Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,447
- 7,829
Kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake itaendelea leo katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, ambapo upande wa mashitaka utaleta shahidi mwingine.
Fuatilia hapa kujua kitakachojiri katika mchakato mzima wa kesi hiyo kwa siku ya leo 11/01/2021
==========
Watuhumiwa wote wamekwishawasili katika ukumbi wa mahakama tayari kuanza kwa kesi.
Jaji: Ameingia sasa
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa
Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe na wenzake
Wakili wa Serikali, Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
1. Pius Hilla
2. Abdallah Chavula,
3. Jenitreza Kitali,
4. Nasorro Katuga,
5. Esther Martin,
6. Ignasi Mwinuka
7. Tulimanywa Majige
Wakili Peter Kibatala anawatambulisha Mawakili Wa Utetezi
1.Jeremiah Mtobesya
2.Michael Mwangasa
3.Seleman Matauka
4.Nashon Nkungu
5.Alex Massaba
6.Michael Lugina
7.Maria Mushi
8.Hadija Aron
9.Dickson Matata
10.Jonathan Mndeme
11.Fredrick Kihwelo
12.John Malya
Jaji: anawait Washitakiwa 1,2,3 na 4 Wanasimama Kuitikia
Wakili wa Serikali: Kwa Upande wetu tuna shahidi Mmoja kwa Leo na tupo tayari Kuendelea Kwa Upande wetu tupo tayari kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Tupo tayari na sisi Kuendelea
Wakili wa Serikali: Mmoja anatoka Kwenda Kumuita Shahidi Nje ya Chumba Cha Mahakama Mahakama Ipo Kimya Kidogo
Shahidi anapita ni Mdada Kajitanda Buibui na Kavaa Barakoa Kubwa sana Kumziba Sura,
Jaji: Majina Yako
Shahidi: Anita Varelian Mtali
Jaji: umri Shahidi: 45yrs
Jaji: Kabila
Shahidi: Mchaga
Jaji: Shughuli Zako
Shahidi: Nafanya Biashara
Jaji: Dini yako
Shahidi: R. C
Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii Kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa ni kweli, kweli tupu Eeeh Mungu nisaidie
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Shahidi Ataongozwa na Wakili Esther Martin
Wakili wa Serikali: Esther Ikumbushe Mahakama Majina yako
Shahidi: Anita Varelian Mtali
Wakili wa Serikali: Unaishi Wapi
Shahidi: Moshi, RAU madukani.
Jaji: Jina lako la Tatu sijalipata Vizuri ni Mtali.?
Shahidi: Mtaro
Wakili wa Serikali: Umeishi kwa Muda gani Rau
Shahidi: Miaka 08
Wakili wa Serikali: Unafanya Shughuli gani
Shahidi: Nafanya Biashara ya Kuuza Mbege
Wakili wa Serikali: Ulianza lini Biashara yako ya Mbege
Shahidi: Miaka 08 ninayo
Wakili wa Serikali: Mbali na Biashara yako ya Mbege una bishara gani Nyingine
Shahidi: Kuna Glocery, Stationary, Banda la Tigo Pesa na Kuna Sehemu ya Kutolea Movie
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama 05 Mwezi 08 2020 ulikuwa wapi
Shahidi: Sehemu yangu ya Biashara, Nikifanya Usafi
Wakili wa Serikali: Saa ngapi
Shahidi: Saa Saba Kasoro
Wakili wa Serikali: Ya Muda gani
Shahidi: Ya Mchana
Wakili wa Serikali : Kabla ya Kufika eneo lako la Biashara ulikuwa umetoka wapi?
Shahidi: Nilikuwa Nimetoka Nyumbani Nikaenda Saloon Kuosha Nywele
Wakili wa Serikali: Na Ulipotoka Saloon kuelekea sehemu yako Kufanya Usafi
Shahidi: Nilikuta Wakaka Watatu walikuwa wamekaa Mbele Yangu walikuwa wanakunywa na Kusajili Laini
Wakili wa Serikali: Walikuwa wanakunywa nini
Shahidi: Walikuwa wanakunywa Bia
Wakili wa Serikali: Hizo laini walikuwa wanasajili wapi
Shahidi: Kuna Vijana wanapitaga Mitaani Kusajili Laini
Wakili wa Serikali: Ukiwa unafanya Usafi kitu gani Kingine ulishuhudia
Shahidi: Kuna wakaka wawili walikuwa wanapitapita wakiongea na simu, Wanaenda wanarudi wakiongea na Simu
Wakili wa Serikali: Hao wanaopita ni tofauti na wale uliposema walikuwa wanakunywa Bia
Shahidi: Hapana ni walewale
Wakili wa Serikali: Kutoka Kwako Unapofanyia Kazi Mpaka Glocery ni Umbali gani
Shahidi: Kama Hatua 10
Wakili wa Serikali: Hapo Katikati sasa, Kati ya Glocery na ulipo, pana kitu gani
Shahidi: Pana uwazi
Wakili wa Serikali: Baada ya Muda kitu gani kilitokea
Shahidi: Wakati wanaongea na Simu Walitokea watu wawili wakaongea kwa sauti kali "Mpo chini ya Ulinzi Mnahusika na Mambo ya Kigaidi, chuchumaa Chini Mikono Juu"
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine ulisikia
Shahidi: Chuchumaa Chini Mnahusika na Mambo ya Kigaidi Wakili wa Serikali: Ni watu gani sasa hao
Shahidi: Ni Askari
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unafanya nini wakati huo
Shahidi: Nafanya Usafi
Wakili wa Serikali: Pana umbali gani kutoka Walipo na Mpaka Ulipokuwa unafanya Usafi
Shahidi: Hatua 05
Wakili wa Serikali: Ulisikia nini Kingine
Shahidi: Sikusikia Kingine zaidi ya Chuchumaa Chini Nyoosha Mikono Juu
Wakili wa Serikali: Walikuwa Askari wangapi
Shahidi: Wawili
Wakili wa Serikali: Hali ya Pale ilikuwaje
Shahidi: Ilikuwa ni Utulivu
Wakili wa Serikali: Nini Kilifuata
Shahidi: Walitokea Askari Wengine watatu wakawa wamefika eneo la Tukio
Wakili wa Serikali: Ongeza Sauti
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kiliendelea
Shahidi: Baada ya Kuwa Askari watano alitokea Mmoja akaniambia anaomba nisogee anahitaji Kuwafanyia Upekuzi
Wakili wa Serikali: Ni Askari gani huyo
Shahidi: Alinitambulisha anaitwa Askari Polisi Jumanne
Wakili wa Serikali: Ulifanya nini kujiridhisha?
Shahidi: Alitoa Kitambulisho Akanionyesha
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo nini kilifanyika
Shahidi: Alimsimamisha Mmoja
Wakili wa Serikali: Kabla ya Kumsimamisha..?
Shahidi: Afande Jumanne alijipekua kuanzia Kifuani akatoa Mifuko Nje
Wakili wa Serikali: We ulikuwa na nani wakati huo
Shahidi: Dada Mmoja anaitwa Esther
Wakili wa Serikali: Kutoka Eneo la walioambiwa Wachuchumae Chini, palikuwa na Umbali gani?
Shahidi: Kama Hatua Mbili
Wakili wa Serikali: Kuna Kitu gani Kingine
Shahidi: Raia walikuwa wamekuja
Wakili wa Serikali: Kabla ya Raia Kusogea eneo hilo palikuwa na hali gani?
Shahidi: Palikuwa na Jua
Wakili wa Serikali: ahaa ahaaa yani hali ya pale ilikuwaje?
Shahidi: Palikuwa pametulia
Wakili wa Serikali: Ikaendelea nini?
Shahidi: Alimsimamisha Mmoja akamuuliza Unaitwa nani?
Wakili wa Serikali: Akajibu anaitwa nani?
Shahidi: Adam Kasekwa
Wakili wa Serikali: Akamwambia nini?
Shahidi: Akiwa amenyoosha Mikono Juu akamwambia Geuka, akageuka
Wakili wa Serikali: Baada ya Kugeuka
Shahidi: Askari Jumanne alianza Kumpekua Kuanzia Kichwani, Mabegani, Alipofika Kiunoni alikuta Kitu kigumu
Wakili wa Serikali: Alikikuta Upande gani
Shahidi: Kushoto
Wakili wa Serikali: Maeneo Gani?
Shahidi: Niliona ni Bastola
Wakili wa Serikali: Ulijuaje kama ni Bastola?
Shahidi: Afande Jummane alituambia ni Bastola
Wakili wa Serikali: Halafu
Shahidi: akatuonyesha namba
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni namba gani.?
Shahidi: A5340
Wakili wa Serikali: Zilikuwa kwenye nini
Shahidi: Kwenye Bastola
Wakili wa Serikali: Wakati anakuonyesha Bastola Adam alikuwa wapi?
Shahidi: Alikuwa amesimama
Wakili wa Serikali: Ukiona na nini Kingine
Shahidi: Risasi 03
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi, alipofika Upande wa Kulia akakuta Vitu vidogo vidogo Kwenye Karatasi ya Nailon akasema inasadikiwa ni Madawa ya Kulevya ila itajulikana Mbele.
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ngapi Shahidi: 58
Wakili wa Serikali: ikawaje
Shahidi: Aliendelea Kumpekua akamkuta na Simu Ndogo aina ya Itel
Wakili wa Serikali: Hiyo simu akaifanyaje
Shahidi: Akatoa laini akakuta namba akaziandika
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo aliendelea na nini
Shahidi: Akamwambia Naomba fomu, .......akaleta fomu
Wakili wa Serikali: fomu ngapi
Shahidi: Zilikuwa Mbili
Wakili wa Serikali: Akafanya nini sasa Kwenye ile Fomu
Shahidi: Kaandika Vitu alivyokuwa amempekua
Wakili wa Serikali: Umesema palikuwa na fomu Mbili, fomu ya kwanza akijaza nini
Shahidi: fomu ya kwanza alijaza Bastola, Risasi na Laini
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni laini gani
Shahidi: Laini ya Voda na Airtel
Wakili wa Serikali: Baada ya Kumalizia fomu ya kwanza
Shahidi: alichukua fomu Nyingine
Wakili wa Serikali: Kabla ya Kujaza Fomu Nyingine
Shahidi: Alipomaliza Kujaza akampa akasaini na Baadae akasaini yeye alipo maliza Kusaini.
Wakili wa Serikali: alimpa nani
Shahidi: Alimpa Adam
Wakili wa Serikali: baada ya fomu ya kwanza nini kiliendelea
Shahidi: alichukua Fomu Nyingine
Wakili wa Serikali: alijaza nini
Shahidi: alijaza vile Vikete vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vingapi Vilikuwa Vingapi
Shahidi: Vilikuwa 58
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: akampa Adam asome alafu asaini na sisi akamtupa tusaini
Wakili wa Serikali: Wewe na nani..?
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada Kumalizia nini kilifuata
Shahidi: akamuita Mwingine
Wakili wa Serikali: huyo Mwingine anaitwa nani
Shahidi: Mohamed Abdulahi Ling'wenya
Wakili wa Serikali: akamwambia nini
Shahidi: asimame ageuke, Baada ya kugeuka akaanza Kumpekua
Wakili wa Serikali: alianzaje Kumpekua
Shahidi: Kichwani Mikononi
Wakili wa Serikali: ilikuwaje
Shahidi: Upande wa Kulia alikuta na Vikete Vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi
Shahidi: 25
Wakili wa Serikali: akafanyeje
Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua
Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua
Shahidi: alikuta Simu aina ya Tecno
Wakili wa Serikali: Rangi gani
Shahidi: Nyeusi
Wakili wa Serikali: akafanya nini
Shahidi: akapekua akakuta kuna laini
Wakili wa Serikali: laini gani
Shahidi: Hallotel
Wakili wa Serikali: baada ya Kupata simu akafanyeje
Shahidi: akazitoa zile Laini, Akampa yule Mwingine akazishika
Wakili wa Serikali: Na Yeye Akaendelea na nini
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi
Wakili wa Serikali: hizo laini alikuwa anafanya nazo nini?
Shahidi: Alimpa Askari wa Pembeni akazishika
Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi
Shahidi: Aliendelea na Upekuzi lakini hakukuta kitu Kingine
Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi
Shahidi: aliomba fomu Mbili
Wakili wa Serikali: fomu ya Kwanza alijaza nini
Shahidi: alijaza vile Vikete Vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi
Shahidi: 25
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo
Shahidi: Alimpa akasema akasaini
Wakili wa Serikali: Nani Yeye, afande Jumanne?
Shahidi: Ndiyo na Baadae Mohamed
Wakili wa Serikali: na baadae
Shahidi: tukasaini sisi
Wakili wa Serikali: Wewe na nani
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: Ile fomu Nyingine akajaza Simu na laini Nyingine
Wakili wa Serikali: Za Mtandao gani
Shahidi: Airtel na Hallotel
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo
Shahidi: Alimpa Mohamed asome kisha akasaini
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: afande Jumanne alituomba na sisi tusome Kisha tusaini
Wakili wa Serikali: Wewe na nani
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada ya Upekuzi
Shahidi: walivalishwa Pingu
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: afande Jumanne akatuomba tuelekee Kituoni
Wakili wa Serikali: Hao walivalishwa Pingu walikuwa ni akina nani
Shahidi: Adam na Mohamed
Wakili wa Serikali: baada ya kuvalishwa Pingu..?
Shahidi: Wakaelekea kwenye Magari, Barabarani
Wakili wa Serikali: Palikuwa na Askari wangapi
Shahidi: Watano
Wakili wa Serikali: Walikuwa wamebeba nini
Shahidi: Wawili walikuwa wamebeba Bunduki
Wakili wa Serikali: Hali ya hewa eneo lile ilikuwaje
Shahidi: ilikuwa imetulia
Wakili wa Serikali: Hali ya hewa ilikuwaje
Shahidi: Kulikuwa na Jua na Mwanga
Wakili wa Serikali: Mlichukua Muda gani kwenye lile eneo Mpaka Mnamaliza Zoezi
Shahidi: Kama Dakika 45
Wakili wa Serikali: Baada ya Kufanya Upekuzi Kuna Vitu Vilipatikana na Kwamba Kuna fomu zilijazwa Sasa fomu ukiziona hapa utaweza Kuzitambua?
Wakili wa Serikali: sasa bada ya Kumalizia Mkaelekea kituoni, kituo gani..?
Shahidi: Central Moshi
Wakili wa Serikali: baada ya Kufika police central
Shahidi: Tuliandika Maelezo
Wakili wa Serikali: Maelezo ya nini
Shahidi: Kitu gani Kilichofanyika ......
Wakili wa Serikali: Tukianza na fomu ya Adam utaitambuaje
Shahidi: Kwa vitu vilivyoaandikwa, Jina langu na sahihi yangu
Wakili wa Serikali: Kulikuwa na nini Kingine Bastola
Wakili wa Serikali: Kingine
shahidi: Palikuwa na Risasi
Wakili wa Serikali namba gani Shahidi: A5340
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba nimpe fomu aweze Kuitambua
Wakili wa Serikali: Shika hii Karatasi iangalie kwa Makini
Shahidi: Ndiyo yenyewe
Wakili wa Serikali: Yenyewe nini
Shahidi: Fomu niliyo saini
Wakili wa Serikali: Umeitambuaje
Shahidi: Kwa Jina langu na Sehemu niliyosaini
Wakili wa Serikali: Jina lipo wapi, Ni Jina gani
Wakili Peter Kibatala: ALICHOKIFANYA DADA YANGU ESTHER HAIRUHUSIWI, ANAKWEMDA KWENYE DETAILS
Wakili wa Serikali: Sawa naondoa hilo swali
Wakili wa Serikali: Ungependa hii fomu ipokelewe Mahakamani
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi anaomba Fomu ipokelewe
Jaji: Wakili wa Mshtakiwa wa kwanza
MTOBESYA: HATUNA PINGAMIZI
Mallya: Hatuna Pingamizi Fredrik
Kiwhero: kwa Niaba ya Mshitakiwa.....wa tatu hatunapingamizi
Peter Kibatala: Kwa niaba ya Mshitakiwa wa Nne hatuna Pingamizi
Jaji: anaandika Kidogo
Jaji: Mahakama inaipokea kwa ID 1
Wakili wa Serikali: Shahidi pia ulisema kwenye huo Upekuzi pana Bastola na Risasi unaweza hapa Mahakamani ukavitambua Tuanze na Bastola
Shahidi: Ndiyo nitavitambua
Wakili wa Serikali: Bastola unazitambuaje
Shahidi: Kwa Namba A5340
Wakili wa Serikali: na Kwa Upande wa Risasi
Shahidi: namtambua, zilikuwa na Rangi ya Dhahabu
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Naona Exibit nimuonyeshe Shahidi
Afisa Wa Mahakama anafungua Bahasha ya Kaki Anamkabidhi Wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: Hebu Kiangalie hiki kitu hapa, Iambie Mahakama ni nini
Shahidi: anaingilia bila Kushika, ni Bastola
Wakili wa Serikali: ambayo Imetoka wapi
Shahidi: Imetoka Kwa Adam
Wakili wa Serikali: Uliona wapi?
Shahidi: iliyotoka kwa Adam
Wakili wa Serikali: ni Kitu gani Kilichokufanya ukagundua
Shahidi: kwa namba
Wakili wa Serikali: Namba gani
Shahidi: A5340
Wakili wa Serikali: Umeeleza pia ulishuhudia Upekuzi wa watu wa wili ambao kwa Majina yao ni Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya, Je ukiwaona unaweza Kuwatambua
Shahidi: naweza Kuwatambua
WAKILI WA SERIKALI: WAPO HAPA MAHAKAMANI?
