Wivu na chuki ya maendeleo mbaya sana: Waigbo wa Nigeria ndio kabila lenye akili na uwezo mkubwa kibiashara, wanakomolewa ila bado wanadunda

Uncle bright

JF-Expert Member
Feb 9, 2023
1,040
4,080
1706185080651.png

Nigeria kuna makabila 371 ila kuna makabila matatu maarufu

1. Hausa = Hili ndio kabila lenye watu wengi zaidi Nigeria na Afrika, Hawa wapo nyuma sana mambo ya elimu na hata huko kwao hakuna sana maendeleo miji imejaa omba omba lakini ndio walioshikilia power ya nchi kwenye siasa, Jeshini wamejazana wao na kazi za serikali nyingi wamejaa wao. Tatizo la hili kabila ni ubinafsi mtu akipata ni yeye na ukoo wake. Wengi ni wasilamu na maeneo yao mengi huongozwa kwa mifumo ya kiarabu, machifu wa mikoa yao hujulikana kama Emir. picha ya mfano ipo chini

1706185365900.png

Nigeria imewahi kufanyiwa mapinduzi mara kadhaa, mara nyingi wahusika wakiwa kabila hili ikitokea hawajampenda rais hasa asipotokea kwao japo mara ya mwisho kufanyika mapinduzi ni miaka ya 90s.

Wananufaika sana kushika power ya nchi sababu hata kama hawana elimu hizi tenda nono huwa wanapeana wao, vyeo vinono wanapeana wao, visima vingi vya mafuta ambavyo mikoa ya mbali isio yao wanamiliki wao, Ndiko anakotokea Tajiri Aliko Dangote.

Haya ni majibu ya chat-gpt kwa swali nililoiuliza "sehemu inayoongoza umaskini Nigeria"

Kaskazini Magharibi na kaskazini mashariki zimejaa wahausa

1706192591234.png


2. Yoruba - Hawa wapo Kusini Magharibi, ndio wasomi zaidi kwenye taifa hilo, na kwa sasa hata raisi anatokea huko, wengi wanategemea ajira kuendesha maisha yao, elimu kwao ndio kipaumbele japo kuna tatizo kubwa sana la ajira huko Nigeria, Pia wasanii wengi kama kina Davido na wanamichezo wengi hutokea huko. ila udhaifu wao nao hawana umoja sana.

3. Igbo - Hawa licha ya kwamba kwao ni Nigeria ya Mashariki kusini, wametapakaa sehemu nyingi Nigeria hasa kwenye majiji yenye fursa za biashara kama Lagos na Abuja, Hawa ndio wengi tunawaona kwenye muvi, maisha yale ya muvi za kinaijeria yanaonyesga zaidi maisha na tamaduni za waigbo sio wanaijeria wote, muvi hizi zilifanya hata wengi kuamini Nigeria imejaa wakristo ilhali Nigeria ni nchi iliyojaa waislam. Nadhani hata kwenye uandishi wamo, kwa wale tulioweza kusoma mpaka sekondari nadhani mnakijua kitabu cha Things fall apart, muandishi Chinua Achebe ni wa huko na aligusia zaidi maisha ya waigbo kabla na baada ya ukoloni.

1706186342017.png

Walitaka wawe na nchi yao wenyewe na kukawa na vita ya jeshi la Nigeria dhidi yao mwaka 1970, Jeshi la Nigeria lilikuwa kubwa sana na lenye nguvu likawachapa, kuanzia hapo Serikali ya Nigeria ilihakikisha hawa watu hawaji kuinuka tena, hakuna maendeleo yanapelekwa huko kwao hata barabara ni changamoto, wana akili za darasani lakini hata wasome vipi suala la ajira wanatengwa sana, kwenye mambo ya siasa nako wanatengwa sana hawapewi vyeo vikubwa, jeshini nako wanachujwa sana.

