu binafsi wanaomkubali kama kina Jokate and the likes.

So Kwa Mama nadhani Yuko sawa Wacha waparuane madam hakuna Kambi inatoshia nafasi yake 2025.

Walijaribh ila Wameshindwa so wanajipanga Kwa 2030.
CCM inamwamini Mwenyekiti, Mwenyekiti anamwamini Makonda na Makonda anakiamini CCM

Asiyekubaliana ahamie Chadema 🐼
 
Simuoni JK akiwa amepunguza mahaba yake kwa kina Makamba zaidi zaidi namuona akiwa huru ndani ya Chama.

Wastaafu waliomtangulia wameshaaga dunia hivyo yeye ndiye mkongwe wa CCM tofauti na siku za nyuma walipokuwepo kina RIP Mkapa, Mwinyi wakongwe waliomtangulia na kuwa na uwezo wa kumkosoa hadharani muda wowote.

Samia anapowavuta hao kina Sabaya, Biteko na Makonda anatengeneza kambi yake mwenyewe kwa ajili ya 2025, hivyo unapoona Nchimbi anamkosoa hadharani Makonda anakuwa akifikisha ujumbe kwa Samia kwamba mambo sio rahisi kihivyo kama anavyodhania.

Lakini Mungu anaipenda sana Tanzania, hii ni nchi iliyowekwa chini ya usimamizi wa nguvu za Mungu siku ya tarehe 8 Desemba 1961 kina Makamba na wengine wenye sifa za upigaji wasahau kabisa kuja kuwa warithi wa Samia atakapostaafu.
Samia hahitaji Kambi 2025 Kwa sababu hakuna mgombea mwingine wa kushindana nae 2025 sana sana ni hizo Kambi kumsumbua Ili awaweke Serikalini watu wao Waendelee kujipanga kuelekea 2030.

Minyukano itakuwa mikubwa baada ya 2025 Kwa sababu Kila Kambi itajitutumua na ndio hapo vyombo Huwa vinaamua wa kumuweka na Rais anasimamia Hilo.
 
CCM inamwamini Mwenyekiti, Mwenyekiti anamwamini Makonda na Makonda anakiamini CCM

Asiyekubaliana ahamie Chadema 🐼
Makonda ni WA kutumika ni chawa kama chawa wengine,anaweza ahidiwa Uongozi ila baada ya 2025 habari yake inaweza Isiwe na umuhimu japo itategemeana na Nguvu za Kambi na upepe wa Kisiasa.

Mwisho Huwa sipendi kujadili mambo ya Kisiasa ila masuala ya Uchumi so endeleeni na mijadala yenu.
 
Makonda ni WA kutumika ni chawa kama chawa wengine,anaweza ahidiwa Uongozi ila baada ya 2025 habari yake inaweza Isiwe na umuhimu japo itategemeana na Nguvu za Kambi na upepe wa Kisiasa.

Mwisho Huwa sipendi kujadili mambo ya Kisiasa ila masuala ya Uchumi so endeleeni na mijadala yenu.
Makonda yuko tangia Bungeni BMK na ataendelea kuwepo Sana tu 🐼
 
Kuna siasa za majibizano zinaendelea ndani ya uongozi wa juu kabisa wa CCM na serikali kuu. Mheshimiwa Nchimbi haonekani kufurahishwa na hulka za kikazi za RC wa Arusha na hakai na kitu moyoni mwake, anaweka wazi kabisa kutofurahishwa na kauli pamoja na tabia za Paul Makonda.

Wakati Makonda akifanya kazi nzuri mkoa wa Dar Mheshimiwa Nchimbi alikuwa nje ya nchi akifanya shughuli za ubalozi, Samia alikuwa msaidizi wa moja kwa moja hayati JPM hivyo anamfahamu vyema Makonda.

Naamini Samia anawavuta vijana wa hayati JPM karibu yake wakiwa na uwezo wa kujilipua na hawana aibu kabisa wakiwa kazini. Ni utamaduni mpya wa hayati ambao kwa serikali ya Samia ni wa kawaida kabisa.

Hata kutolewa kwake nafasi ya uenezi ni kwa shinikisho la wakubwa ndani ya CCM wakongwe hawaonekani kufurahishwa na hulka za vijana wa kisasa kina Makonda na wenzake wote wa rika lake na Nchimbi anawakilisha siasa za umri fulani wenye kuheshimu busara na hekima kabla ya kutoa hotuba na baada ya hapo.

Kitendo cha Rais Samia kufurahia namna Makonda alivyokipeleka mchakamchaka chama katika kipindi cha muda mfupi ni ushahidi wa uwepo wa sintofahamu ya chini kwa chini katika uongozi wa juu wa serikali na CCM.

Nchimbi akiwa katibu mkuu wa CCM anapopingana katika hotuba na bosi wake Samia juu ya hulka za kikazi za Makonda sio suala lenye afya nzuri ya kisiasa kwa maana ya muelekeo mzima wa serikali. Nchimbi hana la kufanya vinginevyo Makonda angeondolewa kabisa kutoka kwenye serikali na kurudi mtaani.

Na mpaka muda huu Mzee Kikwete bado ana nguvu ndani ya serikali na anaonekana ni mtu mwenye kupenda sana kuwa karibu na kila kinachoendelea, kule kuombwa kushauri na kutumwa kwenye mikutano mikubwa huko ughaibuni ni ushahidi wa kuhitajika kama mshauri wa masuala nyeti na yenye kuhitaji uzoefu.

Anatumia huko kuhitajika kwake kama tiketi ya kuingiza ushauri wake katika shughuli za kila siku, ni hapa tunapoona namna ambavyo Rais aliyepo madarakani anavyokwazwa na mstaafu anayekuwa nje ya ofisi. Sioni namna yoyote ambayo Nchimbi anakuwa na uhuru wa kufanya kazi pasipo maamuzi yake kutokuwa na chembechembe za hisia za Jakaya Kikwete.

Maamuzi ni yake kumhusu Makonda, Sabaya na Biteko ambao ni masalia halisi ya Bosi wake wa zamani hayati JPM, aendelee kuwa karibu nao kikazi akiwa anaujua uwezo wao au aachane nao kwani Mstaafu Kikwete na kund lake kubwa hawapendi hulka zao za kikazi.

Kinachofikirisha ni ukweli kwamba Kikwete akiwa Rais hakuingiliwa kwa namna yoyote ile na Hayati Mkapa, haonekani kuondoka kabisa kwenye duru za kisiasa akihitajika kwa uzoefu wa ushauri wake na wakati huo huo akiwa na hulka ya kupenda kuhusika kwenye mengi zaidi ya ustaafu wake.
Dai katiba mpya acha kulia lia kijana
 
Back
Top Bottom