Shahidi: Wapo hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali: Wapo wapi
Shahidi: hapa Mbele, Mohammed amevaa Tshirt ya Amevaa Meupe Kijani na Nyeusi
Wakili wa Serikali: na Adam yupo wapi Shahidi: amevaa Shati lenye Rangi Nyeupe Nyeupe
Wakili wa Serikali: Yupo wapi hapa Mahakamani
Shahidi: Yupo pale
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu
Jaji: Upande wa Utetezi
Mtobesya: Ndiyo Mheshimiwa Jaji
Mtobesya: naomba Nipatiwe ID 1 Mahakama Inampatia
Mtobesya: Shahidi umeomba Mahakama Ipokee Kielelezo hiki Onyesha Sehemu ipo saini
Shahidi: Nimesaini hapa
Mtobesy: Kwa Ushahidi wako Unasema ulisaini Nyaraka ngapi
Shahidi: Nne
Mtobesya: Ushahidi wako kwamba Sahihi zako Lote zinafanana
Mtobesya: Naomba kwa Kifungu 75(1) Sheria ya Ushahidi, Shahidi asaini tena sehemu Nyingine ili Mahakama iweze Kufananisha Saini zake
Jaji: Unaweza Kutusomea.? Mtobesya: anasoma Kifungu cha 75(1) cha Sheria ya Ushahidi
Jaji: hicho Kifungu kinaitaka Mahakama shahidi asaini ili iweze Kufanya ufafananisho
Mtobesya: Ndiyo ili Mahakama iweze kufananisha, kwa sababu tuna Nyaraka Nyingine inasaini yake tofauti
JAJI: lakini hiyo Nyaraka itakuwa imetengenezwa hapa, Utakuwa umeiiingiza Mhakama .....
Jaji : Bwana Matata una jambo la Ku-she na sisi
Matata: Sheria Anayosoma Wakili Mtobesya Ni Sheria inasema kuwa Shahidi anaweza kuandika sehemu tu 75(2) Mahakama inaweza Kuagiza Mtu yoyote Mahakamani Kulingananisha.
Jaji: Je hiyo inahusiana na Mahakama kumuelekeza Shahidi asaini?
Matata: ni tafasiri yangu kuwa Mahakama Inaweza Kuruhusu Shahidi Kuandika ili Kufananisha Kama alichokiandika ni sawa
Mallya: Pale kwenye 75(2) inasema any Documents haijambana wapi kwa hiyo anaweza Kusaini popote (any documents) ili Mahakama ifanye Uamuzi iwe imepata kwa Usahihi wake....kwa usahihi Kifungu cha 75 lakini siyo kwa Kumtaja Shahidi aandike
Jaji: Upande wa Mashitaka
Wakili wa Serikali: Maombi ya Mtobesya Pamoja na Kuegemea kutoka kifungu 75 cha Sheria ya Ushahidi tunaona amekimbia Sana na siyo wakati wake Lakini pangekuwa na Nyaraka Nyingine ambayo Ndiyo Ingekuwa imekuja Rasmi Mahakamani ndipo angetumia.......Njia yako ya Kutaka Shahidi Asaini Ni sahihi Kama watapinga tutashughulikia Kupinga huko wakati huo.
Jaji: Kwa tafsiri yangu Mamlaka iliyopewa Mahakama 75(2) ni naona Mahakama inayo Mamlaka kumuelekeza Mtu yoyote Kufanya Mlinganisho wa Maneno au Namba kwa Nia ya Kuiwezesha Mahakama Kufanya Ulinganisho, ila huyu Mtu aliye na maarifa Kuliko Mahakama Yenyewe. Najiuliza kama ...Leo nilikuwa na Avoid Upande wa Utetezi Kutuzuia Kutumia Nyaraka hii ambayo sisi tumeipata kwenye Comito.
Mtobesya///; Kifungu cha 47 cha Sheria ya Ushahidi ndiyo kinaruhusu Maoni ya Kitaalamu katika Ushahidi Lakini Kifungu cha 48 au 49 Sikumbuki Vizuri kinaruhusu hata mtu asiye Mbobezi Kufanya Maoni yake Hili Kifungu cha 75 chenyewe Kinataka Mahakama Kufanya Ulinganisho.
Jaji: Na Mimi na kubaliana na wewe Lakini kwenye Document uliyonayo hatujui baada ya Kumkabidhi Karatasi at asaini Sahihi gani kati ya hizo Mbili
Jaji: Ndiyo nasema wewe endelea na Jukumu lako kama Walitokea Wakapinga tutashughulikia Pingamizi hilo wakati huo ...na Sheria ya Ushahidi wa Kifungu cha 75 Vyote Vinafanya washitakiwa Kupewa Nyaraka zinazokusudiwa Kutumika dhidi yao kwenye Makosa Makubwa Kama haya kupitia Comito Kwa hiyo watupatie
Mtobesya: Asante Mheshimiwa Jaji
Mtobesya: Naomba nikabidhi iwe Nyaraka Original ya Hati ya Kuchukua Mali iliyosainiwa tarehe 25 2020 inayomhusu Mohamed Ling'wenya Kwa sababu sisi tunayo Moja
Jaji: chini ya Sheria Gani
Mtobesya: Kifungu cha 246 na 146 ya Makosa ya Jinai ...
..Angetoa basi Maombi Rasmi lakini hata kama no Original haiwezi kuitumia kwa wakati huu Haki yake ya Kuhoji aendelee nayo na anaweza Kuitumia hata sasa Sisi tuna tatizo na Procedure jinsi gani Ushahidi huu unataka Kuletwa Mahakamani
Jaji: Jamani Mmeelewa
Wakili wa Serikali: Sisi Haja yetu ni Swala la Procedure Ni kweli Tulianika Ushahidi Tutaokuja kutumia Mahakamani lakini ieleweka Kuwa Ushahidi hi ni Wa Kwetu. Hakuna mahala popote ambapo Mteja wake anaweza Kuwa na haki ya kutumia Nyaraka hizo ......
.Ubishi ulikuwa kama Mshitakiwa Alikuwa ametahiriwa au haja tahiriwa Mahakama ya Rufani ikasema kuwa Hilo ni Kubwa sana Kwake na Isingeweza Kujiingiza katika Risk. Kwa kesi hii basi Kama anataka Mahakama Ijiridhishe. Swala ni Kama Nyaraka hiyo imepokelewa na Kama .......imekubali imeandikwa na Mtu huyu Na pia kama Nyaraka hiyo Nyingine kama Ingekuwa hapa angekuwa na Haki
KESI YA buying wa John dhidi ya Jamhuri criminal appeal namba 450 ya Mwaka 2017 Mahakama iliyoketi Shinyanga Katika Ukurusa wa 11 paragraph ya Mwisho ya a Ukurasa huo wa 11 Ambapo swala Lililojitokeza tangu wakati wa Trial Court na Kesi Ilikuwa ni ya Ubakaji ........
Mheshimiwa Jaji: tunatakiwa tuzingatie Mfumo wetu wa Utoaji haki, Mahakama kwa Kutimiza Wajibu wake anakuwa ni refa na siyo kwa kukaribishwa Kutaka Kufanya Uchunguzi Zoezi kama hilo ni Kuingiza Mahakama katika riski ambazo zinaweza Kuepukika.
...imekubali imeandikwa na Mtu huyu Na pia kama Nyaraka hiyo Nyingine kama Ingekuwa hapa angekuwa na Haki
Na Hilo Ndiyo Dhumuni la Comito Trial kwamba Mshitakiwa ajue anachokuja akujitetea nacho
Upande wa serikali: Sisi tunaona ni Kukiuka Procedure na Maombi hayo tunaomba uyakatae Mheshimiwa jaji Mtobesya: Tunapoteza sana Muda Mheshimiwa Jaji, Shahidi ni wa Kwao na Ushahidi ni wa Kwao Na sijui ni wakati gani tena sisi tutapata Kuwa na wasaa wa kuwa na Shahidi huyu
Na hapa swala la Copy kwa Washitakiwa halijazungumziwa wakati ni Haki kwa Mshitakiwa Kupatiwa Hiyo Nyaraka
Nashon Nkungu: Naona nisaidie Mahakama kama Afisa wa Mahakama alichosema Wakili Robert Kidando Amejieleza Kwenye Kifungu cha 76 tuh asemi kwa nini kuna Haki ya Kukabidhi wa Nyaraka za Comito Na Kingine Kifungu 30 cha Sheria inasema tupewe Copy siyo Photocopy ....
Ambapo wewe Umegundua Sahihi Katika Nyaraka hizo na Zilizopo hapa Mahakamani Sahihi zinatofautiana Kwa Maana hiyo Ukaomba Mahakama ikupatia Nakala halisi Jaji Jambo la Pili Kwakuwa wanasema Ushahidi huo watautumia basi Wahurumie Mapema ili uweze Kuutumia.
Jaji: Mtobesya
Mtobesya: naam Mheshimiwa Jaji
Jaji: hoja zako ulizijenga katika a Mazingira Matatu Haki za Mahakama Jinai hasa akatika Mahakama Kuu, amtu anasomewa na Kukabidhi wa Nyaraka Kwamba wewe Una taarifa Kwamba zipo Nyaraka wanazolenga kuzitumia Kama Ushahidi Wao
Mtobesya: Mheshimiwa nilikuwa naomba Mashauriano na Mahakama ilitusiiipe Mahakama Mzigo wa a kuandika Rulling
Jaji: mnasemaje Jamuhuri
Wakili wa Serikali: Ni Sawa Mheshimiwa
Jaji: Basi tuta Break kwa Dakika 10, tukutane pande zote pale Ofisini
Jaji: anatoka
Mawakili wamerudi
Jaji ameingia tena Saa 6 NA Dakika 24
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa tena Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe Kisha Mahakama Kimyaaaaaa
Jaji: Muda Mfupi Uliopita Tuli-break kwa Nia ya Kuweka Sawa Mambo ya Kitaaluma Baada ya Kuyaweka Sawa na Kualika Sasa Mtobesya Kuendelea
MTOBESYA: Wakati Unaongozwa na Dada Yangu Esther Ulisema Uliandika Maelezo
Shahidi: Niliandika Tarehe 05 Mwezi 08 2020
Mtobesya: aliyeandika Maelezo yako
Shahidi: Sijui Jina lake
Shahidi: anaitwa Jumanne
Mtobesya: Ulishawahi Kukutana na Askari anaitwa Detective Coplo Francis.?
Shahidi: Sikumbuki kama nimekutana naye
Mtobesya: Lakini walikupa Maelezo Ukasoma na kisha Ukaona sawa
Shahidi Ndiyo
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Nipewe Statement (Handwritten Statement) Naomba Chini ya Kifungu Cha 164 (1h) cha Sheria ya Ushahidi
Wakili wa Serikali Wapo Kimya Jaji anawasubiri
Wakili wa Serikali: Hatuna Pingamizi la Kumpatia hii Nyaraka
Jaji: Pokea
Mtobesya: Shahidi Unajua Kusoma na Kuandika
Shahidi: Ndiyo
MTOBESYA: Shika Karatasi zipo Mbili Soma kama Ndiyo Uliyosoma Ukasaini na Kama Kuna Majina yako na Askari aliye andika Ihakiki Kwanza
Shahidi Anaipekua, anaikazia Macho anafunua funua mara Nyingiyingi
Mtobesya: Ndiyo hiyo.?
Shahidi: Kimyaaaa anatizama tena ile Karatasi, anaipekua
Shahidi: Ndiyo Yenyewe
Mtobesya: Soma Kuanzia Juu Kwa Sauti
Shahidi: Mimi Ndiyo Mwenye Majina na anuani takwa hapo Juu Mkazi Wa Kilimanjaro Nimezaliwa Mwaka 1979 Familia ya watoto Nilikuwa naelekea Saloon Rau Madukani Na baada ya Kumalizia nilieleza Sehemu yangu ya Biashara Kufanya Usafi. Mbele Kuna Bar Na Kukikuwa na Vijana walikuwa wanakunywa Pale Sikuwa nawafahamu Kwa Maana walikuwa ni wageni
Mtobesya: Soma Kote
Shahidi: Sikuwafahamu kwa Maana walikuwa ni Wageni maeneo haya Kwa Muda Mwingi walikuwa wanaongea na simu. Kwangu Afande Mmoja akajitambulisha Jina Afande Jumanne Akaniomba niwe Shahidi huru Ambapo nilishuduia Kufanya Upekuzi Kwenye Kupekuliwa Kijana Mmoja alikuwa na Bastola Zenye nmabaA A 5340 Pia alikutwa na Kete 58 za Madawa ya Kulevya
Shahidi: Shahidi ananendelea kusoma Baada ya Muda walikuja watu watano na a Kuwafuata wale Vijana Na wakaambiwa wapo Chino ya Ulinzi Askari hao walitaka Kufanya Upekuzi ndipo walipokuka Kuni.... Kamyamaza Kidogo Askari hao walihitaji Kufanya Upekuzi ndipo walikuja.......Adam Kasekwa mbaye nilimfahamu Jina baada ya Kuulizwa Jina lake baada ya Upekuzi Na huyo Mwingine aliyekuwa naye alitaka anaitwa Mohammed Ling'wenya ambaye pia kwenye Upekuzi alikutwa na Simu Moja ya Samrt Yenye Line ya Airtel na Hallotel na Kete 21 za Madawa ya Kulevya
Watu hawa wawili nilikuwa siwafahamu Majina wala Sura niliwafahamu baada ya Kutaja Majina yao Baada ya Kukamatwa na Polisi, Askari wale nilikuwa siwafahamu Na Kiongozi wao aliyekuwa anafanya a upekuzi aliwatambulisha kwangu ASP Jumanne.
Baada ya Majina hayo Nilijaza Hati ya Upekuzi Na Kuzuia Mali Walisaini wote na Watu tulioshuhudia Na Afande Jumanne Na baada ya Upekuzi Nilijaza Hati ambayo inaonyesha Upekuzi umefanyika Ambapo tukasaini wote na tulioshuhudia Haya Ndiyo Maelezo Yangu, Sahihi Kama Nilivyoyatoa.
Mtobesya: Nitakurudisha Kwenye baadhi ya Maeneo kama Ulivyosoma
Mtobesya: Ni sahihi Katika Ushahidi wako ulisema Askari wawili walifika wakawaambia Mpo chini ya Ulinzi na Wakawatajia Makosa yao
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Kwenye Maelezo yako hapo, hayo Maneno Yapo au hayapo
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: Nilikusikia Unasema hawa Vijana waliokamatwa wao walikuwa wanakunywa wakati wewe unafanya usafi katika Eneo lako la Biashara
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Kwenye Maelezo yako hiyo Taarifa ipo
Shahidi: Haipo
Mtobesya: Nilikusikia Ukisema Kwamba afande Jumanne alikuja kwako akatoa Kitambulisho
Shahidi: Ndiyo alitoa Kitambulisho
Mtobesya: Hayo Maelezo ya kutoa Kitambulisho yapo kwenye Statement yako
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: kwenye Maelezo yako nilikusikia watuhumiwa Waliposimamishwa kabla ya Upekuzi walijitambulisha Majina yao kwa Polisi aliyekuwa anafanya Upekuzi Nitakuwa sahihi nikisema Statement Yako inasema Uliwajua Majina Baada ya Upekuzi
Shahidi: Niliwajua Majina kabla ya Upekuzi
Mtobesya: Soma sehemu inayosema nilishuduia wakipekuliwa........ Mpaka inaisha Jina la Afande Jumanne, Soma kwa Sauti
Shahidi: Nilishuhudia Kupekuliwa kwa Vijana hao, na Kupekuliwa Mmoja wao alikutwa na Bastola yenye namba A5340 pamoja na Magazine yanye Risasi 3 .......pia alikuwa na Madawa ya Kulevya Ambae nilimfahamu kwa Jina baada ya Kuulizwa baada ya Upekuzi.
Mtobesya: Kwa hiyo Statement Ulifahamu Kabla au Baada
Shahidi: Baada ya Kupekuliwa
Mtobesya: Nitakuwa sahihi, kwenye Ushahidi wako ulielezea ulisaini Nyaraka Nne za Kushuhudia Upekuzi
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Nenda Sasa baada Upekuzi huo,
Shahidi: Nilijaza Hati ya Upekuzi na Hati ya Kuzuia Mali ilionyesha Upekuzi Umefanyika, ambao tulisaini wote tulioshuhudia pale.
Mtobesya: Ishia hapo, Nitakuwa sahihi nikisema Nyaraka hiyo Uliyosoma inaonyesha ulisaini Nyaraka Moja..? Na siyo Nne kama Ulivyosema Asubuhi ya Leo
Shahidi: kwa Mujibu wa Mstari huu ni Kweli
Mtobesya: Isaidie Mahakama sehemu nataka Usome Kwa Sauti, Soma baada ya Neno Watuhumiwa wale wawili
Shahidi: Baada ya Upekuzi huo na Kusaini Hati ya Kuzuia Mali ambapo tukisaini wote.
Mtobesya: Wakati Wakili Wa Serikali Esther anakuongoza Ulisema aliyekuongoza hapo ni Jumanne
Shahidi: Nilisema ni Afande ambaye sikujua Kwa Jina
Mtobesya: Ipo Kwenye Rekodi, Jaji ataona
Shahidi: hapana
Mtobesya: Ungependa hayo Maelezo Yawe sehemu ya Ushahidi Wako Siku ya Leo
Shahidi: Ndiyo ningependa uwe Ushahidi Wangu Siku ya Leo
Wakili wa Serikali: Hatuna Pingamizi
Jaji: Mahakama imeyapokea Maelezo hayo Kama Kielelezo namba 02 kwa Upande wa Utetezi
Mtobesya: Kwa Ruhusa yako Mheshimiwa naomba Kuendelea
Mtobesya: Ulielezea Mahakama Ulisaini Nyaraka za Uzuiaji wa Mali, zaidi ya Nne
Shahidi: Ndiyo
MTOBESYA: ieleze Mahakama Hati hizo zilijazwa na nani Mpaka Nyie Mkasaini
Shahidi: Zilijazwa na Askari Jumanne
MTOBESYA: na wewe Unakumbuka ulisaini kwenye Hati zote
Shahidi: Ndiyo
MTOBESYA: Unaweza Kuisaidia Mahakama Ulisaini Upande gani
Shahidi: Pale Mwisho Kwa Pembeni
Mtobesya: Naomba Nimuonyeshe Shahidi ID 1 Nitakuwa Sahihi Nikisema Nyaraka zote Nne ulisaini hapa Kwenye Jina lako
Shahidi: Siyo zote sehemu hii, Zingine Nilisaini Upande wa Kushoto na Zingine Upande wa Kulia.
