Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Nilifahamu juu ya mazungumzo ya baadhi ya uongozi wa juu wa CCJ na Chadema kwa muda kidogo; Yalitokana vile vile na ushauri wa watu mbalimbali kuwa CCJ iunganishe nguvu na Chadema. Hata hivyo hadi hivi sasa kilichofanyika ni baadhi tu yaviongozi wake kujiunga na Chadema na siyo CCJ nzima. Kuna sababu.
Wapo wanaosema kwa vile hawa ndugu zetu wameingia Chadema basi CCJ na wazo la CCJ nalo limekufa kwa hiyo sote tuliounga mkono CCJ tuinamishe vichwa vyetu kwa kushindwa na kujiunga na Chadema. Hizi ni fikra potofu. Ni potofu kwa sababu zinafikiria Chama kikifa au kikishindwa ina maana mawazo yake nayo yameshindwa. Yanafikiria kuwa kama watu wakitoka kujiunga na chama kingine au kutoka katika siasa maana yake siasa za chama hicho nazo zimeshindwa.
Ukweli unabakia kuwa ukweli kwamba siasa za kutaka ushirikiano wenye lengo la kuitoa tu CCM madarakani halafu ndiyo tujue tunataka kufanya nini ni siasa ambazo katika dhamira yangu siwezi kuziunga mkono. Siasa za kutosema nini unataka kufanya, kwa vipi na kwa muda gani ukionesha ukali kuhusu ufisadi miye siziwezi kwa sababu niaamini tatizo la Tanzania ni ufisadi kuliko kitu kingine chochote kile.
Kutuambia kuwa "panya hawakamatani" lakini hutuambii wewe utawakamata vipi na kwa namna gani, haitoshi vile vile.
Chadema ni tumaini kubwa sana kwa wengi wetu na kwa muda mrefu limekuwa kwangu ni tumaini vile vile. Lakini bado haijataka kuvuta mstari ule wa kiungozi kwa miaka kadhaa sasa. Siamini kama ndani ya siku chache zilizobakia wataweza kuvuka mstari huo. Na watakapogundua kuwa walipaswa kuuvuka watajikuta wanagalagazwa kwenye uchaguzi mkuu huku wakilalamika "CCM", "Tume ya uchaguzi", "Wizi wa kura", "Vyombo vya dola".
Ninawatakia kila la kheri wale wanaojiunga na Chadema wakiamini kitabeba matarajio yao. Hiyo ni demokrasia na kwa hakika kabisa nawatakia mafanikio.
Kwangu mimini bora nirudi na kutokuwa na chama nikiendelea kusimamia fikra na itikadi na mambo ninayoyaamini kuliko kupanda treni ambalo siju linakwenda wapi na kwa nini ati kwa sababu wengine wamepanda na wanashangilia!
Kundi zima la wabunge wa CCM wanaweza kutoka baada ya bunge kuvunjwa na kujiunga na Chadema na kutoka hao akapatikana mgombea wa Urais wa Chadema kama inavyotarajiwa. Hii inaweza kuwa habari kubwa sana na mtikisiko kwa jukwaa la siasa. Kwa wengine hilo laweza kutosha kabisa kufanya waamini kuwa saa ya mabadiliko imefika. Kwangu mimi bado nitaangalia kwa macho ya shuku hadi nijue wanataka kufanya nini. Wakisema wanataka tu KUINDOA CCM MADARAKANI au KUONGEZA IDADI WA WABUNGE, nitawaangalia halafu nitacheeeeeeeka!
Chadema kinaweza kabisa kuwa chama ambacho kitachukua uongozi wa nchi mwaka huu, endapo tu KITATAKA.
MM
Wapo wanaosema kwa vile hawa ndugu zetu wameingia Chadema basi CCJ na wazo la CCJ nalo limekufa kwa hiyo sote tuliounga mkono CCJ tuinamishe vichwa vyetu kwa kushindwa na kujiunga na Chadema. Hizi ni fikra potofu. Ni potofu kwa sababu zinafikiria Chama kikifa au kikishindwa ina maana mawazo yake nayo yameshindwa. Yanafikiria kuwa kama watu wakitoka kujiunga na chama kingine au kutoka katika siasa maana yake siasa za chama hicho nazo zimeshindwa.
Ukweli unabakia kuwa ukweli kwamba siasa za kutaka ushirikiano wenye lengo la kuitoa tu CCM madarakani halafu ndiyo tujue tunataka kufanya nini ni siasa ambazo katika dhamira yangu siwezi kuziunga mkono. Siasa za kutosema nini unataka kufanya, kwa vipi na kwa muda gani ukionesha ukali kuhusu ufisadi miye siziwezi kwa sababu niaamini tatizo la Tanzania ni ufisadi kuliko kitu kingine chochote kile.
Kutuambia kuwa "panya hawakamatani" lakini hutuambii wewe utawakamata vipi na kwa namna gani, haitoshi vile vile.
Chadema ni tumaini kubwa sana kwa wengi wetu na kwa muda mrefu limekuwa kwangu ni tumaini vile vile. Lakini bado haijataka kuvuta mstari ule wa kiungozi kwa miaka kadhaa sasa. Siamini kama ndani ya siku chache zilizobakia wataweza kuvuka mstari huo. Na watakapogundua kuwa walipaswa kuuvuka watajikuta wanagalagazwa kwenye uchaguzi mkuu huku wakilalamika "CCM", "Tume ya uchaguzi", "Wizi wa kura", "Vyombo vya dola".
Ninawatakia kila la kheri wale wanaojiunga na Chadema wakiamini kitabeba matarajio yao. Hiyo ni demokrasia na kwa hakika kabisa nawatakia mafanikio.
Kwangu mimini bora nirudi na kutokuwa na chama nikiendelea kusimamia fikra na itikadi na mambo ninayoyaamini kuliko kupanda treni ambalo siju linakwenda wapi na kwa nini ati kwa sababu wengine wamepanda na wanashangilia!
Kundi zima la wabunge wa CCM wanaweza kutoka baada ya bunge kuvunjwa na kujiunga na Chadema na kutoka hao akapatikana mgombea wa Urais wa Chadema kama inavyotarajiwa. Hii inaweza kuwa habari kubwa sana na mtikisiko kwa jukwaa la siasa. Kwa wengine hilo laweza kutosha kabisa kufanya waamini kuwa saa ya mabadiliko imefika. Kwangu mimi bado nitaangalia kwa macho ya shuku hadi nijue wanataka kufanya nini. Wakisema wanataka tu KUINDOA CCM MADARAKANI au KUONGEZA IDADI WA WABUNGE, nitawaangalia halafu nitacheeeeeeeka!
Chadema kinaweza kabisa kuwa chama ambacho kitachukua uongozi wa nchi mwaka huu, endapo tu KITATAKA.
MM