MwanzoMugumu
Member
- Jan 27, 2012
- 24
- 22
WanaJF baadaya kusoma maelezo na mapendekezo yenu katika "TOPIC" ya jana ilisomeka hii ndiyo hali halisi kwa heshima na unyenyekevu mkubwa naomba kumleta kwenu Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Wiliam Mganga Ngereja aka Mr.Megawat.kuwa ndiye mmiliki wa nyumba ya ghorofa kama tano hivi make sijaingia. Nyumba hiyo inajengwa jijini Mwanza katika mtaa wa Rufiji, kwa kibali namba 5955 na Planning Consent No_21390. Project ni construction of Commercial Building Plot No. 7 Block O, ndani ya Mwanza city. Inasomeka kwamba client ni Jakandom Investment Co. Ltd,Box No_7528 Mwanza. Architect ni Mellow Architects wa jijini Mwanza, Quality surveyor ni A.M Quantity Surveying Consultancy na Main Contractor ni CF Builders Ltd wa Box No_ 1755 Mwanza.Kwa taarifa tu ni kwamba huyo client ni kupitia tu, huyo bwana ni mfanyabiashara wa samaki jijini mwanza wala hana hata uwezo wa kujenga jengo hilo. Ndugu zangu Waziri kujenga jengo kubwa kama hilo sio nongwa hata kidogo hoja hapa ni anapokuwa mtumishi wa umma tena katika wizara inayolalamikiwa na Watanzania walio wengi hapo ndipo maswali yanapoanzia. Tunamuomba Mhe Waziri ajitokeze hadharani kulitolea ufafanuzi jambo hili la sivyo patakuwa hapatoshi. Kwa kumbukumbu tu jengo hili limeanza kujengwa mwaka jana tu yaani linaota kama uyoga. NALETA KWENU WAUNGWANA