oh yeah?
Bila shaka post no 124 ya kijana wetu Mnyika imenijibia hili?
oh yeah?
WanaJF,
Kwa muda nimekosa kuchangia ndani ya jukwaa hili, hata hivyo nimevutwa na mjadala huu unaondelea kuandika machache. Yapo makundi makubwa mawili ya mawazo katika michango mbalimbali inayotolewa; upande mmoja ni wale wanaojenga hoja kwamba jambo la msingi la kwanza kabisa ni KUINDOA CCM MADARAKANI na mengine yatafuata; kundi la pili ni lile linalotaka kwanza MBADALA WA CCM UONEKANE BAYANA KWANZA na ndio iwe sababu na msingi wa kuiondoa CCM madarakani. Kundi hili linataka swali la nini kinafuata baada ya kuiondoa CCM madarakani litangulie kabla ya uamuzi wa kuindoa CCM madarakani. Kwa maoni yangu, nakubaliana na wenye mtizamo kwamba mambo yote haya mawili yanapaswa kwenda sambamba ama kwa pamoja; yote ni muhimu na yote yanahitajiana.
Kwa hatua ambayo nchi yetu imekifikia hivi sasa ya dola kutekwa (state capture) na chama kinachotawala kufunga fungate na ufisadi/mafisadi ni dhamira yoyote ya kuleta sera na uongozi mbadala haiwezi kutimia bila kubadili mfumo wa utawala. Utatu uliopo baina ya watendaji wa serikali kwa upande mmoja, wanasiasa viongozi wa kuchaguliwa na wananchi na viongozi wa chama kwa upande mwingine na maslahi ya kibiashara ya ndani na nje ya nchi kwa upande wa tatu; mkazo wowote wa kufikiria sera unakuwa ni mchezo wa kinadharia kama hautaenda sambamba na kubadili mfumo wa utawala labda kama kubadili huko mfumo wa utawala kuwe ndio sera yenyewe.
Katika hali iliyofikia sasa kuiondoa CCM madarakani ambayo ni sawa na kuikomboa dola iliyotekwa kunaonekana kuwa ni suala la lazima na la dharura kwa ajili ya demokrasia, maendeleo na hata kudumisha usalama na amani ya nchi ambayo inaelekea kuwa mashakani siku za usoni kama hali itaendelea kama ilivyo sasa.
Lakini katika kutekeleza azma hii, vipo vyama vimeonyesha uthabiti na uthubutu wa kuwa mbadala, CHADEMA ikiwa moja ya tumaini jipya la watanzania ndio maana naamini mjadala huu umejikita katika chama tajwa. Unaweza kujiuliza kwanini katika msururu wa vyama kumi na nane (18) vya Tanzania, mabadiliko ya kweli yaonekane yanaweza kupatikana kupitia CHADEMA?
Harakakati za kisiasa zilizofanywa na CHADEMA ndani na nje ya Bunge kwa kushirikiana na vyombo vya habari na wadau wengine waliokubali kutanguliza mbele maslahi ya taifa kwa zimesalisha AJENDA ya kisiasa-ambayo imepewa jina la mapambano dhidi ya ufisadi na kutetea rasilimali za taifa ambayo yamefanya uwajibikaji katika utawala kutazamwa kama moja ya sera za muhimu sana za taifa letu.
Naamini jambo hili lisingepata mafanikio ya kutosha kama CHADEMA kwa upande wake isingekuwa na misingi mizuri ya uongozi na ya kisera tangu kuasisiwa kwake. Kama falsafa, itikadi na sera za CHADEMA zingekuwa kinyume sana na matarajio tunayoyatazamia harakati hizi za miaka ya karibuni zingeonekana kama kiini macho ama upepo wa wakati.
