Akili za kibiashara kwa Watanzania ni za kutafuta, ndio sababu tuna Watanzania wachache matajiri

OLS

JF-Expert Member
Oct 12, 2019
419
670
1709531075768.png

Uchumi wa Tanzania kwa asilimia kubwa upo kwa wageni. Yes! Matajiri wengi waliopo Tanzania sio watanzania kwa asili, wengi wana asili za nchi nyingine. Hii ni kwasababu hatuna akili za biashara kabisa. Niliposoma gazeti hili la majira kuhusu sakata linaloendelea ndio nikaona shida zaidi.

Agha Khan moja kati ya hospitali inayotumiwa na wengi wenye hela zao inasifiwa kwa huduma bora, sasa mtu anataka the so called "Utu" kwa gharama ya nani?. Nadhani tunakwepa jukumu msingi au hatutaki kuona shida iko kwa anayepaswa kulipa.

Niseme tu, sisi (wananchi) tunachangia hela ya kutosha, NHIF waangalie fedha wanazowapa hospitali ili kuweka mambo sawa na sio kutaka wananchi wadhani wanaonewa wakati NHIF inaweka fedha kidogo kwa watoa huduma.

Lazima tujue ili kutoa huduma nzuri, kunahitaji gharama, maisha ya Dkt wa Agha Khan huwezi fananisha na maisha ya Dkt kwenye zahanati ya kijiji ambayo siku zote dawa hawana. kwa hili wananchi tulishwe matangopori kwa jina la "UTU". Hizi hospital zinahitaji fedha kujiendesha, sisi tumeshatoa fedha kupeleka NHIF, hivyo NHIF waache uhuni.

Kingine, tusifikirie kwamba afya yako ni jukumu la fulani, watu wanafanya biashara, kama wananchi kweli mnataka mfanyiwe utu, fungueni hospitali zenu jitibieni bure. To hell with philanthropism.

Signed!

OLS
 
Kama tu hawa wadogowadogo tulionao mitaani hawajui customer care na advertisement hao wakubwa si ndio watakuwa hawajui kitu kuhusu kukuza biashara zao? Kuna wengi wanafanya biashara lakini hawajui strategy za biashara
 
Ukoo wako umezalisha wafanyabiashara wangapi?
Kama na wewe huna biashara inayoendelea ambayo kizazi chako kinaweza kuirithi miaka ijayo basi acha talantalila
 

Uchumi wa Tanzania kwa asilimia kubwa upo kwa wageni. Yes! Matajiri wengi waliopo Tanzania sio watanzania kwa asili, wengi wana asili za nchi nyingine. Hii ni kwasababu hatuna akili za biashara kabisa. Niliposoma gazeti hili la majira kuhusu sakata linaloendelea ndio nikaona shida zaidi.

Agha Khan moja kati ya hospitali inayotumiwa na wengi wenye hela zao inasifiwa kwa huduma bora, sasa mtu anataka the so called "Utu" kwa gharama ya nani?. Nadhani tunakwepa jukumu msingi au hatutaki kuona shida iko kwa anayepaswa kulipa.

Niseme tu, sisi (wananchi) tunachangia hela ya kutosha, NHIF waangalie fedha wanazowapa hospitali ili kuweka mambo sawa na sio kutaka wananchi wadhani wanaonewa wakati NHIF inaweka fedha kidogo kwa watoa huduma.

Lazima tujue ili kutoa huduma nzuri, kunahitaji gharama, maisha ya Dkt wa Agha Khan huwezi fananisha na maisha ya Dkt kwenye zahanati ya kijiji ambayo siku zote dawa hawana. kwa hili wananchi tulishwe matangopori kwa jina la "UTU". Hizi hospital zinahitaji fedha kujiendesha, sisi tumeshatoa fedha kupeleka NHIF, hivyo NHIF waache uhuni.

Kingine, tusifikirie kwamba afya yako ni jukumu la fulani, watu wanafanya biashara, kama wananchi kweli mnataka mfanyiwe utu, fungueni hospitali zenu jitibieni bure. To hell with philanthropism.

Signed!

OLS
Kichwa cha mada ni tofauti na maelezo ya mada.

Hapa unalalamika kuhusu serikali kushindwa kutimiza wajibu wake kwa hospitali kuhusu bima ya NHIF. Badala yake siasa (propaganda) inatumika kulaumu hospitali kwa kugoma kuhudumia wagonjwa bila kujali suala la malipo. Kwamba hospitali ziwe na “utu”.

