Wizara ya Ujenzi. Hivi ndo barabara zinavyojengwa kwenye miji mikubwa ya Biashara

Kwamba Angola ina rasilimali kuliko Tanzania?
Angola wana mafuta. Sisi tunategemea tozo tu. Mkono mtupu haulambwi au unataka tuongeze tozo na kodi ili tuweze kujenga barabara za aina hizo unazotamani? Serikali ikiongeza tozo kidogo tu nyie ndoo wa kwanza kupiga kelele sana na kuitukana serikali.
 
JPM alikuwa ni genius sana, yule mzee nilimkubali sana.
JPM alijaribu kujenga kuanzia Kimara Mwisho hadi Kibaha.

Kila nikiwa natumia zile barabara hua naendelea kumkumbuka legendary

Yaani huwa napepea na speed 120 hadi 160km/hr.

Let the Man rest in peace, despite his bad side lakini kwenye hili the Oldman was good at
 
Serikali iliyofeli kila haiwezi kujenga barabara za kiwango hicho.
 
Ni kweli mkuu na tulikuwa na mipango ya Tanzania kuwa a donor country kwa uwingi wa rasilimali tulizonazo. Tukatunga na hiyo sheria ya Natural Wealth ambayo cdm waliipinga sana lakini tukatumia nguvu ya wengi wape huko bungeni.

Bahati mbaya yakatokea yaliyotokea. Hizo rasilimali zetu siyo za kwetu tena. Umesikia hata hiyo SGR, bwawa la Nyerere, bandari nk tunatarajia kuwapa watu au kampuni binafsi tunaowaita wawekezaji. Hiyo gesi tayari tuliwapa wawekezaji kipindi cha awamu ya nne, siyo ya kwetu tena na hutubidi ili kuitumia tuinunue kwa bei mbaya kutoka kwa hao wawekezaji. Madini tulishawapa wawekezaji kipindi cha awamu ya tatu. Wakina Kitila Mkumbo hawana cha kufanya isipokuwa kutegemea tu tozo.
Imekuwaje tena ccm wasitetee hizo rasmlimali zenu, wakati dhalimu alipora uchaguzi na kujaza wanaccm kote kwakuwa ni wazalendo? Au walikuwa ni wazalendo wa mdomoni?
 
Angola wana mafuta. Sisi tunategemea tozo tu. Mkono mtupu haulambwi au unataka tuongeze tozo na kodi ili tuweze kujenga barabara za aina hizo unazotamani? Serikali ikiongeza tozo kidogo tu nyie ndoo wa kwanza kupiga kelele sana na kuitukana serikali.
acha unafiki jombaa.
 
Angola wana mafuta. Sisi tunategemea tozo tu. Mkono mtupu haulambwi au unataka tuongeze tozo na kodi ili tuweze kujenga barabara za aina hizo unazotamani? Serikali ikiongeza tozo kidogo tu nyie ndoo wa kwanza kupiga kelele sana na kuitukana serikali.
Mkuu, utalii, madini, na kilimo vinatosha kabisa kutuingizia pato la kutuwezesha kufanya mambo makubwa kuliko hata wenye mafuta. Ujinga na ubabaishaji ndivyo vizuizi vyetu vikuu, siyo kukosa raslimali!
 
Angola wana mafuta. Sisi tunategemea tozo tu. Mkono mtupu haulambwi au unataka tuongeze tozo na kodi ili tuweze kujenga barabara za aina hizo unazotamani? Serikali ikiongeza tozo kidogo tu nyie ndoo wa kwanza kupiga kelele sana na kuitukana serikali.
Mawazo yako ni mfu, Nairobi wametuzidi miundombinu compared to Dsm nako wana mafuta, namibia Botswana kote wametuzidi miundombinu nako kuna mafuta? Mafuta sio kigezo cha mtu kukuzidi maendeleo angalia mataifa kama Luxembourg ina nini? Then angalia maendeleo yake na huko Kuwait kwenye mamilion ya cubic meters za mafuta. Maendeleo ni mipango ya ulichonahco naweza kulipwa laki na nikajenga na ukalipwa one million na ushindwe kuwa na nyumba. Its not about resource its about resource management and utilization
 
Mkuu, utalii, madini, na kilimo vinatosha kabisa kutuingizia pato la kutuwezesha kufanya mambo makubwa kuliko hata wenye mafuta. Ujinga na ubabaishaji ndivyo vizuizi vyetu vikuu, siyo kukosa raslimali!
Unadhani hajui? Usikute ni mtumishi wa Wizara ya Ujenzi au Tanroads anatetea ujinga wao humu

Ni akili zao fupi tu. We fikiria tu kwa akili ya kawaida tu, katika karne hii ya 21 unawezaje kujenga upya barabara ya Posta hadi Uwanja wa ndege alafu unaiwekea njia mbili kila upande? Kwenye jiji lenye watu Mil sita kasoro??
Hizi ni akili au matope?

