Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Kuna taarifa takribani kila wiki za ama wanachama au viongozi wa CCM kuhamia Chadema. Hadi sasa imechukuliwa kwamba ni jambo jema. Wengi wanalihisisha na kazi ya "Mungu"
Nilitarajia kwa kasi hiyo ya kuhamia, Chadema wangekuwa wametangaza mkakati wa kuwapokea, na kuwapunga mapepo ya CCM. Au kuimarisha uongozi katika maeneo ambao Chadema imepokea wanachama wengi kutoka CCM.
Hayo siyo ya msingi sana! Tatizo ninaloliona mimi ni kwamba Chadema hivyo inakua na kupanuka kwa kasi na namna ambayo hawakutarajia. Hivyo kuna hatari ya kuanguka badala ya kuimarika, pengine katika maeneo fulani. Wakashindwa kuhimili growth.
Isipokuwa pia kama Chadema ikifanikiwa basi pengine itakuwa imetuonesha, japo kidogo kwamba wao wanajua na wana uwezo aw kutawala tofauti na CCM. Ingawa hiyo haitatuthibitishia kwamba wanaweza kuongoza nchi, japo tungependa kuwajaribu kama tutapata ahuweni ya matatizo tuliyo nayo sasa
Hivyo kuhamia kwa wingi wanachama wa CCM Kwenda Chadema ni fursa kwa Chadema kutuonesha uwezo wao
Nilitarajia kwa kasi hiyo ya kuhamia, Chadema wangekuwa wametangaza mkakati wa kuwapokea, na kuwapunga mapepo ya CCM. Au kuimarisha uongozi katika maeneo ambao Chadema imepokea wanachama wengi kutoka CCM.
Hayo siyo ya msingi sana! Tatizo ninaloliona mimi ni kwamba Chadema hivyo inakua na kupanuka kwa kasi na namna ambayo hawakutarajia. Hivyo kuna hatari ya kuanguka badala ya kuimarika, pengine katika maeneo fulani. Wakashindwa kuhimili growth.
Isipokuwa pia kama Chadema ikifanikiwa basi pengine itakuwa imetuonesha, japo kidogo kwamba wao wanajua na wana uwezo aw kutawala tofauti na CCM. Ingawa hiyo haitatuthibitishia kwamba wanaweza kuongoza nchi, japo tungependa kuwajaribu kama tutapata ahuweni ya matatizo tuliyo nayo sasa
Hivyo kuhamia kwa wingi wanachama wa CCM Kwenda Chadema ni fursa kwa Chadema kutuonesha uwezo wao