Tafakari yetu
JF-Expert Member
- Apr 19, 2021
- 1,502
- 4,408
Kuna wanaosema ajira hizi za sensa wapewe ambao ni watumishi ili kudhibiti uzembe utakaojitokeza na wengine wanadai wapewe ambao hawana ajira ili walau wapate mitaji.
Makundi yote ukiwasoma katikati ya mstari wana hoja zenye mashiko lakini kuna sehemu nakubaliana kutokukubaliana.
Kundi la kwanza ambao wanadai watumishi waangaliwe zaidi wamesahau Jambo moja. Ajira hizi za sensa hazina uhusiano kabisa na ajira nyingine mtu aliyonayo, kwamba muajiriwa wa TRA aliyeomba nafasi za sensa za NBS aadhibiwe na TRA kwa uzembe atakaofanyia NBS? Hapa inakosekana logic kabisa
Ninachojua kila ajira kuna utaratibu wake wa kinidhamu na hivyo ajira za sensa zina utaratibu wake uliowekwa na NBS na mtu anapoonyesha utovu wa nidhabu ni NBS wanatakiwa kumuwajibisha pekee kwa kosa la ajira ya sensa na si nyingineyo aliyonayo kutoka mamlaka nyingine.
Tukija kwa kundi la pili, hawa wanadai wasio na ajira wafikiriwe kwanza. Kwa kundi hili Nina haya machache, ajira zinapotolewa zinaangalia uwezo wa mtu, katika walioomba sensa na wasio na ajira kuna watu Wana Elimu ya kidato Cha nne tu lakini kuna mwenye ajira na kaomba sensa ana Elimu ya chuo kikuu. Hawa ni watu wawili tofauti, wa kidato Cha nne reasoning yake ipo chini kuliko wa chuo kikuu. Elimu inasaidia kufikirisha ubongo na kutoa maamuzi yenye busara. Madhara ya kutumia vijana wa form 4 ni mengi na ushahidi ninao wa kilichotokea kwenye zoezi la ANUANI ZA MAKAZI NA POSTIKODI kwenye Halmashauri fulani.
Maoni yangu
i) Kusiwepo na upendeleo wa aina yoyote ile kwenye kazi hii ya sensa, ama mtu ana vigezo vyote achukuliwe yeye bila kujali ni mtumishi au hana ajira. Upendeleo ndio hupelekea kupatikana wasio na sifa wakafanya vituko.
ii) Wote watakaofanikiwa kupata ajira wale viapo vya uaminifu na uadilifu kwa zoezi zima na viapo hivyo viwe vinaweza kumshtaki mtu na kumtia hatiani.
iii) Yawepo makubaliano maalumu kwamba muombaji alipwe baada ya kazi kukamilika na baada ya uhakiki wa kazi ya mtu. Kwa Sababu ni zoezi la kidigitali naamini uhakiki utakuwa wa haraka na yakibainika makosa yoyote akatwe sehemu fulani ya malipo yake. Hii itadhibiti kufanya kazi hovyo. Na pia naamini kunaweza kufanywa hujuma ili kulipa pungufu na hela kupigwa.
iv) Kwa sababu zoezi hili litakuwa na wasimamizi kigezo Cha kusema watumishi wa eneo husika wanayajua maeneo yao ndio wapewe sio sawa. Usimamizi na ufuatiliaji ukiwepo mzuri hata mtu akiletwa kutoka Burundi ahesabu watu wa manzese hatoshindwa. Kigezo Cha kujua eneo kwa kuishi eneo sio sawa kwa Sababu kuna wengi Sana wapo eneo hilohilo kwa miaka 15 lakini hajui mipaka ya mtaa wake.
Mwisho,
Kuna kikundi Cha watu kinataka kuhalalisha umuhimu wako kwa zoezi hili ili wengine wasipewe, kikundi hicho ni hatari Sana. Sifa na vigezo Kama mtu anavyo apewe.
Makundi yote ukiwasoma katikati ya mstari wana hoja zenye mashiko lakini kuna sehemu nakubaliana kutokukubaliana.
Kundi la kwanza ambao wanadai watumishi waangaliwe zaidi wamesahau Jambo moja. Ajira hizi za sensa hazina uhusiano kabisa na ajira nyingine mtu aliyonayo, kwamba muajiriwa wa TRA aliyeomba nafasi za sensa za NBS aadhibiwe na TRA kwa uzembe atakaofanyia NBS? Hapa inakosekana logic kabisa
Ninachojua kila ajira kuna utaratibu wake wa kinidhamu na hivyo ajira za sensa zina utaratibu wake uliowekwa na NBS na mtu anapoonyesha utovu wa nidhabu ni NBS wanatakiwa kumuwajibisha pekee kwa kosa la ajira ya sensa na si nyingineyo aliyonayo kutoka mamlaka nyingine.
Tukija kwa kundi la pili, hawa wanadai wasio na ajira wafikiriwe kwanza. Kwa kundi hili Nina haya machache, ajira zinapotolewa zinaangalia uwezo wa mtu, katika walioomba sensa na wasio na ajira kuna watu Wana Elimu ya kidato Cha nne tu lakini kuna mwenye ajira na kaomba sensa ana Elimu ya chuo kikuu. Hawa ni watu wawili tofauti, wa kidato Cha nne reasoning yake ipo chini kuliko wa chuo kikuu. Elimu inasaidia kufikirisha ubongo na kutoa maamuzi yenye busara. Madhara ya kutumia vijana wa form 4 ni mengi na ushahidi ninao wa kilichotokea kwenye zoezi la ANUANI ZA MAKAZI NA POSTIKODI kwenye Halmashauri fulani.
Maoni yangu
i) Kusiwepo na upendeleo wa aina yoyote ile kwenye kazi hii ya sensa, ama mtu ana vigezo vyote achukuliwe yeye bila kujali ni mtumishi au hana ajira. Upendeleo ndio hupelekea kupatikana wasio na sifa wakafanya vituko.
ii) Wote watakaofanikiwa kupata ajira wale viapo vya uaminifu na uadilifu kwa zoezi zima na viapo hivyo viwe vinaweza kumshtaki mtu na kumtia hatiani.
iii) Yawepo makubaliano maalumu kwamba muombaji alipwe baada ya kazi kukamilika na baada ya uhakiki wa kazi ya mtu. Kwa Sababu ni zoezi la kidigitali naamini uhakiki utakuwa wa haraka na yakibainika makosa yoyote akatwe sehemu fulani ya malipo yake. Hii itadhibiti kufanya kazi hovyo. Na pia naamini kunaweza kufanywa hujuma ili kulipa pungufu na hela kupigwa.
iv) Kwa sababu zoezi hili litakuwa na wasimamizi kigezo Cha kusema watumishi wa eneo husika wanayajua maeneo yao ndio wapewe sio sawa. Usimamizi na ufuatiliaji ukiwepo mzuri hata mtu akiletwa kutoka Burundi ahesabu watu wa manzese hatoshindwa. Kigezo Cha kujua eneo kwa kuishi eneo sio sawa kwa Sababu kuna wengi Sana wapo eneo hilohilo kwa miaka 15 lakini hajui mipaka ya mtaa wake.
Mwisho,
Kuna kikundi Cha watu kinataka kuhalalisha umuhimu wako kwa zoezi hili ili wengine wasipewe, kikundi hicho ni hatari Sana. Sifa na vigezo Kama mtu anavyo apewe.