Mtobesya: Unaweza Kutuambia Ulizosaini Upande wa Kushoto zinaruhusu nani na Kwaajili ya Vifaa Vipi
Shahidi: NilizoSaini Upande wa Kushoto zilikuwa zinamhusu Adam
Mtobesya: Hizo Ulisaini Upande wa Kushoto
Shahidi: Nilisaini Upande wa Kulia
Mtobesya: na Zilizomuhusi Mohammed Ulisaini Upande gani
Shahidi: Upande WA Kushoto
Mtobesya: Ulisaini Baada au Kabla ya Jina lako
Shahidi: Nilisaini baada ya Jina langu
Mtobesya: Na Ni Ushahidi wako Mbele ya Mahakama zote Ulisaini wewe Mwenyewe na kwa Mwandiko wako
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Na Kwa Ushahidi Wako Saini zako umesaini wewe Zikiwa zinafanana
Shahidi: Kuna zingine zilikuwa hazifanani kwa sababu nilikuwa na Hali tofauti
Mtobesya: Mweleze Mheshimiwa Jaji Sasa ni hali ipi Ulikuwa nayo ikapelekea Saini zako Kutofautiana
Shahidi: Kuna saa, wakati wa Ukamataji Nilisaini wakati nimesimama na Zingine nimesaini wakati nimekaa kwenye Meza.
Mtobesya: Unaieleza Mahakama Ukisaini ukiwa umesimama na Wakati Umekaa saini lazima zitofautiane
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Nilisikia wakati anakuongoza Dada Yangu Wakili wa Serikali Kuwa Mlisaini wakati Wa Tukio
Shahidi: Wakati natoa Maelezo Nilisaini Nikiwa mezani lakini Zile zingine Nilisaini nikiwa nimesimama
Mtobesya: Ni Signature zipi sasa zinazofanana ukiwa Umekaa au Umesimama
Shahidi: Nikiwa Nimekaa ndiyo zinafanana
Mtobesya: Ukiwa Umekaa umesaini Mara Ngapi na Nyaraka zipi
Shahidi: Zile ambazo nilikuwa kituoni kutoa Maelezo.
Mtobesya: Zote ambazo ulisaini Ukiwa Umekaa Zina fanana..?
Shahidi: Hapana
Mtobesya: Zote ulizoSaini Ukiwa Umesimama Zinafanana au hazifanani
Shahidi: Zinafanana
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Kuishia Hapo
Mtobesya: naomba Kurudisha Kielelezo
Jaji: Wakili Malya unahitaji Muda gani
Mallya: Nusu saa hivi
Mallya: Bado unauza Mbege
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Mbege unayouza wewe inalewesha
Shahidi: Kuna Inayolewesha na Isiyolewesha
Mallya: Una Ndugu au Mume ambaye ni Polisi
Shahidi: Hapana
Mallya: Ulitambuaje kuwa hiki ni Kitambulisho cha Polisi?
Shahidi: Niliona Chapa ya Taifa
Mallya: Kitu gani Kingine Uliona
Shahidi: Niliona Jina lake
Mallya: Lilikuwa limeandikwaje
Shahidi: kwa kweli hapo Sikumbuki
Mallya: Umesema Wakati Unafanya Shughuli zako za Usafi na Vijana walikuwa wanakunywa Bia, Ni hatua ngapi
Shahidi: Ni hatua 10
Mallya: Napiga hatua Mahakamani
Mallya: Hapa Kuna Hatua Saba tu
Mallya: Umbali wa Hatua 10 Macho yako yanaona Vizuri
Shahidi: Yanaona Vizuri
Mallya: hapa Kuna Umbali Wa Hatua 7 tu Unasema Mtu Amevaa Tshirt yenye Rangi Nyeusi wakati ni Dark Green Je unataka Mahakama iamini kwamba unaona Vizuri?
Jaji: umeelewa swali..?
Shahidi: ..natumiaga Miwani, Sema Leo nimesahau Miwani
Mallya: Ulielezea Kuwa siku ya Tukio ulivaa a Miwani
Shahidi: Hapana
Mallya: Siku ya Tukio ulikuwa Umbali wa Mita 10 Leo Mshitakiwa yupo hatua 10 tu hakuna aliyevaa Tshirt Nyeusi, unataka Kumwambia Mheshimiwa Jaji unaona Vizuri?
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
JAJI: umelielewa Swali
Shahidi: Ndiyo
JAJI: Jibu Basi
Shahidi: Kuna saa Macho yanashida.
Mallya: Wakati Unatoa Maelezo Leo Uliomba Miwani uweze Kuangalia Vizuri.?
Shahidi: Sikuomba
Mallya: Ni sahihi Kuwa Usajili wa Simu unafanya kwa Kitambulisho?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: na wewe Uliwaona watu waliopo Mahakamani walikuwa wanasajili Line za simu
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwenye Maelezo Yako kuna sehemu umesema Wanasajili lini?
Shahidi: Hakuna
Mallya: pale Rau Bia wanauza au Bure?
Shahidi: Wanauza
Mallya: Wakati mnawapekua Mliwakuta na Bastola na Siyo Pesa
Shahidi: Hakuwa na Pesa
Jaji: Watakuwa walishalipaaaaaa
MAHAKAMA kichekoooooo
Mallya: zoezi la Kufanya usafi Lilichukua muda gani?
Shahidi: Kwa muda wa Kufanya Usafi kama Dakika 10
Mallya: Wakati Tukio linatoka Ulishamaliza Usafi au Ulikuwa unaendelea
Shahidi: nilikuwa naendelea ikabidi Nisimame
Mallya: Tukio la kukamatwa lilichukua Muda gani?
Shahidi: Rudia swal?
Mallya: Kitendo Cha Kukamatwa hawa watu Mpaka unaitwa kushuhudia ilichukua muda gani?
Shahidi: kama Dakika 03
Mallya: Kwa hiyo tukijumlisha Dakika 10 za Usafi na Dakika 3 wakakuita wewe Zoezi la Kusachiwa lilidumu kwa a muda gani?
Shahidi: Kwa Dakika 45
Malya: Saa Nane ilikuwa imefika
Shahidi: Kama saa Nane Kasoro
Mallya: Kwa Maelezo Yako wewe yalitolewa Umesaini Ukiwa polisi saa 7 kamili Je, tukuamini wewe au?
Shahidi: Muamini Maneno Yangu
Mallya: Tuchukue Yote.?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kabla ya kwenda Kwenye Tukio Siku hiyo ulikuwa wapi na wapi
Shahidi: Nilitoka Nyumbani baada ya Usafi, Nikaenda Kwa Mgonjwa na Baadae Saloon
Mallya: Umeulizwa aliyekuchukua maelezo Yako ni nani
Shahidi: Simfahamu Kwa Majina
Mallya: Hakukuonyesha Kitambulisho ndiyo Maana Humkumbuki?
Shahidi: Hapana alinitajia nimemsahau
Mallya: Kwa kutazama Kwa Macho yako sahihi yako uliyosaini Hapa na Hapa Kwenye Exibit 02 zinafanana
Shahidi: Hazifanani lakini ni sahihi zangu
Mallya: Kwenye Maelezo Yako umeeleza Mahali Kiongozi wao, Afande nani
Shahidi: Afande Jumanne
Mallya: akitokea Mtu akisema yeye ndiyo Kiongozi aliyekwepo atakuwa Muongo
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Unamfahamu Kingai
Shahidi: Hapana
Mallya: na Ulisema Mapolisi walikuja kujitambulisha kwako.?
Shahidi: alikuja Mmoja
Mallya: Askari waliowakamata watuhumiwa walikuwangapi
Shahidi: Walikuwa watano
Mallya: Mheshimiwa Jaji ni hayo tuh
Jaji: Mnasemaje Tubreak au tuendelee
Wakili wa Serikali: Tubreak
Jaji: kwa Muda gani
Peter Kibatala: Kwa Sababu tulisha Kaa Dakika 30 tupumzike Kwa Dakika 45
Jaji: Mnasemaje Serikali
Wakili wa Serikali: Sawa
Jaji: Shahidi Tunapumzika, tunywe Maji tutarudi baadae Kidogo
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe
Jaji anaandika Kidogo
Wakili wa Serikali: Kwa Upande wa Jamhuri
Upande Wa Utetezi: tupo tayari Kuendelea
Matata: Shahidi nitakuhoji Maswali Machache utajibu kwa Sauti
Matata: Umesema wewe ni Mwenyeji Wa Miaka 08 pale Rau Madukani
Shahidi: Katika Biashara
Matata: Lakini pia Umesema Unaishi Pale pale
Shahidi: Ndiyo
Matata: Umesema Pale Rau Madukani ni Kata, Kijiji au Kitongoji
Shahidi: Kata ya RAU Madukani
Matata: Utakubaliana na Mimi Hukusema Pale no Kata ya RAU Madukani
Shihidi: Ndio
Matata: Utakubaliana na Mimi hujatutajia Unatoka Mtaa Gani hiyo Kata Ya Rau
Shahidi: Sikuulizwa
Matat: Hujatutajia Hata MwenyeKiti wa Mtaa wako
Shahidi: Sijaulizwa
Matata: hujatuambia pia Kuwa unaishi kwenye Nyumba yako au Nyumba ya Kupanga
Shahidi: Sikuulizwa
Matata: Unaishi Nyumba yako au Umepanga
Shahidi: Nimepangisha
Matata: Kuna Mkataba Ulileta hapa Kwamba wewe Umepanga Rau
Shahidi: Sikuleta
Matata: umetutajia Umepanga Nyumba ya Nani
Shahidi: Sijaulizwa
Matata: Umesema Unafanya Shughuli Ya Kuuza Mbege
Shahidi: Ndiyo
Matata: hujasema kama Mbege Unanunua au Unaitengeneza
Shahidi: Sijaulizwa
Matata: Umesema Pale Rau Una eneo la Biashara
Shahidi: Ndiyo
Matata: Umeonyesha Hati wala mKataba wa Pango
Shahidi: Hapana
Matata: Umesema Wakati wa Maelezo Yako Una Glocery, Stationary, Kibanda Cha Simu
Shahidi: Ni sahihi lakini sasa....
Matata: Inatosha
Matata: hujatutajia Mtu Yoyote zaidi ya Huyo Esther ambaye ni Shahidi
Shahidi: Sijataja
Matata: hujatutajia Hata Saloon au Mtu aliyekuosha Hizo Nywele
Shahidi: Sijaulizwa
Matata: Wakati Ukiwa eneo lako la Biashara uliona Vijana wangapi wakiwa wanakunywa Bia
Shahidi: Niliona watatu
Matata: Ukasema Walikuwa wanasajili laini za Simu
Shahidi: ndiyo
Matata: Wakati Unahojiwa na Wakili Mallya Ukasema hawasajili laini
Shahidi: walikuwa wamekaa Meza Moja na Kijana anayesajili laini
Matata: Mahakama Ichukue Lipi walikuwa Wanakunywa Bia, Wanasajili Laini au Walikuwa waMekaa Mezani?
Shahidi: Ichukue Yote kwa sababu yalikuwa yanafanyika kwa Pamoja
Matata: Mtu anaweza Kuwa anakunywa Bia, anasajili Line na wakati huo huo amekaa mezani..?
Shahidi: Ndiyo
Matata: ulielezea Mahakama Kwamba Mlifika Saa ngapi Polisi
Shahidi: Hapana Sikuulizwa
Matata: naomba Exhibit P2
Matata: Shika Maelezo Yako
Matata: Wakati Unaulizwa na Wakili ulisema aliyekuwa anashuhudia ni wewe na Esther Sasa iambie Mahakama Katika Maelezo yako ni wapi Esther ametajwa
Shahidi: Hajaandikwa
Matata: Mheshimiwa ni hayo tu
Kibatala: Shahidi saa hizi ni Saa ngapi?
Shahidi: Saa 9 Kasoro
Kibatala: umeona wapi
Shahidi: Kwenye Saa
Kibatala: unaona yake Magari pale Nje
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Rangi gani
Shahidi: Ni Pink, Nyeupe na Blue
Kibatala: na Hapo hujavaa Miwani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mallya alipokuuliza kwa sababu ya kutomtambua Mshitakiwa Ukasema Unatatizo la Macho na Sababuhujava Miwani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ila Kwa Sasa wakati nakuuliza hujava Miwani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na wala hujamuomba Mheshimiwa Jaji Uvae Miwani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Umekuja Hapa ukitokea wapi
Shahidi: Gesti
Kibatala: Mara ya Mwisho Kuwa Rau Madukani ni lini?
Shahidi: Ijumaa
Kibatala: Ulikuwa Unaendelea na Kuuza Mbege Rau..?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: aliyekuuzia Mbege Mwezi wa 05 ni nani?
Shahidi: Mama kazi Moto na Mmoja anaitwa Paulo
Kibatala: Wewe Majina Mengine ni Mama Pendo..?
Shahidi: Ni kweli
Kibatala: na Ni kweli husimami wewe Peke yako kuna Mtu anakusaidia
Shahidi: Wakati upi
Kibatala: Ni Kipindi Kipi Binti yako alikuwa anauza pale
Shahidi: Alianza Juzi Jumamosi
Shahidi: ananyoosha Kidole
Kibatala: Unataka Kurekebisha Jibu
Shahidi: Kuna Binti yangu ananisaidiaga Usafi
Kibatala: anaitwa Nani
Shahidi: Naitwa Pendo
Kibatala: katika Ushahidi wako Ulizungumza Lolote kuhusu huyu Pendo
Shahidi: Sikuzungumza
Kibatala: pale Rau Madukani Karibu na Tukio lilipotokea kuna Mtu anaduka la Vipodozi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kuna Mtu ana Duka la Jumla
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Mtu huyo Mwenye Duka la Jumla Ndiyo yenye fremu za Vipodozi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Na Pana Flemu 4 kwa Upande Mmoja
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Upande wa Pili ndiyo wanauza Vinywaji
shahidi: ndio
Kibatala: Anayeuza Duka la Vipodozi anaitwa Athima
Shahidi: Sijui Jina lake
Kibatala: ila Unajua ni Mmama au Mdada
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na ndiyo anakaa Mbele ya Duka lake
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Picha hii tunayozungumza, ulimchorea Jaji hiyo Picha
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unajua kuwa kwanini unajua kwanini Ujamchorea Jaji
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ni Kwasababu wewe Ni Shahidi wa Kupanga
Shahidi: Hapana Kabisa
Jaji: Naliondoa hilo Swali
Kibatala: Twende kwenye Bastola
Kibatala: Ulikuwa unampekua
Shahidi: Hapana
Kibatala: ulijuaje Kuwa kulikuwa na Vitu vigumu
Shahidi: Baada ya kutoa kwenye mfuko
Kibatala: na Ulishuhudia MADAWA ya Kulevya
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unga ni kitu kigumu
Shahidi: Kitu kilaini
Kibatala: Kuna sehemu uliona namba za Bastola CZ 100
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mpaka unamaliza Zoezi la Kuulizwa na Serikali hakuna aliyekutajia hizo namba
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unakumbuka ulisema zilipatikana Risasi tatu na Magazine
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: hapa Mahakamani Umeonyeshwa hizo Risasi
Shahidi: Hapana
Kibatala: kwa hiyo hujamsaidia Mheshimiwa Jaji Kuwa kutambua Risasi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Umesema Kuhusu Magazini, unajua magazine inakaa wapi kwenye Bastola
Shahidi: Upande wa Chini
Kibatala: Umemwambia Mhe. Jaji Kwa Kufafanua Kuwa Magazine inakaa hapa
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati Umetoa maelezo yako ambayo yapo katika D2 kwamba Kuna Afisa Wa Askari Alichomoa Magazine Ukaona Risasi 03
Shahidi: Nilisema
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba Kielelezo Namba D2
Kibatala: Nionyeshe ni wapi
Shahidi: Hakuna Sehemu Kama hiyo
Kibatala: Kwa hiyo tunakubaliana Jibu la Kwanza ni Uongo
Shahidi: Hapana siyo Uongo, Makosa ya Mwandishi
Kibatala: Nichukie lipi sasa
Shahidi: Chukua Yote
Kibatala: ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuna Kitu Mwandishi amekiacha ambacho Mimi nilikisema. Ulimwambia Mheshimiwa Jaji
Shahidi: sikumwambia
Kibatala: Ni sahihi Kuwa Kielelezo D2 haitaji Jina la Askari yoyote isipokuwa Jumanne
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: kwa sababu walijitambulisha ukajisahau
Shahidi: Ndiyo walijitambulisha Nikasahau
Kibatala: Unatatizo la Kumbukumbu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Soma Kuanzia Neno baada ya Upekuzi huo
Shahidi: Nilishuhudia na Kusaini Fomu za Upekuzi
Kibatala: Mwambie Mhe. Jaji hapo kwenye watu wawili kama Umefafanua
Shahidi: Hapana
Kibatala: Pia Mlisaini Wote
Shahidi: Ulifafanua, Neno Watu wote
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati yanaandikiwa Uliambiwa ni Maelezo ya Kisheria au Mapambo
Shahidi: niliambiwa ni Maelezo Yangu
Kibatala: Kwa Mujibu wa maelezo haya Adam Kasekwa Ulifahamu Jina Lake Baada ya Upekuzi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unafahamu Mshitakiwa tuliye naye ni Adam Kasekwa Maarufu Kama Adamoo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unakubali Hakuna Sehemu uliyotaja Adamoo
Shahidi: Ndiyo Sikutaja
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji ni kweli au siyo Kweli Kwamba Katika Kielelezo ukichosema hapo Hakuna Adamoo
Shahidi: Hakuna Adamoo
Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kwamba Unatakiwa Kusema Ukweli ndiyo Maana Unaapishwa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Jaji akupime Ukweli au Uongo wako kwa hilo Soma hapa
Shahidi: Adam Kasekwa Adamoo
Kibatala: awali ulisema ipo au haipo
Shahidi:Nilisema Haipo
Kibatala: Sasa wewe ni Muongo au Mkweli
Wakili wa serikali: OBJECTION Pius Hilla Swala la Kweli au Uongo aiachie mahakama
Jaji: Naona Shahidi anaweza Kujibu yeye ni Mkweli au Muongo
Wakili wa Serikali: Sawa Mheshimiwa
Kibatala: Swali langu lipo palepale Kutokana na Mgongano wa Majibu, Mwanzoni Ulisema jins ls Adamoo Haipo na baadae tukasema Kwa pamoja Ukaona Ipo, Wewe ni Shaidi wa Ukweli au Uongo
Shahidi: Mimi ni Shahidi wa Ukweli
Wakili wa Serikali: Robert Kidando Hiyo sehemu ichukuliwe kwa makini
Kibatala: Sijaona Objection na Shahidi amejibu
Jaji: Mimi sijasikia Swali
Kibatala: Unakumbuka ulisema uligundua namba ya Bastola..?