Ulichoeleza ni sahihi kabisa lakini hakihusiani na “akili za biashara za watanzania”. Kinahusiana zaidi na utawala bora. Kilichotokea ni “mismanagement” ya NHIF na janja ya serikali kutaka kuhamisha failure yake kwa hospitali na kueneza propaganda ya “utu”, “uzalendo”. Si mara ya kwanza. Imefanyika kwenye mengi. Kikokotoo na mifuko ya pensheni, stahiki za wafanyakazi, vitendea kazi vya huduma za hospitali za serikali (rejea mgomo wa kina Ulimboka), n.k. Hakuna Mtanzania asiyejua kuwa huduma za hospitali zina gharama. Wasingekata bima.

Ni tatizo la uongozi wa kisiasa (leadership crisis). Propaganda na patronage vimetamalaki nchini hadi kwenye mambo ya msingi sana.

Katika mada yako hii laumu Watanzania kwa kushindwa kutatua tatizo la uongozi wa nchi na kukumbatia propaganda na u-chawa. HALAFU anzisha uzi mwingine kuhusu akili za Watanzania katika biashara. Kuna hoja ya kutosha katika hili.
 
Ukoo wako umezalisha wafanyabiashara wangapi?
Kama na wewe huna biashara inayoendelea ambayo kizazi chako kinaweza kuirithi miaka ijayo basi acha talantalila
Dah swali lako limenifikirisha sana ukoo wetu wote hakuna wafanya biashara isee wa maana yaani ukitoboa ni mfanyakzi serikalini watu wananyadhifa ila biashara hawana wakistaaf wanabaki nyumbani tu na shambani. Basi ata ukitaka kuongelea biashara unaonekana umechanganyikiwa flani hivi alafu bahati mbaya zaidi hadi hadi ukoo wa ukweni hakuna wafanya biashara waliofanikiwa.

Ila nitaivunja hii spirit lazima biashara zizalishe bilionea kwenye ukoo na napambana sana kufanikisha hili..
 
Dah swali lako limenifikirisha sana ukoo wetu wote hakuna wafanya biashara isee wa maana yaani ukitoboa ni mfanyakzi serikalini watu wananyadhifa ila biashara hawana wakistaaf wanabaki nyumbani tu na shambani. Basi ata ukitaka kuongelea biashara unaonekana umechanganyikiwa flani hivi alafu bahati mbaya zaidi hadi hadi ukoo wa ukweni hakuna wafanya biashara waliofanikiwa.

Ila nitaivunja hii spirit lazima biashara zizalishe bilionea kwenye ukoo na napambana sana kufanikisha hili..
All the best and usiache wazee wa propaganda za kwamba kama kwenu hamna asili ya biashara hutoweza.... kila jambo lina muanzilishi
 
Kichwa cha mada ni tofauti na maelezo ya mada.

Hapa unalalamika kuhusu serikali kushindwa kutimiza wajibu wake kwa hospitali kuhusu bima ya NHIF. Badala yake siasa (propaganda) inatumika kulaumu hospitali kwa kugoma kuhudumia wagonjwa bila kujali suala la malipo. Kwamba hospitali ziwe na “utu”.

Ulichoeleza ni sahihi kabisa lakini hakihusiani na “akili za biashara za watanzania”. Kinahusiana zaidi na utawala bora. Kilichotokea ni “mismanagement” ya NHIF na janja ya serikali kutaka kuhamisha failure yake kwa hospitali na kueneza propaganda ya “utu”, “uzalendo”. Si mara ya kwanza. Imefanyika kwenye mengi. Kikokotoo na mifuko ya pensheni, stahiki za wafanyakazi, vitendea kazi vya huduma za hospitali za serikali (rejea mgomo wa kina Ulimboka), n.k. Hakuna Mtanzania asiyejua kuwa huduma za hospitali zina gharama. Wasingekata bima.

Ni tatizo la uongozi wa kisiasa (leadership crisis). Propaganda na patronage vimetamalaki nchini hadi kwenye mambo ya msingi sana.

Katika mada yako hii laumu Watanzania kwa kushindwa kutatua tatizo la uongozi wa nchi na kukumbatia propaganda na u-chawa. HALAFU anzisha uzi mwingine kuhusu akili za Watanzania katika biashara. Kuna hoja ya kutosha katika hili.
Biashara nyingi kubwakubwa zilizosimama ni generation wealth toka vizazi na vizazi, biashara ina mambo mengi yanayofanyika nyuma ya pazia, biashara zina dhulma na utapeli mwingi, biashara zina kafara nyingi ingawaje si wote wanatoa kafara, mfumo wetu Wa elimu pia umetujenga kwenye akili ya kuajiriwa zaidi na kutujengea uoga Wa kujiajiri, mfumo Wa siasa ya ujamaa na azimio la arusha ulifilsi mitaji ya watu wengi ambao Leo hii watoto na wajukuu wao wangeweza kuwa wafanyabiashara wakubwa na wasimamizi Wa biashara kubwa za familia, hivyo watanzania wasilaumiwe Bali serikali iwe na mikakati na Sera ya kulinda wafanyabiashara wazalendo.
 
Back
Top Bottom