(Falsafa, itikadi na malengo ya chama yanaweza kutazamwa kupitia katiba ya chama ambayo inapatikana pia katika mtandao www.chadema.or.tz, pia katika mtandao huo inapatikana ilani fupi(popular version) ya CHADEMA ya mwaka 2005)
Hata hivyo katika nchi yenye uoza katika utawala kwa kiwango cha Tanzania taasisi zake nyingi huru- si CHADEMA tu, hujikuta katika hali ya kupinga uozo iliopo na kukosoa badala ya kutumia muda mwingi zaidi katika kueleza mbadala na kutoa matumaini. Huu ni mtego wa kawaida kwa silika ya binadamu na ubinadamu na taasisi zake; huwezi kwenda eneo lenye rundo la takataka kubwa kuliko usafi uliopo ukazungumza usafi kabla ya kuzungumzia kuondoa uchafu. Katika mazingira hayo unaweza kujikuta unazungumzia kuliondoa rundo la taka kabla hata ya kufikiria utafanya nini mbadala baada ya kuliondoa.
Lakini maelezo haya hayaondoi wala kupinga umuhimu wa swali la msingi lililoulizwa; kwamba CHADEMA ITAFANYA NINI IKIINGIA MADARAKANI ama NINI TAIFA LITARAJIE KUTOKANA NA MABADILIKO YA MFUMO WA UTAWALA?
Jibu la muda mrefu la swali hili linapatikana katika misingi ya muda mrefu ya kifalsafa, kiitikadi, kisera, kimalengo na kitaasisi ya CHADEMA. Je, misingi hii haitoi tumaini kwa watanzania na dira ya mabadiliko ya kweli? Ni maeneo gani yanayohitaji kuboreshwa zaidi? Hapa ni muhimu badala ya viongozi wa CHADEMA kujibu, mawazo yangetoka kwanza kwa wanachama na wananchi kwa ujumla. Naamini viongozi wa CHADEMA wapo tayari kusikiliza.
Jibu la muda mfupi linapatikana katika ilani ya uchaguzi (2010-2015) ambayo kutokana na misingi ya muda mrefu na hali ya taifa ya sasa inapaswa kutolewa; jibu ya swali hili kwa maoni yangu hawawezi kulitoa kwa ukamilifu wake leo kwa kuwa chama bado hakijazindua ilani yake ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Chama kiko kwenye mchakato wa majadiliano na mashauriano ya ndani (consultations), kabla ya kupata maoni ya nje na kabla ya kupitisha ilani katika vikao vya kikatiba vya chama ambavyo ni kamati kuu, baraza kuu na mkutano mkuu.
Hivyo, chama kiko wazi kupokea maoni kuhusu nini ambacho wanachama na wananchi kwa ujumla wangependa kitiliwe mkazo katika ilani ya CHADEMA. Hivyo, nawaomba wote ambao mngependa kushiriki katika kupanga CHADEMA IFANYE NINI IKIINGIA KWENYE UONGOZI au TAIFA LITARAJIE NINI KUTOKANA NA MABADILIKO YA MFUMO WA UTAWALA mtuandikie; unaweza kuandika kupitia info@chadema.or.tz, nakala kwa slaa@chadema.or.tz na mnyika@chadema.or.tz ama unaweza kumtumia kiongozi mwingine wa CHADEMA.
Kwa tafsiri rahisi, chama cha siasa ni jumuia ya watu wenye dhamira inayoendana wenye kulenga kuchukua mamlaka ya dola kupitia uchaguzi ama njia nyingine za kidemokrasia kwa lengo la kuitekeleza azma hiyo. Kwa hiyo badala ya kuhoji tu, CHADEMA itafanyaje ama taifa litarajie nini ni muhimu kushiriki katika kuamua hatma yako na ya taifa kwa ujumla. Badala ya kusubiri chama kutoa ilani na baadaye kuikosoa ama kuikana ni muhimu kushiriki katika kuiandika.