1706186436170.png

Vita vilipoisha akaunti zote za wa igbo zilifungwa na kutaifishwa, kabla ya vita waigbo ndio walikuwa wanashikilia uchumi wa Nigeria na wafanyabiashara wengi walikuwa waigbo, vita ilipoanza wafanyabiashara wengi waliuawa na mali zao ziliporwa, akaunti zilifungwa, baada ya vita familia nyingi walipewa noti ya pauni 20 tu na ilibidi wasafiri umbali mrefu kuzibadili ziwe pesa za Nigeria na huko bado walipata usumbufu, hii ilikuwa ni kuwakomoa.

1706186483155.png

Lakini amini usiamini hata ushindane na samaki kuogelea kwa kumuweka kilomira nyuma bado atakupita tu, wa igbo kufikia mwaka 1990 tayari walikuwa wameshaanza kutengeneza mabilionea, hadi kufikia sasa Nigeria watu wenye pesa nyingi zaidi ni waigbo, wengi ni wamiliki wa viwanda, miji mikubwa imegeuzwa kuwa maeneo ya maduka, n.k. ni kawaida sana kukuta kijana wa Igbo mwenye miaka 35 ana utajiri wa kutisha (Ni kweli wapo wanaofanya biashara haramu lakini ni aslimia ndogo sana ya waigbo wanaofanya biashara kihalali )

1706186647933.png

Lakini kumbuka kwamba nserikali ilikuwa na lengo la kuwamaliza kabisa wasije kuinuka tena, mafanikio yao yamekuwa ni mwiba na tofauti na ilivyotegemewa, Serikali inayoongozwa na wahausa na wayoruba kwa kiasi flani inaendeleza itikadi za kuwadidimiza, wanabomoa nyumba zao kwa notisi za siku 2 kwa visingizio vya ajabu, wanachoma masoko yao, wanabomoa maduka yao, n.k. lakini hawa jamaa bado wanadunda tu, siri yao ni ushirikianao, umoja na mshikamano.

1706186959589.png

Wana akili za shuleni lakini wanakosa motisha ya kusoma sana kwasababu wanabaguliwa kwenye system, wengi husoma ili kumalizana tu na mambo ya shule waanza kujitafuta kivyao ama waongeze nguvu biashara za family. Ni tofauti kwa upande wa wayoruba wanapata motisha zaidi ya kusoma sababu wao angalau wanaweza kupata ajira kwenye system japo Nigeria ni nchi yenye tatizo kubwa sana la ajira na bado kuna wale wahausa wanapeana sana ajira za kiukoo bila kuwekea uzito elimu,

Kwa Hali hii kuna system ilianzishwa inaitwa Quota Sytem, Mitihani ya sekondari kwenda vyuoni huwa ina maksi 400 kwa ujumla, Marks za kuingia vyuoni ni tofauti kulingana na ukanda na jamii za wanaiheria, Muhausa akipata marks 150 anaingia chuo, Myoruba inabidi apate 200, kwa waigbo kamba imekazwa sana inabidi wapate kuanzia 250.

Haya ni matokeo ya mtihani wa taifa wa sekondari 2023, hao wote wanne wanoongoza ni waigbo

1706189305856.png

Mtu maarufu msomi kutoka Afrika kwenye uwanja wa computer ni Philip Emeagwali, Akiwa na miaka 13 aliwahi kusitisha masomo yake huko kijijini kwao ili aende kupigana vita iliyokuwa ikiendelea, Uwezo wale mkubwa wa hesabu ulimvusha mpaka Marekani kwenda kusomea sayansi ya computer na kuweza kubuni teknolojia inayaotwa parallel Processing, kuwezesha computer kutekeleza shughuli nyingi kwa wakati mmoja badala ya kufanya kazi moja baada ya nyingine, hata hio somu ama laptop unayotumia inatumia teknolojia aliyoigundua, Mwaka 1989 alitengeneza computer yenye spidi kubwa mno kuziunganisha processor elf 65 zilizoweza kupiga hesabu bilioni 3.1 kwa sekunde, Ni jambo lililoushangaza ulimwengu wa teknolojia na mchango wake ulitambulika kwa kupewa tuzo ya Gordon Bell ambayo ni kama Noble Prize kwenye mambo ya teknolojia, Wengine pia wanamuita ni "Father of omternet" yaani baba wa internet kwa mchango wake mkubwa kwenye mifumo ya networking.

