je huyu jamaa yupo au ameuawa?
therad inanichanganya
nimeelewa shem, aikamaeshem...aliyekufa ni bwana anaitwa Willy Muga......aliyeripoti hii habari ya kuvamiwa kwa hilo basi asubuhi anaitwa Mu-Sir ni member wa JF....umeelewa sasa?
Kwa mujibu wa walionusurika na watu waliokuwa eneo la tukio waliokufa ni wawili.habari iliyotangazwa saa mbili na ITV inasema majeruhi wapo 20 na hali zao ni mbaya kutokana na majeraha ya risasi, na aliyekufa ni mtu mmoja....tuzidi kuwaombea majeruhi wapone haraka
Taarifa nilizozipata hivi punde zinasema Wilfred Muga Katibu wa CCM vijana Musoma Mjini ameuawa na majambazi leo asubuhi kwa kupigwa risasi akiwa njiani kutoka Kigoma Kuelekea Mwanza.
Mwenye taarifa za kina naomba atusaidie. Nlichosikia kuwa kuna watu wengine wawili pia wameuawa kwenye tukio hilo
je huyu jamaa yupo au ameuawa?
therad inanichanganya
Hukusia Hotuba ya JK??? Hakuna uhalifu.....na akawapongeza Polisi.... then wanajeshi wataongezewa marupurupu.....na sure wapo hapa mjini na kwenye makambi mengine kibao nchi nzima...............Kwa nini hii serikali isipeleke jeshi huko???hawa watakuwa Intarahamwe tu....polisi haiwawezi hawa.Wanajeshi wapo hapo mijini wana vitambi???AIBU!!!
RIP wote walofariki kwenye tukio hilo.
Basi hilo la Kampuni ya China ya Golden Intercity Express lenye namba za usajili T 457 ARC lilikuwa limebeba abiria 51 lilitekwa na Majambazi hayo katika eneo la Mkugwa wilayani Kibondo, inasemekana majambazi hao walipiga sana Risasi, akielezea Mkasa huo kwa njia ya simu kutoka eneo la tukio, mmoja wa Wasafiri aliyekuwa ndani ya Basi hilo kutoka Kigoma kwenda Mwanza, Sophia Nasibu alieleza kwamba tukio hilo lilitokea majira ya saa tatu asubuhi ambapo alishuhudia Majambazi yakipiga risasi ovyo kwenye Basi hilo na hivyo Dereva kulazimika kusimama porini hapo.