Shahidi: afande Jumanne
Kibatala: Na ndiyo Unavyosema Katika Maelezo yako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Hakuna mahala Umesema Kuwa "Mimi ndiye niliyesoma na Kugundua Namba za Bastola
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo
Shahidi: Kwenye hiyo Fomu Hakuna
MAHAKAMA kichekoooooo
Kibatala: Wacha Nirudie tena
Kibatala: Kuna Mahala Umesema wewe Ulisema namba za Bastola
Shahidi: Kwenye maelezo haijaandikwa
Kibatala: Katika MAELEZO yako kuna Mahala au Kuna sehemu Yoyote Kuna Jina Luger..?
Shahidi: Lipo
Kibatala: hii fomu alijaza nani?
Shahidi: afande Jumanne ndiyo alijaza
Kibatala: ulimfafanulia jaji tofauti ya Kielelezo Kimoja kina Luger na Kingine hakina
Shahidi: Hapana sikumfafanulia
Kibatala: Katika Maelezo Yako E2 ulitaja Aina za simu, Je Namba ya Simu Uliweka Kwenye Kielelezo Chako
Shahidi: Hapana Sikuweka
Kibatala: na wala hiyo Tofauti hukufafanua
Shahidi: Sikufafanua
Kibatala: Shahidi Unafahamu IMEI namba za Simu ya Adama Kasekwa?
Shahidi: Hapana
Kibatala: na wala hukufahamu kuwa kuna IMEI Moja wala 02
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikal hukufafanua kuhusu IMEI Moja au Mbili kwa Mtu anayeitwa kasekwa
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wala Hukuomba Ujikumbushe labda kwa Sababu Namba ni Nyingi, Ulifanya hilo zoezi
Shahidi: Hapana
Kibatala: katika hiyo Karatasi Kuna Maneno kama CZ 100 ya Kufafanua hiyo Bastola
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Walikwambia Karatasi hii Ndiyo inatakiwa kumtia Hatiani Mshitakiwa bila Kuacha Shaka yoyote
Shahidi: Niliambiwa
Kibatala: Twende Simu Card ya Vodacom
Kibatala: Unafahamu Kwanza hiyo ICCD namba
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo Unakubaliana nami kwamba hizo ICCD Namba ambazo ndiyo Utambulisho katika Ushahidi wako hazijaingia
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: hata namba ya Adam Kasekwa ya Hallotel kuhusu ICCD namba, hukutaja hivyo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: wala hukufafanua
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: wala hujazungumzia Kabisaaaa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: katika Ushahidi wako ulitambua huyu kama nani
Shahidi: Kama Mohammed Ling'wenya
Kibatala: Katika Ushahidi Wako ulimtambua Mtu anaitwa Mohamed Abdilah Ling'wenya
Shahidi: Hapana Sikutaja Ling'wenya
Kibatala: Kwenye Statement D2 Ulimtaja huyu Kama nani tunakubaliana tutakachokipata pia tukitumie
Shahidi: ndiyo
Kibatala: Naomba D2 Kibatal:a Taja huyo Mtu humo Umemtaja Kama Mohammed Abdalahi Ling'wenya
Shahidi: Ndiyo Mohamed Abdilah Ling'wenya
Kibatala: Mwanzoni Umesema Halipo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulifafanua Kuwa Katika Utambuzi hapa Mahakamani na ile Hati yako ya maelezo pamoja Na kutofautiana, Ulifafanua Kwa Jaji kwamba huyo ni Mtu Mmoja
Shahidi: Shapana
Kibatala: Katika Ushahidi Wako Kuna Mahala Popote umezungumzia Kuna Afisa Wa Polisi anaitwa Ramadhan Kingai
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati Maafisa Wa Polisi wanajitambukisha ulikwepo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala Hakuna Mahali Umezungumzia Kuhusu Kingai, Kwamba alikwepo ila hujamtaja
Shahidi: Sijazungumza hilo
Kibatala: Wakati Unaulizwa Maswali na Mtobesya kuhusiana na Saini zako na Kuna Mazingira zinatofautiana na Kwamba Kuna fomu ulisaini Ukiwa Umesimama
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Wakati Jumanne anajaza hii fomu pia alikuwa amesimama?
Shahidi: Ndiyo alikuwa amesimama
Kibatala: mara zote wakati Unatoa Ushahidi wako Ulikuwa Unatoa Maneno "Glocery" Mwambie Mheshimiwa Jaji Katika Maelezo yako kuna Neno Glocery?
Shahidi: hakuna
Kibatala: Maneno gani uliyatumia
Shahidi: Bar
Kibatala: Ulifafanua kwa Mheshimiwa Jaji Kwamba Ulikuwa unalenga Kitu Kimoja hicho hicho
Shahidi: Sikufafanua
Kibatala: Kati yako wewe na Fremu 4 za Jumla na Vipodozi na Upande wa Pili Ndiyo Glocery na Kwamba Sehemu yako ya Mbege ni Nyuma kabisa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kutoka Kwenye Fremu 4 Duka la Vipodozi hadi eneo la Tukio ni hatua ngapi?
Wakili wa serikali: Objection Shahidi ameshasema hamfahamu Athma
Kibatala: Kutokaa kwenye Flemu 4 Mpaka waliokamatwa hawa ni Kama Hatua ngapi
Shahidi: Kama 10
Kibatala: Bado Unasisitiza Ushahidi wako waliwaacha hawa wa kwenye Fremu hatua Tatu wakakufuata wewe wa Hatua 10
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Shahidi Unafahamu au hufahamu Mmlilki wa hilo Duka la Jumla na Duka la Vipodozi ni Dada yake Ling'wenya.?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: hilo eneo lina Kiongozi wa Mtaa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: anaitwa nani
Shahidi: Sigfrid Malewa
Kibatala: Katika hizi Hati hapa unaona Jina la Sigfrid Malewa
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Msaidizi Wake anaitwa nani
Shahidi: Namjua Kwa Jina Moja la Temba
Kibatala: anaishi wapi na eneo hilo
Shahidi: anaishi Mbali
Kibatala: katika Kielelezo chako Namba 02 Mnamo tarehe 05/08/2020
Shahidi: Ni kweli nilisema hivi
Kibatala: Kwamba Saa 7 Kamili Mchana
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi Wako Ulitoa Ufafanuzi kwamba Ulikuwa ni Muda wa Makadirio
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Huko Saloon Ulikaa Muda gani?
Shahidi: Kama Robo Saa
Kibatala: Na Ukamwambia Mallya Ukarudi Sehemu ya Biashara Kwa muda gani
Shahidi: Kama Robo saa
Kibatala: kwa hiyo kama Saa Saba Na Nusu
Kibatala: kwa hiyo kama Saa Saba Na Nusu
Kibatala: Na Katika Kielelezo Chako D1 Maelezo uliyoyatoa Ulisema ni Saa Saba, Si Unaona kuna tatizo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Tatizo ambalo hukulitolea Ufafanuzi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Nani atutatulie hili tatizo
Shahidi: Mimi Mwenyewe
Kibatala: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali nilikusikia ulisema, hawa washitakiwa wawili walipigwa Pingu, ulimwambia Mheshimiwa Jaji Sasa Kama baada ya Kupigwa Pingu nini Kiliwatokea
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Mlifika central police Kwa usafiri gani
Shahidi: Watuhumiwa WALIENDA kwa Gari Nyingine na sisi tukaenda na Gari Lingine
Kibatala: na ukamwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba na hilo gari lina Maofisa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Aliwahi Kukwambia Kesi Mama ipo Dar es Salaam
Shahidi: Hakuwahi kuniambia
Kibatala: Wewe ulikuwa unajua kesi na Kila kitu kipo Moshi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: ulisikia hao Maaskari wanaongea na Mtu yoyote kuhusu washitakiwa Kukamatwa
Shahidi: Hapana
Kibatala: ulisikia Maofisa Wa Askari, Kwamba Yupo wapi Moses Lijenje
Shahidi: Nilisikia akimuuliza Mwenzenu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji huyo Mwenzao Katika Statement Yako D2 umezungumza Walikuwa wangapi
Shahidi: Watatu
Kibatala: Maelezo yako chini ya Kiapo, Kielelezo D2 ulizungumzia kuhusu Vijana watatu
Shahidi: Hapana
Kibatala: we Umezungumzia wangapi
Shahidi: wawili
Kibatala: palikuwa na Vijana wawili wanakunywa pale, Ndiyo ukivyosema
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji huyo Kijana wa tatu, umezungumzia Nini Kilitokea huyo Kijana wa tatu.?
Shahidi: Hapana
Kibatala: zoezi la Kusajili laini ya Simu, uliona kwamba wanasajili Simu
Shahidi: Ndiyo niliona
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji walikuwa wanasajili Laini ya kampuni Gani
Shahidi: Sijui sasa Kibatala: Unafahamu iwapo Ndiyo au Lah kwamba hii laini ya Hallotel au Airtel ndiyo zilikuwa zinasajijiwa Siku hiyo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mlivyofika pale Polisi Central Station Moshi Iwapo Ulimwambia Chochote Kuhusu Kushuhudia Vile Vifaa Vikiingizwa Kwenye Daftari rasmi
Shahidi: Hapana
Kibatala ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Iwapo hawa washitakiwa wawili walikuwa na vitu kama Wallet au Kitu Kingine anavyobeba Kijana wa Kiume.
Shahidi: Sijazungumzia
Kibatala: Wewe Kama shahidi Huru, Kama Ulishuhudia MALI Binafsi za Washitakiwa Kuingiziwa kwenye Daftari Maalum pale Kituoni
Shahidi: Si kumwambia
Kibatala: nimesikia mara kadhaa unataja DADA Esther ulifafanua Kwa namna yoyote ile
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba huyu Dada Esther Unamfahamu anaishi wapi
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unafahamu Watu wenye Biashara Ndogo Ndogo hupewa Kitambulisho Maarufu Kama Kitambulisho cha Wamachinga
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: ulimuonyesha Mheshimiwa Jaji ili ajue Kuwa Unakitambulisho
Shahidi: Hapana
Kibatala: ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Biashara yako inaitwaje kama vile Mama Mbege
Shahidi: Hapana
Kibatala: hata kumwambia Mheshimiwa Jaji kwamba Umesahau kutaja Jina la Biashara yako ulisema
Shahidi: Sikusema
Kibatala: ulisema hapa kwamba Mohamed Abdilah Ling'wenya Alikuwa amevaa Nguo gani wakati anakamtwa
Shahidi: Sikusema
Kibatala: na Adamu Kasekwa ulisema amevaa Nguo gani
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama Ulisema ulishuhudia kielelezo Namba Moja kilijazwa Kwenye Fomu tatu na Fomu Moja akapewa Adam kasekwa
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulisema Kwamba Ulisikia Afisa wa polisi akisema Unahaki ya kupata fomu Moja ya Hati za Kuchukulia hiyo Bastola
Shahidi: Hapana
Kibatala: unasema Ulifanya Kazi na Afisa wa Askari Wa a Polisi Jumanne, na baadae wakakuonyesha Afisa Mwingine wa Polisi aliyekuchukua maelezo Je ulitolea Ufafanuzi kwa Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Hapana
Kibatala: Leo umesema Kwamba Bastola Ina Rangi Nyeusi, Je katika Maelezo yako Kuna Sehemu Umetaja Rangi ya Bastola
Shahidi: Hapana
Kibatala: kwa hiyo Rangi umetaja Leo
Shahidi; Ndiyo
Kibatala: ulifafanua Kwa Mheshimiwa Jaji kamba wewe kabla Ulikuwa Unaifahamu kabla
Shahidi: Hapana
Kibatala: Pamoja na Kwamba Wakati Ule ndiyo Ulikuwa na Kumbukumbu, Maana umesema wewe Tukio la Muda Mrefu, Mpaka unasahau, Lakini wakati Ule Hukusema Rangi ya bastola.
Kibatala: nimesikia umesema Vitu vinavyodhaniwa kuwa Madawa ya kulevya, Je kuna Mtu yoyote alimtuhumu baada ya Kupatikana kwa Madawa ya kukevya
Shahidi: Hapana?
Kibatala: kwa Ushahidi wako wewe unasema Adam Kasekwa alipatikana na Madawa ya Kulevya
Shahidi: Sikufahamu hatima yake
Kibatala: Kuhusu Saini ya D01 na D02 ulifafanua kabla ya Wakili Mtobesya Kuuliza maswali
Shahidi: Hapana Sikufafanua
Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwa Shahidi Huyu naomba Kuishia hapo
Jaji anaandika
Wakili wa Serikali: Tunaomba Hairisho ili tuweze Kumalizia Asubuhi
Jaji: Kuna Kama Dakika 50 hivi ilituweze Kuhitimisha Leo
Wakili wa Serikali: Sawa Mheshimiwa Ngoja tuendelee
Jaji: Wakili wa Serikali Esther Martin
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Mahakamani na Malya Kuhusiana na Rangi za Tshirt na ukasema siyo Nyeusi Bali Rangi ya Dark Green, Wewe ulikuwa Unaona nini
Shahidi: Nyeupe, Kijani na nyeusi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Maswali Kwenye Kielelezo D2 ukaambiwa Vitu mbalimbali Kwenye Maelezo hayo uliyoandika Polisi Watuhumiwa hawakujulishwa Makosa yao, Na Mengine Mengi fafanulia mahakama ni Vipi hayo yamejitokeza
Shahidi: Rudia Swali
Wakili wa serikali: Swala la Watuhumiwa baada ya Kuambiwa Kaa chini kama walijulishwa Makosa yao, Mahakamani umesema lakini humu hayapo
Mtobesya: samahani, Shahidi anaenda kujazia Statement
Jaji: tungemuacha ajibu kwanza
Wakili wa Serikali: Nasema wakati wakili anamuuliza Maswali akakuuliza kuhusu Maswali Ambayo Hapa Mahakamani umesema ila Kwenye Maelezo Hakuna, Ni kwa vipi hayo yamejitokeza
Shahidi: Yamejitokeza kwa sababu ni uandishi tu
Wakili wa Serikali: Kivipi Shahidi: Katika Kutoa......Maelezo niliyoandika na maelezo ya hapa mahakamani.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Kuhusu Maelezo haya, pia kwamba Fomu iliyosainiwa eneo la Tukio ni Moja lakini Mahakamani umesema Fomu nne
Shahidi: Kimetokea tu Lakini fomu zilikuwa Nne
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kwamba Ulijuaje kwamba Ulichokiona ni Kitambulisho Cha Polisi, Ukasema Ukaona Chata ya Taifa
Jaji: Siyo Chata Bali Chapa
Shahidi: Nilikuwa namaanisha Chapa ya Kipolisi
Wakili Malya: Tunapinga hilo Jibu
Jaji: sahihi, Hakujibu hivyo
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kama Ulionyesha CZ 100, Fafanunua Mahakamani wewe Uliona nini
Shahidi: Niliona A5340
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Kwamba Kwenye Maelezo haya Uliyasoma na Uliyajua Majina Baada ya Upekuzi lakini Mahakamani Umesema Kabla ya Upekuzi
Shahidi: Niliyajua hayo Majina Kabla ya Upekuzi
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Mimi nimemaliza namuachia Mwenzangu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Uliulizwa Kama Vijana wawili pale Rau Uliwaona Wakisajili laini na Baadae Ukasema Walikuwa na Kijana anayesajili laini
Shahidi: Mimi niliwaona na Kijana anayesajili Laini
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kwamba hao Vijana walikuwa wawili na Baadae Ukasema watatu. Wakati gani Uliwaona wakiwa watatu
Shahidi: Wakiwa wanasajili laini
Wakili wa Serikali: Wakati gani walikuwa wawili
Shahidi: Wakati wa Ukamatwaji
Kibatala: Objection anasema Jina la Amelifahamu lini it's a New fact
Jaji: hili swali limezungumza Katika Mazingira Matatu Kama alitaja, Kama ALIJAZA fomu na Kama alitaja kabla Hili Jibu la Lini alimfahamu nafikiri siyo Fact Mpya
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kwenye Fomu kuhusiana na Neno Adamoo Kama Ulikuwa umelisema, Fafanua Hapa Mahakamani Jina la Adamoo Umelifahamu lini
Shahidi: Nimelifahamu Leo
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kuhusiana na Ukamataji kuhusiana na Lile Neno CZ100 Halipo, elezea Kilichoandikwa kwenye Hati hiyo ni nini
Shahidi: Iliandikwa namba A5340
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia na Kuhusu Hati yako Kuhusu Glocery na Huku ni Bar, Kwa Mujibu wa Ushahidi wako walikuwa kwenye eneo lipi
Shahidi: walikuwa kwenye Glocery ya Dada Esther
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kuhusiana na maeneo waliokamatwa watuhumiwa haswa tarehe 05 Mwezi 08 Ukasema Duka la Jumla na Vipodozi na ulipokuwa wewe Eneo lipi walikuwa karibu
Shahidi: eneo waliokamatwa ni Karibu na Sehemu yangu ya biashara.
Wakili wa Serikali: kwanini jina Sweetfred Malewa Halipo kwenye Hati ya Upekuzi
Shahidi: Sikuulizwa
Wakili wa Serikali: Kuhusu wewe Kufika kwemye eneo lako la Biashara, Muda gani ulienda Saloon na Muda wa Ukamataji kuwa saa Saba, Kilichotokea kilikuwa saa ngapi
Shahidi: ilikuwa majira ya Saa Saba Mchana
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kama uliona Watuhumiwa kama walipofikishwa Polisi, Kama Ulishuhudia Uandikishwaji wa vitu vyao Kwanini hukutoa Ushahidi huo
Shahidi: Sikutoa sababu Sijaulizwa
Jaji: Jamani Mnasikia hukoooooo.? Mahakama Hatusikiiiiiii
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kwamba kama katika Ushahidi wako alikwepo Askari anayeitwa Kingai kama alikwepo Askari yupi aliyehusika Kwenye eneo la Ukamataji Kwa Siku hiyo
Shahidi: sikumzungumzia kwa sababu Sikuulizwa ni Askari gani aliyekamata anajibu Kwa Sauti ya Chini sana
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Tukomee hapa
Jaji: Shahidi Nashukuru kwa Ushahidi Wako
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tunaomba Hairisho Mpaka Kesho Saa 03 Asubuhi ambapo tutaendelea na Shahidi Mwingine
Upande wa Mashitaka
Kibatala: Mheshimiwa hatuna Pingamizi
Jaji anaandika Kidogo
Jaji : basi Maombi ya hairisho yanakubaliwa hadi Kesho saa 03 Asubuhi Upande wa Mashitaka Maelekezo ni kwamba Mtatakikwa mlete shahidi Na Washitakiwa wataendelea Kuwa Rumande Mpaka Kesho saa 3 Asubuhi
Jaji anatoka
Fuatilia hapa kujua kitakachojiri katika mchakato mzima wa kesi hiyo kwa siku ya leo 11/01/2021
==========
Watuhumiwa wote wamekwishawasili katika ukumbi wa mahakama tayari kuanza kwa kesi.
