Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,446
- 7,820
Salaam Wakuu,
Leo tarehe 19/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHEDEMA Freeman Mbowe inaendelea.
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
=======
Kufahamu ilipoishia, soma hapa:Yaliyojiri mahakamani kwenye Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake 3. Kesi imeahirishwa hadi 19/01/2022
Jaji ameingia, kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa.
Jaji: Shahidi Nakukumbusha Upo Chini ya Kiapo Bado na Wakili wa Mshtakiwa Namba Mbili Ilikuwa Unaendelea, Karibu
Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba nikumbushwe niliishia wapi
Jaji: Uliishia Wakati anakusomea Kielelezo H
Mallya: Shahidi tusomee hii ni Tarehe
Shahidi: Imeandikwa 05 August 2020
Mallya: Kuna Entry imeandikwa Owner of Article, Kwenye PF Je imeandikwa Jina gani?
Shahidi: Nashindwa Kusemea Sana Mheshimiwa Jaji sababu Siyo Mimi Niliyeandaa
Jaji: Hujaambiwa Uisemee Umeambiwa Usome
Shahidi: Imeandikwa Mohammed Abdallah Ling'wenya.. Lakini sijaandaa mimi
Mallya: Kwa Hiyo nani kaleta Mahakamani
Shahidi: Ni Mimi
Mallya: Kwa hiyo tuiondoe Mahakamani?
Shahidi: Hapana
MALLYA: Soma Sasa
Shahidi: Mwisho Imeandikwa DOYI
Mallya: Kutoka Tarehe 05 August 2020 Mpaka Tarehe Uliyo letewa Kwenye Ofisi yako Kuna Interval ya Siku Ngapi
Shahidi: Kuna Interval Ya Siku 08
Mallya: Na wewe Ulifanyia Kazi Tarehe Ngapi
Shahidi: Mwezi Wa July 2021
Mallya: Tarehe Ngapi
Shahidi: Sikumbuki Tarehe
Mallya: Kutoka Muda Umeletewa Mpaka Unafanya Uchunguzi Kuna Muda gani
Shahidi: Angalau Miezi 10
Mallya: aliyekuletea hiyo Item "H" alikwambia alikamata katika Physical Condition gani
Shahidi: Hakuniambia
Mallya: Alikwambia alikuwa Amehifadhi Siku gani
Shahidi: Hakuniambia
Mallya: alikwambia Kwamba aliondoa au Kutumbukiza Physically Kitu gani
Shahidi: Hakuna Kitu kama hicho Unachosema, kuwa alitoa chochote, Utaratibu Wa Kutunza Kielelezo Unajulikana, Kwa Utaratibu Wa Polisi Kielelezo Umapo Ki Seize unapaswa Umantain Kilivyo
Mallya: aliyekuletea alikwambia alifuata Utaratibu au Haku fuata Utaratibu huo
Shahidi: Ni Askari Polisi ni Imani yangu alifuata
Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba ajibu Swali Langu
Shahidi: Mheshimiwa Jaji swali linahitaji Maelezo,
Jaji: Nani sasa, Maelezo ya Wakili au Ya Kwako?
Shahidi: Mimi Naamini Kuwa Utaratibu ulifuatwa
Jaji: Swali lake Halipo Huko kama Utaratibu ulifuatwa au Lah Bali Je alikueleza
Shahidi: Mheshimiwa Jaji hakunieleza
Mallya: Ndiyo Jibu ndiyo Nilikuwa nayafuata
Mallya: Kwenye Kielelezo H Kuna Physical Damage inaonekana hapa, Kuna gaps, Je Macho yangu ya naona sawasawa
Shahidi: Condition Siwezi Kuzungumzia hapa
Mallya: Hilo Sijakuuliza, Nauliza Kuna Damage hapa Inaonekana, Je Kinachoonekana ni nini
Shahidi: Kinachoonekana ni Simu
Mallya: Siulizi simu hapa Mahakamani, usilete mahakamani michezo yako..
Mallya: Unachokiona ni Kitu gani
Shahidi: Ninachokiona ni Simu Mheshimiwa Jaji
Mallya: Ngoja Nichukue Simu F tulinganishe na H, Zote Umeleta Wewe, Swali langu hii yenye haya Ma gaps unahitaji?
Shahidi: Mhe Jaji Hizi ni simu Mbili tofauti, Siyo lazima zifanane..
Wakili wa Serikali: Mhe Jaji Wakili amebakia Muda Mrefu na Majibu yameshatolewa, Swali lake limeshajibiwa
Mallya: Mheshimiwa Jaji Swali langu halijajibiwa bado
Jaji: Muulize swali tena
Mallya: Kwenye Kielelezo H Kuna Ma' gaps, Je kitaalamu Unayaitaje?
Shahidi: Miye siwezi Kuongelea chochote
Mallya: Hii difference ya Kuwa hii ina button Kwenye simu na hii haina, unasemaje?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji siwezi Kuzungumzia kuhusu tofauti
Mallya: Kwenye Riport yako Kwenye Kielelezo F Je aina Positive Results..?
Shahidi: Ndiyo Ilikuwa na Positive Results
Mallya: Kuna Simu Ulizo letewa ukakuta Hazina Positive Results Kama Ulivyoletewa kwenye Terms of reference
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwa Mujibu wa Sheria Askari Polisi anaruhusiwa Kukamata simu.?
Shahidi: ndiyo Kwa Mujibu wa Sheria
Mallya: Kama Askari Polisi anataka Kujiridhisha Juu ya Kitu anachotafuta analeta Forensic?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Unafahamu Simu ni Personal Property ya Mtu?
Shahidi: Inaweza Kuwa Simu ya Ofisi
Mallya: Yapo Mazingira Mtu anaweza Kuwa na Simu Kama Mali yake Binafsi.?
Shahidi: Kama amenunua ni Mali yake Binafsi
Mallya: Je Yule ambaye amekamata kama Hajakuta Kitu anatakiwa kumrudishia Simu yake..?
Shahidi: Sifahamu
Mallya: Unafahamu Kwenye Simu ya Mtu Binafsi ambayo kanunua Kwa Pesa Yake, Inaweza Kuwa na Taarifa zake Binafsi?
Shahidi: Simu ya Mtu anaweza Kuweka Taarifa ambazo anahisi anaweza Kuhifadhi
Mallya: Kuna uwezekano Kuwa Mtu akahifadhi Taarifa au Nyaraka ya Utetezi kwenye Simu?
Shahidi: Sifahamu
Mallya: Taarifa Uliyompelekea huyo aliyekuomba Umfanyie Uchunguzi, Je akipokea Kwa Mkono au Kwa Email?
Shahidi akipokea Kwa Mkono
Mallya: Je alisoma hiyo Taarifa Yako ya Uchunguzi
Shahidi: Naamini alisoma
Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba 23 Samahani
Mallya: Shahidi Interest yangu Katika Riport Yako ni Ukurasa Wa Sita Unapozumgumzia Kuhusu Kielelezo A, B, C, D
Shahidi: Vielelezo Tajwa A, B, C, D hazina Taarifa Zenye Maudhui
Mallya: Kwenye Hicho Kielelezo namba C ulikuta ni Cha Nani
Shahidi: Ni Cha Khalfani Bwire
Mallya: Kwa hiyo Katika simu ya Khalfani Bwire hukukuta Jambo Lolote?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Ulifanya Uchunguzi Wako Lini
Shahidi: July 2021
Mallya: Ulikuja Kutoa Ushahidi wako lini
Shahidi: Juzi January 2022
Mallya: Kuna Interval ya Muda gani kati ya Wewe Kufanyia Uchunguzi Mpaka Kutoa Ushahidi
Shahidi: Usio Pungia Miezi Mitano
Mallya: Hiyo Content ambayo ulikuta negative Results upo wapi
Shahidi: Sikuona Haja ya Kuweka Kwa sababu sikukuta Kitu
Mallya: Bwana Bwire alikuwa anataka Negative Results ambayo Ingekuja Mahakamani Kuonyesha Kuwa Hakuna Maswala ya Ugaidi
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Nilipewa Terms of Reference, Kwa Hiyo Kama Haipo siwezi Kutoa
Mallya: Shahidi Umesha wahi Kupima Malaria
Shahidi: Hilo swali Limeingiaje hapa
Mallya: Kwa Sababu Wewe ni Mtu wa Laboratory na Malaria inapimwa Laboratory?
Shahidi: Sioni likihusiana
Mallya: Kwa Sababu Wewe ni Mtu wa Laboratory na Malaria inapimwa Laboratory
Shahidi: Sioni likihusiana
Mallya: Lina husiana Kwa Sababu Malaria Ukipimwa Wakikuta Negative Results wanakupa Majibu Yako
Shahidi: Kuna Baadhi ya Simu Zina Taarifa zaidi ya GB 20 huwezi Ku Print zote
Mallya: Je ulitoa taarifa Kwamba hukukuta kwa sababu ni Kubwa
Shahidi: Kwa sababu ni Out of Context
Mallya: Ulishajibu Kuwa Hukuona Haja
Shahidi: Siku Jibu hivyo
Jaji: Hapo Ndipo Mr. Malya Unapotuchanganya, Ni wapi Tutaona Huku uliza
Mallya: Nilikuwa namkumbusha Majibu Yake
Jaji: Basi Kama Unaulizwa Swali Hakuna Haja ya Kuongea Yote hayo
Mallya: Shahidi Nilisikia Unasema Mnatumia Legitimate Software Ku Updates yenu, Je Ulizungumzia Mnapewaje
Shahidi: Hapana Sikuzungumzia
Mallya: Mheshimiwa Jaji Naomba Barua ya Airtel na Ya Tigo
Mallya: Nakuonyesha Kielelezo P15 na Interest yangu ni Mtu aliyepewa hii Barua
Shahidi: Barua hii Imeelekezwa Kwa Kamishina wa Uchunguzi wa Kisayansi
Mallya: wewe sasa hivi ni Inspector Wa Polisi, Je Mwaka 2021 uliwahi Kuwa Kamishina wa Polisi
Shahidi: Mimi Sijawahi Kuwa Kamishina
Mallya: Kwenye hii Barua wapi Umekuwa Adressed.?
Shahidi: imekuwa Adressed Kwa Kamishina wa Uchunguzi Wa Kisayansi
Mallya: Naomba na ya Tigo
Mallya: Umesema Ofisini Kwenu Mkubwa wa Command ni Nani
Shahidi: Anaitwa CP SHABANI
Mallya: Kuna Departments Ngapi katika Forensic Beaural
Shahidi: Tuna Units Mbalimbali Ka Cyber crime ambayo Natoka Mimi, Toxicology, DNA, Pathology, Fingerprints, Ballistic, Documents, Crime scenes
Mallya: Kwa Mahesabu yangu ni Nane, Kwa Kiswahili zinaitwaje?
Shahidi: Kamisheni ya Uchunguzi Wa Kisayansi
Mallya: Zote hizi Ukubwa Wake Kwa Maana ya Commanding Ofisa wake ni CP SHABANI.?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Naomba uniseme Adress ambayo Tigo Wameitumia
Shahidi: UCHUNGUZI WA KISAYANSI
S. L. P 9094
DAR ES SALAAM
TANZANIA
Malya: naomba Mwenzangu Wakili Faraji Mangula aendelee
Mangula: Shahidi Pole na kuuguq Kichwa Siku ya Kwanza
Mangula: Ni sahihi ulisema Kuwa umesema Advanced Diploma ya Computer Science
Shahidi: Ndiyo
Mangula: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali, Ulielezea Kuwa Baada ya Masomo Ulipata Award gani
Shahidi: Nilisema nilikuwa napata Certificate
Mangula: Wakati Unafanya Uchunguzi Ulisema Ulikuwa una cheo Gani
Shahidi: Mkaguzi Msaidizi
Mangula: kwa sasa Una cheo Gani
Shahidi: Inspector
Mangula: Wakati Mawakili Wanakuongoza Hapa Mahakamani, Je ulisema Kuwa Ulipata Mafunzo gani Mpaka Ukapanda Cheo
Shahidi: Unakuwa Awarded siyo Kwa Kwenda Kozi
Mangula: Cheo chako umekipata wakati awamu ya 5 au ya 6?
Shahidi: Sijaelewa logic ya swali lako
Jaji: Swali la nani alikuwa Rais, unataka kujenga nini
Mangula: Mhe Jaji kuna premise nataka kutengeneza
Jaji: hiyo premises ndiyo utengeneze kupitia Rais aliye madarakani?
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Mahakama Ilisha wahi Kutoa Maelekezo Juu ya Kutaja Majina ya Watu ambao Hawapo Mahakamani
Jaji: nilitoa Maelezo Kuhusiana na Kutaja Majina ya Watu ambao Hawapo Mahakamani, lakini pia nataka Kujiuliza Kuhusu Kuuliza Maswali ya Rais wa Awamu ya Tano au Lah
Sasa Unachotaka hapo ni nini.?
Mangula: Ngoja Niulize Kwa Namna Nyingine
Mangula Naomba Kielelezo Namba 23,Shahidi Naomba Usome Kwa Sauti Kichwa Cha Habari cha Hicho Kielelezo
Shahidi Kamisheni ya Uchunguzi Wa Kisayansi, ya Makosa ya Kimtandao Chini ya Sheria ya Mtandao namba 14
Mangula: Je ni kifungu Kipi ambacho umekitumia?
Shahidi: Mimi siyo Mtaalamu wa sheria, Ila nilifanya kwa sheria ya mtandao
Mangula: Mwambie Mheshimiwa Jaji sasa ni kifungu kipi ulitumia
Shahidi: Mheshimiwa sikutumia kifungu
Mangula: Nikikupa hiyo sheria, unaweza Kunitajia kifungu ulichotumia
Shahidi: Mimi sina UFAHAMU WA MAMBO YA KISHERIA
Mangula: Kwa hiyo nyie Ofisini kwenye mnafanya bila ufahamu wa Sheria
Shahidi: Nishasema mheshimiwa SINA UFAHAMU WA SHERIA
Mangula: Fungua sasa Ndani, Ieleze Mahakama ni Kielelezo Kipi Ulichofanyia Kazi Ukagundua Kuna Makosa ya Ugaidi Uliyaona, Ni wapi Umeandika hivyo..
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Jibu linahitaji Maelezo, Mimi nililetewa tu Kufanya Uchunguzi.
Mangula: Kwa hiyo wewe hujui Kuwa Kuna Ugaidi au Hakuna Ugaidi kwenye hicho Kielelezo?
Shahidi: Sahihi
Mangula: bado unataka Mahakama ichukue Kielelezo Hiki Kama Kielelezo Cha Umuhimu?
Shahidi: Nimesema ni Kazi ya Mpelelezi
Mangula: Umesomeshwa na Serikali?
Shahidi: Ni Sahihi
Mangula: Na Umelipiwa Masomo Kwa Kodi ya Watanzania
Shahidi: Sahihi
Mangula: wewe Umesomea Udukuzi
Shahidi: Nimesomea Ethical Hacking
Mangula: Ulisema Mwanzo Kuwa Vifaa Vyako Vya Uchunguzi Vina Uadilifu
Shahidi: Ndiyo
Mangula: Na Kila Unachotaka Kwenye hiyo Simu, Mambo wako Unakuonyesha
Shahidi: Yes
Mangula: Kama Kuna video inakuomyesha.?
Shahidi: Inaonyesha Vile Vitu ambavyo Inaweza Ku Extract Kwenye Kielelezo
Mangula: Inakupa kila Kitu ambacho Kipo Kwenye simu?
