Wimbo uliohit huku ukiwa na maneno yasiyo eleweka hata kidogo

Wimbo wa HILI GAME ulioimbwa na JUMA NATURE KIROBOTO.

Huu wimbo ukiuzikiliza hata huo wa gangwe mob un afadhali. Yaani sentensi zimeungwa ungwa tu, neno hili na linalofuata hayahusiani, na hata maneno yenyewe pia hayaeleweki.

Wimbo una maneno ya kiswahili, ya kiengereza, kizaramo sijui hukohuko mixer ki-bondeni. Wimbo hata maana nzima ya hilo gemu alilosema ni tafu sijaipata bado, na hata haieleweki alimaanisha nini huu wimbo.

Mwenye lyrics za huu wimbo aziweke hapa
 
Juma Nature kibra na Inspector Haroun hao ndo magwiji wa rap katuni kipindi hichooo unakula burudan huku unafurah na roho yako hzo nyimbo kwng zinaishi mpaka leo
 
asante sana ulileta huu uzi kwa wana fasihi hapa hii ni kazi nzuri sana hasa kipengele cha matumizi ya lugha maana kuna rejesta humo kuna simo tamathali za semi humo yani kweli hii ilikuwa rap katuni na imekizi vigezo cha kuitwa kazi ya sanaa ya msanii

wimbo unaeleweka kabisa huu mkuu sema tu haumo katika kundi ambalo wasanii waliliandikia
 
Hadhira ya hawa jamaa ni yakivingine kabisa, sasa ukisubiri wafuasi wa basata mje kusikiliza michano ya hawa watoto wa uswaz hamtoambua kitu...

Mkuu hii kitu inaitwa rap katuni a.k.a michano mikalii, enzi hizo ilishikiliwa na akina nature kiroboto, insp. Haruna, luten karama, gangwe mob na gwm, wachuja nafaka, lwp, dully syks, solid ground family, mabaga flesh, kr mura jibaba mstitu mnene, d chief, na wana kibao wa temeke

Kumbuka tracks kama Sonia, asali wa moyo, jinsi kijana, ugali, salio la verse, staki demu, hili gamu, mtulize, mechi kali, tunajirusha, mzee wa busara 1 and 2,Julieta, nyambizi, historia ya kweli, mke wa mtu ni sumu, akuvaa kondomu...

Yaani tunaongea kipindi wakati akina mangwea hawajazaliwa kimziki, akina fa na ay kama maunderground, akina sugu wanapiga rap kali za harakati, prof j wanatoa vitu vya chemsha bongo na ndio mzee, na zali la mentali, akina dudu baya wanachipkia na vitu kama mwanangu huna nidhamu, akina qchief ndo wanatoka na namtafta, akina jmoo wanatoka na vitu kama jua na mvua na bishoo, akina afande wangonga mkuki moyoni, akina solo thang wanapiga mambo ya pwani.. Fid q akiwa underground na kibao cha huyu na yule, mr blue hata hjulikani ni nani!

Sasa hapo kati kuelekea 2000's ndio ikaja commercial rap ilio letwa na watoto wengi wa upanga kino na sehem za ilala..
Ndio kidogo mziki ukaanza kuonekana wa maana coz zaman kipindi cha katuni mziki na uhuni vilikua havitofautishiki..

Daaah kuna mengi sana kwenye game hili... Acha tu!
Yaani nikikumbuka zamani, akina pfunk, mika mwamba, mj, soundcrafters, mawingu studio, coplex n.k huwa naingiwa na furaha ya machoz, mziki wa bongo umetoka mbali sana maan!
 
utafikiri mkusanyiko wa matoleo ya kifimbo cheza. huu wimbo anauelewa mwenyewe tyu.
 
Wimbo umesimama sana...
Fasihi sio lazima ujumbe tu..hata kuburudisha wakuu...lakini hata hivyo ukimwuliza aliyetunga maana utaipata.
 
