Wizara ya Elimu ya Juu irudishwe!

Masaki

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
3,463
753
Kwa kipindi kirefu sasa tumekuwa tukisoma kwenye vyombo vya habari juu ya migomo na maandamano ya wanafunzi na walimu kuanzia ngazi ya shule za msingi hadi vyuo vikuu. Wanafunzi wana matatizo makubwa kuanzia ukosefu wa vyoo, madawati, chakula, maabara, malazi na huduma nyingine muhimu. Walimu nao hawajalipwa mafao yao na mishahara yao kwa kipindi kirefu kiasi cha kuonekana kwenye vyombo vya habari wakiwa wanalia machozi hadharani!

Wakati Rais anapangua Baraza lake la Mawaziri na kuunda jipya, watu wengi tulifurahia kwamba alipunguza ukubwa wa Baraza hilo. Lakini katika vitu vilivyonitia shaka sana ni kitendo cha kuunganisha Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na ile ya Elimu ya Juu.

Ifahamike kwamba, moja kati ya sekta zenye matatizo mengi sana katika nchi yetu ni Elimu. Wakati Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ikiwa peke yake na ile ya Elimu ya Juu pia ikiwa peke yake, bado kulikuwa na matatizo lukuki ya kutatua.

Leo hii mzigo wote umerundikwa kwenye mabega ya Waziri mmoja ambaye sasa ni dhahiri kabisa kwamba ameelemewa!

Napendekeza Wizara hizi mbili zirudishwe kama ilivyokuwa mwanzo ili kuongeza ufanisi na tija katika utendaji. Elimu ndio mhimili wa maendeleo ya taifa hili na sio kitu cha kufanyia mzaha mzaha tu!!!

Naomba kuwakilisha!!!
 
Hakuna haja ya kuirudisha ni kuongeza mzigo tu kwa serikali wizara moja inatosha kabisa
 
Kwa kipindi kirefu sasa tumekuwa tukisoma kwenye vyombo vya habari juu ya migomo na maandamano ya wanafunzi na walimu kuanzia ngazi ya shule za msingi hadi vyuo vikuu. Wanafunzi wana matatizo makubwa kuanzia ukosefu wa vyoo, madawati, chakula, maabara, malazi na huduma nyingine muhimu. Walimu nao hawajalipwa mafao yao na mishahara yao kwa kipindi kirefu kiasi cha kuonekana kwenye vyombo vya habari wakiwa wanalia machozi hadharani!

Wakati Rais anapangua Baraza lake la Mawaziri na kuunda jipya, watu wengi tulifurahia kwamba alipunguza ukubwa wa Baraza hilo. Lakini katika vitu vilivyonitia shaka sana ni kitendo cha kuunganisha Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na ile ya Elimu ya Juu.

Ifahamike kwamba, moja kati ya sekta zenye matatizo mengi sana katika nchi yetu ni Elimu. Wakati Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ikiwa peke yake na ile ya Elimu ya Juu pia ikiwa peke yake, bado kulikuwa na matatizo lukuki ya kutatua.

Leo hii mzigo wote umerundikwa kwenye mabega ya Waziri mmoja ambaye sasa ni dhahiri kabisa kwamba ameelemewa!

Napendekeza Wizara hizi mbili zirudishwe kama ilivyokuwa mwanzo ili kuongeza ufanisi na tija katika utendaji. Elimu ndio mhimili wa maendeleo ya taifa hili na sio kitu cha kufanyia mzaha mzaha tu!!!

Naomba kuwakilisha!!!

Kwani waziri ndo mtendaji? ninachofahamu mimi hakuna watendaji waliopunguzwa baada ya kuunganisha wizara hizo. endapo itadhihirika kuwa utendaji wa wizara unashuka kwa sababu waziri anamajukumu makubwa basi tumekwisha.

Wizara ya elimu kuna Katibu Mkuu, naibu katibu Mkuu, wakurugenzi (elimu ya Msingi, Sekondari, elimu ya watu wazima,elimu ya juu) pia kuna idara ...

Mtazamo wangu ni kuzidi kupunguza Wizara ili wanasiasa wawe wachache katika ngazi za utendaji. Wanasiasa ndiyo wanaosababisha matatizo ya ovyo kama Richmond, IPTL etc. watendaji wasipoingiliwa wanaweza kufanya kazi nzuri sana.

Hivyo Mkuu, ninapingana na wewe kabisa kimsimamo. Ningefurahi endapo tungekuwa na mawaziri 10 - 15 tu.
 
There is no need for that, waziri hawezi kuzuia matatizo yaliyopo unless serikali itoe resources zaidi na watu wapewe haki zao kama zinavyotakiwa.
 
Kwa kipindi kirefu sasa tumekuwa tukisoma kwenye vyombo vya habari juu ya migomo na maandamano ya wanafunzi na walimu kuanzia ngazi ya shule za msingi hadi vyuo vikuu. Wanafunzi wana matatizo makubwa kuanzia ukosefu wa vyoo, madawati, chakula, maabara, malazi na huduma nyingine muhimu. Walimu nao hawajalipwa mafao yao na mishahara yao kwa kipindi kirefu kiasi cha kuonekana kwenye vyombo vya habari wakiwa wanalia machozi hadharani!