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Mangula: Mheshimiwa Jaji Naomba Extraction Report
Mangula: Katika huo Mambo unaosema Ulikuwa upo Sawa Kukupa Kila Kitu, Ukisoma Kielelezo Cha Kwanza hicho namba 25
Mwambie Mheshimiwa Jaji kwenye hicho Kifaa Ulichofanyia Uchunguzi Kulikuwa na Content gani
Shahidi: Kukikuwa na Proxy Ya Chat ya WhatsApp
Mangula: Kulikuwa na Picha Kwa Maana Images
Shahidi: Picha Hakuna, Zipo Profile Picture
Mangula: ambazo ni za nani
Shahidi: Sijui za nani
Mangula: Katika hivyo Vielelezo ambavyo Vimepokelewa Mahakamani, Palikuwa na Mazungmzo ya Simu kati ya Watuhumiwa
Shahidi: Hakuna ila kwenye Kielelezo namba 26 zipo
Mangula: apewe Namba 26,,tuchagulie Mazungmzo Marefu Kuliko yote
Shahidi: Kuna Mazungmzo ya Dakika 9
Mangula: Bila Shaka Ndipo walikuwa wanapanga Ugaidi, Haya Mwambie Mheshimiwa Jaji Walizungumza nini hawa Watuhumiwa
Shahidi: Kuna Call Logs tu
Mangula: zile Sauti zipo wapi
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Kama Mahakama Yako itaniruhusu Kwa sababu za Ki Usalama nisijibu Hilo swali
Mangula: Swali langu ni Juu ya Watuhumiwa Ukiwa Mchunguzi wa Hizo Simu, Nauliza Mazungmzo ya Watuhumiwa Wale Wanne, Narudia Swali Sauti zao Watuhumiwa Zipo wapi ndugu shahidi?
Shahidi: Sababu za Kiusalama huwezi Kuzungumzia suala la Sauti
Mangula: Shahidi Nimesikia unasema Kuwa huwezi Kuzungumzia Kwa sababu ya Kiusalama, Je Sheria gani inakuzuia Usizungumzie hilo Suala?
Shahidi: Sijataja Sheria
Mangula: haya Sasa Mwambie Mheshimiwa Jaji, Sauti za Watuhumiwa Zipo wapi????
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Hazikuwa zinahitajika katika Terms Of Reference
Mangula: Ni sahihi nikisema Kuwa Katika Extraction Uliyo fanya, Kuna Vitu Uliviondoa sababu hazikuhitajika?
Shahidi: Swali linahitaji Maelezo, Mwanzoni Nilisema Kuwa Tunafanya Kwa Hatua tatu, Aquisation, Analysis na Extraction
Mangula: Kwa hiyo ni sahihi Kuwa Kwenye Mtambo Kuna Baadhi Ya Taarifa Hukutoa Sababu Hazikuhitajika?
Shahidi Wa Jamhuri: Kimya
Mangula: Kwa Mujibu Wa Kielelezo Namba 22, Mwambie Mheshimiwa Jaji Vitu gani Viliombwa Kwa ajili ya kufanyia Uchunguzi
Shahidi: Kwa Mujibu wa Barua yako Yenye Reference........
Mangula: Hoja ya Barua Ilikuwa unahitaji Ufanyie nini
Shahidi: Pamoja na Taarifa Hii Nakuletea Uchunguzi Niliofanya .... Mimi Inspector Innocent Ndowo
Mangula: Ni wapi Walikutaka Wewe Usitoe Sauti za Watuhumiwa?
Shahidi: Mimi nilifuata Terms of reference
Mangula: Nikisema Kuwa Wewe Inspector Ndowo na Viongozi Wako wa Polisi Kwa Makusudi Mliamua kuficha Baadhi ya Taarifa katika
Kesi hii kwa Maslahi yenu Itakuwa sahihi au siyo Sahihi Ukizingatia Kuna Taarifa Hazipo hapa?
Shahidi: Siyo Sahihi, Hatufanyi Kazi kwa interest zetu
Mangula: Fungua Kielelezo H, na Umwambie Mheshimiwa Jaji IMEI namba ya hicho Kielelezo Ni namba Ngapi Kwa Mujibu wa PF 145
Shahidi: Kwa Mujibu wa PF Hakuna IMEI namba
Mangula: Soma huo Mstari Wa Pili Kwa Sauti Umeandikwaje
Shahidi: Simu TECNO IMEI imefutika
Mangula: Wakati Unaongozwa Kwenye Ushahidi Ulisema nani aliyefuta hizo IMEI namba
Shahidi: Si Kuulizwa hilo swali
Mangula: Wewe unafahamu aliye futa hiyo IMEI namba
Shahidi: Simfahamu
Mangula: Katika hicho Kikaratasi Umeeleza IMEI namba Imefutwa Wapi.?
Shahidi: Sikusema
Mangula: ukiacha Kielelezo namba 35 ambacho kimechezewa na Watu wasiojulikana , Ni Kielelezo Kipi Kingine Mlichochezea
Shahidi: Hakuna Kielelezo Kilichochezewa
Mangula: Fungua Kielelezo namba 23, Mheshimiwa Jaji Namuonyesha Kielelezo namba 23
Mangula: Nataka Majibu ya Riport Yako ya Uchunguzi
Mangula: Mwambie Mheshimiwa Jaji ni wapi Katika Report Yako ya Uchunguzi Umeandika IMEI namba Imefutika
Shahidi: Hakuna Mahala Nilipo andika
Mangula: Nilisikia Unasema Ulichukua simu Ukiweka Katika Mtambo Wa Uchunguzi, Ule Mtambo utakuonyesha Kuwa Simu ni Original au Feki
Shahidi: Mtambo hauonyeshi Kuwa Simu ni Feki au Original
Mangula: Kitu gani Kinaonyesha kuwa Simu ni Feki au Original
Shahidi: Kitu nilichosema Kuna Kama zile Simu za Kichina, Mtambo una Operate kwa OS
Mangula: Kwa hiyo nini Kina onyesha ni FEKI Au ORIGINAL?
Shahidi: Nilichosema naomba Unisikie Vizuri, Mtambo una Option ya Kufanya Kazi hata Kwa kutumia Chip
Mangula: Mheshimiwa Jaji naomba NIISHIE Hapo
Shahidi: Samahani Mheshimiwa Jaji NAOMBA KWENDA WASHROOM (CHOONI)....
Shahidi anatoka na kuelekea katika vyoo vya nje..
Mahakama Ipo kimya inasubiri arejee kizimbani.
Shahidi amerejea kizimbani kutokea kwa fasii ya chooni.
Kihwelo: Shahidi Nilisikia Unazungumzia Kuhusu Celebrite Physical analyser Je ni Software Au.?
Shahidi: Ni software
Kiwhelo: nani alifanya Development ya Software
Shahidi: Celebrite Wenyewe
Kiwhelo: Nilisikia Umesomea Kuhusu Penetration Test
Shahidi: Ndiyo
Kihwelo: Je Penetration Testing, Ni sawa na Fazzing
Shahidi: Sifahamu
Kiwhelo: Je Wakati Unafundishwa Kuhusu Penetration Testing, Walikufundisha Kuhusu Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao (High Tech Cyber Attack)
Shahidi: Sijafundishwa hiyo
Kiwhelo: kwakuwa Ujafundisshwa kuhusu Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao, Ni sahihi Celebrite Ingeweza Kuingiliwa
Shahidi: Haiwezi Kuingiliwa
Kiwhelo: pale Ofisini kwenu ni nani Network Provider
shahidi: ni TTCL
Kiwhelo: Ni sahihi Kuwa Network Services Provider anaweza Kuingilia Data Zako
Shahidi: Hawezi
Kiwhelo: Nyinyi Kama Jeshi la Polisi Mnatumia Nini Kujilinda na Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao
Shahidi: Naomba nisijibu sababu za Kimtandao
Kiwhelo: Nilisikia Kuwa unazungumzia kuhusu DECORDING
Shahidi: Ndiyo
Kiwhelo: Shahidi Pegasus Technology ni Moja ya Technology mnayotumia?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji naomba Nisijibu Sababu za Kiusalama
Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji naomba anijibu sababu Baadae Nitataka kujua Intergrity ya Technology Wanayotumia
Jaji: Shahidi ame raise suala la Security, Au mnasemaje Upande wa Serikali?
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shahidi amesha Sema kuwa awezi Kusema Sababu za Kiusalama, Sisi tunaona Sababu hizo ni Valid, lakini siyo kutulazimisha
Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji Shahidi Wakati Shahidi anataka Ushahidi Wake Jana Alitaja Hapa Kuhusu Microsoft na Celebrite, alitaja hizo Mbili Maana yake ameshataja
Jaji: Sasa Shahidi Kaja na suala la Security kwa hii Uliyotaja
Kiwhelo: Basi Ngoja Niendelee na Kingine, Shahidi Wakati Una Extract Data Kwenye Celebrite Ulihifadhi Kwenye nini
Shahidi: Nili hifadhi Kwenye Computer
Kiwhelo: Vipi kuhusiana na Usalama wa computer yenyewe
Shahidi: Kimya
Kiwhelo: Uliandika Taarifa ya Simu Nne..?
Shahidi: Simu zote Nane
Kiwhelo: Siku ya Tarehe 09 July 2020 Uliingia Saa ngapi
Shahidi: Niliingia Saa 1 na Nusu Asubuhi
Kiwhelo: na Ulitoka Muda gani
Shahidi: Unatoka Muda wowote, hupangiwi kwa Sababu tunafanya Kazi Masaa 24
Kiwhelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji ulikuwa unaandika summary kisha unafuata extraction
Shahidi: Siyo sahihi
Kiwhelo: Soma hapo kwenye report yako
Shahidi: Inaanza na summary kisha extraction
Kiwhelo: Kwa hiyo imeanza na summary
Shahidi: Ni sawa, imeanza na Summary
Kiwhelo: Tuzungumze Kidogo Kuhusu Kampuni ya CELEBRITE Ukasema Kuwa Ni Moja ya Kampuni inayodevelop Software
Je unafahamu Celebrite Ni Kampuni Ya Kijasusi wa Kidigitali ya Nchi Israel
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kiwhelo: Je Unafahamu Kuwa Hiyo Kampuni inahusishwa na Unyanyasaji wa Waandishi Wa Habari na Wana Harakati Duniani
Shahidi: Sifahamu
Kiwhelo: na Je Unafahamu Kuwa Celebrite Mashine Inaweza Kuingiliwa.?
Shahidi: Haiwezi Kuingiliwa
Kiwhelo: Je Nitakuwa Sahihi Nikisema Kuwa Celebrite Mashine Inaweza Kuingiliwa na Kubadili Taarifa Zilizotamgukia na zilizopo
Shahidi: Hapana Siyo Sahihi
Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji naomba nimkabidhi Shahidi Nyaraka asome Kuhusiana na Celebrite
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba wakili azuiwe Kusoma hiyo Nyaraka
Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji Kwa ajili ya Muda nitaomba Kuachana na hiyo
Naomba nipatiwe P23 na P35
Naomba Sasa Nimkabidhi Shahidi
Kiwhelo: naomba Unisomee description hapo Juu
Shahidi: Imeanza Neno Station, Date 05 August 2020, CF imeandikwa. Simu Imeandikwa Tecno IMEI imefutika, Ilipatikana Maungoni (Mwilini)
Kiwhelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji Wewe Umetoa wapi Namba kwa Mujibu wa IMEI namba ambayo Imefutika
Shahidi: Inawezekana Physically Isionekane ila akuna Namna unaweza Kuona, au Kwenye Barua
Kiwhelo: hiyo Barua Ipo Hapa Mahakamani
Shahidi: Haipo Mahakamani
Kiwhelo: Ulizungumzia Kuwa IMEI namba ulitoa Kwenye Barua.?
Shahidi: Nili zungumza Kwa Ujumla
Adv. @FrederickWakili
: Mheshimiwa Jaji nimeishia hapo na naomba kurudisha vielelezo
Anasimama Wakili Msomi Peter Kibatala.
Kibatala: Inspector Ndowo Mambo Vipi
Shahidi: Salama
Kibatala: Siku ya Kwanza Uliomba Kusitisha Ushahidi Kwa sababu uliumwa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Ulipitia Hospitali.?
Shahidi: Nilienda Ofisini, nikarudisha Vielelezo
Kibatala: Kwa hiyo Baada ya Kutoka Hapa Hukwenda Hospitali Moja kwa Moja
Shahidi: Si kwenda Hospitali Moja Kwa Moja
Kibatala: Ulisema Kichwa Kilikuwa Kinafanya nini Vile
Shahidi: Kilikuwa Kinaniuma Kadri nilivyokuwa natoa Ushahidi
Kibatala: Na Kwa hiyo Ofisi Yako Ilikuwa wapi Vile
Shahidi: Posta
Kibatala: na Baada ya Hapo Ukaenda Hospitali Wapi
Shahidi: Kilwa Road
Kibatala: Twende Kwingine, Shahidi Je Uliwahi Kufanyiwa Training na Watu wa CELEBRITE
Shahidi: Yes Wawakilishi Wao
Kibatala: Unakumbuka Kozi Mbalimbali Ulizo taja Siku ya Kwanza Ukiwa unataja Mafunzo mbalimbali uliyopata.
Kibatala: Je kwa Kumbukumbu yako Ulitaja Mafunzo Yaliyo endeshwa na Celebrite au Wawakilishi wao
Shahidi: Jibu Lina hitaji Maelezo, Nilitaja Kozi Mbalimbali na Baadhi walitoka Nairobi.
Kibatala: Maelezo Ambayo Umeyatoa, Kuna Mahali Umesema Kuna watu Walitoka Nairobi Kuja Kuku train Kuhusu Celebrite.%?
Shahidi: Nilipata Kozi Mbalimbali, sikudadavua
Jaji: Swali Lake Ulisema Kuwa Kuna Wataalamu Kutoka Nairobi Kuja Kuku Fundisha Kuhusiana na Celebrite.
Shahidi: Sikutaja Mheshimiwa
Kibatala: Katika Maelezo yako, Ulisema Ulienda Training Mahala Mbalimbali, Je Ulisema Kuwa ulienda Israeli.?
Shahidi: Israel Sikutaja
Kibatala: Unafahamu Kuwa Makao Makuu ya CELEBRITE Yapo Nchini Israel
Shahidi: Nafahamu Yapo Israel
Kibatala: Je Unafahamu Kuwa Israel Kwa Wivu na Technology yao Hawaja Outsource kwa Mtu Kuhusiana na Training wala Technology?
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kuwa Nairobi Hakuna Wakala Wa CELEBRITE?
Shahidi: Hapana Sifahamu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Wakili anataka Misamiati Migumu ya Technology shahidi anaweza asijue ni nini Kinaongelewa.
Kibatala: Mheshimiwa Jaji hakuna hoja hapo, Mbona shahidi anajibu, Eti ndugu shahidi, ni kweli huelewi Kitu?
Shahidi: Ndiyo sielewi
Kibatala Kwanini sasa ulikuwa unajibu?
Shahidi wa Jamhuri: Kimya
Kibatala: unafahamu sababu ya Wivu Wa Technology, Israel Hawana Mwakilishi wa CELEBRITE Duniani katika Nchi yoyote
Shahidi: Yupo Nairobi
Kibatala: Anaitwa Nani
Shahidi: SAM
Kibatala: Unafahamu Kuwa Technology ya Pegasus ni Technology ya Israel Pia
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: una Cornfirm kwetu bila kwenda kwenye details kuwa Jeshi la Polisi mnatumia pegasus?
Shahidi: Naomba nisijibu hilo swali kwa sababu za Kiusalama
Kibatala: Baadae Nitakuja hapo na nitakutaka kwa lazima ujibu hilo swali, kwa sasa ngoja niende kwingine.
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Celebrite unatumia Software Mbili UFET na physical analyser?