Hiyo track inaeleweka sana.Napenda sana rap katuni kuliko kawaida.sina kabisa nyimbo za sasa.mimi kwangu Juma,Haruna,Mabaga Fresh,GWM Majitu,bado ni wakali kwangu.hawa machizi ni mara chache sana kurap mapenzi,na wakichana mapenzi hawalii-lii....Sikiza Mtoto wa Geti Kali na Sonia wanavyopewa michano,sikia Sitaki Demu ukizinguliwa...ukiniambia hata jina la nyimbo moja ya Young Kila siijui....niambie kuhusu Wachuja Nafaka na Gagwe Mob na machizi wengine miaka ya 90

bana pia mimi sijui wasanii sasa wanaimba nini? sikiliza miziki ya bongo pindi kile kama:-
1.siku za hukukumu-boyz from army ft inspector haroon
2.kipye kipe kitu-gwm
3.mtulize-mabaga ft j.nature
4.upanga side-crazy gk
5.kukurukara zako-sos b
6.dunia inaumwa-solothang
7.bamiza-x-plastaz
8.kula kona-manzese crew
9.bado nipo-balouz
10.salome-dully sykes


basi inatosha sasa hivi hakuna ladha
 
Inspector alikuwa anamdhalilisha kalama anamnanga kwa kujisifia kwenye studio za radio kuwa yeye ndo huwa anatunga nyimbo, sasa hivyo ni vitu vya kuongea radioni? Yote hiyo aonekane yeye ndo kichwa kwenye group. Yale yale ya juma nature na wanaume, aliona bila yeye group halitosimama, mwisho wa siku na yeye chali!
 
bana pia mimi sijui wasanii sasa wanaimba nini? sikiliza miziki ya bongo pindi kile kama:-
1.siku za hukukumu-boyz from army ft inspector haroon
2.kipye kipe kitu-gwm
3.mtulize-mabaga ft j.nature
4.upanga side-crazy gk
5.kukurukara zako-sos b
6.dunia inaumwa-solothang
7.bamiza-x-plastaz
8.kula kona-manzese crew
9.bado nipo-balouz
10.salome-dully sykes


basi inatosha sasa hivi hakuna ladha

Homa ya dunia - solothang
 
Wimbo wa HILI GAME ulioimbwa na JUMA NATURE KIROBOTO.

Huu wimbo ukiuzikiliza hata huo wa gangwe mob un afadhali. Yaani sentensi zimeungwa ungwa tu, neno hili na linalofuata hayahusiani, na hata maneno yenyewe pia hayaeleweki.

Wimbo una maneno ya kiswahili, ya kiengereza, kizaramo sijui hukohuko mixer ki-bondeni. Wimbo hata maana nzima ya hilo gemu alilosema ni tafu sijaipata bado, na hata haieleweki alimaanisha nini huu wimbo.

Mwenye lyrics za huu wimbo aziweke hapa

Wasanii wa temeke utawaweza hahahahh waswahili balaa haahahahab
 
Ila kuna wimbo wa TID aka WARIOBA unaitwa ZEZE....mpaka leo sijaweza kuelewa by zeze alikusudia nini maana neno zeze limetumika kila pahala.
 
Duuuuuh baraaa, nakumbuka niko sekondari Enzi hizo, ngoma linapigwa usiku wa manane wazee wa msuli nyumba wanasokumia manamba magumu
 
asante sana ulileta huu uzi kwa wana fasihi hapa hii ni kazi nzuri sana hasa kipengele cha matumizi ya lugha maana kuna rejesta humo kuna simo tamathali za semi humo yani kweli hii ilikuwa rap katuni na imekizi vigezo cha kuitwa kazi ya sanaa ya msanii

wimbo unaeleweka kabisa huu mkuu sema tu haumo katika kundi ambalo wasanii waliliandikia

daaah yaan mtu amevuta bange yupo chakali amekunywa gongo hajielewi ameandika mistari haieleweki watu wanajilazimisha tu kuielewa ili nao waonekane ni ma pro wa fasihi,, kweli leo nature nae eti kawa mwanafasihi?!! fasihi ipi jaman? ama kweli halimtapishi lake mtu
 
Back
Top Bottom