Kesho wazungu wakituita manyani tunakasirika?
 
Angola wana mafuta. Sisi tunategemea tozo tu. Mkono mtupu haulambwi au unataka tuongeze tozo na kodi ili tuweze kujenga barabara za aina hizo unazotamani? Serikali ikiongeza tozo kidogo tu nyie ndoo wa kwanza kupiga kelele sana na kuitukana serikali.

Tanzanite, almasi na dhahabu yote uliyonayo huoni aibu kusema unategemea tozo?

Hapo bado hujagusa utalii, halafu nankilimo ambacho mazao ya biashara kama korosho, katani, pamba na kahawa tumeua kabisa uzalishaji wake uliokuwa ni mkubwa Afrika...
 
Kwenu Wizara ya Ujenzi

Hizi ni barabara za Jiji la Biashara Luanda. Mji Mkuu wa Angola

Jifunzeni kuwa kwenye miji mikubwa ya biashara wenzenu wanajenga barabara njia 3 hadi 4 kila upande sio vituko vyenu vya njia 2 kila upande mnavyotujengea barabara za mbagala na Gongo la Mboto hapo Dar kama tupo karne ya 19 huko

Najua kwa somo hili hamtajenga hivyo vituko Mwenge- Kurasini na Bunju hadi PostaView attachment 2847820
Naunga mkono hoja
P
 
Kwenu Wizara ya Ujenzi

Hizi ni barabara za Jiji la Biashara Luanda. Mji Mkuu wa Angola

Jifunzeni kuwa kwenye miji mikubwa ya biashara wenzenu wanajenga barabara njia 3 hadi 4 kila upande sio vituko vyenu vya njia 2 kila upande mnavyotujengea barabara za mbagala na Gongo la Mboto hapo Dar kama tupo karne ya 19 huko

Najua kwa somo hili hamtajenga hivyo vituko Mwenge- Kurasini na Bunju hadi PostaView attachment 2847820
Sawa kabisa!
 
Angola wana mafuta. Sisi tunategemea tozo tu. Mkono mtupu haulambwi au unataka tuongeze tozo na kodi ili tuweze kujenga barabara za aina hizo unazotamani? Serikali ikiongeza tozo kidogo tu nyie ndoo wa kwanza kupiga kelele sana na kuitukana serikali.
hata mngekuwa na mafuta yasingesaidia....gesi imewasaidia?
 
Serikali iliyofeli kila haiwezi kujenga barabara za kiwango hicho.
Tuna watu wa hovyo sana katika haya maofisi ya Serikali. Wanafanya watu wote kuonekana wajinga tusio na akili na exposure
 
Unadhani hajui? Usikute ni mtumishi wa Wizara ya Ujenzi au Tanroads anatetea ujinga wao humu

Ni akili zao fupi tu. We fikiria tu kwa akili ya kawaida tu, katika karne hii ya 21 unawezaje kujenga upya barabara ya Posta hadi Uwanja wa ndege alafu unaiwekea njia mbili kila upande? Kwenye jiji lenye watu Mil sita kasoro??
Hizi ni akili au matope?

Kesho wazungu wakituita manyani tunakasirika?
Nimeshangaa sana jana kupita hiyo barabara kutoka gongo la mboto mpaka posta,

Sikuamini kama hii nchi yetu tuna viongozi au hata sielwei nini hasa,
Labda ushamba sugu fulani,
Maana unashindwa hata kuelewa , hivi kweli hiyo barabara imejengwa miaka zaidi yarobaini, ndio miaka 40, Airport to city centre, ikiwa hivyo hivyo njia mbil, halafu leo baada ya miaka yote hiyo tena kipindi ambacho magari waliokuwa wsnamiliki ni wahindi na wstu binafsi wachache tu( Madocta na maafisa wa jeshi na pick up zao) halafu leo miaka 40 unafumua barabara nzima kwa ajili ya kuweka barabara ya mwendokasi tu?, hii ni akili au matope.
 
Back
Top Bottom