Shahidi: Ndiyo ni baadhi ya product za kwake
Kibatala: UFEN kazi yake I naingia katika Simu au Computer kisha Inatengeneza Back up
Shahidi: Inategemea na level ya Extraction Unayofanya
Kibatala: Ni sahihi Kuwa katika kazi Uliyo kuwa unafanya unaunganisha Simu Kwa Kutumia Cable kisha Celebrite inachofanya Kwa kutumia UFEN Kutengeneza Back up
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kuwa physical analyser Inafanya kazi Kwa Ku arrange Taarifa In Chronological Order
Shahidi: Sahihi ila inategemea Level
Kibatala: Jaji akimaliza Ku Rekodi Mwambie Kuwa Kazi ya Physical Analyser Kama Software Ni kuyapanga Mafaili Kwa Mchunguzi ili Ku Make Sense na hiyo Process inaitwa PASSING
Shahidi: Naomba nijibu kwa Maelezo Kuwa Physical analyser, Inafanya kazi 3 ila Kwa Ujumla Ndiyo PASSING
Kibatala: Katika Report Yako Kuna Item Ya PASSING
Shahidi: Kama Software Include hizo Taarifa zake, Basi itaonekana
Kibatala: Basically Physical analyser haina Jipya Zaidi ya kupanga Mafaili
Shahidi: Hapana Physical analyser ni zaidi ya hapo
Kibatala: Tofauti Yake nini, Kama Unaingia Kwenye simu yangu ya Telegram na kisha unapamga Mafaili
Shahidi: Ni zaidi ya hapo kwa sababu ina Uwezo Kuwa Kufanya Back Up Kwa Vitu Vilivyofutwa
Kibatala: Physical ANALYSER inaweza za KubadiliSha Chochote
Shahidi: Hapana
Kibatala Physical analyser Ina extract
Shahidi: Hapana
Kibatala: unapokuwa na Kifaa kama Simu Kutoka Kwa DCI Nini Kilianza Kati ya kutumia UFEN Kufanya Extraction au Physical Analyser Kupamga kazi yako
Shahidi: Nilianza Kutumia UFEN
Kibatala: Wewe Umeletewa 8 applications phones, Je zile Data zilizokuwa katika Hizo phones, Je ni Software gani zilikuwezesha Kuingia Kwenye simu na Kusoma Meseji
Shahidi: Ni Physical analyser
Kibatala: Sasa Mbona Mwanzo Ulikataa, Wacha sasa Ikae Hivyo
Kibatala: Jana Ulizungumzia Kuwa huwezi Ku impose Vitu Vyako Kutoka Nje,
Shahidi: Ndiyo WRITE BLOCK
Kibatala: Unafahamu Kuhusu Software ya CELEBRITE Kuhusu Soft Write Block?
Shahidi: Hiyo sifahamu kwa kweli
Kibatala: Ni kweli au siyo Kweli Kuwa Celebrite Soft Write Block Ndiyo inayomzuia Mtu Kuingilia Mashine ya CELEBRITE
Shahidi: Hiyo sifahamu
Shahidi: Na Bado Ukitaka Kutuaminisha Kuwa Mashine zenu zina Intergrity?
Shahidi: Ndiyo Sijataja
Kibatala: Je ulitaja Jana software zaidi ya Mbili
Shahidi: Sikutaja
Kibatala: Ulizungumzia Forensic Cables,
Shahidi: Sawasawa
Kibatala: Ni Cables kama za USB tuh au Kuna tofauti
Shahidi: Ni Tofauti Kabisa
Kibatala: Inasifa gani Kitaalamu ambayo ni zaidi za USB
Shahidi: Ni Cable Zenye namba pembeni
Kibatala: Je Hapa Umetaja Namba za Cables
Shahidi: Hapana
Kibatala: Hizi Simu ambazo wewe Ulifanyia Extraction, Makers ni Tofauti
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Jana Nilisikia Unasema wewe siyo Mpelelezi ni Mchunguzi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ni wapi au Kwenye Instrument ipi Inatofautisha Mpelelezi na Mchunguzi?
Shahidi: Ukija Ofisini Utajua
Kibatala: Mpaka Nije Ofisini kwenu, Vipi PGO Inatambua?
Shahidi: Sijui
Kibatala: PGO ya 8 Sehemu Ndogo ya 4 inasema Kuwa Ofisi Ya DCI inagawanywa katika Divisheni Nne, Mmoja wapo ndiyo hiyo ya Forensic Beaural
Shahidi: Sijui ni PGO gani
Kibatala: zote mbili
Shahidi: Mimi ninachojua Forensic Beaural ni Imtependent Beaural
Kibatala: na Ndiyo Maana ni Kuuliza Unapata wapi Mgawanyo huo
Shahidi: Ukienda Ofisini Makao Makuu ya Jeshi la Polisi au Dodoma
Kibatala: Mhe Jaji naomba Kielelezo 6,7,
Kibatala: angalia Maneno ya DCI Katika hiyo Barua. Unafahamu Kirefu chake?
Shahidi: nimesahau kidogo
Kibatala: Mimi nikikwambia kwamba kirefu cha hayo maneno uliyoandika wewe kwenye barua yako ni DIRECTOR OF CRIMINAL INVESTIGATION?
Shahidi: Sijui mpaka Nipate Mwongozo Wa Wakubwa zangu
Kibatala: Juu pia maneno ya DFSI kuwa ni DIRECTORATE OF FORENSIC SCIENCE INVESTIGATION?
Shahidi: Sifahamu mpaka Nikumbushwe na wakubwa zangu
Kibatala: Na Bado wewe Unasema ni inspector wa Jeshi la polisi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala Mheshimiwa Jaji muda wetu wa kupumzika umefika, labda nipate mawazo kutoka kwa wenzetu nina maswali mengi bado
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Tu' break dakika 45
Wakili Peter Kibatala Saa Saba na Dakika 45
Jaji: Tuna break kwa dakika 45 tutarudi saa saba na dakika 45
====
Jaji ameingia Mahakamani Muda huu Saa 8 na Dakika 5
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani Muda huu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Quorum yetu ipo Vile vile
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji na sisi Quorum yetu ipo Vile vile
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba Nikumbushwe Nilipo Ishia
Jaji: ulimuuliza Kuwa Bado yeye ni Inspector akajibu Ndiyo
Kibatala: PGO ya 9 inasema Subject to the Direction of the DCI
Je wewe Unapata Mwanga kuwa Ofisi ya Forensic Beaural Bado ni Ofisi inayojitegemea
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji tunaomba tujiridhishe
Kibatala: wacha nibadili swali
Kibatala: Shahidi ulipokea Barua Kutoka Kwa DCI lini
Shahidi: 13 August 2020
Kibatala: Kwakumbu Kumbu yako Version ya PGO ipi ilikuwa Inafanya Kazi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: kwa hiyo nikikusomea PGO ya wakati Unapewa Barua, ilikuwa Inatumika ambayo ni Ile inayosema Mpo Chini ya DCI?
Shahidi: Naomba Kutoa Maelezo, Mimi siyo Msemaji wa Jeshi la Polisi
Kibatala: na hilo nalo ni Jibu, Sijui Kwanini upo Hapa
Kibatala: Katika PGO ambayo ulikuwa unafanyia kazi wakati huo 9(c) Vifaa Kama Simu Vimetajwa?
Shahidi: Mhe samahani wakili NIMEMWAMBIA sifahamu KUHUSU PGO LAKINI NAONA MWENZANGU KAJIKUTA KWENYE PGO TU..
Kibatala: Nivumilie tu, mimi nisipokuuliza swali kuna sehemu nitaulizwa
Kibatala: Katika Majukumu yako Ulifanya Kazi Baada ya Kupata Barua Kutoka kwa DCI
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: na Kilicho Pelekea Wewe Kufanya Uchunguzi yalikuwa ni Maombi Kutoka kwa DCI
Shahidi: Sahihi
Kibatala: na Maombi hayo yalikuwa na Terms of Reference
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Ofisi ambayo inajitegemea Kimamlaka Je Inaweza Kupokea Terms of reference katika Utendaji wake wa Kazi
Shahidi: Sitaki Kujiunga katika Maneno yako, lakini Uchunguzi Ulifanyika Ujue Kuna Sababu ulizopewa
Kibatala: Bado Haujajibu swali, Je Ofisi Ambayo inajitegemea Kimamlaka Je Inaweza Kupokea Terms of reference
Shahidi: Barua Zinapokuja, na Hatujui lolote linaloendelea
Kibatala: Swali langu lipo pale pale Kwamba Je Taasisi ambayo inajitegemea inaweza Kupewa Terms of reference
Shahidi: Kesi husika Inapokuwa kwetu, Kuomba Kufanya Uchunguzi, Lazima. Ije na Barua na Lazima isema Vitu ambavyo inaomba Ichunguze
Jaji: Taasisi ambayo inajitegemea inaweza Kupewa Hadidu za Rejea?
Shahidi: Ndiyo tunavyofanya hivyo hivyo
Kibatala: Wewe Kwa Ufahamu Wako, Taasisi inayofanya Uchunguzi Inaweza Kukusanya Ushahidi
Shahidi: Sijasema Kuku Sanya Ushahidi
Kibatala: Ulisema Nini
Shahidi: nilisema Kuandaa Ushahidi
Kibatala: Taasisi inayofanya Uchunguzi Inaandaa Ushahidi au Findings
Shahidi: inaandaa Findings kwa ajili ya a Kutumika kwenye Ushahidi
Kibatala: Wewe in Inspector Wa Forensic au Inspector Wa Jeshi la Polisi
Shahidi: Ni Inspector Wa Jeshi la Polisi
Kibatala: Unapofanya Uchunguzi, unafanya Uchunguzi wa akosa la Jinai au Uchunguzi Wa Vifaa
Shahidi: Nafanya Uchunguzi wa Vifaa
Kibatala: Kwa hiyo Unafanya Uchunguzi Wa tuhuma Za Jinai au Hufanyi
Shahidi: Sisi Kazi yetu ni Kuchunguza Vile Vifaa Vilivyotumika katika Jinai
Kibatala: Katika kesi hii wewe ulichunguza tuhuma Za Jinai au Lah
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Vifaa Vinavyo kuja Ofisini, is a must Vifaa Vile na Namba ya Kesi husika, Kwa hiyo Jinai Wanaopeleleza Ni Wa pelelezi
Kibatala: kwa hiyo wewe Unachaguza tuhuma Za Jinai au Lah
Jaji: amesema anachunguza Vifaa ambavyo Vinahusishwa na Jinai
Kibatala! Okey any way, Twende Kwenye Barua ya Tigo Soma
Shahidi: "Ofisi Inafanya Uchunguzi Wa Tuhuma Za Jinai....."
Kibatala: kwa Mujibu wa Barua hiyo uliyoandika Wewe Mwenyewe Ulikuwa unachunguza Tuhuma Za Jinai
Shahidi: Ofisi yangu hai Chunguzi Tuhuma Za Jinai
Kibatala: hiyo Barua uliyoandika wewe Kwenda Tigo, na Majibu ya Barua ya Tigo na Vielelezo Kutoka Tigo ni sehemu ya Riport Yako au Siyo sehemu Riport yako
Shahidi: Ni sehemu ya Riport yangu
Kibatala: Ile Originating letter Kutoka Ofisi ya DCI ipo au Haipo Hapa Mahakamani
Shahidi: Hapa Mahakamani Haipo
Kibatala: Shahidi hapa Kuna namba zimeandikwa CD IR 2020..... Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa hizo ni Reference kutoka Forensic au Kutoka Kwa DCI
Shahidi: Hizo ni Reference namba Kutoka Ofisi ya DCI
Kibatala: ambazo hizo hizo Uliwaandikia Tigo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Shahidi Ni sahihi Ume nukuu Sheria ya Makosa ya Mtandao Kifungu cha 34
Shahidi: Ndiyo Niliandika
Kibatala: Tigo walikuwa na nafasi ya Kukataa
Shahidi: Ukisoma Sheria Utajua
Kibatala: Hii Barua Kaandika nani?
Shahidi: Mimi Mwenyewe
Kibatala: Je unafahamu hicho Kifungu ni Kifungu Pelelezi?
Shahidi: Sijui
Kibatala: Kama Tigo Wasingewapa hizo Taarifa Mgewachukilia Hatua?
Shahidi: Kwanini uongee Kitu ambacho akijatokea
Kibatala: Je Mahakama Ikuchukulie wewe ni Afisa Wa Polisi Makini?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Barua Kutoka Tigo ambayo Ulitoa kama Kielelezo hapa Mahakamani, Uliwahi Kuiona?
Shahidi Ndiyo Niliwahi Kuiona
Kibatala Na Ukafanyia Uchunguzi Wako
Shahidi ndiyo
Kibatala Nenda Kielelezo namba P7 some Kumbukumbu namba iliyotajwa hapo
Shahidi CD/ IR/ 2007/ 2020
Kibatala Hilo ndiyo Jalada Mama Kutoka Ofisi ya DCI
Shahidi Ndiyo
Kibatala Kama Usingeona hii namba ya Jalada ungefanyia Uchunguzi?
Shahidi: kimyaa
Kibatala: Nenda Barua ya Tigo, Soma Jalada walilo kujibu pale
Shahidi: CD/IR/2097/2021
Kibatala: Inafanana au Inatofautiana?
Shahidi Inatofautiana sababu ya Typing Error
Kibatala: Sijakutuma utaje sababu hala, Wewe sema Imefanana au haijafanana
Shahidi: haijafanana
Kibatala: Katika Barua Yako inasema 2020 na Barua ya Tigo inasema 2021, Je Ipo wapi Barua ya DCI Kuondoa huu Mtanziko?, Umetoa Mahakamani Kama Kielelezo
Shahidi: Barua sijaitoa Mahakamani
Kibatala: Hii Barua Kutoka Tigo ya Tarehe 01 July 2021, ulipokea wewe Binafsi
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulimwambia Jaji Nani alipokea pale Ofisi ya Forensics
Shahidi: Hapana Sikusema
Kibatala: Wewe ni Inspector wa Jeshi la Polisi unafahamu Chain of Custody?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala Ulimwambia Jaji ulipoitoa hii barua?
Shahidi: Nishajibu hilo
Kibatala: Huyu NAFTALI J MANTAMBA yupo au alikufa?
Shahidi: Yupo
Kibatala: yule Kamishina Wenu anaitwa Nani Vile?
Shahidi CP SHABANI HITI
Kibatala: Je Ulimwambia Jaji Kwamba, Wakati Unaandika Barua, Yeye Kamishina Alikuwa anafahamu au hafahamu?
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Ulimwambia Jaji Wakati Bwana NAFTALI J MANTAMBA Wakati unasaini Barua hii SHABANI HIKI ALIKUWA Magonjwa au Lah
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Je Ulimwambia Jaji Kuwa upo familiar na Sahihi ya Bwana NAFTALI MANTAMBA, JE Ulimwambia Hukumwambia
Shahidi: Sikusema Mheshimiwa Jaji
Kibatala: Shahidi Kuan Kielelezo namba P8, Ambapo Kuna Rekodi ya Mihamala Kutoka Namba Fulani Kwenda Namba fulani Ambapo wewe Uliombea namba 0719931389
Shahidi: Naweza Kuelezea kama Nimavyoona
Kibatala: Kwenye Rrport yako Umesemaje
Shahidi: Kwa Mujibu wa Report ya Tigo
Kibatala: Nini primary Source kati Mhamala Wa Tigo au Riport yako wewe
Shahidi: Mimi sijaelewa
Jaji: liweke Vizuri Swali
Kibatala: Ipi ni Primary source kati ya Taarifa ya Tigo na Report Yako
Shahidi: Primary Source ni Report Kutoka Tigo
Kibatala: Kwa Maana hiyo ufahamu Kiasi cha Fedha TSh 500,000 pesa hiyo ilipotoka?
Shahidi: Sender na Receiver anaonekana
Kibatala: Unafahamu Kitu kinaitwa Collection Akaunti au Wallet?
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: kwa hiyo Kwenye Muamala Huo wanaoweza Kuzungumzia zaidi ni Airtel?
Shahidi: Airtel ndiyo wanaweza Kuzungumza
Kibatala: Hiyo namba, Ilikuwa ni sehemu ya Terms of reference Uliyopewa na DCI?
Shahidi: Ndiyo Kutaka Miamala Ya Fedha
Kibatala: Katika originating later ilisema Pamoja na Taarifa zingine, ilikupa wigo Mpana
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa katika Uchunguzi Wako wa Vifaa, ambacho wewe Uliona ni Kiashiria cha Kutenda Makosa ya Ugaidi
Shahidi: Nilichokiona Ndicho nilichokitoa
Kibatala: Katika Uchunguzi Wako Uliona Mawasiliano yoyote yanamtaja Mtu anaitwa Sabaya
Shahidi: Terms of reference Hazikuelekeza Kumtafuta Sabaya
Kibatala: Katika Uchunguzi Wako Uliona Popote Watu wanapanga Kufanya Ugaidi
Shahidi: Mimi sikuelekezwa Kutafuta hilo
Kibatala Katika Uchunguzi Wako wote, Uliwahi Kuona au Kusoma Wakati Wa Extraction Watu wakipanga Kulipua Madaraja
Shahidi: Kimya
Kibatala: Wakati Unafanya Extraction Kuna Mahala Popote uliona Mawasilisho watu wamepamgwa Kuandaa Maandamamo Nchi Nzima
Shahidi: Sikuelekezwa
Kibatala: Uliwahi kuona mawasiliano katika Subject Phones wakizungumzia bunduki aina ya A5340 aina ya Luger?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji ananiuliza mambo ambayo sijafanyia kazi
Kibatala: Nakuuliza kuhusu miamala, Je Kuna Telegram text, WhatsApp, au SMS Umeona meseji kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya kutenda ugaidi?