Jaji: Ameingia sasa
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa
Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe na wenzake
Wakili wa Serikali, Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
1. Pius Hilla
2. Abdallah Chavula,
3. Jenitreza Kitali,
4. Nasorro Katuga,
5. Esther Martin,
6. Ignasi Mwinuka
7. Tulimanywa Majige
Wakili Peter Kibatala anawatambulisha Mawakili Wa Utetezi
1.Jeremiah Mtobesya
2.Michael Mwangasa
3.Seleman Matauka
4.Nashon Nkungu
5.Alex Massaba
6.Michael Lugina
7.Maria Mushi
8.Hadija Aron
9.Dickson Matata
10.Jonathan Mndeme
11.Fredrick Kihwelo
12.John Malya
Jaji: anawait Washitakiwa 1,2,3 na 4 Wanasimama Kuitikia
Wakili wa Serikali: Kwa Upande wetu tuna shahidi Mmoja kwa Leo na tupo tayari Kuendelea Kwa Upande wetu tupo tayari kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Tupo tayari na sisi Kuendelea
Wakili wa Serikali: Mmoja anatoka Kwenda Kumuita Shahidi Nje ya Chumba Cha Mahakama Mahakama Ipo Kimya Kidogo
Shahidi anapita ni Mdada Kajitanda Buibui na Kavaa Barakoa Kubwa sana Kumziba Sura,
Jaji: Majina Yako
Shahidi: Anita Varelian Mtali
Jaji: umri Shahidi: 45yrs
Jaji: Kabila
Shahidi: Mchaga
Jaji: Shughuli Zako
Shahidi: Nafanya Biashara
Jaji: Dini yako
Shahidi: R. C
Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii Kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa ni kweli, kweli tupu Eeeh Mungu nisaidie
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Shahidi Ataongozwa na Wakili Esther Martin
Wakili wa Serikali: Esther Ikumbushe Mahakama Majina yako
Shahidi: Anita Varelian Mtali
Wakili wa Serikali: Unaishi Wapi
Shahidi: Moshi, RAU madukani.
Jaji: Jina lako la Tatu sijalipata Vizuri ni Mtali.?
Shahidi: Mtaro
Wakili wa Serikali: Umeishi kwa Muda gani Rau
Shahidi: Miaka 08
Wakili wa Serikali: Unafanya Shughuli gani
Shahidi: Nafanya Biashara ya Kuuza Mbege
Wakili wa Serikali: Ulianza lini Biashara yako ya Mbege
Shahidi: Miaka 08 ninayo
Wakili wa Serikali: Mbali na Biashara yako ya Mbege una bishara gani Nyingine
Shahidi: Kuna Glocery, Stationary, Banda la Tigo Pesa na Kuna Sehemu ya Kutolea Movie
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama 05 Mwezi 08 2020 ulikuwa wapi
Shahidi: Sehemu yangu ya Biashara, Nikifanya Usafi
Wakili wa Serikali: Saa ngapi
Shahidi: Saa Saba Kasoro
Wakili wa Serikali: Ya Muda gani
Shahidi: Ya Mchana
Wakili wa Serikali : Kabla ya Kufika eneo lako la Biashara ulikuwa umetoka wapi?
Shahidi: Nilikuwa Nimetoka Nyumbani Nikaenda Saloon Kuosha Nywele
Wakili wa Serikali: Na Ulipotoka Saloon kuelekea sehemu yako Kufanya Usafi
Shahidi: Nilikuta Wakaka Watatu walikuwa wamekaa Mbele Yangu walikuwa wanakunywa na Kusajili Laini
Wakili wa Serikali: Walikuwa wanakunywa nini
Shahidi: Walikuwa wanakunywa Bia
Wakili wa Serikali: Hizo laini walikuwa wanasajili wapi
Shahidi: Kuna Vijana wanapitaga Mitaani Kusajili Laini
Wakili wa Serikali: Ukiwa unafanya Usafi kitu gani Kingine ulishuhudia
Shahidi: Kuna wakaka wawili walikuwa wanapitapita wakiongea na simu, Wanaenda wanarudi wakiongea na Simu
Wakili wa Serikali: Hao wanaopita ni tofauti na wale uliposema walikuwa wanakunywa Bia
Shahidi: Hapana ni walewale
Wakili wa Serikali: Kutoka Kwako Unapofanyia Kazi Mpaka Glocery ni Umbali gani
Shahidi: Kama Hatua 10
Wakili wa Serikali: Hapo Katikati sasa, Kati ya Glocery na ulipo, pana kitu gani
Shahidi: Pana uwazi
Wakili wa Serikali: Baada ya Muda kitu gani kilitokea
Shahidi: Wakati wanaongea na Simu Walitokea watu wawili wakaongea kwa sauti kali "Mpo chini ya Ulinzi Mnahusika na Mambo ya Kigaidi, chuchumaa Chini Mikono Juu"
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine ulisikia
Shahidi: Chuchumaa Chini Mnahusika na Mambo ya Kigaidi Wakili wa Serikali: Ni watu gani sasa hao
Shahidi: Ni Askari
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unafanya nini wakati huo
Shahidi: Nafanya Usafi
Wakili wa Serikali: Pana umbali gani kutoka Walipo na Mpaka Ulipokuwa unafanya Usafi
Shahidi: Hatua 05
Wakili wa Serikali: Ulisikia nini Kingine
Shahidi: Sikusikia Kingine zaidi ya Chuchumaa Chini Nyoosha Mikono Juu
Wakili wa Serikali: Walikuwa Askari wangapi
Shahidi: Wawili
Wakili wa Serikali: Hali ya Pale ilikuwaje
Shahidi: Ilikuwa ni Utulivu
Wakili wa Serikali: Nini Kilifuata
Shahidi: Walitokea Askari Wengine watatu wakawa wamefika eneo la Tukio
Wakili wa Serikali: Ongeza Sauti
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kiliendelea
Shahidi: Baada ya Kuwa Askari watano alitokea Mmoja akaniambia anaomba nisogee anahitaji Kuwafanyia Upekuzi
Wakili wa Serikali: Ni Askari gani huyo
Shahidi: Alinitambulisha anaitwa Askari Polisi Jumanne
Wakili wa Serikali: Ulifanya nini kujiridhisha?
Shahidi: Alitoa Kitambulisho Akanionyesha
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo nini kilifanyika
Shahidi: Alimsimamisha Mmoja
Wakili wa Serikali: Kabla ya Kumsimamisha..?
Shahidi: Afande Jumanne alijipekua kuanzia Kifuani akatoa Mifuko Nje
Wakili wa Serikali: We ulikuwa na nani wakati huo
Shahidi: Dada Mmoja anaitwa Esther
Wakili wa Serikali: Kutoka Eneo la walioambiwa Wachuchumae Chini, palikuwa na Umbali gani?
Shahidi: Kama Hatua Mbili
Wakili wa Serikali: Kuna Kitu gani Kingine
Shahidi: Raia walikuwa wamekuja
Wakili wa Serikali: Kabla ya Raia Kusogea eneo hilo palikuwa na hali gani?
Shahidi: Palikuwa na Jua
Wakili wa Serikali: ahaa ahaaa yani hali ya pale ilikuwaje?
Shahidi: Palikuwa pametulia
Wakili wa Serikali: Ikaendelea nini?
Shahidi: Alimsimamisha Mmoja akamuuliza Unaitwa nani?
Wakili wa Serikali: Akajibu anaitwa nani?
Shahidi: Adam Kasekwa
Wakili wa Serikali: Akamwambia nini?
Shahidi: Akiwa amenyoosha Mikono Juu akamwambia Geuka, akageuka
Wakili wa Serikali: Baada ya Kugeuka
Shahidi: Askari Jumanne alianza Kumpekua Kuanzia Kichwani, Mabegani, Alipofika Kiunoni alikuta Kitu kigumu
Wakili wa Serikali: Alikikuta Upande gani
Shahidi: Kushoto
Wakili wa Serikali: Maeneo Gani?
Shahidi: Niliona ni Bastola
Wakili wa Serikali: Ulijuaje kama ni Bastola?
Shahidi: Afande Jummane alituambia ni Bastola
Wakili wa Serikali: Halafu
Shahidi: akatuonyesha namba
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni namba gani.?
Shahidi: A5340
Wakili wa Serikali: Zilikuwa kwenye nini
Shahidi: Kwenye Bastola
Wakili wa Serikali: Wakati anakuonyesha Bastola Adam alikuwa wapi?
Shahidi: Alikuwa amesimama
Wakili wa Serikali: Ukiona na nini Kingine
Shahidi: Risasi 03
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi, alipofika Upande wa Kulia akakuta Vitu vidogo vidogo Kwenye Karatasi ya Nailon akasema inasadikiwa ni Madawa ya Kulevya ila itajulikana Mbele.
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ngapi Shahidi: 58
Wakili wa Serikali: ikawaje
Shahidi: Aliendelea Kumpekua akamkuta na Simu Ndogo aina ya Itel
Wakili wa Serikali: Hiyo simu akaifanyaje
Shahidi: Akatoa laini akakuta namba akaziandika
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo aliendelea na nini
Shahidi: Akamwambia Naomba fomu, .......akaleta fomu
Wakili wa Serikali: fomu ngapi
Shahidi: Zilikuwa Mbili
Wakili wa Serikali: Akafanya nini sasa Kwenye ile Fomu
Shahidi: Kaandika Vitu alivyokuwa amempekua
Wakili wa Serikali: Umesema palikuwa na fomu Mbili, fomu ya kwanza akijaza nini
Shahidi: fomu ya kwanza alijaza Bastola, Risasi na Laini
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni laini gani
Shahidi: Laini ya Voda na Airtel
Wakili wa Serikali: Baada ya Kumalizia fomu ya kwanza
Shahidi: alichukua fomu Nyingine
Wakili wa Serikali: Kabla ya Kujaza Fomu Nyingine
Shahidi: Alipomaliza Kujaza akampa akasaini na Baadae akasaini yeye alipo maliza Kusaini.
Wakili wa Serikali: alimpa nani
Shahidi: Alimpa Adam
Wakili wa Serikali: baada ya fomu ya kwanza nini kiliendelea
Shahidi: alichukua Fomu Nyingine
Wakili wa Serikali: alijaza nini
Shahidi: alijaza vile Vikete vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vingapi Vilikuwa Vingapi
Shahidi: Vilikuwa 58
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: akampa Adam asome alafu asaini na sisi akamtupa tusaini
Wakili wa Serikali: Wewe na nani..?
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada Kumalizia nini kilifuata
Shahidi: akamuita Mwingine
Wakili wa Serikali: huyo Mwingine anaitwa nani
Shahidi: Mohamed Abdulahi Ling'wenya
Wakili wa Serikali: akamwambia nini
Shahidi: asimame ageuke, Baada ya kugeuka akaanza Kumpekua
Wakili wa Serikali: alianzaje Kumpekua
Shahidi: Kichwani Mikononi
Wakili wa Serikali: ilikuwaje
Shahidi: Upande wa Kulia alikuta na Vikete Vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi
Shahidi: 25
Wakili wa Serikali: akafanyeje
Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua
Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua
Shahidi: alikuta Simu aina ya Tecno
Wakili wa Serikali: Rangi gani
Shahidi: Nyeusi
Wakili wa Serikali: akafanya nini
Shahidi: akapekua akakuta kuna laini
Wakili wa Serikali: laini gani
Shahidi: Hallotel
Wakili wa Serikali: baada ya Kupata simu akafanyeje
Shahidi: akazitoa zile Laini, Akampa yule Mwingine akazishika
Wakili wa Serikali: Na Yeye Akaendelea na nini
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi
Wakili wa Serikali: hizo laini alikuwa anafanya nazo nini?
Shahidi: Alimpa Askari wa Pembeni akazishika
Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi
Shahidi: Aliendelea na Upekuzi lakini hakukuta kitu Kingine
Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi
Shahidi: aliomba fomu Mbili
Wakili wa Serikali: fomu ya Kwanza alijaza nini
Shahidi: alijaza vile Vikete Vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi
Shahidi: 25
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo
Shahidi: Alimpa akasema akasaini
Wakili wa Serikali: Nani Yeye, afande Jumanne?
Shahidi: Ndiyo na Baadae Mohamed
Wakili wa Serikali: na baadae
Shahidi: tukasaini sisi
Wakili wa Serikali: Wewe na nani
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: Ile fomu Nyingine akajaza Simu na laini Nyingine
Wakili wa Serikali: Za Mtandao gani
Shahidi: Airtel na Hallotel
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo
Shahidi: Alimpa Mohamed asome kisha akasaini
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: afande Jumanne alituomba na sisi tusome Kisha tusaini
Wakili wa Serikali: Wewe na nani
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada ya Upekuzi
Shahidi: walivalishwa Pingu
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: afande Jumanne akatuomba tuelekee Kituoni
Wakili wa Serikali: Hao walivalishwa Pingu walikuwa ni akina nani
Shahidi: Adam na Mohamed
Wakili wa Serikali: baada ya kuvalishwa Pingu..?
Shahidi: Wakaelekea kwenye Magari, Barabarani
Wakili wa Serikali: Palikuwa na Askari wangapi
Shahidi: Watano
Wakili wa Serikali: Walikuwa wamebeba nini
Shahidi: Wawili walikuwa wamebeba Bunduki
Wakili wa Serikali: Hali ya hewa eneo lile ilikuwaje
Shahidi: ilikuwa imetulia
Wakili wa Serikali: Hali ya hewa ilikuwaje
Shahidi: Kulikuwa na Jua na Mwanga
Wakili wa Serikali: Mlichukua Muda gani kwenye lile eneo Mpaka Mnamaliza Zoezi
Shahidi: Kama Dakika 45
Wakili wa Serikali: Baada ya Kufanya Upekuzi Kuna Vitu Vilipatikana na Kwamba Kuna fomu zilijazwa Sasa fomu ukiziona hapa utaweza Kuzitambua?
Wakili wa Serikali: sasa bada ya Kumalizia Mkaelekea kituoni, kituo gani..?
Shahidi: Central Moshi
Wakili wa Serikali: baada ya Kufika police central
Shahidi: Tuliandika Maelezo
Wakili wa Serikali: Maelezo ya nini
Shahidi: Kitu gani Kilichofanyika ......
Wakili wa Serikali: Tukianza na fomu ya Adam utaitambuaje
Shahidi: Kwa vitu vilivyoaandikwa, Jina langu na sahihi yangu
Wakili wa Serikali: Kulikuwa na nini Kingine Bastola
Wakili wa Serikali: Kingine
shahidi: Palikuwa na Risasi
Wakili wa Serikali namba gani Shahidi: A5340
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba nimpe fomu aweze Kuitambua
Wakili wa Serikali: Shika hii Karatasi iangalie kwa Makini
Shahidi: Ndiyo yenyewe
Wakili wa Serikali: Yenyewe nini
Shahidi: Fomu niliyo saini
Wakili wa Serikali: Umeitambuaje
Shahidi: Kwa Jina langu na Sehemu niliyosaini
Wakili wa Serikali: Jina lipo wapi, Ni Jina gani
Wakili Peter Kibatala: ALICHOKIFANYA DADA YANGU ESTHER HAIRUHUSIWI, ANAKWEMDA KWENYE DETAILS
Wakili wa Serikali: Sawa naondoa hilo swali
Wakili wa Serikali: Ungependa hii fomu ipokelewe Mahakamani
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi anaomba Fomu ipokelewe
Jaji: Wakili wa Mshtakiwa wa kwanza
MTOBESYA: HATUNA PINGAMIZI
Mallya: Hatuna Pingamizi Fredrik
Kiwhero: kwa Niaba ya Mshitakiwa.....wa tatu hatunapingamizi
Peter Kibatala: Kwa niaba ya Mshitakiwa wa Nne hatuna Pingamizi
Jaji: anaandika Kidogo
Jaji: Mahakama inaipokea kwa ID 1
Wakili wa Serikali: Shahidi pia ulisema kwenye huo Upekuzi pana Bastola na Risasi unaweza hapa Mahakamani ukavitambua Tuanze na Bastola
Shahidi: Ndiyo nitavitambua
Wakili wa Serikali: Bastola unazitambuaje
Shahidi: Kwa Namba A5340
Wakili wa Serikali: na Kwa Upande wa Risasi
Shahidi: namtambua, zilikuwa na Rangi ya Dhahabu
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Naona Exibit nimuonyeshe Shahidi
Afisa Wa Mahakama anafungua Bahasha ya Kaki Anamkabidhi Wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: Hebu Kiangalie hiki kitu hapa, Iambie Mahakama ni nini
Shahidi: anaingilia bila Kushika, ni Bastola
Wakili wa Serikali: ambayo Imetoka wapi
Shahidi: Imetoka Kwa Adam
Wakili wa Serikali: Uliona wapi?
Shahidi: iliyotoka kwa Adam
Wakili wa Serikali: ni Kitu gani Kilichokufanya ukagundua
Shahidi: kwa namba
Wakili wa Serikali: Namba gani
Shahidi: A5340
Wakili wa Serikali: Umeeleza pia ulishuhudia Upekuzi wa watu wa wili ambao kwa Majina yao ni Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya, Je ukiwaona unaweza Kuwatambua
Shahidi: naweza Kuwatambua
WAKILI WA SERIKALI: WAPO HAPA MAHAKAMANI?
Shahidi: Wapo hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali: Wapo wapi
Shahidi: hapa Mbele, Mohammed amevaa Tshirt ya Amevaa Meupe Kijani na Nyeusi
Wakili wa Serikali: na Adam yupo wapi Shahidi: amevaa Shati lenye Rangi Nyeupe Nyeupe
Wakili wa Serikali: Yupo wapi hapa Mahakamani
Shahidi: Yupo pale
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu
Jaji: Upande wa Utetezi
Mtobesya: Ndiyo Mheshimiwa Jaji
Mtobesya: naomba Nipatiwe ID 1 Mahakama Inampatia
Mtobesya: Shahidi umeomba Mahakama Ipokee Kielelezo hiki Onyesha Sehemu ipo saini
Shahidi: Nimesaini hapa
Mtobesy: Kwa Ushahidi wako Unasema ulisaini Nyaraka ngapi
Shahidi: Nne
Mtobesya: Ushahidi wako kwamba Sahihi zako Lote zinafanana
Mtobesya: Naomba kwa Kifungu 75(1) Sheria ya Ushahidi, Shahidi asaini tena sehemu Nyingine ili Mahakama iweze Kufananisha Saini zake
Jaji: Unaweza Kutusomea.? Mtobesya: anasoma Kifungu cha 75(1) cha Sheria ya Ushahidi
Jaji: hicho Kifungu kinaitaka Mahakama shahidi asaini ili iweze Kufanya ufafananisho
Mtobesya: Ndiyo ili Mahakama iweze kufananisha, kwa sababu tuna Nyaraka Nyingine inasaini yake tofauti
JAJI: lakini hiyo Nyaraka itakuwa imetengenezwa hapa, Utakuwa umeiiingiza Mhakama .....