Wakati Rais anapangua Baraza lake la Mawaziri na kuunda jipya, watu wengi tulifurahia kwamba alipunguza ukubwa wa Baraza hilo. Lakini katika vitu vilivyonitia shaka sana ni kitendo cha kuunganisha Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na ile ya Elimu ya Juu.

Ifahamike kwamba, moja kati ya sekta zenye matatizo mengi sana katika nchi yetu ni Elimu. Wakati Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ikiwa peke yake na ile ya Elimu ya Juu pia ikiwa peke yake, bado kulikuwa na matatizo lukuki ya kutatua.

Leo hii mzigo wote umerundikwa kwenye mabega ya Waziri mmoja ambaye sasa ni dhahiri kabisa kwamba ameelemewa!

Napendekeza Wizara hizi mbili zirudishwe kama ilivyokuwa mwanzo ili kuongeza ufanisi na tija katika utendaji. Elimu ndio mhimili wa maendeleo ya taifa hili na sio kitu cha kufanyia mzaha mzaha tu!!!

Naomba kuwakilisha!!!

Pole sana ndugu yangu Masaki!!!

Tatizo kwani ni wizara?? Kama ungejua historia ya wizara hiyo Tangu iko chini akina Ben Mkapa na Bilal basi hungepoteza muda wako kuililia.

Hapa tatizo si wizara bali ni kushindwa kwa mfumo mzima wa utawala (governing system). Sidhani kama unaweza kunipa mfano wa wizara yoyote katika nchi hii imbayo imeweza kutekeleza majukumu yake angalau kwa 50%! Ukipata mfano huo basi ulete hapa tuanze mjadala upya.

Kwa hiyo kazi tuliyonayo ni moja tu. Kufumua mfumo mzima wa kiuongozi na utawala wa nchi hii (total revamption) ili tuanze moja; kwa kuweka vipau mbele upya (setting priorities) na mikakati mipya (road map) ambayo imekubalika na wadau wote. Hapa hakuna chama wala mtu wa kushika hatamu, it's National concensus. Baada ya hapo tuanze kwenda mbele. Kwa hiyo jukumu langu na lako ni kufanya ukombozi mpya wa taifa letu kwa kuondoa watawala hawa wasio na malengo yoyote ya maana kwetu (mission and vision) badala yake wanafanya usanii na maisha yetu!
 
Kwa kipindi kirefu sasa tumekuwa tukisoma kwenye vyombo vya habari juu ya migomo na maandamano ya wanafunzi na walimu kuanzia ngazi ya shule za msingi hadi vyuo vikuu. Wanafunzi wana matatizo makubwa kuanzia ukosefu wa vyoo, madawati, chakula, maabara, malazi na huduma nyingine muhimu. Walimu nao hawajalipwa mafao yao na mishahara yao kwa kipindi kirefu kiasi cha kuonekana kwenye vyombo vya habari wakiwa wanalia machozi hadharani!

Wakati Rais anapangua Baraza lake la Mawaziri na kuunda jipya, watu wengi tulifurahia kwamba alipunguza ukubwa wa Baraza hilo. Lakini katika vitu vilivyonitia shaka sana ni kitendo cha kuunganisha Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na ile ya Elimu ya Juu.

Ifahamike kwamba, moja kati ya sekta zenye matatizo mengi sana katika nchi yetu ni Elimu. Wakati Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ikiwa peke yake na ile ya Elimu ya Juu pia ikiwa peke yake, bado kulikuwa na matatizo lukuki ya kutatua.

Leo hii mzigo wote umerundikwa kwenye mabega ya Waziri mmoja ambaye sasa ni dhahiri kabisa kwamba ameelemewa!

Napendekeza Wizara hizi mbili zirudishwe kama ilivyokuwa mwanzo ili kuongeza ufanisi na tija katika utendaji. Elimu ndio mhimili wa maendeleo ya taifa hili na sio kitu cha kufanyia mzaha mzaha tu!!!

Naomba kuwakilisha!!!

Bwana Masaki,
Mimi nadhani tatizo sio idadi ya wizara kuwa chache, ila ni wizara kuwa nyingi, matokeo yake maamuzi ya wanasiasa yanaingilia zaidi utendaji wa kitaalamu katika sector nyingi.

Ukibahatika kuzungumza na watendaji wa wizara mbali mbali, watakuwambia hawajui nini ni kazi za mawaziri na manaibu waziri kiasi cha wizara nyingine kuwa na hawa watu 3 (waziri 1?manaibu 2). Mimi nadhani tatizo ni mfumo wa utawala, na ndio sababu sehemu nyingi zimekwama.

Si ndio sababu unaona kila kitu anasubiriwa rais atoe kauli! wewe huoni hii shida? Isingekuwa hivyo sakata nyingi nchini zimekuwa zimekwisha kwani richmond, epa, meremeta, ubinafsishaji usiozingatia sheria n.k yangekuwa tayari yalishaisha, lakini tatizo ni uchache wa wizara au mfumo?
 
Back
Top Bottom