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Katika meseji zako kuna sehemu ina neno SABAYA?
Shahidi: HAKUNA
Kibatala: Tuambie Muamala upi wewe kama Inspector uliona watu wanapanga tendo la kihalifu....
Shahidi: Hakuna terms of reference yenye Jambo hilo
Kibatala: Kwa uchunguzi wako wewe ungekuta taarifa za kupanga uhalifu, ungeacha kuandika kwenye report yako kwa sababu haujaambiwa kwenye terms of reference?
Shahidi: Mimi ni Askari Polisi, kama ningekuta meseji za kupanga uhalifu ningeweka kwenye report yangu.
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba nipewe Kielelezo namba 24,25, 26 na 27
Kibatala: Shahidi Nakuonyesha Kielelezo namba P25
Kibatala: Unakumbuka Siku Unaandika Covering Letter
Shahidi: ilikuwa Tarehe 09 July 2021
Kibatala: Ilikuwa Saa ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Kwa Mujibu Ushahidi Wako Wa awali ulisema Vifaa Vilichukuliwa Tarehe ngapi?
Shahidi: Tarehe 10 July 2021
Kibatala: alikuja Kuchukua nani
Shahidi: Inspector Swila
Kibatala: ulimkabidhi Vipi.?
Shahidi: Alifika pale Nikamkabidhi
Kibatala: Je Uliandika item Moja Moja akasaini au alichukua Zote akaondoka?
Shahidi: Kwenye Kitabu Kuna sehemu anajaza Pale, kina Items Zote.
Kibatala: Wewe Uliandika wakati Unamkabidhi?
Shahidi: Utaratibu Wa Kwetu Lab Namba, Unapoingia Unasaini, Kuna entry Maalum
Kibatala: Hizi Simu Nane, ambazo zilizokuwa na Taarifa Ulipokea Tarehe ngapi
Shahidi: Tarehe 13 August 2020
Kibatala: na ulipozipokea kwa Utaratibu wenu wa Forensic Ukaandika Kwenye Hicho Kitabu. Kwenye Kitabu Cha Maabara ulisaini?
Shahidi: Utaratibu Ndivyo Ulivyo
Kibatala: Nani alileta Hizo Simu Maabara
Shahidi: Goodluck
Kibatala: Goodluck alipokabidhi alisaini au Hakusaini?
Shahidi: anatakiwa Kusaini Siku anapokuja Kuchukua
Kibatala: na aliyekuja Kuchukua ni nani
Shahidi: Inspector Swila
Kibatala: Na Kuchukua anakuja Kufuata Mtu yoyote au Aliyekabidhi?
Shahidi: aliyekabidhi
Kibatala: Na bado ulimpatia Inspector Swila Pamoja na Kuletwa na Goodluck?
Shahidi: Kimya
Kibatala: Register Ya Siku hiyo Ipo wapi?
Shahidi: Ipo Ofisini Maaabara
Kibatala: umemuonyesha Jaji
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Register Ile imeungua au ni Kubwa sana? Ulimwambia?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji report Creation time ilikuwa Muda gani?
Shahidi: Ilikuwa Tarehe 09 July 2020
Kibatala: Wakati Wa Ushahidi Wako Ulisema Kuwa Ulifanya Kazi hadi Saa Ngapi
Shahidi: Sikuulizwa
Kibatala: Kwa kuwa Hukuulizwa Jaji anajua au Hajui?
Shahidi: Hajui
Kibatala: Extraction ikifanyika lini?
Shahidi: Tarehe 07 July 2020
Kibatala: Extraction time ilikuwa Lini
Shahidi: Tarehe 09 July 2020
Kibatala: Kuna Tofauti ya Siku Ngapi
Shahidi: Kama Siku Moja
Kibatala: Ulimwambia Jaji Kwamba Kuna Delay ya Siku Moja na Data ikiwa Secured
Shahidi Sikueleza hilo
Kibatala: Tafuta Item 89 Mahala imeandikwa ICCID, Je ni Kitu gani
Shahidi: ID ya Kwenye Simu
Kibatala ID ya Kwenye Simu au ID ya Sim Card
Shahidi : ID ya sim Card
Kibatala: Je Ipo Katika Riport Yako au Haipo
Shahidi anatafuta.
Kibatala: angalia Ukurasa Wa Pili
Kibatala: Hiyo ICCID Unakubaliana ni ya Zain?
Shahidi: Nimeona Ndiyo
Kibatala: Katika Kielelezo Cha P25 ni Kweli imeishia na F Ndogo?
Shahidi: Ndiyo ipo
Kibatala: angalia na Kielelezo Kinachofuata, Kipo?
Shahidi: Hakipo
Kibatala: ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa ICCID ni Namba siyo Herufi?
Shahidi: Sikuulizwa
Kibatala: Kwa mujibu wa ICCID yako hapo, Ni ya Simcard la mtandao gani
Shahidi: Ni ZAIN..
Kibatala: Tangu uanze kutoa ushahidi hakuna sehemu umetaja neno ZAIN
Shahidi: Kimya
Shahidi MTN
Kibatala Unajua NI Mtandao wa Nchi Gani
Shahidi: Sijui
Kibatala: hujui Kwamba ni Mtandao Wa South Africa?
Shahidi: Hapana Sijui
Kibatala: Ulimtajia Mheshimiwa Jaji, kuhusiana na MTN
Shahid! i Hapana Sijamwambia
Kibatala: Je ulitoa ufafanuzi Kuhusu Crossing references namba za Divices Dhidi ya Namba ya Kwenye Simu
Shahidi: Si Kuulizwa Swali
Kibatala: Kama Hukuulizwa ulitoa Ufafanuzi au Hukutoa
Shahidi: Si Kuulizwa Kama Ningeukizwa Ningetoa
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi Wako Ulisema UFEN Version auliyotolea Ushahidi Ilikuwa namba Ngapi
Shahidi: UFED 7:4:4
Kibatala: Soma Ukurasa Wa 26 Chini Kwenye File system One, UFED ngapi
Shahidi: 7:4:0
Kibatala: Ulizungumzia hiyo jana
Shahidi: Ndiyo Nilitaja Jana
Kibatala: Leo Nimekuuliza Ukataja Version Ngapi
Shahidi 7:4:4
Kibatala: na Hizo Version Mbili Ulimfafanulia Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Si Kutoa Ufafanuzi
Kibatala Kwakuwa hii Taarifa ni Self Generated, Soma Extraction Process Discription pale Imaposema Kuwa Application...............
Unakumbuka Nilikuuliza hili swali Mwanzo
Shahidi Nakumbuka
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Application ilifanyiwa Kwa Back Up Android
Shahidi: Ndiyo Ilifanyika
Kibatala: Ulitoa Ufafanuzi Kuhusu Down Graded Area ya Version
Shahidi: Hapana Sikutoa Ufafanuzi
Kibatala: Baada ya Kufanyika Down Grading Ilikuweza EFED na Celebrite Physical Analyser, Je ulifafanua Kwa Jaji Kuhusu Storation
Kibatala: Twende Kwenye Plug inns, Contacts and References Je Ulifafanua kuhusu hilo
Shahidi: Hapana Sijaelezea
Kibatala: Nilikuuliza Kuhusu Forensic Cables, Ukasema Inategemea nini
Shahidi: Nilisema Inategemea
Kibatala: Shika Vielelezo Hivi Vinne, Mwambie Mheshimiwa Jaji Ulifanya Kwa Kutumia Device
Shahidi: Cable namba 100, Techno DA2
Kibatala: Nenda Kielelezo na P25 Ulitumia Forensic Cables zipi na Device Ilikuwa Ipi
Shahidi: Hapa Mheshimiwa Hakutaja Cable iliyotumika
Kibatala: ilikuwa Simu gani
Shahidi: Ilikuwa ni simu ya Tecno
Kibatala: Nenda Kwenye Exhibit P26 aina Ya Simu ni Ipi
Shahidi: Tecno V6 na Cable iliyotumika ni Namba 100
Kibatala: Nenda P27 ni simu aina Gani
Shahidi: Nakumbuka Ilikuwa Techno
Kibatala: Aina ya Simu Haitajwi??
Shahidi: Kimya
Kibatala: hapo ambapo aina ya Simu Haitajwi Ulitumia Forensic Cable gani
Shahidi: Haijataja Cable Iliyotumika
Kibatala: Hizo Simu zinafanama au Tofauti
Shahidi: Ni aina Tofauti
Kibatala: Je Ulimfafanulia Mheshimiwa Jaji siala la Utofauti Wa matumzi ya Tofauti ya Cable
Shahidi: Hapana Siku Mfafanulia
Kibatala: aliyeleta Masuala la Forensic Cables hapa Mahakamani
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Ethical Hacking Maana yake ni Udukuzi wa kimaadili.?
Shahidi: Sijui Kiswahili Chake
Kibatala: Nani anasimamia hiyo Ethical Hacking
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Katika Ushahidi wako wote zile simu 8, zinatakiwa Kufanya Extraction zikiwa Off au On
Shahidi: Inategemea Mashine
Kibatala: Unaweza Kufanya Extraction Simu Ikiwa Off?
Shahidi: Ndiyo unaweza
Kibatala: Chini ya Kiapo Kwamba Unaweza Kufanya Extraction simu zikiwa Off
Shahidi: Ndiyo Unaweza
Kibatala: Haya Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa Unaweza Kufanya Extraction simu ikiwa Off
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Katika zile simu Nilisikia Unasema Kuwa Matokeo positive, Maana ya Positive ni nini
Shahidi: Pale ambapo Nilichoombwa Hakijapatika ni Negative
Kibatala: Kwa Ushahidi Wako zile simu Nne zilikuwa hazina Mawasiliano
Shahidi: Hapana Zilikuwa hazina Mawasiliano Zinazo wasiliana na Hizi namba
Kibatala: Nenda Kwenye Terms of Reference, Je Terms of reference Inataja Kwamba Ufanye Uchunguzi Kuanzia Tarehe hii Mpaka Tarehe hii
Shahidi: Hapana Sijaandika
Kibatala: Na Mawasiliano Je
Shahidi: Hakuna Muda wa Limit
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji suala la Kutoa Miamala Na Mawasiliano Kutoka Tarehe fulani Mpaka Tarehe fulani
Shahidi: Kwenye Barua ambayo Ilikuwa Kwangu, Hapa Haipo
Kibatala: Kwanini tusiseme wewe ni miongoni mwa kikundi ndani ya Jeshi la polisi ambacho kilihusika na kupanga njama za Kumpa Freeman Mbowe Kesi ya Ugaidi Ndiyo Maana mlifanya uchunguzi kipindi fulani hadi fulani?
Shahidi: Hapana siyo sahihi
Kibatala: Naishia hapo
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Shahidi Umeulizwa Mambo Mengi sasa ni Muda Wa + Kufanya Ufafanuzi
Wakili wa Serikali: Jana Wakati Uliulizwa Swali hapa Ukasema, Siyo Kweli Kwamba tulifanya Extraction Tupo wengi, Hebu Tufafanulie Ulikuwa na Maan Gani
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Pia Kuhusiana Na Extraction Data Ukasema Ulikuwa nazo wewe
Shahidi: Kama Nilivyosema Awali, Kwenye Hizo Mashine tunaingia kwa Akaunti na Username
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali, Ukasema Kwenye Analysis, Ukajibu siyo Sahihi Kwenye Analysis
Kibatala: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Napinga Namna ya Maswali Kwa Mr. Hilla
Jaji: Kwa Maana anatakiwa kuweka swali na Jibu na vipi Kama aliweka Jibu pekee yake?
Kibatala: Bado Nitapinga
Jaji: Nafikiri sheria inasema kinachofafanuliwa ni Jibu
Wakili wa Serikali: Pius Hilla Mheshimiwa Basi tutafanya hivyo
Wakili wa Serikali: Shahidi Uliulizwa na Wakili Msomi Nashon Nkungu Kuhusiana na Analysis, Ulieleza Vitu VITATU ikiwemo , Extraction na Analysis, Maan yake nini.
Shahidi:Report Yako Ita Include Kile ambacho Umekipata tu.. Haito Include Kile ambacho haujakipata
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Maswali Kwamba Kwakuwa umepata Kozi Kuhusiana Na Terrorism, Wewe Ukasema Unafahamu Kuhusu Terrorism Kwa Perspective Ya Kiuchunguzi, Maana yake nini.
Shahidi: Software Yenyewe Ina Components ambazo Zina Jijaza Zenyenwe Kwa Pamoja
Nashon Nkungu: OBJECTION Mheshimiwa Jaji naomba Kupinga Jibu na Kinachoendelea, System Kwamba Yenyewe Ina Pick hizo Ingridients na Elements
Wakili wa Serikali: Tuache Shahidi ajibu Mheshimiwa Jaji kisha tupime Kama Linaendana na Jibu lake
Wakili wa Serikali: Shahidi Uliulizwa Pia na Wakili Mallya hapa, Mheshimiwa Jaji naomba P1, P23, P28
Wakili wa Serikali: Shahidi Uliulizwa na Malya, Kwenye Riport ya Kingai akamwambia Usome Kwenye IMEI namba
Alikuonyesha Pia simu na pia Kwenye Report yako, Akakuuliza Swali Kuwa IMEI namba zinatofautiana, wewe Ukasema kuna Digits Mbili Zina Miss, Ulikuwa na Maana Gani?
Shahidi: Kwenye hicho KIELELEZO D Kielelezo P31 zina Tally ila Kwa IMEI namba ya Pili Zina Miss namba mbili inaweza kama amesahau namba kadhaa
Kibatala: HAYO SIYO MAJIBU YA Re:Examination
Shahidi: Katika Report yangu Ipo ya Kwanza hii IMEI namba ya Kwanza ya Kingai 353736289120273 ila IMEI ya Pili Kwangu ni tofauti Inasomeka 3537289120273
WS: Je Zipo Namba Ngapi
Shahidi: Namba 15 au 13
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuwa Kuna Uwezekano wa IMEI Namba Kufanana
Shahidi: Hazifanani Sababu ni Unique Identification ya Kifaa Cha Mawasiliano
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuhusu Owenership Za Simcard
Shahidi: Taarifa Zote zinazo husika na Usajili au Taarifa Ya Simu Kadi Zinapatikana kwa watoa huduma
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusiana na software ambazo Ulizitumia kufanya Extraction, ukasema zilikuwa developed na microsoft na celebrite
Kibatala: OBJECTION Hakuna swali wala Hapaawzi kuwa na Jibu, sababu Haiwezekani microsoft a' develop software za celebrite
Wakili wa Serikali: Nimeachana na hilo swali
Wakili wa Serikali: Bado nina maswali mengi naomba Niletee maombi tumalizie kesho
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Kwa sasa ni Saa 11, Tunaomba hairisho Mpaka kesho Tarehe 20 Mwezi January
Wakili Peter Kibatala: Hatuna Pingamizi, Ila tunaomba Waje na Shahidi Mwingine, Ili tulimalizane na Shahidi huyu tuingie Kwa Mwingine
Jaji: Je kuna shida Katika Kumpata Shahidi Kesho?, Siamini Mtatumia Utaratibu wa Utetezi wa Kuuliza Maswali Siku Nzima
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji tutajitahidi, Kulingana na Muda Wenyewe Huu
Jaji anaandika Kidogo.
Jaji: Shauri linahailishwa hadi Kesho 20.1.2022, Shahidi ataendelea Kutoa ushahidi wake
Upande wa Jamhuri naelekezwa kuja na shahidi mwingine
Washtakiwa wataendelea kuwa rumande chini ya magereza mpaka kesho asubuhi saa 3 kamili
Jaji anatoka
Leo tarehe 19/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHEDEMA Freeman Mbowe inaendelea.