Jaji : Bwana Matata una jambo la Ku-she na sisi
Matata: Sheria Anayosoma Wakili Mtobesya Ni Sheria inasema kuwa Shahidi anaweza kuandika sehemu tu 75(2) Mahakama inaweza Kuagiza Mtu yoyote Mahakamani Kulingananisha.
Jaji: Je hiyo inahusiana na Mahakama kumuelekeza Shahidi asaini?
Matata: ni tafasiri yangu kuwa Mahakama Inaweza Kuruhusu Shahidi Kuandika ili Kufananisha Kama alichokiandika ni sawa
Mallya: Pale kwenye 75(2) inasema any Documents haijambana wapi kwa hiyo anaweza Kusaini popote (any documents) ili Mahakama ifanye Uamuzi iwe imepata kwa Usahihi wake....kwa usahihi Kifungu cha 75 lakini siyo kwa Kumtaja Shahidi aandike
Jaji: Upande wa Mashitaka
Wakili wa Serikali: Maombi ya Mtobesya Pamoja na Kuegemea kutoka kifungu 75 cha Sheria ya Ushahidi tunaona amekimbia Sana na siyo wakati wake Lakini pangekuwa na Nyaraka Nyingine ambayo Ndiyo Ingekuwa imekuja Rasmi Mahakamani ndipo angetumia.......Njia yako ya Kutaka Shahidi Asaini Ni sahihi Kama watapinga tutashughulikia Kupinga huko wakati huo.
Jaji: Kwa tafsiri yangu Mamlaka iliyopewa Mahakama 75(2) ni naona Mahakama inayo Mamlaka kumuelekeza Mtu yoyote Kufanya Mlinganisho wa Maneno au Namba kwa Nia ya Kuiwezesha Mahakama Kufanya Ulinganisho, ila huyu Mtu aliye na maarifa Kuliko Mahakama Yenyewe. Najiuliza kama ...Leo nilikuwa na Avoid Upande wa Utetezi Kutuzuia Kutumia Nyaraka hii ambayo sisi tumeipata kwenye Comito.
Mtobesya///; Kifungu cha 47 cha Sheria ya Ushahidi ndiyo kinaruhusu Maoni ya Kitaalamu katika Ushahidi Lakini Kifungu cha 48 au 49 Sikumbuki Vizuri kinaruhusu hata mtu asiye Mbobezi Kufanya Maoni yake Hili Kifungu cha 75 chenyewe Kinataka Mahakama Kufanya Ulinganisho.
Jaji: Na Mimi na kubaliana na wewe Lakini kwenye Document uliyonayo hatujui baada ya Kumkabidhi Karatasi at asaini Sahihi gani kati ya hizo Mbili
Jaji: Ndiyo nasema wewe endelea na Jukumu lako kama Walitokea Wakapinga tutashughulikia Pingamizi hilo wakati huo ...na Sheria ya Ushahidi wa Kifungu cha 75 Vyote Vinafanya washitakiwa Kupewa Nyaraka zinazokusudiwa Kutumika dhidi yao kwenye Makosa Makubwa Kama haya kupitia Comito Kwa hiyo watupatie
Mtobesya: Asante Mheshimiwa Jaji
Mtobesya: Naomba nikabidhi iwe Nyaraka Original ya Hati ya Kuchukua Mali iliyosainiwa tarehe 25 2020 inayomhusu Mohamed Ling'wenya Kwa sababu sisi tunayo Moja
Jaji: chini ya Sheria Gani
Mtobesya: Kifungu cha 246 na 146 ya Makosa ya Jinai ...
..Angetoa basi Maombi Rasmi lakini hata kama no Original haiwezi kuitumia kwa wakati huu Haki yake ya Kuhoji aendelee nayo na anaweza Kuitumia hata sasa Sisi tuna tatizo na Procedure jinsi gani Ushahidi huu unataka Kuletwa Mahakamani
Jaji: Jamani Mmeelewa
Wakili wa Serikali: Sisi Haja yetu ni Swala la Procedure Ni kweli Tulianika Ushahidi Tutaokuja kutumia Mahakamani lakini ieleweka Kuwa Ushahidi hi ni Wa Kwetu. Hakuna mahala popote ambapo Mteja wake anaweza Kuwa na haki ya kutumia Nyaraka hizo ......
.Ubishi ulikuwa kama Mshitakiwa Alikuwa ametahiriwa au haja tahiriwa Mahakama ya Rufani ikasema kuwa Hilo ni Kubwa sana Kwake na Isingeweza Kujiingiza katika Risk. Kwa kesi hii basi Kama anataka Mahakama Ijiridhishe. Swala ni Kama Nyaraka hiyo imepokelewa na Kama .......imekubali imeandikwa na Mtu huyu Na pia kama Nyaraka hiyo Nyingine kama Ingekuwa hapa angekuwa na Haki
KESI YA buying wa John dhidi ya Jamhuri criminal appeal namba 450 ya Mwaka 2017 Mahakama iliyoketi Shinyanga Katika Ukurusa wa 11 paragraph ya Mwisho ya a Ukurasa huo wa 11 Ambapo swala Lililojitokeza tangu wakati wa Trial Court na Kesi Ilikuwa ni ya Ubakaji ........
Mheshimiwa Jaji: tunatakiwa tuzingatie Mfumo wetu wa Utoaji haki, Mahakama kwa Kutimiza Wajibu wake anakuwa ni refa na siyo kwa kukaribishwa Kutaka Kufanya Uchunguzi Zoezi kama hilo ni Kuingiza Mahakama katika riski ambazo zinaweza Kuepukika.
...imekubali imeandikwa na Mtu huyu Na pia kama Nyaraka hiyo Nyingine kama Ingekuwa hapa angekuwa na Haki
Na Hilo Ndiyo Dhumuni la Comito Trial kwamba Mshitakiwa ajue anachokuja akujitetea nacho
Upande wa serikali: Sisi tunaona ni Kukiuka Procedure na Maombi hayo tunaomba uyakatae Mheshimiwa jaji Mtobesya: Tunapoteza sana Muda Mheshimiwa Jaji, Shahidi ni wa Kwao na Ushahidi ni wa Kwao Na sijui ni wakati gani tena sisi tutapata Kuwa na wasaa wa kuwa na Shahidi huyu
Na hapa swala la Copy kwa Washitakiwa halijazungumziwa wakati ni Haki kwa Mshitakiwa Kupatiwa Hiyo Nyaraka
Nashon Nkungu: Naona nisaidie Mahakama kama Afisa wa Mahakama alichosema Wakili Robert Kidando Amejieleza Kwenye Kifungu cha 76 tuh asemi kwa nini kuna Haki ya Kukabidhi wa Nyaraka za Comito Na Kingine Kifungu 30 cha Sheria inasema tupewe Copy siyo Photocopy ....
Ambapo wewe Umegundua Sahihi Katika Nyaraka hizo na Zilizopo hapa Mahakamani Sahihi zinatofautiana Kwa Maana hiyo Ukaomba Mahakama ikupatia Nakala halisi Jaji Jambo la Pili Kwakuwa wanasema Ushahidi huo watautumia basi Wahurumie Mapema ili uweze Kuutumia.
Jaji: Mtobesya
Mtobesya: naam Mheshimiwa Jaji
Jaji: hoja zako ulizijenga katika a Mazingira Matatu Haki za Mahakama Jinai hasa akatika Mahakama Kuu, amtu anasomewa na Kukabidhi wa Nyaraka Kwamba wewe Una taarifa Kwamba zipo Nyaraka wanazolenga kuzitumia Kama Ushahidi Wao
Mtobesya: Mheshimiwa nilikuwa naomba Mashauriano na Mahakama ilitusiiipe Mahakama Mzigo wa a kuandika Rulling
Jaji: mnasemaje Jamuhuri
Wakili wa Serikali: Ni Sawa Mheshimiwa
Jaji: Basi tuta Break kwa Dakika 10, tukutane pande zote pale Ofisini
Jaji: anatoka
Mawakili wamerudi
Jaji ameingia tena Saa 6 NA Dakika 24
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa tena Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe Kisha Mahakama Kimyaaaaaa
Jaji: Muda Mfupi Uliopita Tuli-break kwa Nia ya Kuweka Sawa Mambo ya Kitaaluma Baada ya Kuyaweka Sawa na Kualika Sasa Mtobesya Kuendelea
MTOBESYA: Wakati Unaongozwa na Dada Yangu Esther Ulisema Uliandika Maelezo
Shahidi: Niliandika Tarehe 05 Mwezi 08 2020
Mtobesya: aliyeandika Maelezo yako
Shahidi: Sijui Jina lake
Shahidi: anaitwa Jumanne
Mtobesya: Ulishawahi Kukutana na Askari anaitwa Detective Coplo Francis.?
Shahidi: Sikumbuki kama nimekutana naye
Mtobesya: Lakini walikupa Maelezo Ukasoma na kisha Ukaona sawa
Shahidi Ndiyo
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Nipewe Statement (Handwritten Statement) Naomba Chini ya Kifungu Cha 164 (1h) cha Sheria ya Ushahidi
Wakili wa Serikali Wapo Kimya Jaji anawasubiri
Wakili wa Serikali: Hatuna Pingamizi la Kumpatia hii Nyaraka
Jaji: Pokea
Mtobesya: Shahidi Unajua Kusoma na Kuandika
Shahidi: Ndiyo
MTOBESYA: Shika Karatasi zipo Mbili Soma kama Ndiyo Uliyosoma Ukasaini na Kama Kuna Majina yako na Askari aliye andika Ihakiki Kwanza
Shahidi Anaipekua, anaikazia Macho anafunua funua mara Nyingiyingi
Mtobesya: Ndiyo hiyo.?
Shahidi: Kimyaaaa anatizama tena ile Karatasi, anaipekua
Shahidi: Ndiyo Yenyewe
Mtobesya: Soma Kuanzia Juu Kwa Sauti
Shahidi: Mimi Ndiyo Mwenye Majina na anuani takwa hapo Juu Mkazi Wa Kilimanjaro Nimezaliwa Mwaka 1979 Familia ya watoto Nilikuwa naelekea Saloon Rau Madukani Na baada ya Kumalizia nilieleza Sehemu yangu ya Biashara Kufanya Usafi. Mbele Kuna Bar Na Kukikuwa na Vijana walikuwa wanakunywa Pale Sikuwa nawafahamu Kwa Maana walikuwa ni wageni
Mtobesya: Soma Kote
Shahidi: Sikuwafahamu kwa Maana walikuwa ni Wageni maeneo haya Kwa Muda Mwingi walikuwa wanaongea na simu. Kwangu Afande Mmoja akajitambulisha Jina Afande Jumanne Akaniomba niwe Shahidi huru Ambapo nilishuduia Kufanya Upekuzi Kwenye Kupekuliwa Kijana Mmoja alikuwa na Bastola Zenye nmabaA A 5340 Pia alikutwa na Kete 58 za Madawa ya Kulevya
Shahidi: Shahidi ananendelea kusoma Baada ya Muda walikuja watu watano na a Kuwafuata wale Vijana Na wakaambiwa wapo Chino ya Ulinzi Askari hao walitaka Kufanya Upekuzi ndipo walipokuka Kuni.... Kamyamaza Kidogo Askari hao walihitaji Kufanya Upekuzi ndipo walikuja.......Adam Kasekwa mbaye nilimfahamu Jina baada ya Kuulizwa Jina lake baada ya Upekuzi Na huyo Mwingine aliyekuwa naye alitaka anaitwa Mohammed Ling'wenya ambaye pia kwenye Upekuzi alikutwa na Simu Moja ya Samrt Yenye Line ya Airtel na Hallotel na Kete 21 za Madawa ya Kulevya
Watu hawa wawili nilikuwa siwafahamu Majina wala Sura niliwafahamu baada ya Kutaja Majina yao Baada ya Kukamatwa na Polisi, Askari wale nilikuwa siwafahamu Na Kiongozi wao aliyekuwa anafanya a upekuzi aliwatambulisha kwangu ASP Jumanne.
Baada ya Majina hayo Nilijaza Hati ya Upekuzi Na Kuzuia Mali Walisaini wote na Watu tulioshuhudia Na Afande Jumanne Na baada ya Upekuzi Nilijaza Hati ambayo inaonyesha Upekuzi umefanyika Ambapo tukasaini wote na tulioshuhudia Haya Ndiyo Maelezo Yangu, Sahihi Kama Nilivyoyatoa.
Mtobesya: Nitakurudisha Kwenye baadhi ya Maeneo kama Ulivyosoma
Mtobesya: Ni sahihi Katika Ushahidi wako ulisema Askari wawili walifika wakawaambia Mpo chini ya Ulinzi na Wakawatajia Makosa yao
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Kwenye Maelezo yako hapo, hayo Maneno Yapo au hayapo
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: Nilikusikia Unasema hawa Vijana waliokamatwa wao walikuwa wanakunywa wakati wewe unafanya usafi katika Eneo lako la Biashara
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Kwenye Maelezo yako hiyo Taarifa ipo
Shahidi: Haipo
Mtobesya: Nilikusikia Ukisema Kwamba afande Jumanne alikuja kwako akatoa Kitambulisho
Shahidi: Ndiyo alitoa Kitambulisho
Mtobesya: Hayo Maelezo ya kutoa Kitambulisho yapo kwenye Statement yako
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: kwenye Maelezo yako nilikusikia watuhumiwa Waliposimamishwa kabla ya Upekuzi walijitambulisha Majina yao kwa Polisi aliyekuwa anafanya Upekuzi Nitakuwa sahihi nikisema Statement Yako inasema Uliwajua Majina Baada ya Upekuzi
Shahidi: Niliwajua Majina kabla ya Upekuzi
Mtobesya: Soma sehemu inayosema nilishuduia wakipekuliwa........ Mpaka inaisha Jina la Afande Jumanne, Soma kwa Sauti
Shahidi: Nilishuhudia Kupekuliwa kwa Vijana hao, na Kupekuliwa Mmoja wao alikutwa na Bastola yenye namba A5340 pamoja na Magazine yanye Risasi 3 .......pia alikuwa na Madawa ya Kulevya Ambae nilimfahamu kwa Jina baada ya Kuulizwa baada ya Upekuzi.
Mtobesya: Kwa hiyo Statement Ulifahamu Kabla au Baada
Shahidi: Baada ya Kupekuliwa
Mtobesya: Nitakuwa sahihi, kwenye Ushahidi wako ulielezea ulisaini Nyaraka Nne za Kushuhudia Upekuzi
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Nenda Sasa baada Upekuzi huo,
Shahidi: Nilijaza Hati ya Upekuzi na Hati ya Kuzuia Mali ilionyesha Upekuzi Umefanyika, ambao tulisaini wote tulioshuhudia pale.
Mtobesya: Ishia hapo, Nitakuwa sahihi nikisema Nyaraka hiyo Uliyosoma inaonyesha ulisaini Nyaraka Moja..? Na siyo Nne kama Ulivyosema Asubuhi ya Leo
Shahidi: kwa Mujibu wa Mstari huu ni Kweli
Mtobesya: Isaidie Mahakama sehemu nataka Usome Kwa Sauti, Soma baada ya Neno Watuhumiwa wale wawili
Shahidi: Baada ya Upekuzi huo na Kusaini Hati ya Kuzuia Mali ambapo tukisaini wote.
Mtobesya: Wakati Wakili Wa Serikali Esther anakuongoza Ulisema aliyekuongoza hapo ni Jumanne
Shahidi: Nilisema ni Afande ambaye sikujua Kwa Jina
Mtobesya: Ipo Kwenye Rekodi, Jaji ataona
Shahidi: hapana
Mtobesya: Ungependa hayo Maelezo Yawe sehemu ya Ushahidi Wako Siku ya Leo
Shahidi: Ndiyo ningependa uwe Ushahidi Wangu Siku ya Leo
Wakili wa Serikali: Hatuna Pingamizi
Jaji: Mahakama imeyapokea Maelezo hayo Kama Kielelezo namba 02 kwa Upande wa Utetezi
Mtobesya: Kwa Ruhusa yako Mheshimiwa naomba Kuendelea
Mtobesya: Ulielezea Mahakama Ulisaini Nyaraka za Uzuiaji wa Mali, zaidi ya Nne
Shahidi: Ndiyo
MTOBESYA: ieleze Mahakama Hati hizo zilijazwa na nani Mpaka Nyie Mkasaini
Shahidi: Zilijazwa na Askari Jumanne
MTOBESYA: na wewe Unakumbuka ulisaini kwenye Hati zote
Shahidi: Ndiyo
MTOBESYA: Unaweza Kuisaidia Mahakama Ulisaini Upande gani
Shahidi: Pale Mwisho Kwa Pembeni
Mtobesya: Naomba Nimuonyeshe Shahidi ID 1 Nitakuwa Sahihi Nikisema Nyaraka zote Nne ulisaini hapa Kwenye Jina lako
Shahidi: Siyo zote sehemu hii, Zingine Nilisaini Upande wa Kushoto na Zingine Upande wa Kulia.
Mtobesya: Unaweza Kutuambia Ulizosaini Upande wa Kushoto zinaruhusu nani na Kwaajili ya Vifaa Vipi
Shahidi: NilizoSaini Upande wa Kushoto zilikuwa zinamhusu Adam
Mtobesya: Hizo Ulisaini Upande wa Kushoto
Shahidi: Nilisaini Upande wa Kulia
Mtobesya: na Zilizomuhusi Mohammed Ulisaini Upande gani
Shahidi: Upande WA Kushoto
Mtobesya: Ulisaini Baada au Kabla ya Jina lako
Shahidi: Nilisaini baada ya Jina langu
Mtobesya: Na Ni Ushahidi wako Mbele ya Mahakama zote Ulisaini wewe Mwenyewe na kwa Mwandiko wako
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Na Kwa Ushahidi Wako Saini zako umesaini wewe Zikiwa zinafanana
Shahidi: Kuna zingine zilikuwa hazifanani kwa sababu nilikuwa na Hali tofauti
Mtobesya: Mweleze Mheshimiwa Jaji Sasa ni hali ipi Ulikuwa nayo ikapelekea Saini zako Kutofautiana
Shahidi: Kuna saa, wakati wa Ukamataji Nilisaini wakati nimesimama na Zingine nimesaini wakati nimekaa kwenye Meza.