Nitaomba kwa kadiri inavyowezekana mawazo ya awali ya ujumla yafike kabla ya tarehe 20 Julai 2010. Mawazo mahususi yanaweza kutolewa katika hatua za baadaye kwenye rasimu kabla ya mkutano mkuu wa chama ambao unatarajiwa kufanyika mwezi Agosti. Hata hivyo, kuna mtanziko(dilemma) katika mchakato wa utengenezaji wa ilani kwa kuwa kwa upande mmoja unaweza kuwa na shauku ya kumhusisha kila mtu/mwanachama katika hatua zote lakini kwa upande mwingine unataka baadhi ya mambo katika ilani yawe siri hususani yale yenye ubunifu wa pekee ili yazinduliwe wakati wa kampeni au wakati wa karibu na uchaguzi kuweza kumsha hamasa ya kuungwa mkono; changamoto ipo katika kuwianisha(balancing) matakwa hayo mawili. Najua vipo vyama ambavyo vimeshazindua ilani zao, CHADEMA itafanya hivyo kwa kadiri ya ratiba yake ambayo ilishaitangaza toka Aprili 27 mwaka huu. Nawatakia mjadala mwema
JJ
Wakuu,
Naona wengi wamekazana sana kumjibu Mzee Mwanakijiji kwa madhumuni ya kutaka kumshinda kwa hoja kiasi cha ku-miss points muhimu zinazoletwa na wachangiaji wengine.
Nampongeza Mwanakijiji, aelewe kwamba kichwa chake kimejaa ubongo na anayoyatoa humo kichwani na moyoni mwake yanachoma kama nchi ya mkuki ndio maana watu hawaishi kukereketwa na kumjibu.
Nguruvi3, tunaweza kuongoza nchi bila sera? Yaani tunawafuata watu tu alimradi wanasema wao ni bora kuliko waliokuwepo kabla?
MKJJ chukua muda kidogo umsome tena Nguruvi3 ameeleza vizuri tu kuwa na sera makini ni muhimu lakini kama hakuna [level field] tena kataja neno hili mara mbili ni ngumu sana kushinda uchaguzi. Sasa wewe kama husomi na kuwaelewa watoa mada utabaki kuuliza swali hilo moja kwa muda mrefu sana.Nguruvi3, tunaweza kuongoza nchi bila sera? Yaani tunawafuata watu tu alimradi wanasema wao ni bora kuliko waliokuwepo kabla?
Yes and No, Nchi inaongozwa kwa kufuata katiba na sio sera, sera inavaliwa na kuvuliwa kama shati kila asubuhi. Ndio maana chama tawala chenye sera fulani kinaweza kikapigwa chini na chama kingine chenye sera pingamizi kikapewa uongozi, ndio maana ya Uchaguzi Mkuu.tunaweza kuongoza nchi bila sera?
Hawa ni watu gani unaowaongelea ambao unadai wanasema wao ni bora kuliko waliokuwapo bila kusema watafanya nini tofauti.Yaani tunawafuata watu tu alimradi wanasema wao ni bora kuliko waliokuwepo kabla?
Mkuu,je kwa mtizamo wako unadhani tulipaswa kujiandaa kwanza namna ya kujitawala kabla ya kupata uhuru?Je muda gani ungetosha kwa maandalizi hayo kabla ya kuwa tayari kupata uhuru?Je matatizo tuliyonayo takriban miaka 50 baada ya uhuru ni matokeo ya kupata uhuru pasipo kujiandaa au ni matokeo ya sera mbovu (au nzuri lakini utekelezaji mbovu)?Je wenzetu waliopata uhuru kisha wakamudu kufanya vizuri walikwenda kwenye chuo au taasisi ya kujifunza kujitawala?Rev Kishoka Labda turudi kwenye historia ya kupata Uhuru wetu, tulipigania Uhuru tukataka tujitawale, lakini tangu tumepata Uhuru huo miaka karibu 50 sasa , tumekuwa sawa na ile merikebu iliyoweka nanga inayoyumba mbele nyuma kufuata mkondo wa bahari.