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
=======
Kufahamu ilipoishia, soma hapa:Yaliyojiri mahakamani kwenye Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake 3. Kesi imeahirishwa hadi 19/01/2022
Jaji ameingia, kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa.
Jaji: Shahidi Nakukumbusha Upo Chini ya Kiapo Bado na Wakili wa Mshtakiwa Namba Mbili Ilikuwa Unaendelea, Karibu
Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba nikumbushwe niliishia wapi
Jaji: Uliishia Wakati anakusomea Kielelezo H
Mallya: Shahidi tusomee hii ni Tarehe
Shahidi: Imeandikwa 05 August 2020
Mallya: Kuna Entry imeandikwa Owner of Article, Kwenye PF Je imeandikwa Jina gani?
Shahidi: Nashindwa Kusemea Sana Mheshimiwa Jaji sababu Siyo Mimi Niliyeandaa
Jaji: Hujaambiwa Uisemee Umeambiwa Usome
Shahidi: Imeandikwa Mohammed Abdallah Ling'wenya.. Lakini sijaandaa mimi
Mallya: Kwa Hiyo nani kaleta Mahakamani
Shahidi: Ni Mimi
Mallya: Kwa hiyo tuiondoe Mahakamani?
Shahidi: Hapana
MALLYA: Soma Sasa
Shahidi: Mwisho Imeandikwa DOYI
Mallya: Kutoka Tarehe 05 August 2020 Mpaka Tarehe Uliyo letewa Kwenye Ofisi yako Kuna Interval ya Siku Ngapi
Shahidi: Kuna Interval Ya Siku 08
Mallya: Na wewe Ulifanyia Kazi Tarehe Ngapi
Shahidi: Mwezi Wa July 2021
Mallya: Tarehe Ngapi
Shahidi: Sikumbuki Tarehe
Mallya: Kutoka Muda Umeletewa Mpaka Unafanya Uchunguzi Kuna Muda gani
Shahidi: Angalau Miezi 10
Mallya: aliyekuletea hiyo Item "H" alikwambia alikamata katika Physical Condition gani
Shahidi: Hakuniambia
Mallya: Alikwambia alikuwa Amehifadhi Siku gani
Shahidi: Hakuniambia
Mallya: alikwambia Kwamba aliondoa au Kutumbukiza Physically Kitu gani
Shahidi: Hakuna Kitu kama hicho Unachosema, kuwa alitoa chochote, Utaratibu Wa Kutunza Kielelezo Unajulikana, Kwa Utaratibu Wa Polisi Kielelezo Umapo Ki Seize unapaswa Umantain Kilivyo
Mallya: aliyekuletea alikwambia alifuata Utaratibu au Haku fuata Utaratibu huo
Shahidi: Ni Askari Polisi ni Imani yangu alifuata
Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba ajibu Swali Langu
Shahidi: Mheshimiwa Jaji swali linahitaji Maelezo,
Jaji: Nani sasa, Maelezo ya Wakili au Ya Kwako?
Shahidi: Mimi Naamini Kuwa Utaratibu ulifuatwa
Jaji: Swali lake Halipo Huko kama Utaratibu ulifuatwa au Lah Bali Je alikueleza
Shahidi: Mheshimiwa Jaji hakunieleza
Mallya: Ndiyo Jibu ndiyo Nilikuwa nayafuata
Mallya: Kwenye Kielelezo H Kuna Physical Damage inaonekana hapa, Kuna gaps, Je Macho yangu ya naona sawasawa
Shahidi: Condition Siwezi Kuzungumzia hapa
Mallya: Hilo Sijakuuliza, Nauliza Kuna Damage hapa Inaonekana, Je Kinachoonekana ni nini
Shahidi: Kinachoonekana ni Simu
Mallya: Siulizi simu hapa Mahakamani, usilete mahakamani michezo yako..
Mallya: Unachokiona ni Kitu gani
Shahidi: Ninachokiona ni Simu Mheshimiwa Jaji
Mallya: Ngoja Nichukue Simu F tulinganishe na H, Zote Umeleta Wewe, Swali langu hii yenye haya Ma gaps unahitaji?
Shahidi: Mhe Jaji Hizi ni simu Mbili tofauti, Siyo lazima zifanane..
Wakili wa Serikali: Mhe Jaji Wakili amebakia Muda Mrefu na Majibu yameshatolewa, Swali lake limeshajibiwa
Mallya: Mheshimiwa Jaji Swali langu halijajibiwa bado
Jaji: Muulize swali tena
Mallya: Kwenye Kielelezo H Kuna Ma' gaps, Je kitaalamu Unayaitaje?
Shahidi: Miye siwezi Kuongelea chochote
Mallya: Hii difference ya Kuwa hii ina button Kwenye simu na hii haina, unasemaje?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji siwezi Kuzungumzia kuhusu tofauti
Mallya: Kwenye Riport yako Kwenye Kielelezo F Je aina Positive Results..?
Shahidi: Ndiyo Ilikuwa na Positive Results
Mallya: Kuna Simu Ulizo letewa ukakuta Hazina Positive Results Kama Ulivyoletewa kwenye Terms of reference
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwa Mujibu wa Sheria Askari Polisi anaruhusiwa Kukamata simu.?
Shahidi: ndiyo Kwa Mujibu wa Sheria
Mallya: Kama Askari Polisi anataka Kujiridhisha Juu ya Kitu anachotafuta analeta Forensic?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Unafahamu Simu ni Personal Property ya Mtu?
Shahidi: Inaweza Kuwa Simu ya Ofisi
Mallya: Yapo Mazingira Mtu anaweza Kuwa na Simu Kama Mali yake Binafsi.?
Shahidi: Kama amenunua ni Mali yake Binafsi
Mallya: Je Yule ambaye amekamata kama Hajakuta Kitu anatakiwa kumrudishia Simu yake..?
Shahidi: Sifahamu
Mallya: Unafahamu Kwenye Simu ya Mtu Binafsi ambayo kanunua Kwa Pesa Yake, Inaweza Kuwa na Taarifa zake Binafsi?
Shahidi: Simu ya Mtu anaweza Kuweka Taarifa ambazo anahisi anaweza Kuhifadhi
Mallya: Kuna uwezekano Kuwa Mtu akahifadhi Taarifa au Nyaraka ya Utetezi kwenye Simu?
Shahidi: Sifahamu
Mallya: Taarifa Uliyompelekea huyo aliyekuomba Umfanyie Uchunguzi, Je akipokea Kwa Mkono au Kwa Email?
Shahidi akipokea Kwa Mkono
Mallya: Je alisoma hiyo Taarifa Yako ya Uchunguzi
Shahidi: Naamini alisoma
Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba 23 Samahani
Mallya: Shahidi Interest yangu Katika Riport Yako ni Ukurasa Wa Sita Unapozumgumzia Kuhusu Kielelezo A, B, C, D
Shahidi: Vielelezo Tajwa A, B, C, D hazina Taarifa Zenye Maudhui
Mallya: Kwenye Hicho Kielelezo namba C ulikuta ni Cha Nani
Shahidi: Ni Cha Khalfani Bwire
Mallya: Kwa hiyo Katika simu ya Khalfani Bwire hukukuta Jambo Lolote?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Ulifanya Uchunguzi Wako Lini
Shahidi: July 2021
Mallya: Ulikuja Kutoa Ushahidi wako lini
Shahidi: Juzi January 2022
Mallya: Kuna Interval ya Muda gani kati ya Wewe Kufanyia Uchunguzi Mpaka Kutoa Ushahidi
Shahidi: Usio Pungia Miezi Mitano
Mallya: Hiyo Content ambayo ulikuta negative Results upo wapi
Shahidi: Sikuona Haja ya Kuweka Kwa sababu sikukuta Kitu
Mallya: Bwana Bwire alikuwa anataka Negative Results ambayo Ingekuja Mahakamani Kuonyesha Kuwa Hakuna Maswala ya Ugaidi
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Nilipewa Terms of Reference, Kwa Hiyo Kama Haipo siwezi Kutoa
Mallya: Shahidi Umesha wahi Kupima Malaria
Shahidi: Hilo swali Limeingiaje hapa
Mallya: Kwa Sababu Wewe ni Mtu wa Laboratory na Malaria inapimwa Laboratory?
Shahidi: Sioni likihusiana
Mallya: Kwa Sababu Wewe ni Mtu wa Laboratory na Malaria inapimwa Laboratory
Shahidi: Sioni likihusiana
Mallya: Lina husiana Kwa Sababu Malaria Ukipimwa Wakikuta Negative Results wanakupa Majibu Yako
Shahidi: Kuna Baadhi ya Simu Zina Taarifa zaidi ya GB 20 huwezi Ku Print zote
Mallya: Je ulitoa taarifa Kwamba hukukuta kwa sababu ni Kubwa
Shahidi: Kwa sababu ni Out of Context
Mallya: Ulishajibu Kuwa Hukuona Haja
Shahidi: Siku Jibu hivyo
Jaji: Hapo Ndipo Mr. Malya Unapotuchanganya, Ni wapi Tutaona Huku uliza
Mallya: Nilikuwa namkumbusha Majibu Yake
Jaji: Basi Kama Unaulizwa Swali Hakuna Haja ya Kuongea Yote hayo
Mallya: Shahidi Nilisikia Unasema Mnatumia Legitimate Software Ku Updates yenu, Je Ulizungumzia Mnapewaje
Shahidi: Hapana Sikuzungumzia
Mallya: Mheshimiwa Jaji Naomba Barua ya Airtel na Ya Tigo
Mallya: Nakuonyesha Kielelezo P15 na Interest yangu ni Mtu aliyepewa hii Barua
Shahidi: Barua hii Imeelekezwa Kwa Kamishina wa Uchunguzi wa Kisayansi
Mallya: wewe sasa hivi ni Inspector Wa Polisi, Je Mwaka 2021 uliwahi Kuwa Kamishina wa Polisi
Shahidi: Mimi Sijawahi Kuwa Kamishina
Mallya: Kwenye hii Barua wapi Umekuwa Adressed.?
Shahidi: imekuwa Adressed Kwa Kamishina wa Uchunguzi Wa Kisayansi
Mallya: Naomba na ya Tigo
Mallya: Umesema Ofisini Kwenu Mkubwa wa Command ni Nani
Shahidi: Anaitwa CP SHABANI
Mallya: Kuna Departments Ngapi katika Forensic Beaural
Shahidi: Tuna Units Mbalimbali Ka Cyber crime ambayo Natoka Mimi, Toxicology, DNA, Pathology, Fingerprints, Ballistic, Documents, Crime scenes
Mallya: Kwa Mahesabu yangu ni Nane, Kwa Kiswahili zinaitwaje?
Shahidi: Kamisheni ya Uchunguzi Wa Kisayansi
Mallya: Zote hizi Ukubwa Wake Kwa Maana ya Commanding Ofisa wake ni CP SHABANI.?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Naomba uniseme Adress ambayo Tigo Wameitumia
Shahidi: UCHUNGUZI WA KISAYANSI
S. L. P 9094
DAR ES SALAAM
TANZANIA
Malya: naomba Mwenzangu Wakili Faraji Mangula aendelee
Mangula: Shahidi Pole na kuuguq Kichwa Siku ya Kwanza
Mangula: Ni sahihi ulisema Kuwa umesema Advanced Diploma ya Computer Science
Shahidi: Ndiyo
Mangula: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali, Ulielezea Kuwa Baada ya Masomo Ulipata Award gani
Shahidi: Nilisema nilikuwa napata Certificate
Mangula: Wakati Unafanya Uchunguzi Ulisema Ulikuwa una cheo Gani
Shahidi: Mkaguzi Msaidizi
Mangula: kwa sasa Una cheo Gani
Shahidi: Inspector
Mangula: Wakati Mawakili Wanakuongoza Hapa Mahakamani, Je ulisema Kuwa Ulipata Mafunzo gani Mpaka Ukapanda Cheo
Shahidi: Unakuwa Awarded siyo Kwa Kwenda Kozi
Mangula: Cheo chako umekipata wakati awamu ya 5 au ya 6?
Shahidi: Sijaelewa logic ya swali lako
Jaji: Swali la nani alikuwa Rais, unataka kujenga nini
Mangula: Mhe Jaji kuna premise nataka kutengeneza
Jaji: hiyo premises ndiyo utengeneze kupitia Rais aliye madarakani?
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Mahakama Ilisha wahi Kutoa Maelekezo Juu ya Kutaja Majina ya Watu ambao Hawapo Mahakamani
Jaji: nilitoa Maelezo Kuhusiana na Kutaja Majina ya Watu ambao Hawapo Mahakamani, lakini pia nataka Kujiuliza Kuhusu Kuuliza Maswali ya Rais wa Awamu ya Tano au Lah
Sasa Unachotaka hapo ni nini.?
Mangula: Ngoja Niulize Kwa Namna Nyingine
Mangula Naomba Kielelezo Namba 23,Shahidi Naomba Usome Kwa Sauti Kichwa Cha Habari cha Hicho Kielelezo
Shahidi Kamisheni ya Uchunguzi Wa Kisayansi, ya Makosa ya Kimtandao Chini ya Sheria ya Mtandao namba 14
Mangula: Je ni kifungu Kipi ambacho umekitumia?
Shahidi: Mimi siyo Mtaalamu wa sheria, Ila nilifanya kwa sheria ya mtandao
Mangula: Mwambie Mheshimiwa Jaji sasa ni kifungu kipi ulitumia
Shahidi: Mheshimiwa sikutumia kifungu
Mangula: Nikikupa hiyo sheria, unaweza Kunitajia kifungu ulichotumia
Shahidi: Mimi sina UFAHAMU WA MAMBO YA KISHERIA
Mangula: Kwa hiyo nyie Ofisini kwenye mnafanya bila ufahamu wa Sheria
Shahidi: Nishasema mheshimiwa SINA UFAHAMU WA SHERIA
Mangula: Fungua sasa Ndani, Ieleze Mahakama ni Kielelezo Kipi Ulichofanyia Kazi Ukagundua Kuna Makosa ya Ugaidi Uliyaona, Ni wapi Umeandika hivyo..
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Jibu linahitaji Maelezo, Mimi nililetewa tu Kufanya Uchunguzi.
Mangula: Kwa hiyo wewe hujui Kuwa Kuna Ugaidi au Hakuna Ugaidi kwenye hicho Kielelezo?
Shahidi: Sahihi
Mangula: bado unataka Mahakama ichukue Kielelezo Hiki Kama Kielelezo Cha Umuhimu?
Shahidi: Nimesema ni Kazi ya Mpelelezi
Mangula: Umesomeshwa na Serikali?
Shahidi: Ni Sahihi
Mangula: Na Umelipiwa Masomo Kwa Kodi ya Watanzania
Shahidi: Sahihi
Mangula: wewe Umesomea Udukuzi
Shahidi: Nimesomea Ethical Hacking
Mangula: Ulisema Mwanzo Kuwa Vifaa Vyako Vya Uchunguzi Vina Uadilifu
Shahidi: Ndiyo
Mangula: Na Kila Unachotaka Kwenye hiyo Simu, Mambo wako Unakuonyesha
Shahidi: Yes
Mangula: Kama Kuna video inakuomyesha.?
Shahidi: Inaonyesha Vile Vitu ambavyo Inaweza Ku Extract Kwenye Kielelezo
Mangula: Inakupa kila Kitu ambacho Kipo Kwenye simu?