Mtobesya: Unaieleza Mahakama Ukisaini ukiwa umesimama na Wakati Umekaa saini lazima zitofautiane
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Nilisikia wakati anakuongoza Dada Yangu Wakili wa Serikali Kuwa Mlisaini wakati Wa Tukio
Shahidi: Wakati natoa Maelezo Nilisaini Nikiwa mezani lakini Zile zingine Nilisaini nikiwa nimesimama
Mtobesya: Ni Signature zipi sasa zinazofanana ukiwa Umekaa au Umesimama
Shahidi: Nikiwa Nimekaa ndiyo zinafanana
Mtobesya: Ukiwa Umekaa umesaini Mara Ngapi na Nyaraka zipi
Shahidi: Zile ambazo nilikuwa kituoni kutoa Maelezo.
Mtobesya: Zote ambazo ulisaini Ukiwa Umekaa Zina fanana..?
Shahidi: Hapana
Mtobesya: Zote ulizoSaini Ukiwa Umesimama Zinafanana au hazifanani
Shahidi: Zinafanana
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Kuishia Hapo
Mtobesya: naomba Kurudisha Kielelezo
Jaji: Wakili Malya unahitaji Muda gani
Mallya: Nusu saa hivi
Mallya: Bado unauza Mbege
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Mbege unayouza wewe inalewesha
Shahidi: Kuna Inayolewesha na Isiyolewesha
Mallya: Una Ndugu au Mume ambaye ni Polisi
Shahidi: Hapana
Mallya: Ulitambuaje kuwa hiki ni Kitambulisho cha Polisi?
Shahidi: Niliona Chapa ya Taifa
Mallya: Kitu gani Kingine Uliona
Shahidi: Niliona Jina lake
Mallya: Lilikuwa limeandikwaje
Shahidi: kwa kweli hapo Sikumbuki
Mallya: Umesema Wakati Unafanya Shughuli zako za Usafi na Vijana walikuwa wanakunywa Bia, Ni hatua ngapi
Shahidi: Ni hatua 10
Mallya: Napiga hatua Mahakamani
Mallya: Hapa Kuna Hatua Saba tu
Mallya: Umbali wa Hatua 10 Macho yako yanaona Vizuri
Shahidi: Yanaona Vizuri
Mallya: hapa Kuna Umbali Wa Hatua 7 tu Unasema Mtu Amevaa Tshirt yenye Rangi Nyeusi wakati ni Dark Green Je unataka Mahakama iamini kwamba unaona Vizuri?
Jaji: umeelewa swali..?
Shahidi: ..natumiaga Miwani, Sema Leo nimesahau Miwani
Mallya: Ulielezea Kuwa siku ya Tukio ulivaa a Miwani
Shahidi: Hapana
Mallya: Siku ya Tukio ulikuwa Umbali wa Mita 10 Leo Mshitakiwa yupo hatua 10 tu hakuna aliyevaa Tshirt Nyeusi, unataka Kumwambia Mheshimiwa Jaji unaona Vizuri?
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
JAJI: umelielewa Swali
Shahidi: Ndiyo
JAJI: Jibu Basi
Shahidi: Kuna saa Macho yanashida.
Mallya: Wakati Unatoa Maelezo Leo Uliomba Miwani uweze Kuangalia Vizuri.?
Shahidi: Sikuomba
Mallya: Ni sahihi Kuwa Usajili wa Simu unafanya kwa Kitambulisho?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: na wewe Uliwaona watu waliopo Mahakamani walikuwa wanasajili Line za simu
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwenye Maelezo Yako kuna sehemu umesema Wanasajili lini?
Shahidi: Hakuna
Mallya: pale Rau Bia wanauza au Bure?
Shahidi: Wanauza
Mallya: Wakati mnawapekua Mliwakuta na Bastola na Siyo Pesa
Shahidi: Hakuwa na Pesa
Jaji: Watakuwa walishalipaaaaaa
MAHAKAMA kichekoooooo
Mallya: zoezi la Kufanya usafi Lilichukua muda gani?
Shahidi: Kwa muda wa Kufanya Usafi kama Dakika 10
Mallya: Wakati Tukio linatoka Ulishamaliza Usafi au Ulikuwa unaendelea
Shahidi: nilikuwa naendelea ikabidi Nisimame
Mallya: Tukio la kukamatwa lilichukua Muda gani?
Shahidi: Rudia swal?
Mallya: Kitendo Cha Kukamatwa hawa watu Mpaka unaitwa kushuhudia ilichukua muda gani?
Shahidi: kama Dakika 03
Mallya: Kwa hiyo tukijumlisha Dakika 10 za Usafi na Dakika 3 wakakuita wewe Zoezi la Kusachiwa lilidumu kwa a muda gani?
Shahidi: Kwa Dakika 45
Malya: Saa Nane ilikuwa imefika
Shahidi: Kama saa Nane Kasoro
Mallya: Kwa Maelezo Yako wewe yalitolewa Umesaini Ukiwa polisi saa 7 kamili Je, tukuamini wewe au?
Shahidi: Muamini Maneno Yangu
Mallya: Tuchukue Yote.?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kabla ya kwenda Kwenye Tukio Siku hiyo ulikuwa wapi na wapi
Shahidi: Nilitoka Nyumbani baada ya Usafi, Nikaenda Kwa Mgonjwa na Baadae Saloon
Mallya: Umeulizwa aliyekuchukua maelezo Yako ni nani
Shahidi: Simfahamu Kwa Majina
Mallya: Hakukuonyesha Kitambulisho ndiyo Maana Humkumbuki?
Shahidi: Hapana alinitajia nimemsahau
Mallya: Kwa kutazama Kwa Macho yako sahihi yako uliyosaini Hapa na Hapa Kwenye Exibit 02 zinafanana
Shahidi: Hazifanani lakini ni sahihi zangu
Mallya: Kwenye Maelezo Yako umeeleza Mahali Kiongozi wao, Afande nani
Shahidi: Afande Jumanne
Mallya: akitokea Mtu akisema yeye ndiyo Kiongozi aliyekwepo atakuwa Muongo
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Unamfahamu Kingai
Shahidi: Hapana
Mallya: na Ulisema Mapolisi walikuja kujitambulisha kwako.?
Shahidi: alikuja Mmoja
Mallya: Askari waliowakamata watuhumiwa walikuwangapi
Shahidi: Walikuwa watano
Mallya: Mheshimiwa Jaji ni hayo tuh
Jaji: Mnasemaje Tubreak au tuendelee
Wakili wa Serikali: Tubreak
Jaji: kwa Muda gani
Peter Kibatala: Kwa Sababu tulisha Kaa Dakika 30 tupumzike Kwa Dakika 45
Jaji: Mnasemaje Serikali
Wakili wa Serikali: Sawa
Jaji: Shahidi Tunapumzika, tunywe Maji tutarudi baadae Kidogo
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe
Jaji anaandika Kidogo
Wakili wa Serikali: Kwa Upande wa Jamhuri
Upande Wa Utetezi: tupo tayari Kuendelea
Matata: Shahidi nitakuhoji Maswali Machache utajibu kwa Sauti
Matata: Umesema wewe ni Mwenyeji Wa Miaka 08 pale Rau Madukani
Shahidi: Katika Biashara
Matata: Lakini pia Umesema Unaishi Pale pale
Shahidi: Ndiyo
Matata: Umesema Pale Rau Madukani ni Kata, Kijiji au Kitongoji
Shahidi: Kata ya RAU Madukani
Matata: Utakubaliana na Mimi Hukusema Pale no Kata ya RAU Madukani
Shihidi: Ndio
Matata: Utakubaliana na Mimi hujatutajia Unatoka Mtaa Gani hiyo Kata Ya Rau
Shahidi: Sikuulizwa
Matat: Hujatutajia Hata MwenyeKiti wa Mtaa wako
Shahidi: Sijaulizwa
Matata: hujatuambia pia Kuwa unaishi kwenye Nyumba yako au Nyumba ya Kupanga
Shahidi: Sikuulizwa
Matata: Unaishi Nyumba yako au Umepanga
Shahidi: Nimepangisha
Matata: Kuna Mkataba Ulileta hapa Kwamba wewe Umepanga Rau
Shahidi: Sikuleta
Matata: umetutajia Umepanga Nyumba ya Nani
Shahidi: Sijaulizwa
Matata: Umesema Unafanya Shughuli Ya Kuuza Mbege
Shahidi: Ndiyo
Matata: hujasema kama Mbege Unanunua au Unaitengeneza
Shahidi: Sijaulizwa
Matata: Umesema Pale Rau Una eneo la Biashara
Shahidi: Ndiyo
Matata: Umeonyesha Hati wala mKataba wa Pango
Shahidi: Hapana
Matata: Umesema Wakati wa Maelezo Yako Una Glocery, Stationary, Kibanda Cha Simu
Shahidi: Ni sahihi lakini sasa....
Matata: Inatosha
Matata: hujatutajia Mtu Yoyote zaidi ya Huyo Esther ambaye ni Shahidi
Shahidi: Sijataja
Matata: hujatutajia Hata Saloon au Mtu aliyekuosha Hizo Nywele
Shahidi: Sijaulizwa
Matata: Wakati Ukiwa eneo lako la Biashara uliona Vijana wangapi wakiwa wanakunywa Bia
Shahidi: Niliona watatu
Matata: Ukasema Walikuwa wanasajili laini za Simu
Shahidi: ndiyo
Matata: Wakati Unahojiwa na Wakili Mallya Ukasema hawasajili laini
Shahidi: walikuwa wamekaa Meza Moja na Kijana anayesajili laini
Matata: Mahakama Ichukue Lipi walikuwa Wanakunywa Bia, Wanasajili Laini au Walikuwa waMekaa Mezani?
Shahidi: Ichukue Yote kwa sababu yalikuwa yanafanyika kwa Pamoja
Matata: Mtu anaweza Kuwa anakunywa Bia, anasajili Line na wakati huo huo amekaa mezani..?
Shahidi: Ndiyo
Matata: ulielezea Mahakama Kwamba Mlifika Saa ngapi Polisi
Shahidi: Hapana Sikuulizwa
Matata: naomba Exhibit P2
Matata: Shika Maelezo Yako
Matata: Wakati Unaulizwa na Wakili ulisema aliyekuwa anashuhudia ni wewe na Esther Sasa iambie Mahakama Katika Maelezo yako ni wapi Esther ametajwa
Shahidi: Hajaandikwa
Matata: Mheshimiwa ni hayo tu
Kibatala: Shahidi saa hizi ni Saa ngapi?
Shahidi: Saa 9 Kasoro
Kibatala: umeona wapi
Shahidi: Kwenye Saa
Kibatala: unaona yake Magari pale Nje
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Rangi gani
Shahidi: Ni Pink, Nyeupe na Blue
Kibatala: na Hapo hujavaa Miwani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mallya alipokuuliza kwa sababu ya kutomtambua Mshitakiwa Ukasema Unatatizo la Macho na Sababuhujava Miwani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ila Kwa Sasa wakati nakuuliza hujava Miwani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na wala hujamuomba Mheshimiwa Jaji Uvae Miwani
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Umekuja Hapa ukitokea wapi
Shahidi: Gesti
Kibatala: Mara ya Mwisho Kuwa Rau Madukani ni lini?
Shahidi: Ijumaa
Kibatala: Ulikuwa Unaendelea na Kuuza Mbege Rau..?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: aliyekuuzia Mbege Mwezi wa 05 ni nani?
Shahidi: Mama kazi Moto na Mmoja anaitwa Paulo
Kibatala: Wewe Majina Mengine ni Mama Pendo..?
Shahidi: Ni kweli
Kibatala: na Ni kweli husimami wewe Peke yako kuna Mtu anakusaidia
Shahidi: Wakati upi
Kibatala: Ni Kipindi Kipi Binti yako alikuwa anauza pale
Shahidi: Alianza Juzi Jumamosi
Shahidi: ananyoosha Kidole
Kibatala: Unataka Kurekebisha Jibu
Shahidi: Kuna Binti yangu ananisaidiaga Usafi
Kibatala: anaitwa Nani
Shahidi: Naitwa Pendo
Kibatala: katika Ushahidi wako Ulizungumza Lolote kuhusu huyu Pendo
Shahidi: Sikuzungumza
Kibatala: pale Rau Madukani Karibu na Tukio lilipotokea kuna Mtu anaduka la Vipodozi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kuna Mtu ana Duka la Jumla
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Mtu huyo Mwenye Duka la Jumla Ndiyo yenye fremu za Vipodozi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Na Pana Flemu 4 kwa Upande Mmoja
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Upande wa Pili ndiyo wanauza Vinywaji
shahidi: ndio
Kibatala: Anayeuza Duka la Vipodozi anaitwa Athima
Shahidi: Sijui Jina lake
Kibatala: ila Unajua ni Mmama au Mdada
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na ndiyo anakaa Mbele ya Duka lake
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Picha hii tunayozungumza, ulimchorea Jaji hiyo Picha
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unajua kuwa kwanini unajua kwanini Ujamchorea Jaji
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ni Kwasababu wewe Ni Shahidi wa Kupanga
Shahidi: Hapana Kabisa
Jaji: Naliondoa hilo Swali
Kibatala: Twende kwenye Bastola
Kibatala: Ulikuwa unampekua
Shahidi: Hapana
Kibatala: ulijuaje Kuwa kulikuwa na Vitu vigumu
Shahidi: Baada ya kutoa kwenye mfuko
Kibatala: na Ulishuhudia MADAWA ya Kulevya
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unga ni kitu kigumu
Shahidi: Kitu kilaini
Kibatala: Kuna sehemu uliona namba za Bastola CZ 100
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mpaka unamaliza Zoezi la Kuulizwa na Serikali hakuna aliyekutajia hizo namba
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unakumbuka ulisema zilipatikana Risasi tatu na Magazine
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: hapa Mahakamani Umeonyeshwa hizo Risasi
Shahidi: Hapana
Kibatala: kwa hiyo hujamsaidia Mheshimiwa Jaji Kuwa kutambua Risasi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Umesema Kuhusu Magazini, unajua magazine inakaa wapi kwenye Bastola
Shahidi: Upande wa Chini
Kibatala: Umemwambia Mhe. Jaji Kwa Kufafanua Kuwa Magazine inakaa hapa
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati Umetoa maelezo yako ambayo yapo katika D2 kwamba Kuna Afisa Wa Askari Alichomoa Magazine Ukaona Risasi 03
Shahidi: Nilisema
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba Kielelezo Namba D2
Kibatala: Nionyeshe ni wapi
Shahidi: Hakuna Sehemu Kama hiyo
Kibatala: Kwa hiyo tunakubaliana Jibu la Kwanza ni Uongo
Shahidi: Hapana siyo Uongo, Makosa ya Mwandishi
Kibatala: Nichukie lipi sasa
Shahidi: Chukua Yote
Kibatala: ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuna Kitu Mwandishi amekiacha ambacho Mimi nilikisema. Ulimwambia Mheshimiwa Jaji
Shahidi: sikumwambia
Kibatala: Ni sahihi Kuwa Kielelezo D2 haitaji Jina la Askari yoyote isipokuwa Jumanne
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: kwa sababu walijitambulisha ukajisahau
Shahidi: Ndiyo walijitambulisha Nikasahau
Kibatala: Unatatizo la Kumbukumbu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Soma Kuanzia Neno baada ya Upekuzi huo
Shahidi: Nilishuhudia na Kusaini Fomu za Upekuzi
Kibatala: Mwambie Mhe. Jaji hapo kwenye watu wawili kama Umefafanua
Shahidi: Hapana
Kibatala: Pia Mlisaini Wote
Shahidi: Ulifafanua, Neno Watu wote
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati yanaandikiwa Uliambiwa ni Maelezo ya Kisheria au Mapambo
Shahidi: niliambiwa ni Maelezo Yangu
Kibatala: Kwa Mujibu wa maelezo haya Adam Kasekwa Ulifahamu Jina Lake Baada ya Upekuzi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unafahamu Mshitakiwa tuliye naye ni Adam Kasekwa Maarufu Kama Adamoo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unakubali Hakuna Sehemu uliyotaja Adamoo
Shahidi: Ndiyo Sikutaja
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji ni kweli au siyo Kweli Kwamba Katika Kielelezo ukichosema hapo Hakuna Adamoo
Shahidi: Hakuna Adamoo
Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kwamba Unatakiwa Kusema Ukweli ndiyo Maana Unaapishwa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Jaji akupime Ukweli au Uongo wako kwa hilo Soma hapa
Shahidi: Adam Kasekwa Adamoo
Kibatala: awali ulisema ipo au haipo
Shahidi:Nilisema Haipo
Kibatala: Sasa wewe ni Muongo au Mkweli
Wakili wa serikali: OBJECTION Pius Hilla Swala la Kweli au Uongo aiachie mahakama
Jaji: Naona Shahidi anaweza Kujibu yeye ni Mkweli au Muongo
Wakili wa Serikali: Sawa Mheshimiwa
Kibatala: Swali langu lipo palepale Kutokana na Mgongano wa Majibu, Mwanzoni Ulisema jins ls Adamoo Haipo na baadae tukasema Kwa pamoja Ukaona Ipo, Wewe ni Shaidi wa Ukweli au Uongo
Shahidi: Mimi ni Shahidi wa Ukweli
Wakili wa Serikali: Robert Kidando Hiyo sehemu ichukuliwe kwa makini
Kibatala: Sijaona Objection na Shahidi amejibu
Jaji: Mimi sijasikia Swali
Kibatala: Unakumbuka ulisema uligundua namba ya Bastola..?
Shahidi: afande Jumanne
Kibatala: Na ndiyo Unavyosema Katika Maelezo yako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Hakuna mahala Umesema Kuwa "Mimi ndiye niliyesoma na Kugundua Namba za Bastola
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo
Shahidi: Kwenye hiyo Fomu Hakuna
MAHAKAMA kichekoooooo
Kibatala: Wacha Nirudie tena
Kibatala: Kuna Mahala Umesema wewe Ulisema namba za Bastola
Shahidi: Kwenye maelezo haijaandikwa
Kibatala: Katika MAELEZO yako kuna Mahala au Kuna sehemu Yoyote Kuna Jina Luger..?
