Stuxnet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 10,390
- 17,977
Nisaidieni mwenzenu pengine ubongo wangu umefika mwisho wake wa kufikiria. Unapokwenda Tegeta kutokea Mwenge baada ya kanisa la Efata au la Mwingira, kuna kituo cha shirika la uchumi la JKT ambao wamerundila matrekta kwa ajili ya kuuza. Ingawaje sina takwimu za mauzo waliyofanya lakini nadhani kwa nchi iliyotamka kuwa KILIMO KWANZA basi si sahihi matrekta hayo kuwa hapo. Hayo matrekta yanapaswa kuwa yako huko Sumbawanga, Mbeya, Morogoro, Songea, Shinyanga kwa ajili ya kunyanyua kilimo chetu duni cha jembe la mkono. Kuyaweka hapo Mwenge hakuna tofauti na biashara za akina yakhe za show rooms za magari zilizoenea kila mahali DSM.
Kama muhusika ni Jenerali Mwamunyange au Dr Hussein Mwinyi au kama ni Waziri Wa Kilimo basi nasema hawaisaidii chochote nchi hii kwa upande wa Kilimo. Najua watasema ni biashara lakini Kama wangewatumia wataalamu Wa biashara wangewaonyesha namna ya kuyauza kwa mifumo ya hire purchase
Kama muhusika ni Jenerali Mwamunyange au Dr Hussein Mwinyi au kama ni Waziri Wa Kilimo basi nasema hawaisaidii chochote nchi hii kwa upande wa Kilimo. Najua watasema ni biashara lakini Kama wangewatumia wataalamu Wa biashara wangewaonyesha namna ya kuyauza kwa mifumo ya hire purchase