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Mangula: Mheshimiwa Jaji Naomba Extraction Report
Mangula: Katika huo Mambo unaosema Ulikuwa upo Sawa Kukupa Kila Kitu, Ukisoma Kielelezo Cha Kwanza hicho namba 25
Mwambie Mheshimiwa Jaji kwenye hicho Kifaa Ulichofanyia Uchunguzi Kulikuwa na Content gani
Shahidi: Kukikuwa na Proxy Ya Chat ya WhatsApp
Mangula: Kulikuwa na Picha Kwa Maana Images
Shahidi: Picha Hakuna, Zipo Profile Picture
Mangula: ambazo ni za nani
Shahidi: Sijui za nani
Mangula: Katika hivyo Vielelezo ambavyo Vimepokelewa Mahakamani, Palikuwa na Mazungmzo ya Simu kati ya Watuhumiwa
Shahidi: Hakuna ila kwenye Kielelezo namba 26 zipo
Mangula: apewe Namba 26,,tuchagulie Mazungmzo Marefu Kuliko yote
Shahidi: Kuna Mazungmzo ya Dakika 9
Mangula: Bila Shaka Ndipo walikuwa wanapanga Ugaidi, Haya Mwambie Mheshimiwa Jaji Walizungumza nini hawa Watuhumiwa
Shahidi: Kuna Call Logs tu
Mangula: zile Sauti zipo wapi
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Kama Mahakama Yako itaniruhusu Kwa sababu za Ki Usalama nisijibu Hilo swali
Mangula: Swali langu ni Juu ya Watuhumiwa Ukiwa Mchunguzi wa Hizo Simu, Nauliza Mazungmzo ya Watuhumiwa Wale Wanne, Narudia Swali Sauti zao Watuhumiwa Zipo wapi ndugu shahidi?
Shahidi: Sababu za Kiusalama huwezi Kuzungumzia suala la Sauti
Mangula: Shahidi Nimesikia unasema Kuwa huwezi Kuzungumzia Kwa sababu ya Kiusalama, Je Sheria gani inakuzuia Usizungumzie hilo Suala?
Shahidi: Sijataja Sheria
Mangula: haya Sasa Mwambie Mheshimiwa Jaji, Sauti za Watuhumiwa Zipo wapi????
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Hazikuwa zinahitajika katika Terms Of Reference
Mangula: Ni sahihi nikisema Kuwa Katika Extraction Uliyo fanya, Kuna Vitu Uliviondoa sababu hazikuhitajika?
Shahidi: Swali linahitaji Maelezo, Mwanzoni Nilisema Kuwa Tunafanya Kwa Hatua tatu, Aquisation, Analysis na Extraction
Mangula: Kwa hiyo ni sahihi Kuwa Kwenye Mtambo Kuna Baadhi Ya Taarifa Hukutoa Sababu Hazikuhitajika?
Shahidi Wa Jamhuri: Kimya
Mangula: Kwa Mujibu Wa Kielelezo Namba 22, Mwambie Mheshimiwa Jaji Vitu gani Viliombwa Kwa ajili ya kufanyia Uchunguzi
Shahidi: Kwa Mujibu wa Barua yako Yenye Reference........
Mangula: Hoja ya Barua Ilikuwa unahitaji Ufanyie nini
Shahidi: Pamoja na Taarifa Hii Nakuletea Uchunguzi Niliofanya .... Mimi Inspector Innocent Ndowo
Mangula: Ni wapi Walikutaka Wewe Usitoe Sauti za Watuhumiwa?
Shahidi: Mimi nilifuata Terms of reference
Mangula: Nikisema Kuwa Wewe Inspector Ndowo na Viongozi Wako wa Polisi Kwa Makusudi Mliamua kuficha Baadhi ya Taarifa katika
Kesi hii kwa Maslahi yenu Itakuwa sahihi au siyo Sahihi Ukizingatia Kuna Taarifa Hazipo hapa?
Shahidi: Siyo Sahihi, Hatufanyi Kazi kwa interest zetu
Mangula: Fungua Kielelezo H, na Umwambie Mheshimiwa Jaji IMEI namba ya hicho Kielelezo Ni namba Ngapi Kwa Mujibu wa PF 145
Shahidi: Kwa Mujibu wa PF Hakuna IMEI namba
Mangula: Soma huo Mstari Wa Pili Kwa Sauti Umeandikwaje
Shahidi: Simu TECNO IMEI imefutika
Mangula: Wakati Unaongozwa Kwenye Ushahidi Ulisema nani aliyefuta hizo IMEI namba
Shahidi: Si Kuulizwa hilo swali
Mangula: Wewe unafahamu aliye futa hiyo IMEI namba
Shahidi: Simfahamu
Mangula: Katika hicho Kikaratasi Umeeleza IMEI namba Imefutwa Wapi.?
Shahidi: Sikusema
Mangula: ukiacha Kielelezo namba 35 ambacho kimechezewa na Watu wasiojulikana , Ni Kielelezo Kipi Kingine Mlichochezea
Shahidi: Hakuna Kielelezo Kilichochezewa
Mangula: Fungua Kielelezo namba 23, Mheshimiwa Jaji Namuonyesha Kielelezo namba 23
Mangula: Nataka Majibu ya Riport Yako ya Uchunguzi
Mangula: Mwambie Mheshimiwa Jaji ni wapi Katika Report Yako ya Uchunguzi Umeandika IMEI namba Imefutika
Shahidi: Hakuna Mahala Nilipo andika
Mangula: Nilisikia Unasema Ulichukua simu Ukiweka Katika Mtambo Wa Uchunguzi, Ule Mtambo utakuonyesha Kuwa Simu ni Original au Feki
Shahidi: Mtambo hauonyeshi Kuwa Simu ni Feki au Original
Mangula: Kitu gani Kinaonyesha kuwa Simu ni Feki au Original
Shahidi: Kitu nilichosema Kuna Kama zile Simu za Kichina, Mtambo una Operate kwa OS
Mangula: Kwa hiyo nini Kina onyesha ni FEKI Au ORIGINAL?
Shahidi: Nilichosema naomba Unisikie Vizuri, Mtambo una Option ya Kufanya Kazi hata Kwa kutumia Chip
Mangula: Mheshimiwa Jaji naomba NIISHIE Hapo
Shahidi: Samahani Mheshimiwa Jaji NAOMBA KWENDA WASHROOM (CHOONI)....
Shahidi anatoka na kuelekea katika vyoo vya nje..
Mahakama Ipo kimya inasubiri arejee kizimbani.
Shahidi amerejea kizimbani kutokea kwa fasii ya chooni.
Kihwelo: Shahidi Nilisikia Unazungumzia Kuhusu Celebrite Physical analyser Je ni Software Au.?
Shahidi: Ni software
Kiwhelo: nani alifanya Development ya Software
Shahidi: Celebrite Wenyewe
Kiwhelo: Nilisikia Umesomea Kuhusu Penetration Test
Shahidi: Ndiyo
Kihwelo: Je Penetration Testing, Ni sawa na Fazzing
Shahidi: Sifahamu
Kiwhelo: Je Wakati Unafundishwa Kuhusu Penetration Testing, Walikufundisha Kuhusu Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao (High Tech Cyber Attack)
Shahidi: Sijafundishwa hiyo
Kiwhelo: kwakuwa Ujafundisshwa kuhusu Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao, Ni sahihi Celebrite Ingeweza Kuingiliwa
Shahidi: Haiwezi Kuingiliwa
Kiwhelo: pale Ofisini kwenu ni nani Network Provider
shahidi: ni TTCL
Kiwhelo: Ni sahihi Kuwa Network Services Provider anaweza Kuingilia Data Zako
Shahidi: Hawezi
Kiwhelo: Nyinyi Kama Jeshi la Polisi Mnatumia Nini Kujilinda na Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao
Shahidi: Naomba nisijibu sababu za Kimtandao
Kiwhelo: Nilisikia Kuwa unazungumzia kuhusu DECORDING
Shahidi: Ndiyo
Kiwhelo: Shahidi Pegasus Technology ni Moja ya Technology mnayotumia?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji naomba Nisijibu Sababu za Kiusalama
Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji naomba anijibu sababu Baadae Nitataka kujua Intergrity ya Technology Wanayotumia
Jaji: Shahidi ame raise suala la Security, Au mnasemaje Upande wa Serikali?
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shahidi amesha Sema kuwa awezi Kusema Sababu za Kiusalama, Sisi tunaona Sababu hizo ni Valid, lakini siyo kutulazimisha
Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji Shahidi Wakati Shahidi anataka Ushahidi Wake Jana Alitaja Hapa Kuhusu Microsoft na Celebrite, alitaja hizo Mbili Maana yake ameshataja
Jaji: Sasa Shahidi Kaja na suala la Security kwa hii Uliyotaja
Kiwhelo: Basi Ngoja Niendelee na Kingine, Shahidi Wakati Una Extract Data Kwenye Celebrite Ulihifadhi Kwenye nini
Shahidi: Nili hifadhi Kwenye Computer
Kiwhelo: Vipi kuhusiana na Usalama wa computer yenyewe
Shahidi: Kimya
Kiwhelo: Uliandika Taarifa ya Simu Nne..?
Shahidi: Simu zote Nane
Kiwhelo: Siku ya Tarehe 09 July 2020 Uliingia Saa ngapi
Shahidi: Niliingia Saa 1 na Nusu Asubuhi
Kiwhelo: na Ulitoka Muda gani
Shahidi: Unatoka Muda wowote, hupangiwi kwa Sababu tunafanya Kazi Masaa 24
Kiwhelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji ulikuwa unaandika summary kisha unafuata extraction
Shahidi: Siyo sahihi
Kiwhelo: Soma hapo kwenye report yako
Shahidi: Inaanza na summary kisha extraction
Kiwhelo: Kwa hiyo imeanza na summary
Shahidi: Ni sawa, imeanza na Summary
Kiwhelo: Tuzungumze Kidogo Kuhusu Kampuni ya CELEBRITE Ukasema Kuwa Ni Moja ya Kampuni inayodevelop Software
Je unafahamu Celebrite Ni Kampuni Ya Kijasusi wa Kidigitali ya Nchi Israel
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kiwhelo: Je Unafahamu Kuwa Hiyo Kampuni inahusishwa na Unyanyasaji wa Waandishi Wa Habari na Wana Harakati Duniani
Shahidi: Sifahamu
Kiwhelo: na Je Unafahamu Kuwa Celebrite Mashine Inaweza Kuingiliwa.?
Shahidi: Haiwezi Kuingiliwa
Kiwhelo: Je Nitakuwa Sahihi Nikisema Kuwa Celebrite Mashine Inaweza Kuingiliwa na Kubadili Taarifa Zilizotamgukia na zilizopo
Shahidi: Hapana Siyo Sahihi
Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji naomba nimkabidhi Shahidi Nyaraka asome Kuhusiana na Celebrite
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba wakili azuiwe Kusoma hiyo Nyaraka
Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji Kwa ajili ya Muda nitaomba Kuachana na hiyo
Naomba nipatiwe P23 na P35
Naomba Sasa Nimkabidhi Shahidi
Kiwhelo: naomba Unisomee description hapo Juu
Shahidi: Imeanza Neno Station, Date 05 August 2020, CF imeandikwa. Simu Imeandikwa Tecno IMEI imefutika, Ilipatikana Maungoni (Mwilini)
Kiwhelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji Wewe Umetoa wapi Namba kwa Mujibu wa IMEI namba ambayo Imefutika
Shahidi: Inawezekana Physically Isionekane ila akuna Namna unaweza Kuona, au Kwenye Barua
Kiwhelo: hiyo Barua Ipo Hapa Mahakamani
Shahidi: Haipo Mahakamani
Kiwhelo: Ulizungumzia Kuwa IMEI namba ulitoa Kwenye Barua.?
Shahidi: Nili zungumza Kwa Ujumla
Adv. @FrederickWakili
: Mheshimiwa Jaji nimeishia hapo na naomba kurudisha vielelezo
Anasimama Wakili Msomi Peter Kibatala.
Kibatala: Inspector Ndowo Mambo Vipi
Shahidi: Salama
Kibatala: Siku ya Kwanza Uliomba Kusitisha Ushahidi Kwa sababu uliumwa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Ulipitia Hospitali.?
Shahidi: Nilienda Ofisini, nikarudisha Vielelezo
Kibatala: Kwa hiyo Baada ya Kutoka Hapa Hukwenda Hospitali Moja kwa Moja
Shahidi: Si kwenda Hospitali Moja Kwa Moja
Kibatala: Ulisema Kichwa Kilikuwa Kinafanya nini Vile
Shahidi: Kilikuwa Kinaniuma Kadri nilivyokuwa natoa Ushahidi
Kibatala: Na Kwa hiyo Ofisi Yako Ilikuwa wapi Vile
Shahidi: Posta
Kibatala: na Baada ya Hapo Ukaenda Hospitali Wapi
Shahidi: Kilwa Road
Kibatala: Twende Kwingine, Shahidi Je Uliwahi Kufanyiwa Training na Watu wa CELEBRITE
Shahidi: Yes Wawakilishi Wao
Kibatala: Unakumbuka Kozi Mbalimbali Ulizo taja Siku ya Kwanza Ukiwa unataja Mafunzo mbalimbali uliyopata.
Kibatala: Je kwa Kumbukumbu yako Ulitaja Mafunzo Yaliyo endeshwa na Celebrite au Wawakilishi wao
Shahidi: Jibu Lina hitaji Maelezo, Nilitaja Kozi Mbalimbali na Baadhi walitoka Nairobi.
Kibatala: Maelezo Ambayo Umeyatoa, Kuna Mahali Umesema Kuna watu Walitoka Nairobi Kuja Kuku train Kuhusu Celebrite.%?
Shahidi: Nilipata Kozi Mbalimbali, sikudadavua
Jaji: Swali Lake Ulisema Kuwa Kuna Wataalamu Kutoka Nairobi Kuja Kuku Fundisha Kuhusiana na Celebrite.
Shahidi: Sikutaja Mheshimiwa
Kibatala: Katika Maelezo yako, Ulisema Ulienda Training Mahala Mbalimbali, Je Ulisema Kuwa ulienda Israeli.?
Shahidi: Israel Sikutaja
Kibatala: Unafahamu Kuwa Makao Makuu ya CELEBRITE Yapo Nchini Israel
Shahidi: Nafahamu Yapo Israel
Kibatala: Je Unafahamu Kuwa Israel Kwa Wivu na Technology yao Hawaja Outsource kwa Mtu Kuhusiana na Training wala Technology?
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kuwa Nairobi Hakuna Wakala Wa CELEBRITE?
Shahidi: Hapana Sifahamu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Wakili anataka Misamiati Migumu ya Technology shahidi anaweza asijue ni nini Kinaongelewa.
Kibatala: Mheshimiwa Jaji hakuna hoja hapo, Mbona shahidi anajibu, Eti ndugu shahidi, ni kweli huelewi Kitu?
Shahidi: Ndiyo sielewi
Kibatala Kwanini sasa ulikuwa unajibu?
Shahidi wa Jamhuri: Kimya
Kibatala: unafahamu sababu ya Wivu Wa Technology, Israel Hawana Mwakilishi wa CELEBRITE Duniani katika Nchi yoyote
Shahidi: Yupo Nairobi
Kibatala: Anaitwa Nani
Shahidi: SAM
Kibatala: Unafahamu Kuwa Technology ya Pegasus ni Technology ya Israel Pia
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: una Cornfirm kwetu bila kwenda kwenye details kuwa Jeshi la Polisi mnatumia pegasus?
Shahidi: Naomba nisijibu hilo swali kwa sababu za Kiusalama
Kibatala: Baadae Nitakuja hapo na nitakutaka kwa lazima ujibu hilo swali, kwa sasa ngoja niende kwingine.
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Celebrite unatumia Software Mbili UFET na physical analyser?