Shahidi: Lipo
Kibatala: hii fomu alijaza nani?
Shahidi: afande Jumanne ndiyo alijaza
Kibatala: ulimfafanulia jaji tofauti ya Kielelezo Kimoja kina Luger na Kingine hakina
Shahidi: Hapana sikumfafanulia
Kibatala: Katika Maelezo Yako E2 ulitaja Aina za simu, Je Namba ya Simu Uliweka Kwenye Kielelezo Chako
Shahidi: Hapana Sikuweka
Kibatala: na wala hiyo Tofauti hukufafanua
Shahidi: Sikufafanua
Kibatala: Shahidi Unafahamu IMEI namba za Simu ya Adama Kasekwa?
Shahidi: Hapana
Kibatala: na wala hukufahamu kuwa kuna IMEI Moja wala 02
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikal hukufafanua kuhusu IMEI Moja au Mbili kwa Mtu anayeitwa kasekwa
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wala Hukuomba Ujikumbushe labda kwa Sababu Namba ni Nyingi, Ulifanya hilo zoezi
Shahidi: Hapana
Kibatala: katika hiyo Karatasi Kuna Maneno kama CZ 100 ya Kufafanua hiyo Bastola
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Walikwambia Karatasi hii Ndiyo inatakiwa kumtia Hatiani Mshitakiwa bila Kuacha Shaka yoyote
Shahidi: Niliambiwa
Kibatala: Twende Simu Card ya Vodacom
Kibatala: Unafahamu Kwanza hiyo ICCD namba
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo Unakubaliana nami kwamba hizo ICCD Namba ambazo ndiyo Utambulisho katika Ushahidi wako hazijaingia
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: hata namba ya Adam Kasekwa ya Hallotel kuhusu ICCD namba, hukutaja hivyo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: wala hukufafanua
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: wala hujazungumzia Kabisaaaa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: katika Ushahidi wako ulitambua huyu kama nani
Shahidi: Kama Mohammed Ling'wenya
Kibatala: Katika Ushahidi Wako ulimtambua Mtu anaitwa Mohamed Abdilah Ling'wenya
Shahidi: Hapana Sikutaja Ling'wenya
Kibatala: Kwenye Statement D2 Ulimtaja huyu Kama nani tunakubaliana tutakachokipata pia tukitumie
Shahidi: ndiyo
Kibatala: Naomba D2 Kibatal:a Taja huyo Mtu humo Umemtaja Kama Mohammed Abdalahi Ling'wenya
Shahidi: Ndiyo Mohamed Abdilah Ling'wenya
Kibatala: Mwanzoni Umesema Halipo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulifafanua Kuwa Katika Utambuzi hapa Mahakamani na ile Hati yako ya maelezo pamoja Na kutofautiana, Ulifafanua Kwa Jaji kwamba huyo ni Mtu Mmoja
Shahidi: Shapana
Kibatala: Katika Ushahidi Wako Kuna Mahala Popote umezungumzia Kuna Afisa Wa Polisi anaitwa Ramadhan Kingai
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati Maafisa Wa Polisi wanajitambukisha ulikwepo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala Hakuna Mahali Umezungumzia Kuhusu Kingai, Kwamba alikwepo ila hujamtaja
Shahidi: Sijazungumza hilo
Kibatala: Wakati Unaulizwa Maswali na Mtobesya kuhusiana na Saini zako na Kuna Mazingira zinatofautiana na Kwamba Kuna fomu ulisaini Ukiwa Umesimama
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Wakati Jumanne anajaza hii fomu pia alikuwa amesimama?
Shahidi: Ndiyo alikuwa amesimama
Kibatala: mara zote wakati Unatoa Ushahidi wako Ulikuwa Unatoa Maneno "Glocery" Mwambie Mheshimiwa Jaji Katika Maelezo yako kuna Neno Glocery?
Shahidi: hakuna
Kibatala: Maneno gani uliyatumia
Shahidi: Bar
Kibatala: Ulifafanua kwa Mheshimiwa Jaji Kwamba Ulikuwa unalenga Kitu Kimoja hicho hicho
Shahidi: Sikufafanua
Kibatala: Kati yako wewe na Fremu 4 za Jumla na Vipodozi na Upande wa Pili Ndiyo Glocery na Kwamba Sehemu yako ya Mbege ni Nyuma kabisa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kutoka Kwenye Fremu 4 Duka la Vipodozi hadi eneo la Tukio ni hatua ngapi?
Wakili wa serikali: Objection Shahidi ameshasema hamfahamu Athma
Kibatala: Kutokaa kwenye Flemu 4 Mpaka waliokamatwa hawa ni Kama Hatua ngapi
Shahidi: Kama 10
Kibatala: Bado Unasisitiza Ushahidi wako waliwaacha hawa wa kwenye Fremu hatua Tatu wakakufuata wewe wa Hatua 10
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Shahidi Unafahamu au hufahamu Mmlilki wa hilo Duka la Jumla na Duka la Vipodozi ni Dada yake Ling'wenya.?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: hilo eneo lina Kiongozi wa Mtaa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: anaitwa nani
Shahidi: Sigfrid Malewa
Kibatala: Katika hizi Hati hapa unaona Jina la Sigfrid Malewa
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Msaidizi Wake anaitwa nani
Shahidi: Namjua Kwa Jina Moja la Temba
Kibatala: anaishi wapi na eneo hilo
Shahidi: anaishi Mbali
Kibatala: katika Kielelezo chako Namba 02 Mnamo tarehe 05/08/2020
nilikuwa naenda Saloon hapo Rau Madukani
Shahidi: Ni kweli nilisema hivi
Kibatala: Kwamba Saa 7 Kamili Mchana
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi Wako Ulitoa Ufafanuzi kwamba Ulikuwa ni Muda wa Makadirio
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Huko Saloon Ulikaa Muda gani?
Shahidi: Kama Robo Saa
Kibatala: Na Ukamwambia Mallya Ukarudi Sehemu ya Biashara Kwa muda gani
Shahidi: Kama Robo saa
Kibatala: kwa hiyo kama Saa Saba Na Nusu
Kibatala: kwa hiyo kama Saa Saba Na Nusu
Kibatala: Na Katika Kielelezo Chako D1 Maelezo uliyoyatoa Ulisema ni Saa Saba, Si Unaona kuna tatizo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Tatizo ambalo hukulitolea Ufafanuzi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Nani atutatulie hili tatizo
Shahidi: Mimi Mwenyewe
Kibatala: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali nilikusikia ulisema, hawa washitakiwa wawili walipigwa Pingu, ulimwambia Mheshimiwa Jaji Sasa Kama baada ya Kupigwa Pingu nini Kiliwatokea
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Mlifika central police Kwa usafiri gani
Shahidi: Watuhumiwa WALIENDA kwa Gari Nyingine na sisi tukaenda na Gari Lingine
Kibatala: na ukamwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba na hilo gari lina Maofisa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Aliwahi Kukwambia Kesi Mama ipo Dar es Salaam
Shahidi: Hakuwahi kuniambia
Kibatala: Wewe ulikuwa unajua kesi na Kila kitu kipo Moshi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: ulisikia hao Maaskari wanaongea na Mtu yoyote kuhusu washitakiwa Kukamatwa
Shahidi: Hapana
Kibatala: ulisikia Maofisa Wa Askari, Kwamba Yupo wapi Moses Lijenje
Shahidi: Nilisikia akimuuliza Mwenzenu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji huyo Mwenzao Katika Statement Yako D2 umezungumza Walikuwa wangapi
Shahidi: Watatu
Kibatala: Maelezo yako chini ya Kiapo, Kielelezo D2 ulizungumzia kuhusu Vijana watatu
Shahidi: Hapana
Kibatala: we Umezungumzia wangapi
Shahidi: wawili
Kibatala: palikuwa na Vijana wawili wanakunywa pale, Ndiyo ukivyosema
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji huyo Kijana wa tatu, umezungumzia Nini Kilitokea huyo Kijana wa tatu.?
Shahidi: Hapana
Kibatala: zoezi la Kusajili laini ya Simu, uliona kwamba wanasajili Simu
Shahidi: Ndiyo niliona
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji walikuwa wanasajili Laini ya kampuni Gani
Shahidi: Sijui sasa Kibatala: Unafahamu iwapo Ndiyo au Lah kwamba hii laini ya Hallotel au Airtel ndiyo zilikuwa zinasajijiwa Siku hiyo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mlivyofika pale Polisi Central Station Moshi Iwapo Ulimwambia Chochote Kuhusu Kushuhudia Vile Vifaa Vikiingizwa Kwenye Daftari rasmi
Shahidi: Hapana
Kibatala ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Iwapo hawa washitakiwa wawili walikuwa na vitu kama Wallet au Kitu Kingine anavyobeba Kijana wa Kiume.
Shahidi: Sijazungumzia
Kibatala: Wewe Kama shahidi Huru, Kama Ulishuhudia MALI Binafsi za Washitakiwa Kuingiziwa kwenye Daftari Maalum pale Kituoni
Shahidi: Si kumwambia
Kibatala: nimesikia mara kadhaa unataja DADA Esther ulifafanua Kwa namna yoyote ile
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba huyu Dada Esther Unamfahamu anaishi wapi
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unafahamu Watu wenye Biashara Ndogo Ndogo hupewa Kitambulisho Maarufu Kama Kitambulisho cha Wamachinga
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: ulimuonyesha Mheshimiwa Jaji ili ajue Kuwa Unakitambulisho
Shahidi: Hapana
Kibatala: ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Biashara yako inaitwaje kama vile Mama Mbege
Shahidi: Hapana
Kibatala: hata kumwambia Mheshimiwa Jaji kwamba Umesahau kutaja Jina la Biashara yako ulisema
Shahidi: Sikusema
Kibatala: ulisema hapa kwamba Mohamed Abdilah Ling'wenya Alikuwa amevaa Nguo gani wakati anakamtwa
Shahidi: Sikusema
Kibatala: na Adamu Kasekwa ulisema amevaa Nguo gani
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama Ulisema ulishuhudia kielelezo Namba Moja kilijazwa Kwenye Fomu tatu na Fomu Moja akapewa Adam kasekwa
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulisema Kwamba Ulisikia Afisa wa polisi akisema Unahaki ya kupata fomu Moja ya Hati za Kuchukulia hiyo Bastola
Shahidi: Hapana
Kibatala: unasema Ulifanya Kazi na Afisa wa Askari Wa a Polisi Jumanne, na baadae wakakuonyesha Afisa Mwingine wa Polisi aliyekuchukua maelezo Je ulitolea Ufafanuzi kwa Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Hapana
Kibatala: Leo umesema Kwamba Bastola Ina Rangi Nyeusi, Je katika Maelezo yako Kuna Sehemu Umetaja Rangi ya Bastola
Shahidi: Hapana
Kibatala: kwa hiyo Rangi umetaja Leo
Shahidi; Ndiyo
Kibatala: ulifafanua Kwa Mheshimiwa Jaji kamba wewe kabla Ulikuwa Unaifahamu kabla
Shahidi: Hapana
Kibatala: Pamoja na Kwamba Wakati Ule ndiyo Ulikuwa na Kumbukumbu, Maana umesema wewe Tukio la Muda Mrefu, Mpaka unasahau, Lakini wakati Ule Hukusema Rangi ya bastola.
Kibatala: nimesikia umesema Vitu vinavyodhaniwa kuwa Madawa ya kulevya, Je kuna Mtu yoyote alimtuhumu baada ya Kupatikana kwa Madawa ya kukevya
Shahidi: Hapana?
Kibatala: kwa Ushahidi wako wewe unasema Adam Kasekwa alipatikana na Madawa ya Kulevya
Shahidi: Sikufahamu hatima yake
Kibatala: Kuhusu Saini ya D01 na D02 ulifafanua kabla ya Wakili Mtobesya Kuuliza maswali
Shahidi: Hapana Sikufafanua
Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwa Shahidi Huyu naomba Kuishia hapo
Jaji anaandika
Wakili wa Serikali: Tunaomba Hairisho ili tuweze Kumalizia Asubuhi
Jaji: Kuna Kama Dakika 50 hivi ilituweze Kuhitimisha Leo
Wakili wa Serikali: Sawa Mheshimiwa Ngoja tuendelee
Jaji: Wakili wa Serikali Esther Martin
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Mahakamani na Malya Kuhusiana na Rangi za Tshirt na ukasema siyo Nyeusi Bali Rangi ya Dark Green, Wewe ulikuwa Unaona nini
Shahidi: Nyeupe, Kijani na nyeusi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Maswali Kwenye Kielelezo D2 ukaambiwa Vitu mbalimbali Kwenye Maelezo hayo uliyoandika Polisi Watuhumiwa hawakujulishwa Makosa yao, Na Mengine Mengi fafanulia mahakama ni Vipi hayo yamejitokeza
Shahidi: Rudia Swali
Wakili wa serikali: Swala la Watuhumiwa baada ya Kuambiwa Kaa chini kama walijulishwa Makosa yao, Mahakamani umesema lakini humu hayapo
Mtobesya: samahani, Shahidi anaenda kujazia Statement
Jaji: tungemuacha ajibu kwanza
Wakili wa Serikali: Nasema wakati wakili anamuuliza Maswali akakuuliza kuhusu Maswali Ambayo Hapa Mahakamani umesema ila Kwenye Maelezo Hakuna, Ni kwa vipi hayo yamejitokeza
Shahidi: Yamejitokeza kwa sababu ni uandishi tu
Wakili wa Serikali: Kivipi Shahidi: Katika Kutoa......Maelezo niliyoandika na maelezo ya hapa mahakamani.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Kuhusu Maelezo haya, pia kwamba Fomu iliyosainiwa eneo la Tukio ni Moja lakini Mahakamani umesema Fomu nne
Shahidi: Kimetokea tu Lakini fomu zilikuwa Nne
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kwamba Ulijuaje kwamba Ulichokiona ni Kitambulisho Cha Polisi, Ukasema Ukaona Chata ya Taifa
Jaji: Siyo Chata Bali Chapa
Shahidi: Nilikuwa namaanisha Chapa ya Kipolisi
Wakili Malya: Tunapinga hilo Jibu
Jaji: sahihi, Hakujibu hivyo
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kama Ulionyesha CZ 100, Fafanunua Mahakamani wewe Uliona nini
Shahidi: Niliona A5340
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia Kwamba Kwenye Maelezo haya Uliyasoma na Uliyajua Majina Baada ya Upekuzi lakini Mahakamani Umesema Kabla ya Upekuzi
Shahidi: Niliyajua hayo Majina Kabla ya Upekuzi
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Mimi nimemaliza namuachia Mwenzangu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Uliulizwa Kama Vijana wawili pale Rau Uliwaona Wakisajili laini na Baadae Ukasema Walikuwa na Kijana anayesajili laini
Shahidi: Mimi niliwaona na Kijana anayesajili Laini
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kwamba hao Vijana walikuwa wawili na Baadae Ukasema watatu. Wakati gani Uliwaona wakiwa watatu
Shahidi: Wakiwa wanasajili laini
Wakili wa Serikali: Wakati gani walikuwa wawili
Shahidi: Wakati wa Ukamatwaji
Kibatala: Objection anasema Jina la Amelifahamu lini it's a New fact
Jaji: hili swali limezungumza Katika Mazingira Matatu Kama alitaja, Kama ALIJAZA fomu na Kama alitaja kabla Hili Jibu la Lini alimfahamu nafikiri siyo Fact Mpya
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kwenye Fomu kuhusiana na Neno Adamoo Kama Ulikuwa umelisema, Fafanua Hapa Mahakamani Jina la Adamoo Umelifahamu lini
Shahidi: Nimelifahamu Leo
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kuhusiana na Ukamataji kuhusiana na Lile Neno CZ100 Halipo, elezea Kilichoandikwa kwenye Hati hiyo ni nini
Shahidi: Iliandikwa namba A5340
Wakili wa Serikali: Uliulizwa pia na Kuhusu Hati yako Kuhusu Glocery na Huku ni Bar, Kwa Mujibu wa Ushahidi wako walikuwa kwenye eneo lipi
Shahidi: walikuwa kwenye Glocery ya Dada Esther
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kuhusiana na maeneo waliokamatwa watuhumiwa haswa tarehe 05 Mwezi 08 Ukasema Duka la Jumla na Vipodozi na ulipokuwa wewe Eneo lipi walikuwa karibu
Shahidi: eneo waliokamatwa ni Karibu na Sehemu yangu ya biashara.
Wakili wa Serikali: kwanini jina Sweetfred Malewa Halipo kwenye Hati ya Upekuzi
Shahidi: Sikuulizwa
Wakili wa Serikali: Kuhusu wewe Kufika kwemye eneo lako la Biashara, Muda gani ulienda Saloon na Muda wa Ukamataji kuwa saa Saba, Kilichotokea kilikuwa saa ngapi
Shahidi: ilikuwa majira ya Saa Saba Mchana
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kama uliona Watuhumiwa kama walipofikishwa Polisi, Kama Ulishuhudia Uandikishwaji wa vitu vyao Kwanini hukutoa Ushahidi huo
Shahidi: Sikutoa sababu Sijaulizwa
Jaji: Jamani Mnasikia hukoooooo.? Mahakama Hatusikiiiiiii
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kwamba kama katika Ushahidi wako alikwepo Askari anayeitwa Kingai kama alikwepo Askari yupi aliyehusika Kwenye eneo la Ukamataji Kwa Siku hiyo
Shahidi: sikumzungumzia kwa sababu Sikuulizwa ni Askari gani aliyekamata anajibu Kwa Sauti ya Chini sana
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Tukomee hapa
Jaji: Shahidi Nashukuru kwa Ushahidi Wako
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tunaomba Hairisho Mpaka Kesho Saa 03 Asubuhi ambapo tutaendelea na Shahidi Mwingine
Upande wa Mashitaka
Kibatala: Mheshimiwa hatuna Pingamizi
Jaji anaandika Kidogo
Jaji : basi Maombi ya hairisho yanakubaliwa hadi Kesho saa 03 Asubuhi Upande wa Mashitaka Maelekezo ni kwamba Mtatakikwa mlete shahidi Na Washitakiwa wataendelea Kuwa Rumande Mpaka Kesho saa 3 Asubuhi
Jaji anatoka