Masaki
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 3,463
- 753
Kwa kipindi kirefu sasa tumekuwa tukisoma kwenye vyombo vya habari juu ya migomo na maandamano ya wanafunzi na walimu kuanzia ngazi ya shule za msingi hadi vyuo vikuu. Wanafunzi wana matatizo makubwa kuanzia ukosefu wa vyoo, madawati, chakula, maabara, malazi na huduma nyingine muhimu. Walimu nao hawajalipwa mafao yao na mishahara yao kwa kipindi kirefu kiasi cha kuonekana kwenye vyombo vya habari wakiwa wanalia machozi hadharani!
Wakati Rais anapangua Baraza lake la Mawaziri na kuunda jipya, watu wengi tulifurahia kwamba alipunguza ukubwa wa Baraza hilo. Lakini katika vitu vilivyonitia shaka sana ni kitendo cha kuunganisha Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na ile ya Elimu ya Juu.
Ifahamike kwamba, moja kati ya sekta zenye matatizo mengi sana katika nchi yetu ni Elimu. Wakati Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ikiwa peke yake na ile ya Elimu ya Juu pia ikiwa peke yake, bado kulikuwa na matatizo lukuki ya kutatua.
Leo hii mzigo wote umerundikwa kwenye mabega ya Waziri mmoja ambaye sasa ni dhahiri kabisa kwamba ameelemewa!
Napendekeza Wizara hizi mbili zirudishwe kama ilivyokuwa mwanzo ili kuongeza ufanisi na tija katika utendaji. Elimu ndio mhimili wa maendeleo ya taifa hili na sio kitu cha kufanyia mzaha mzaha tu!!!
Naomba kuwakilisha!!!
Wakati Rais anapangua Baraza lake la Mawaziri na kuunda jipya, watu wengi tulifurahia kwamba alipunguza ukubwa wa Baraza hilo. Lakini katika vitu vilivyonitia shaka sana ni kitendo cha kuunganisha Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na ile ya Elimu ya Juu.
Ifahamike kwamba, moja kati ya sekta zenye matatizo mengi sana katika nchi yetu ni Elimu. Wakati Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ikiwa peke yake na ile ya Elimu ya Juu pia ikiwa peke yake, bado kulikuwa na matatizo lukuki ya kutatua.
Leo hii mzigo wote umerundikwa kwenye mabega ya Waziri mmoja ambaye sasa ni dhahiri kabisa kwamba ameelemewa!
Napendekeza Wizara hizi mbili zirudishwe kama ilivyokuwa mwanzo ili kuongeza ufanisi na tija katika utendaji. Elimu ndio mhimili wa maendeleo ya taifa hili na sio kitu cha kufanyia mzaha mzaha tu!!!
Naomba kuwakilisha!!!