Shahidi: Ndiyo ni baadhi ya product za kwake
Kibatala: UFEN kazi yake I naingia katika Simu au Computer kisha Inatengeneza Back up
Shahidi: Inategemea na level ya Extraction Unayofanya
Kibatala: Ni sahihi Kuwa katika kazi Uliyo kuwa unafanya unaunganisha Simu Kwa Kutumia Cable kisha Celebrite inachofanya Kwa kutumia UFEN Kutengeneza Back up
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kuwa physical analyser Inafanya kazi Kwa Ku arrange Taarifa In Chronological Order
Shahidi: Sahihi ila inategemea Level
Kibatala: Jaji akimaliza Ku Rekodi Mwambie Kuwa Kazi ya Physical Analyser Kama Software Ni kuyapanga Mafaili Kwa Mchunguzi ili Ku Make Sense na hiyo Process inaitwa PASSING
Shahidi: Naomba nijibu kwa Maelezo Kuwa Physical analyser, Inafanya kazi 3 ila Kwa Ujumla Ndiyo PASSING
Kibatala: Katika Report Yako Kuna Item Ya PASSING
Shahidi: Kama Software Include hizo Taarifa zake, Basi itaonekana
Kibatala: Basically Physical analyser haina Jipya Zaidi ya kupanga Mafaili
Shahidi: Hapana Physical analyser ni zaidi ya hapo
Kibatala: Tofauti Yake nini, Kama Unaingia Kwenye simu yangu ya Telegram na kisha unapamga Mafaili
Shahidi: Ni zaidi ya hapo kwa sababu ina Uwezo Kuwa Kufanya Back Up Kwa Vitu Vilivyofutwa
Kibatala: Physical ANALYSER inaweza za KubadiliSha Chochote
Shahidi: Hapana
Kibatala Physical analyser Ina extract
Shahidi: Hapana
Kibatala: unapokuwa na Kifaa kama Simu Kutoka Kwa DCI Nini Kilianza Kati ya kutumia UFEN Kufanya Extraction au Physical Analyser Kupamga kazi yako
Shahidi: Nilianza Kutumia UFEN
Kibatala: Wewe Umeletewa 8 applications phones, Je zile Data zilizokuwa katika Hizo phones, Je ni Software gani zilikuwezesha Kuingia Kwenye simu na Kusoma Meseji
Shahidi: Ni Physical analyser
Kibatala: Sasa Mbona Mwanzo Ulikataa, Wacha sasa Ikae Hivyo
Kibatala: Jana Ulizungumzia Kuwa huwezi Ku impose Vitu Vyako Kutoka Nje,
Shahidi: Ndiyo WRITE BLOCK
Kibatala: Unafahamu Kuhusu Software ya CELEBRITE Kuhusu Soft Write Block?
Shahidi: Hiyo sifahamu kwa kweli
Kibatala: Ni kweli au siyo Kweli Kuwa Celebrite Soft Write Block Ndiyo inayomzuia Mtu Kuingilia Mashine ya CELEBRITE
Shahidi: Hiyo sifahamu
Shahidi: Na Bado Ukitaka Kutuaminisha Kuwa Mashine zenu zina Intergrity?
Shahidi: Ndiyo Sijataja
Kibatala: Je ulitaja Jana software zaidi ya Mbili
Shahidi: Sikutaja
Kibatala: Ulizungumzia Forensic Cables,
Shahidi: Sawasawa
Kibatala: Ni Cables kama za USB tuh au Kuna tofauti
Shahidi: Ni Tofauti Kabisa
Kibatala: Inasifa gani Kitaalamu ambayo ni zaidi za USB
Shahidi: Ni Cable Zenye namba pembeni
Kibatala: Je Hapa Umetaja Namba za Cables
Shahidi: Hapana
Kibatala: Hizi Simu ambazo wewe Ulifanyia Extraction, Makers ni Tofauti
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Jana Nilisikia Unasema wewe siyo Mpelelezi ni Mchunguzi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ni wapi au Kwenye Instrument ipi Inatofautisha Mpelelezi na Mchunguzi?
Shahidi: Ukija Ofisini Utajua
Kibatala: Mpaka Nije Ofisini kwenu, Vipi PGO Inatambua?
Shahidi: Sijui
Kibatala: PGO ya 8 Sehemu Ndogo ya 4 inasema Kuwa Ofisi Ya DCI inagawanywa katika Divisheni Nne, Mmoja wapo ndiyo hiyo ya Forensic Beaural
Shahidi: Sijui ni PGO gani
Kibatala: zote mbili
Shahidi: Mimi ninachojua Forensic Beaural ni Imtependent Beaural
Kibatala: na Ndiyo Maana ni Kuuliza Unapata wapi Mgawanyo huo
Shahidi: Ukienda Ofisini Makao Makuu ya Jeshi la Polisi au Dodoma
Kibatala: Mhe Jaji naomba Kielelezo 6,7,
Kibatala: angalia Maneno ya DCI Katika hiyo Barua. Unafahamu Kirefu chake?
Shahidi: nimesahau kidogo
Kibatala: Mimi nikikwambia kwamba kirefu cha hayo maneno uliyoandika wewe kwenye barua yako ni DIRECTOR OF CRIMINAL INVESTIGATION?
Shahidi: Sijui mpaka Nipate Mwongozo Wa Wakubwa zangu
Kibatala: Juu pia maneno ya DFSI kuwa ni DIRECTORATE OF FORENSIC SCIENCE INVESTIGATION?
Shahidi: Sifahamu mpaka Nikumbushwe na wakubwa zangu
Kibatala: Na Bado wewe Unasema ni inspector wa Jeshi la polisi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala Mheshimiwa Jaji muda wetu wa kupumzika umefika, labda nipate mawazo kutoka kwa wenzetu nina maswali mengi bado
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Tu' break dakika 45
Wakili Peter Kibatala Saa Saba na Dakika 45
Jaji: Tuna break kwa dakika 45 tutarudi saa saba na dakika 45
====
Jaji ameingia Mahakamani Muda huu Saa 8 na Dakika 5
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani Muda huu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Quorum yetu ipo Vile vile
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji na sisi Quorum yetu ipo Vile vile
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba Nikumbushwe Nilipo Ishia
Jaji: ulimuuliza Kuwa Bado yeye ni Inspector akajibu Ndiyo
Kibatala: PGO ya 9 inasema Subject to the Direction of the DCI
Je wewe Unapata Mwanga kuwa Ofisi ya Forensic Beaural Bado ni Ofisi inayojitegemea
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji tunaomba tujiridhishe
Kibatala: wacha nibadili swali
Kibatala: Shahidi ulipokea Barua Kutoka Kwa DCI lini
Shahidi: 13 August 2020
Kibatala: Kwakumbu Kumbu yako Version ya PGO ipi ilikuwa Inafanya Kazi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: kwa hiyo nikikusomea PGO ya wakati Unapewa Barua, ilikuwa Inatumika ambayo ni Ile inayosema Mpo Chini ya DCI?
Shahidi: Naomba Kutoa Maelezo, Mimi siyo Msemaji wa Jeshi la Polisi
Kibatala: na hilo nalo ni Jibu, Sijui Kwanini upo Hapa
Kibatala: Katika PGO ambayo ulikuwa unafanyia kazi wakati huo 9(c) Vifaa Kama Simu Vimetajwa?
Shahidi: Mhe samahani wakili NIMEMWAMBIA sifahamu KUHUSU PGO LAKINI NAONA MWENZANGU KAJIKUTA KWENYE PGO TU..
Kibatala: Nivumilie tu, mimi nisipokuuliza swali kuna sehemu nitaulizwa
Kibatala: Katika Majukumu yako Ulifanya Kazi Baada ya Kupata Barua Kutoka kwa DCI
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: na Kilicho Pelekea Wewe Kufanya Uchunguzi yalikuwa ni Maombi Kutoka kwa DCI
Shahidi: Sahihi
Kibatala: na Maombi hayo yalikuwa na Terms of Reference
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Ofisi ambayo inajitegemea Kimamlaka Je Inaweza Kupokea Terms of reference katika Utendaji wake wa Kazi
Shahidi: Sitaki Kujiunga katika Maneno yako, lakini Uchunguzi Ulifanyika Ujue Kuna Sababu ulizopewa
Kibatala: Bado Haujajibu swali, Je Ofisi Ambayo inajitegemea Kimamlaka Je Inaweza Kupokea Terms of reference
Shahidi: Barua Zinapokuja, na Hatujui lolote linaloendelea
Kibatala: Swali langu lipo pale pale Kwamba Je Taasisi ambayo inajitegemea inaweza Kupewa Terms of reference
Shahidi: Kesi husika Inapokuwa kwetu, Kuomba Kufanya Uchunguzi, Lazima. Ije na Barua na Lazima isema Vitu ambavyo inaomba Ichunguze
Jaji: Taasisi ambayo inajitegemea inaweza Kupewa Hadidu za Rejea?
Shahidi: Ndiyo tunavyofanya hivyo hivyo
Kibatala: Wewe Kwa Ufahamu Wako, Taasisi inayofanya Uchunguzi Inaweza Kukusanya Ushahidi
Shahidi: Sijasema Kuku Sanya Ushahidi
Kibatala: Ulisema Nini
Shahidi: nilisema Kuandaa Ushahidi
Kibatala: Taasisi inayofanya Uchunguzi Inaandaa Ushahidi au Findings
Shahidi: inaandaa Findings kwa ajili ya a Kutumika kwenye Ushahidi
Kibatala: Wewe in Inspector Wa Forensic au Inspector Wa Jeshi la Polisi
Shahidi: Ni Inspector Wa Jeshi la Polisi
Kibatala: Unapofanya Uchunguzi, unafanya Uchunguzi wa akosa la Jinai au Uchunguzi Wa Vifaa
Shahidi: Nafanya Uchunguzi wa Vifaa
Kibatala: Kwa hiyo Unafanya Uchunguzi Wa tuhuma Za Jinai au Hufanyi
Shahidi: Sisi Kazi yetu ni Kuchunguza Vile Vifaa Vilivyotumika katika Jinai
Kibatala: Katika kesi hii wewe ulichunguza tuhuma Za Jinai au Lah
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Vifaa Vinavyo kuja Ofisini, is a must Vifaa Vile na Namba ya Kesi husika, Kwa hiyo Jinai Wanaopeleleza Ni Wa pelelezi
Kibatala: kwa hiyo wewe Unachaguza tuhuma Za Jinai au Lah
Jaji: amesema anachunguza Vifaa ambavyo Vinahusishwa na Jinai
Kibatala! Okey any way, Twende Kwenye Barua ya Tigo Soma
Shahidi: "Ofisi Inafanya Uchunguzi Wa Tuhuma Za Jinai....."
Kibatala: kwa Mujibu wa Barua hiyo uliyoandika Wewe Mwenyewe Ulikuwa unachunguza Tuhuma Za Jinai
Shahidi: Ofisi yangu hai Chunguzi Tuhuma Za Jinai
Kibatala: hiyo Barua uliyoandika wewe Kwenda Tigo, na Majibu ya Barua ya Tigo na Vielelezo Kutoka Tigo ni sehemu ya Riport Yako au Siyo sehemu Riport yako
Shahidi: Ni sehemu ya Riport yangu
Kibatala: Ile Originating letter Kutoka Ofisi ya DCI ipo au Haipo Hapa Mahakamani
Shahidi: Hapa Mahakamani Haipo
Kibatala: Shahidi hapa Kuna namba zimeandikwa CD IR 2020..... Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa hizo ni Reference kutoka Forensic au Kutoka Kwa DCI
Shahidi: Hizo ni Reference namba Kutoka Ofisi ya DCI
Kibatala: ambazo hizo hizo Uliwaandikia Tigo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Shahidi Ni sahihi Ume nukuu Sheria ya Makosa ya Mtandao Kifungu cha 34
Shahidi: Ndiyo Niliandika
Kibatala: Tigo walikuwa na nafasi ya Kukataa
Shahidi: Ukisoma Sheria Utajua
Kibatala: Hii Barua Kaandika nani?
Shahidi: Mimi Mwenyewe
Kibatala: Je unafahamu hicho Kifungu ni Kifungu Pelelezi?
Shahidi: Sijui
Kibatala: Kama Tigo Wasingewapa hizo Taarifa Mgewachukilia Hatua?
Shahidi: Kwanini uongee Kitu ambacho akijatokea
Kibatala: Je Mahakama Ikuchukulie wewe ni Afisa Wa Polisi Makini?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Barua Kutoka Tigo ambayo Ulitoa kama Kielelezo hapa Mahakamani, Uliwahi Kuiona?
Shahidi Ndiyo Niliwahi Kuiona
Kibatala Na Ukafanyia Uchunguzi Wako
Shahidi ndiyo
Kibatala Nenda Kielelezo namba P7 some Kumbukumbu namba iliyotajwa hapo
Shahidi CD/ IR/ 2007/ 2020
Kibatala Hilo ndiyo Jalada Mama Kutoka Ofisi ya DCI
Shahidi Ndiyo
Kibatala Kama Usingeona hii namba ya Jalada ungefanyia Uchunguzi?
Shahidi: kimyaa
Kibatala: Nenda Barua ya Tigo, Soma Jalada walilo kujibu pale
Shahidi: CD/IR/2097/2021
Kibatala: Inafanana au Inatofautiana?
Shahidi Inatofautiana sababu ya Typing Error
Kibatala: Sijakutuma utaje sababu hala, Wewe sema Imefanana au haijafanana
Shahidi: haijafanana
Kibatala: Katika Barua Yako inasema 2020 na Barua ya Tigo inasema 2021, Je Ipo wapi Barua ya DCI Kuondoa huu Mtanziko?, Umetoa Mahakamani Kama Kielelezo
Shahidi: Barua sijaitoa Mahakamani
Kibatala: Hii Barua Kutoka Tigo ya Tarehe 01 July 2021, ulipokea wewe Binafsi
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulimwambia Jaji Nani alipokea pale Ofisi ya Forensics
Shahidi: Hapana Sikusema
Kibatala: Wewe ni Inspector wa Jeshi la Polisi unafahamu Chain of Custody?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala Ulimwambia Jaji ulipoitoa hii barua?
Shahidi: Nishajibu hilo
Kibatala: Huyu NAFTALI J MANTAMBA yupo au alikufa?
Shahidi: Yupo
Kibatala: yule Kamishina Wenu anaitwa Nani Vile?
Shahidi CP SHABANI HITI
Kibatala: Je Ulimwambia Jaji Kwamba, Wakati Unaandika Barua, Yeye Kamishina Alikuwa anafahamu au hafahamu?
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Ulimwambia Jaji Wakati Bwana NAFTALI J MANTAMBA Wakati unasaini Barua hii SHABANI HIKI ALIKUWA Magonjwa au Lah
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Je Ulimwambia Jaji Kuwa upo familiar na Sahihi ya Bwana NAFTALI MANTAMBA, JE Ulimwambia Hukumwambia
Shahidi: Sikusema Mheshimiwa Jaji
Kibatala: Shahidi Kuan Kielelezo namba P8, Ambapo Kuna Rekodi ya Mihamala Kutoka Namba Fulani Kwenda Namba fulani Ambapo wewe Uliombea namba 0719931389
Shahidi: Naweza Kuelezea kama Nimavyoona
Kibatala: Kwenye Rrport yako Umesemaje
Shahidi: Kwa Mujibu wa Report ya Tigo
Kibatala: Nini primary Source kati Mhamala Wa Tigo au Riport yako wewe
Shahidi: Mimi sijaelewa
Jaji: liweke Vizuri Swali
Kibatala: Ipi ni Primary source kati ya Taarifa ya Tigo na Report Yako
Shahidi: Primary Source ni Report Kutoka Tigo
Kibatala: Kwa Maana hiyo ufahamu Kiasi cha Fedha TSh 500,000 pesa hiyo ilipotoka?
Shahidi: Sender na Receiver anaonekana
Kibatala: Unafahamu Kitu kinaitwa Collection Akaunti au Wallet?
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: kwa hiyo Kwenye Muamala Huo wanaoweza Kuzungumzia zaidi ni Airtel?
Shahidi: Airtel ndiyo wanaweza Kuzungumza
Kibatala: Hiyo namba, Ilikuwa ni sehemu ya Terms of reference Uliyopewa na DCI?
Shahidi: Ndiyo Kutaka Miamala Ya Fedha
Kibatala: Katika originating later ilisema Pamoja na Taarifa zingine, ilikupa wigo Mpana
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa katika Uchunguzi Wako wa Vifaa, ambacho wewe Uliona ni Kiashiria cha Kutenda Makosa ya Ugaidi
Shahidi: Nilichokiona Ndicho nilichokitoa
Kibatala: Katika Uchunguzi Wako Uliona Mawasiliano yoyote yanamtaja Mtu anaitwa Sabaya
Shahidi: Terms of reference Hazikuelekeza Kumtafuta Sabaya
Kibatala: Katika Uchunguzi Wako Uliona Popote Watu wanapanga Kufanya Ugaidi
Shahidi: Mimi sikuelekezwa Kutafuta hilo
Kibatala Katika Uchunguzi Wako wote, Uliwahi Kuona au Kusoma Wakati Wa Extraction Watu wakipanga Kulipua Madaraja
Shahidi: Kimya
Kibatala: Wakati Unafanya Extraction Kuna Mahala Popote uliona Mawasilisho watu wamepamgwa Kuandaa Maandamamo Nchi Nzima
Shahidi: Sikuelekezwa
Kibatala: Uliwahi kuona mawasiliano katika Subject Phones wakizungumzia bunduki aina ya A5340 aina ya Luger?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji ananiuliza mambo ambayo sijafanyia kazi
Kibatala: Nakuuliza kuhusu miamala, Je Kuna Telegram text, WhatsApp, au SMS Umeona meseji kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya kutenda ugaidi?
