Wimbo wa Taifa urekebishwe!!!

Indume

Member
Apr 11, 2011
81
36
Nimekuwa nikiimba sana wimbo wa Taifa toka nikiwa mdogo ninasoma chekechea hadi sasa hivi. Kuna maneno ambayo katika wimbo huo nadhani unahitaji marekebisho. Pale panapoimbwa........" Wabariki Viongozi wote". Kwa jinsi ilivyo hata kama kiongozi ni Fisadi, ,mwizi, muuza madawa ya kulevya, mtoa rushwa, mbakaji kama yule mzee, tapeli, muuaji, ......basii eti hao viongozi "wabarikiwe na Mungu". Mi nasema hapana. Ni busara inahitajika kutumika ili sehemu ya wimbo huo usomeke na uimbwe " wabariki wazalendo wote".

Labda ndio maana nchi hii hali ya uchumi ni mbaya kwa kuwa hata waovu wanaimbiwa wabarikiwe, matokeo yake viongozi wa nchi hii inakuwa kuwa wamelaaniwa na kushindwa kuleta maendeleo thabiti.

Nawasilisha
 
Maneno hayo yamepitwa na wakati kwakuwa sasa viongozi wanapokea baraka hali wanaitendea maovu nchi yetu
 
Khaa!! Ndiyo maana tuko maskini hadi leo. Tuna mawazo ya ajabuajabu. Hii yote kwasababu hatutaki kufanya kazi za uzalishaji tunapenda kupiga domo tu.
 
Sasa kama "viongozi wake" wanabarikiwa, Je ambao siyo "Viongozi" je???? Nchi hii imelaaniwa.
 
Hoja nzito sana...naunga mkono kabisa ila kuwasaidia hao viongozi badala ya neno wabariki tuweke neno "waongoze" yaani tumuombe Mungu awaongoze kuongoza kwa uadilifu na kwa uaminifu
 
Mmmh!!!tusiingilie kaz ya mungu.Mungu ndiye mtoa baraka.anambariki nani hambariki nan kwanini anajua yeye.tukumbuke Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi za ulimwengu na hasa wadhambi.ni kwa neema yake tu yote yanawezekana na c lazma uwe mwenye haki.anagawa barika na kila Jambo Jema vile apendavyo.mungu anatupenda sote bila ubaguz na hasa hao ambao wew unawaona waovu.we unatenda maovu mangap hata km c wiz ufisadi nk.???je uombewe laana??jambo LA msingi ni kuzidi kuombeana sn ili hata wale viongoz wetu wanaotenda maovu na kukwamisha haki na maendeleo ya nchi waache maovu hayo na kumrudia mungu.kabla hujatoa boriti lililo ktk jicho la mwenzako,toa lililo jichon mwako ili ulione vizur lililo ktk jicho la mwenzio.na bila maombi hii nchi itakuwa hivi hiv au hat a hali kuwa mbaya zaid mpaka Yesu kristo aje!!ubarikiwe mtoa hoja
 
Unaongelea nch gani mkuu?
Wimbo wa taifa la Tanzania hauna maneno "wabariki viongozi wote".
 
Nimekuwa nikiimba sana wimbo wa Taifa toka nikiwa mdogo ninasoma chekechea hadi sasa hivi. Kuna maneno ambayo katika wimbo huo nadhani unahitaji marekebisho. Pale panapoimbwa........" Wabariki Viongozi wote". Kwa jinsi ilivyo hata kama kiongozi ni Fisadi, ,mwizi, muuza madawa ya kulevya, mtoa rushwa, mbakaji kama yule mzee, tapeli, muuaji, ......basii eti hao viongozi "wabarikiwe na Mungu". Mi nasema hapana. Ni busara inahitajika kutumika ili sehemu ya wimbo huo usomeke na uimbwe " wabariki wazalendo wote".

Labda ndio maana nchi hii hali ya uchumi ni mbaya kwa kuwa hata waovu wanaimbiwa wabarikiwe, matokeo yake viongozi wa nchi hii inakuwa kuwa wamelaaniwa na kushindwa kuleta maendeleo thabiti.

Nawasilisha

ni kweli mkuu,kwa watu wengi huwa wanadhani wimbo wa taifa ni wimbo tu wa kawaida,hapana,ile huwa ni sala ya kuliombea taifa.hivyo basi kuna mafisadi yananufaika kutokana na sala hii.tunayaombea yanabarikiwa yanazidi kuiba kwa nguvu
 
Mm wimbo wa Taifa hata siujui tangia niache kuuimba miaka ya 90, ukizingatia nilikuwa nakaa msitari nyuma hata kuimba nilikuwa naiga tu wala hata haukukaa kichwani kabisa.
 
Mm wimbo wa Taifa hata siujui tangia niache kuuimba miaka ya 80, ukizingatia nilikuwa nakaa msitari nyuma hata kuimba nilikuwa naiga tu wala hata haukukaa kichwani kabisa.
 
uondolewe wote tulete mpya , maana tangu tuanze kuomba baraka za mungu tumekataliwa .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom