Facts1
JF-Expert Member
- Dec 23, 2009
- 307
- 28
Nafikiri ni jambo jema kwa NGOs na Wanaharakati wetu sasa kujiunga kwenye mapambano dhidi ya Ufisadi.
Nafikiri jamii pia inaguswa zaidi na Ufisadi kwa njia moja au nyingine kama inavyoguswa na masuala ya ukeketaji, mauaji ya albino,masuala ya jinsia UKIWMI nk.
Ukiangalia NGO zetu nyingi na wanaharakati wetu wengi wamejikita kwenye masuala ya ukimwi na watoto yatima na kusahau kuwa Ufisadi na rushwa ndiyo msingi mkuu wa matatizo hayo, sitaki kusema kuwa wanafanya hivyo kwa sababu ya masilahi yao, hapana.
Tukiondoa ufisadi katika mahakama zetu katika wizara zetu, mabenki yetu nk, haki katika jinsia tunayoitafuta itapatikana, mauaji ya albino yatapungua kama siyo kwisha kabisa kwa maana yanasababishwa na kipato kidogo cha watu.
Kwa hiyo RAI kwa wanaharakati wetu kama akina Ananilea Nkya, Tamwa nk wageuke tuwe tunasikia angalau wamefungua kesi kwa fisadi fulani na siyo kuwaachia wanasiasa kazi ya kupambana na mafisadi papa.
Naomba mwenye mawazo zaidi kwa hoja hii.
Nafikiri jamii pia inaguswa zaidi na Ufisadi kwa njia moja au nyingine kama inavyoguswa na masuala ya ukeketaji, mauaji ya albino,masuala ya jinsia UKIWMI nk.
Ukiangalia NGO zetu nyingi na wanaharakati wetu wengi wamejikita kwenye masuala ya ukimwi na watoto yatima na kusahau kuwa Ufisadi na rushwa ndiyo msingi mkuu wa matatizo hayo, sitaki kusema kuwa wanafanya hivyo kwa sababu ya masilahi yao, hapana.
Tukiondoa ufisadi katika mahakama zetu katika wizara zetu, mabenki yetu nk, haki katika jinsia tunayoitafuta itapatikana, mauaji ya albino yatapungua kama siyo kwisha kabisa kwa maana yanasababishwa na kipato kidogo cha watu.
Kwa hiyo RAI kwa wanaharakati wetu kama akina Ananilea Nkya, Tamwa nk wageuke tuwe tunasikia angalau wamefungua kesi kwa fisadi fulani na siyo kuwaachia wanasiasa kazi ya kupambana na mafisadi papa.
Naomba mwenye mawazo zaidi kwa hoja hii.