1706207187920.png

1706208530915.png


Siri yao kubwa zaidi tofauti na wenzao ni kwamba wana umoja, wanabebana wakijua muda wowote tatizo likimtokea flani basi kesho linaweza kumkukuta mwengine na pia hawajasahau walikotoka (kila christmas wana utaratibu wa kurudi vijijini kwao), wanajua wanabaguliwa na kufanyiwa figisu hivyo inabidi waaminiane na wasaidiane sana, wana system yao imejizolea umaarudu inaitwa Igbo apprenticeship system, ni kwamba wafanyabiashara wote wa igbo wamejiwekea utaratibu wa kuchukua ndugu zao vijijini kuwaleta mjini wawafundishw biashara kisha baada ya miaka mitano hadi 10 nao wanawapa mitaji kuanzisha biashara zao, hivyo hata moja akifanyiwa figisu kuna wengine zaidi wanaendeleza mapambano na kuboresha mbinu za kibiashara.

picha hii inaonyesha mfano wa hio system, hata iwe biashara ndogo watafundishana na kushirikiana kuikuza, mtu hadi awe na kiwanda unaweza kuta alianza kutengeneza viatu kwa mikono mwenyewe ila alipoleta wenzake wa ziada ndio uzalishaji ukaongezeka, Biasahra inaendelezwa hadi kuanza kuuza viatu nje ya nchi. (Umoja ni nguvu kubwa sana)

1706187270027.png

Lagos ndio jiji kubwa zaidi Nigeria na Africa
1706196225659.png

1706196265052.png


Jiji hili kwa asili lipo Nigeria ya Kusini Magharibi walipo Wayoruba lakini ndio kimbilio la waigbo wengi kwenda kytajirikia kwa kutumia uwezo wao mkubwa waliojaliwa kibiashara, Karibu asilimia 60 za biashara katika jiji hili ni waigbo na wanaendeleza ile system yao ya apprenticeship wanazidi kukua, WANACHAPISHA PESA THEY MAKE IT RAIN!!

1706196992886.png


Sasa ubaya ni kwamba wanachapisha pesa kwenye sehemu ambayo kwa asili ni ya wayoruba ina ndio hapo sasa inachangia wachukiwe kwa kufanyiwa figisu za kubomolewa makazi, kuchomewa maduka, n.k. na hata sasa ukiingia twitter ukisechi semolition igbo unakutana na post kibaoo tu maduka yanavunjwa.

Real Estate biashara za Kujenga na kukodisha Nyumba, Hotels, n.k. jamaa wamewekeza vilivyo - Hapa sasa hata Wayoruba wanajikuta kwenye mji wao wanalipa kodi kwa wageni ili wapate pa kulala,

1706198602467.png


Viwanda vingi sanaaaa, vingi mno vinamilikiwa na hawa waigbo hapo Lagos,

1706198570846.png


Masoko makubwa ya Lagos yamejaza wa igbo kama

Baligun Market - Ni kariakoo ya Lagos ila ni kubwa sana kuzidi Kariakoo na ina msongamano sana

1706197636866.png


Idumota - Ni kariakoo nyingine ya Lagos ila bado ni kubwa kuzidi hii ya Tz
1706198070394.png


Computer Village - Hii ni kama kariakoo nzima iwe imejaza masoko maalum ya mambo ya electronics kama simu, laptops, speaker, tv, n.k.

1706197215331.png


Ladipo Market - Hii ni kama kariakoo nzima ijae maduka ya spea za magari

1706197391520.png
 
Mkuu mimi nilidhani wa Yoruba ndo wenye akili na wasomi sana Nigeria? Igbo wako vizuri kwa biashara na utapeli utapeli.