Mkuu,je kwa mtizamo wako unadhani tulipaswa kujiandaa kwanza namna ya kujitawala kabla ya kupata uhuru?Je muda gani ungetosha kwa maandalizi hayo kabla ya kuwa tayari kupata uhuru?Je matatizo tuliyonayo takriban miaka 50 baada ya uhuru ni matokeo ya kupata uhuru pasipo kujiandaa au ni matokeo ya sera mbovu (au nzuri lakini utekelezaji mbovu)?Je wenzetu waliopata uhuru kisha wakamudu kufanya vizuri walikwenda kwenye chuo au taasisi ya kujifunza kujitawala?
Tukirejea kwenye hoja ya kuiondoa CCM au tusubiri kwanza kipatikane chama mbadala kitakachomudu kutufikisha tunapopaswa kuwepo.Binafsi,naona kosa kubwa linalofanyika katika hoja ya "kusubiri mazingira yawe conducive ie kuwa na chama ambacho hakitarejea yaleyale ya CCM" ni kusahaua au kupuuza ukweli kwamba CCM itakuwepo wakati maandalizi hayo yanafanyika.Na kwa vile itakuwepo,na pia kwa sababu INA NIA,UWEZO na SABABU (hata kama sio sababu halali) ya kutaka kudumisha utawala wake wa kidhalimu,NI LAZIMA ITAHUJUMU JITIHADA HIZO.Tukumbuke kuwa CCM ni kama virus au bakteria anayesababisha ugonjwa mwilini.Ili afya ya mgonjwa husika iboreke au apone kabisa ni muhimu kuteketeza virus au bakteria huyo.Ni sawa pia na ndoo yenye tundu.Hakuna namna tutakavyoweza kujaza maji kwenye ndoo hiyo pasipo kuziba tundu hilo.Ni sawa na jambazi aliyeingia ndani,swali tukishamtimua then what halina nafasi.
Hivi,kwa minajili ya mjadala huu,tukikubaliana kuwa tulipaswa kusubiri tujiandae vya kutosha kabla ya kupata uhuru wetu,na sasa tunapaswa kujiandaa vya kutosha kabla ya kukipa dhamana chama kingine (kwa hofu kinaweza kuturejesha palepale tulipoiacha CCM),je ni muda gani unatosha kwa ajili ya maandalizi hayo?Suala la muda ni muhimu sana kwani sote tunafahamu kasi ya uharibifu unaofanyika kwenye raslimali zetu,umoja wetu,mshikamano wetu na mambo mengine muhimu kwa ajili ya ustawi wa taifa.Je suppose tutakapohitimu maandalizi ya kujitawala pasipo CCM then tukajikuta tuko katika hali kama ya Somalia (naam,CCM wanatusukumia huko) maandalizi hayo yatasaidia nini?
Kama tungemruhusu mkoloni aendelee kututawala kwa vile tu hatujajiandaa vya kutosha kujitawala sie wenyewe,halafu mkoloni akakomba kila raslimali na kuteketeza nguvu kazi yetu,hivi (licha ya mark time tunayopiga hivi sasa) hali si ingekuwa mbaya maradufu?Au kwa mfano jitihada za civil rights movement huko Marekani zingechukua mtizamo huu wa "tujiandae kwanza"....na Amin alipotuvamia,"tujiandae kwanza"...na Wahutu na Watutsi nao,"tujiandae kwanza"...
Tusisahau kuwa tunaweza kusubiri muda mwafaka wa kuiondoa CCM madarakani lakini,unfortunately,muda hautusubiri sie tuwe tayari "kujitawala pasipo CCM".Na licha ya muda kutotusubiri,kila dakika ya CCM kuwa madarakani ni sawa na mazalisho ya kasi ya virusi vya ukimwi mwilini (na ndio maana matabibu wanashauri mwathirika kuanza tiba pindi CD4 count ya mwathirika inapofikia kiwango flani,nadhani 250 or something like that).