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Katika meseji zako kuna sehemu ina neno SABAYA?
Shahidi: HAKUNA
Kibatala: Tuambie Muamala upi wewe kama Inspector uliona watu wanapanga tendo la kihalifu....
Shahidi: Hakuna terms of reference yenye Jambo hilo
Kibatala: Kwa uchunguzi wako wewe ungekuta taarifa za kupanga uhalifu, ungeacha kuandika kwenye report yako kwa sababu haujaambiwa kwenye terms of reference?
Shahidi: Mimi ni Askari Polisi, kama ningekuta meseji za kupanga uhalifu ningeweka kwenye report yangu.
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba nipewe Kielelezo namba 24,25, 26 na 27
Kibatala: Shahidi Nakuonyesha Kielelezo namba P25
Kibatala: Unakumbuka Siku Unaandika Covering Letter
Shahidi: ilikuwa Tarehe 09 July 2021
Kibatala: Ilikuwa Saa ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Kwa Mujibu Ushahidi Wako Wa awali ulisema Vifaa Vilichukuliwa Tarehe ngapi?
Shahidi: Tarehe 10 July 2021
Kibatala: alikuja Kuchukua nani
Shahidi: Inspector Swila
Kibatala: ulimkabidhi Vipi.?
Shahidi: Alifika pale Nikamkabidhi
Kibatala: Je Uliandika item Moja Moja akasaini au alichukua Zote akaondoka?
Shahidi: Kwenye Kitabu Kuna sehemu anajaza Pale, kina Items Zote.
Kibatala: Wewe Uliandika wakati Unamkabidhi?
Shahidi: Utaratibu Wa Kwetu Lab Namba, Unapoingia Unasaini, Kuna entry Maalum
Kibatala: Hizi Simu Nane, ambazo zilizokuwa na Taarifa Ulipokea Tarehe ngapi
Shahidi: Tarehe 13 August 2020
Kibatala: na ulipozipokea kwa Utaratibu wenu wa Forensic Ukaandika Kwenye Hicho Kitabu. Kwenye Kitabu Cha Maabara ulisaini?
Shahidi: Utaratibu Ndivyo Ulivyo
Kibatala: Nani alileta Hizo Simu Maabara
Shahidi: Goodluck
Kibatala: Goodluck alipokabidhi alisaini au Hakusaini?
Shahidi: anatakiwa Kusaini Siku anapokuja Kuchukua
Kibatala: na aliyekuja Kuchukua ni nani
Shahidi: Inspector Swila
Kibatala: Na Kuchukua anakuja Kufuata Mtu yoyote au Aliyekabidhi?
Shahidi: aliyekabidhi
Kibatala: Na bado ulimpatia Inspector Swila Pamoja na Kuletwa na Goodluck?
Shahidi: Kimya
Kibatala: Register Ya Siku hiyo Ipo wapi?
Shahidi: Ipo Ofisini Maaabara
Kibatala: umemuonyesha Jaji
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Register Ile imeungua au ni Kubwa sana? Ulimwambia?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji report Creation time ilikuwa Muda gani?
Shahidi: Ilikuwa Tarehe 09 July 2020
Kibatala: Wakati Wa Ushahidi Wako Ulisema Kuwa Ulifanya Kazi hadi Saa Ngapi
Shahidi: Sikuulizwa
Kibatala: Kwa kuwa Hukuulizwa Jaji anajua au Hajui?
Shahidi: Hajui
Kibatala: Extraction ikifanyika lini?
Shahidi: Tarehe 07 July 2020
Kibatala: Extraction time ilikuwa Lini
Shahidi: Tarehe 09 July 2020
Kibatala: Kuna Tofauti ya Siku Ngapi
Shahidi: Kama Siku Moja
Kibatala: Ulimwambia Jaji Kwamba Kuna Delay ya Siku Moja na Data ikiwa Secured
Shahidi Sikueleza hilo
Kibatala: Tafuta Item 89 Mahala imeandikwa ICCID, Je ni Kitu gani
Shahidi: ID ya Kwenye Simu
Kibatala ID ya Kwenye Simu au ID ya Sim Card
Shahidi : ID ya sim Card
Kibatala: Je Ipo Katika Riport Yako au Haipo
Shahidi anatafuta.
Kibatala: angalia Ukurasa Wa Pili
Kibatala: Hiyo ICCID Unakubaliana ni ya Zain?
Shahidi: Nimeona Ndiyo
Kibatala: Katika Kielelezo Cha P25 ni Kweli imeishia na F Ndogo?
Shahidi: Ndiyo ipo
Kibatala: angalia na Kielelezo Kinachofuata, Kipo?
Shahidi: Hakipo
Kibatala: ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa ICCID ni Namba siyo Herufi?
Shahidi: Sikuulizwa
Kibatala: Kwa mujibu wa ICCID yako hapo, Ni ya Simcard la mtandao gani
Shahidi: Ni ZAIN..
Kibatala: Tangu uanze kutoa ushahidi hakuna sehemu umetaja neno ZAIN
Shahidi: Kimya
Shahidi MTN
Kibatala Unajua NI Mtandao wa Nchi Gani
Shahidi: Sijui
Kibatala: hujui Kwamba ni Mtandao Wa South Africa?
Shahidi: Hapana Sijui
Kibatala: Ulimtajia Mheshimiwa Jaji, kuhusiana na MTN
Shahid! i Hapana Sijamwambia
Kibatala: Je ulitoa ufafanuzi Kuhusu Crossing references namba za Divices Dhidi ya Namba ya Kwenye Simu
Shahidi: Si Kuulizwa Swali
Kibatala: Kama Hukuulizwa ulitoa Ufafanuzi au Hukutoa
Shahidi: Si Kuulizwa Kama Ningeukizwa Ningetoa
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi Wako Ulisema UFEN Version auliyotolea Ushahidi Ilikuwa namba Ngapi
Shahidi: UFED 7:4:4
Kibatala: Soma Ukurasa Wa 26 Chini Kwenye File system One, UFED ngapi
Shahidi: 7:4:0
Kibatala: Ulizungumzia hiyo jana
Shahidi: Ndiyo Nilitaja Jana
Kibatala: Leo Nimekuuliza Ukataja Version Ngapi
Shahidi 7:4:4
Kibatala: na Hizo Version Mbili Ulimfafanulia Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Si Kutoa Ufafanuzi
Kibatala Kwakuwa hii Taarifa ni Self Generated, Soma Extraction Process Discription pale Imaposema Kuwa Application...............
Unakumbuka Nilikuuliza hili swali Mwanzo
Shahidi Nakumbuka
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Application ilifanyiwa Kwa Back Up Android
Shahidi: Ndiyo Ilifanyika
Kibatala: Ulitoa Ufafanuzi Kuhusu Down Graded Area ya Version
Shahidi: Hapana Sikutoa Ufafanuzi
Kibatala: Baada ya Kufanyika Down Grading Ilikuweza EFED na Celebrite Physical Analyser, Je ulifafanua Kwa Jaji Kuhusu Storation
Kibatala: Twende Kwenye Plug inns, Contacts and References Je Ulifafanua kuhusu hilo
Shahidi: Hapana Sijaelezea
Kibatala: Nilikuuliza Kuhusu Forensic Cables, Ukasema Inategemea nini
Shahidi: Nilisema Inategemea
Kibatala: Shika Vielelezo Hivi Vinne, Mwambie Mheshimiwa Jaji Ulifanya Kwa Kutumia Device
Shahidi: Cable namba 100, Techno DA2
Kibatala: Nenda Kielelezo na P25 Ulitumia Forensic Cables zipi na Device Ilikuwa Ipi
Shahidi: Hapa Mheshimiwa Hakutaja Cable iliyotumika
Kibatala: ilikuwa Simu gani
Shahidi: Ilikuwa ni simu ya Tecno
Kibatala: Nenda Kwenye Exhibit P26 aina Ya Simu ni Ipi
Shahidi: Tecno V6 na Cable iliyotumika ni Namba 100
Kibatala: Nenda P27 ni simu aina Gani
Shahidi: Nakumbuka Ilikuwa Techno
Kibatala: Aina ya Simu Haitajwi??
Shahidi: Kimya
Kibatala: hapo ambapo aina ya Simu Haitajwi Ulitumia Forensic Cable gani
Shahidi: Haijataja Cable Iliyotumika
Kibatala: Hizo Simu zinafanama au Tofauti
Shahidi: Ni aina Tofauti
Kibatala: Je Ulimfafanulia Mheshimiwa Jaji siala la Utofauti Wa matumzi ya Tofauti ya Cable
Shahidi: Hapana Siku Mfafanulia
Kibatala: aliyeleta Masuala la Forensic Cables hapa Mahakamani
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Ethical Hacking Maana yake ni Udukuzi wa kimaadili.?
Shahidi: Sijui Kiswahili Chake
Kibatala: Nani anasimamia hiyo Ethical Hacking
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Katika Ushahidi wako wote zile simu 8, zinatakiwa Kufanya Extraction zikiwa Off au On
Shahidi: Inategemea Mashine
Kibatala: Unaweza Kufanya Extraction Simu Ikiwa Off?
Shahidi: Ndiyo unaweza
Kibatala: Chini ya Kiapo Kwamba Unaweza Kufanya Extraction simu zikiwa Off
Shahidi: Ndiyo Unaweza
Kibatala: Haya Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa Unaweza Kufanya Extraction simu ikiwa Off
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Katika zile simu Nilisikia Unasema Kuwa Matokeo positive, Maana ya Positive ni nini
Shahidi: Pale ambapo Nilichoombwa Hakijapatika ni Negative
Kibatala: Kwa Ushahidi Wako zile simu Nne zilikuwa hazina Mawasiliano
Shahidi: Hapana Zilikuwa hazina Mawasiliano Zinazo wasiliana na Hizi namba
Kibatala: Nenda Kwenye Terms of Reference, Je Terms of reference Inataja Kwamba Ufanye Uchunguzi Kuanzia Tarehe hii Mpaka Tarehe hii
Shahidi: Hapana Sijaandika
Kibatala: Na Mawasiliano Je
Shahidi: Hakuna Muda wa Limit
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji suala la Kutoa Miamala Na Mawasiliano Kutoka Tarehe fulani Mpaka Tarehe fulani
Shahidi: Kwenye Barua ambayo Ilikuwa Kwangu, Hapa Haipo
Kibatala: Kwanini tusiseme wewe ni miongoni mwa kikundi ndani ya Jeshi la polisi ambacho kilihusika na kupanga njama za Kumpa Freeman Mbowe Kesi ya Ugaidi Ndiyo Maana mlifanya uchunguzi kipindi fulani hadi fulani?
Shahidi: Hapana siyo sahihi
Kibatala: Naishia hapo
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Shahidi Umeulizwa Mambo Mengi sasa ni Muda Wa + Kufanya Ufafanuzi
Wakili wa Serikali: Jana Wakati Uliulizwa Swali hapa Ukasema, Siyo Kweli Kwamba tulifanya Extraction Tupo wengi, Hebu Tufafanulie Ulikuwa na Maan Gani
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Pia Kuhusiana Na Extraction Data Ukasema Ulikuwa nazo wewe
Shahidi: Kama Nilivyosema Awali, Kwenye Hizo Mashine tunaingia kwa Akaunti na Username
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali, Ukasema Kwenye Analysis, Ukajibu siyo Sahihi Kwenye Analysis
Kibatala: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Napinga Namna ya Maswali Kwa Mr. Hilla
Jaji: Kwa Maana anatakiwa kuweka swali na Jibu na vipi Kama aliweka Jibu pekee yake?
Kibatala: Bado Nitapinga
Jaji: Nafikiri sheria inasema kinachofafanuliwa ni Jibu
Wakili wa Serikali: Pius Hilla Mheshimiwa Basi tutafanya hivyo
Wakili wa Serikali: Shahidi Uliulizwa na Wakili Msomi Nashon Nkungu Kuhusiana na Analysis, Ulieleza Vitu VITATU ikiwemo , Extraction na Analysis, Maan yake nini.
Shahidi:Report Yako Ita Include Kile ambacho Umekipata tu.. Haito Include Kile ambacho haujakipata
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Maswali Kwamba Kwakuwa umepata Kozi Kuhusiana Na Terrorism, Wewe Ukasema Unafahamu Kuhusu Terrorism Kwa Perspective Ya Kiuchunguzi, Maana yake nini.
Shahidi: Software Yenyewe Ina Components ambazo Zina Jijaza Zenyenwe Kwa Pamoja
Nashon Nkungu: OBJECTION Mheshimiwa Jaji naomba Kupinga Jibu na Kinachoendelea, System Kwamba Yenyewe Ina Pick hizo Ingridients na Elements
Wakili wa Serikali: Tuache Shahidi ajibu Mheshimiwa Jaji kisha tupime Kama Linaendana na Jibu lake
Wakili wa Serikali: Shahidi Uliulizwa Pia na Wakili Mallya hapa, Mheshimiwa Jaji naomba P1, P23, P28
Wakili wa Serikali: Shahidi Uliulizwa na Malya, Kwenye Riport ya Kingai akamwambia Usome Kwenye IMEI namba
Alikuonyesha Pia simu na pia Kwenye Report yako, Akakuuliza Swali Kuwa IMEI namba zinatofautiana, wewe Ukasema kuna Digits Mbili Zina Miss, Ulikuwa na Maana Gani?
Shahidi: Kwenye hicho KIELELEZO D Kielelezo P31 zina Tally ila Kwa IMEI namba ya Pili Zina Miss namba mbili inaweza kama amesahau namba kadhaa
Kibatala: HAYO SIYO MAJIBU YA Re:Examination
Shahidi: Katika Report yangu Ipo ya Kwanza hii IMEI namba ya Kwanza ya Kingai 353736289120273 ila IMEI ya Pili Kwangu ni tofauti Inasomeka 3537289120273
WS: Je Zipo Namba Ngapi
Shahidi: Namba 15 au 13
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuwa Kuna Uwezekano wa IMEI Namba Kufanana
Shahidi: Hazifanani Sababu ni Unique Identification ya Kifaa Cha Mawasiliano
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kuhusu Owenership Za Simcard
Shahidi: Taarifa Zote zinazo husika na Usajili au Taarifa Ya Simu Kadi Zinapatikana kwa watoa huduma
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusiana na software ambazo Ulizitumia kufanya Extraction, ukasema zilikuwa developed na microsoft na celebrite
Kibatala: OBJECTION Hakuna swali wala Hapaawzi kuwa na Jibu, sababu Haiwezekani microsoft a' develop software za celebrite
Wakili wa Serikali: Nimeachana na hilo swali
Wakili wa Serikali: Bado nina maswali mengi naomba Niletee maombi tumalizie kesho
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Kwa sasa ni Saa 11, Tunaomba hairisho Mpaka kesho Tarehe 20 Mwezi January
Wakili Peter Kibatala: Hatuna Pingamizi, Ila tunaomba Waje na Shahidi Mwingine, Ili tulimalizane na Shahidi huyu tuingie Kwa Mwingine
Jaji: Je kuna shida Katika Kumpata Shahidi Kesho?, Siamini Mtatumia Utaratibu wa Utetezi wa Kuuliza Maswali Siku Nzima
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji tutajitahidi, Kulingana na Muda Wenyewe Huu
Jaji anaandika Kidogo.
Jaji: Shauri linahailishwa hadi Kesho 20.1.2022, Shahidi ataendelea Kutoa ushahidi wake
Upande wa Jamhuri naelekezwa kuja na shahidi mwingine
Washtakiwa wataendelea kuwa rumande chini ya magereza mpaka kesho asubuhi saa 3 kamili
Jaji anatoka