Yoruba wenyeji halisi wa legos ndio wasomi sana na walihamia wengi uingereza ndo yakina saka arsenal, ndo kina john boyega star wars, ndo kina Antony joshua mama Yoruba baba Mzungu.
 
Mkuu mimi nilidhani wa Yoruba ndo wenye akili na wasomi sana Nigeria? Ignore wako vizuri kwa biashara na utapeli utapeli. Yoruba wenyeji halisi wa legos ndio wasomi sana na walihamia wengi uingereza ndo yakina saka arsenal, ndo kina john boyega star wars, ndo kina Antony joshua mama Yoruba baba Mzungu.
Wayoruba wana shule na vyuo kibao na wakisoma angalau wanapewa nafasi za kuajiriwa japo kuna tatizo kubwa sana la ajira na wale wahausa wanapeana sana ajira ilhali wana shule ndogo,

Waigbo wana akili sana darasani na hata ukicheki mitihani ya taifa wanaiita Jamb, wao ndio huwa wanakimbiza, Ishu ni kwamba wao hata wakisoma wanabaniwa sana ajira za serikali hata jeshini, wengi wanasoma ili wamalizane tu na elimu waingie kwenye biashara, mazingira yenyewe wanayosoma bado mabaya huwezi linganisha na wayoruba kwahio ni akili zao zinawabeba.


Haya ni matokeo ya mitihani ya Nigeria ya sekondari, hao wanne wa kwanza, waigbo

1706188465413.png


Ukija kwenye utapeli nako hao waigbo ni namba nyingine
 
Hao matapeli hawana mpya kuwa vinara sio sababu ,hao yahoo boys wamejazana..

Nijeria suala la ukabila ni hatari sana...Hata ulete facts hamna upande uliopo sahihi ...Igbo kawaida sana dili chafu zote wanapiga ,makatili hawana utu.
 
Mbona Hao Waigbo ni Wachagga kabisa
Hata wakikuyu wa Kenya hawanusi kwa waigbo

Ni kweli "kibongobongo" wachaga wapo vizuri ila bado kwa level za nchi nao wanakimbizwa na waarabu na wahindi, nadhani inabidi kwanza watz wa asili washike usukani ndio tuanze kupimana ubavu na kina Mwangi wa hapo Kenya.

Kumbuka 1970 Waigbo walifilisiwa wote baada ya vita familia zilipewa pauni 20 tu kwa kuwakomoa kabisa lakini baada ya miaka 20 tu wakanesa upya kwa speed ya ajabu na kushikilia biashara kibao.

Wana mahekalu kibao kama haya vijijini,

1706189710443.png
 
Mkuu mimi nilidhani wa Yoruba ndo wenye akili na wasomi sana Nigeria? Ignore wako vizuri kwa biashara na utapeli utapeli. Yoruba wenyeji halisi wa legos ndio wasomi sana na walihamia wengi uingereza ndo yakina saka arsenal, ndo kina john boyega star wars, ndo kina Antony joshua mama Yoruba baba Mzungu.
Hajui kitu igbo ni matapeli hao mpaka Nijeria ilipigwa ban nchi za nje ,hoa wanaiba mitihani wapo yahoo boys
.
Wanajali pesa kwa mbinu yeyote ile wanapata
 
Wewe utakua mkristo ngoja nisubiri na uchambuzi wa muislamu ili kubalance hii stori.
Mkuu labda kama unahisi nimesema Hausa huko kwao hakuna maendeleo ngoja nikuthibitishie.


Haya ni majibu ya chat-gpt kwa swali nililoiuliza "sehemu zinazoongoza umaskini Nigeria"

Kaskazini Magharibi na kaskazini mashariki zimejaa wahausa

1706192591234.png



Sehemu inayoongoza kwa omba omba wengi ni Nigeria ya Kaskazini Magahribi kwa wahausa
 
Back
Top Bottom