Hivi wakati tuko katikati ya "somo la kujiandaa kujitawala pasipo CCM" kisha tukabaini kuwa nchi inatumbukia kwenye handaki lenye kina kirefu,tutakatisha "kozi" hiyo?Tukumbuke pia kwamba kwa kila siku ambayo CCM inakaa madarakani inazidi kutengeneza mazingira ambayo yatatengeneza ugumu mkubwa (kuliko ilivyo sasa) kuwaunganisha Watanzania dhidi ya vikwazo vya maendeleo na stawi wetu.Wanawalaghai Waislam kuwa watawaanzishia mahakama ya kadhi ili wapate kura za Waislam,wanatumia ukabila ili waendelee kuwa madarakani (esp kwenye ubunge,udiwani,nk),wanakumbatia wahalifu hatari ili wawapatie fedha za kuendelea kubaki madarakani,wanakandamiza mawazo mbadala au/na endelevu ili kuficha maovu yao kwa umma,nk,nk,nk....Je hivyo vyote sio raw materials za vurugu hapo baadaye?SASa kama tunaafikiana katika hilo,je busara tu haiwezi kutufahamisha kuwa tunachosubiri ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu kwa maana kwamba kila kilo moja ya jitihada za maandalizi ya kijitawala tutakayofanya,CCM na washirika wake wanaondoa kilo mbili?
Rev. Kishoka
Umeandika marefu lakini umekuwa kila mara huji na mapya, unaonekana unandoto za chama cha kufikirika ambacho hakijawahi kutokea, chama ambacho hakina mawaa kitakachokuwa kinagawa maziwa kwa wananchi wake.
Mwache Kikwete aendelee kujifunza huku akiwa madarakani na waache Chadema wasiwe na majibu unayoyataka ya ili iweje.Tusipoichagua Chadema tutaichagua CCM na maisha yanaendelea.
Hizo hadithi zenu mnazozitoa mkiwa huko ulaya hazitufai sisi, tutachagua hivyo hivyo vyama mnavyovidharau. Hayo mawazo yenu yakutaka kuwapotosha watu mpeane huko huko mliko.
Mkuu Rev. Kushoka, nimesoma maelezo yako marefu kwa umakini mkubwa lakini hadi nafikia mwisho nimeshindwa kukuelewa hasa unataka nini na tatizo lako ni nini, unataka tufanye nini katika uchaguzi mwaka huu au tuendelee tu na hadithi. Kuuliza Chadema wamefanya nini katika huu mfumo tulio nao wa chama-serikali ni kutokutaka kuukubali ukweli kuwa mabadiliko hayasubiri kesho.
Kwanza, Chadema ni kweli hawajazindua bado ilani yao ya uchaguzi wala kumteua rasmi mgombea wao wa Uraisi. Lakini pamoja na yote hayo Chadema wana sera zao ambazo ziko wazi kwa yeyote anayetaka kuzifahamu na ambazo wamejitahidi kwa kadiri ya uwezo wao kuzifiksha kwa wananchi kwa njia mbalimbali kama operation sangara, mikutano na vyombo vya habari. Pia natumaini wanapata ushauri mwingi tu kutoka kwa wadau mbalimbali wengi tu lakini sidhani kama wanalazimika kukubaliana na kila jambo hata kama linatoka kwa Rev
Pili chama cha siasa kinaongozwa na watu, binadamu, na kwa vyovyote wote hawawezi kuelewana kwa wakati wote na kwa mambo yote na hili haliwezi kuchukuliwa kama upungufu wa chama. Huko Marekani tulishuhudia Obama na Clinton ambao wote walikuwa Democrats wakitoana macho wakati wa kumtafuta mshika kibendera lakini lilipofika swali la kuwatoa Republicans walisahau tofauti zao na hivi sasa wanafanya kazi pamoja.
Mimi, kama Mtanzania mwenye uchungu na taifa lake, hata ukiniamsha usiku wa manane sitasita kusema ndoto yangu ni kuiona CCM iking'oka madarakani kabla ya kitu chochote kile. Ninaamini kuwa kila dakika CCM inavyoendelea kubaki madarakani ndivyo nchi inavyozidi kudidimia na kuangamia - ni kama vile unamkuta mwanao anazama majini, cha kwanza unamtoa kwenye maji ndipo unafikiria pa kumpeleka.