William Ngeleja - Waziri Anayetuhumiwa kwa Wizi!

Hv enzi za Mwal huyu Mr Volts angejenga kwel huo mjengo? Tatzo sasa hv ni shamba la bibi kila mtu anachukua chake mapema!!
 
huyu jamaa anauchafu mwingi sana kanda ya ziwa, kajaza ukoo mzima geita gold mining mpaka darasa la nne, ununua magazeti yote mwanza mjini nyenye taarifa yake mbaya yasivuke jimboni kwake (je pesa hii anatoa wapi?) n.k na sasa swahiba wake mr tabasamu(diwani) wenye siri nying za huyu bwana ameamia CDM.... kwisha Mr william mganga ngeleja, mungu unajibu maombi asante.
 
WanaJF baadaya kusoma maelezo na mapendekezo yenu katika "TOPIC" ya jana ilisomeka hii ndiyo hali halisi kwa heshima na unyenyekevu mkubwa naomba kumleta kwenu Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Wiliam Mganga Ngereja aka Mr.Megawat.kuwa ndiye mmiliki wa nyumba ya ghorofa kama tano hivi make sijaingia. Nyumba hiyo inajengwa jijini Mwanza katika mtaa wa Rufiji, kwa kibali namba 5955 na Planning Consent No_21390. Project ni construction of Commercial Building Plot No. 7 Block O, ndani ya Mwanza city. Inasomeka kwamba client ni Jakandom Investment Co. Ltd,Box No_7528 Mwanza. Architect ni Mellow Architects wa jijini Mwanza, Quality surveyor ni A.M Quantity Surveying Consultancy na Main Contractor ni CF Builders Ltd wa Box No_ 1755 Mwanza.Kwa taarifa tu ni kwamba huyo client ni kupitia tu, huyo bwana ni mfanyabiashara wa samaki jijini mwanza wala hana hata uwezo wa kujenga jengo hilo. Ndugu zangu Waziri kujenga jengo kubwa kama hilo sio nongwa hata kidogo hoja hapa ni anapokuwa mtumishi wa umma tena katika wizara inayolalamikiwa na Watanzania walio wengi hapo ndipo maswali yanapoanzia. Tunamuomba Mhe Waziri ajitokeze hadharani kulitolea ufafanuzi jambo hili la sivyo patakuwa hapatoshi. Kwa kumbukumbu tu jengo hili limeanza kujengwa mwaka jana tu yaani linaota kama uyoga. NALETA KWENU WAUNGWANA

MwanzoMugumu,unamaanisha ghorofa mkabala na Mwanza womens clinic au kwa Kironzo?Ni kweli jengo hilo linavyojengwa ni sawa na uyoga,speed yake ni kubwa mno.Kiukweli mimi sina shaka na kujenga ghorofa tano,matatizo yangu ni hiyo speed ya ujenzi,kwa mshahara na posho ingemchukua miaka yake kumi ya kuwa bungeni kufikisha hapa jengo lilipo!Hebu tumwangalie rafiki yake mawe matatu, kihoteli chake pale Usagara amehangaika nacho kweli na mpaka leo bado anasuasua inakuwa vipi Mr. Megawati kuwa na spidi kali hivyo au kakatiwa mshiko na DOWANASI ndo maana alibariki malipo veri fasiti?Hilo ni jengo moja,je Sengerema kafanya vitu gani na Dar kuna nini kafanya kama vyote vitathaminishwa ni kweli itakuwa proposheno na inkamu yake?
 
Hata ningekuwa mimi Ngeleja,ningeingiza ndugu zangu kibao siyo GGM tu bali TANESCO na hata wizarani.Nchi hii imekuwa ya kugombania kati ya watu wa maeneo tofauti tofauti,hakuna mzalendo tena!Huu ujinga umeanza kitambo sana,robo tatu ya bajeti naielekeza jimboni kwangu,mshenzi Mramba!
 
huyu jamaa anauchafu mwingi sana kanda ya ziwa, kajaza ukoo mzima geita gold mining mpaka darasa la nne, ununua magazeti yote mwanza mjini nyenye taarifa yake mbaya yasivuke jimboni kwake (je pesa hii anatoa wapi?) n.k na sasa swahiba wake mr tabasamu(diwani) wenye siri nying za huyu bwana ameamia CDM.... kwisha Mr william mganga ngeleja, mungu unajibu maombi asante.

ukoo wako uko wapi?changamka.
 
Lakini tuwe realistic, Ngeleja kawa waziri kwa miaka mingapi? Kwa mshahara na marupurupu ya waziri kweli atashindwa kujenga nyumba ya ghorofa tano? Ofisini kwetu sisi masecretary wanajenga nyumba zao wenyewe. Almost kila secretary ama ana nyumba au ana gari. Sasa itakuwa waziri jamani? Tena waziri ambaye amekaa madarakani kwa muda wa karibu miaka saba. Sasa mnataka hela anayopata afanyie nini? Ndiyo yale yale ya kumwita Sumaye fisadi kisa kanunua shamba la ekari arobaini. Au ukiwa mtumishi wa umma hutakiwi kufanya shughuli za maendeleo binafsi?

Mkuu, nimependa sana analysis yako. ni kweli, kuwa waziri kwa 7 years tunampa nafasi ya kupata pesa nyingi tu.
Naomba tufanye jambo moja. let us make it operational.

1) Kwanza tuangalie mshahara wa waziri kwa 7 years na marupurupu yake yote kwa muda huo.
2) Tuangalie costs ya kujenga ghorofa 5 kwa jiji kama Mwanza.

Mkuu, hapo tutapata ukweli.
 
Ndugu zake kule Buyagu wanakufa njaa kwa ufisadi wake. Ikifika 2015 watampatia kura baada ya kuhongwa kanga na kofia. Acha wakome.
Lakini Ngeleja asisahau hakuna marefu yasiyokuwa na ncha.
 
Tumechoka sasa! Atakayemwona alipo Mr Megawati niambieni. Potelea mbali!
Avatar hazidanganyi hata kidogo.....Siungi mkono hoja yako. Kwa sababu nina amini katika taratibu za kiungwana (sheria na kanuni bora kwa wote)
 
Taabu yote ya nini, tufanye sensa za nyumba mtaa kwa mtaa uliza mwenyewe nani ndo MTAJUA hali halisi nani ana nini
 
Kwa waziri kujenga nyumba ya ghorofa tano si ajabu lakini kinachongomba hapa ni hiyo speed ya ujenzi,MwanzoMugumu kama sikosei unamaanisha ghorofa lililoko mkabala na hospitali ya Mwanza women's clinic au kwa Kironzo kama panavyojulikana hapa MZA.Nisingeshangaa ujenzi kama ungechukua zaidi ya miaka kumi hapa binafsi nisingekuwa na swali....hamuoni mwenzake mawe matatu!Kahangaika kweli na ujenzi wa kihoteli chake pale Usagara kama sio janja ya nyani.Sasa hilo ghorofa ndo watu wameona je mali ambazo hazijaonekana au na akaunti za nje kabisa zipo....JK anatakiwa afanya maamzi ambayo kwake ni magumu ingawa kiuhalisia ni uwajibikaji wa kawaida tu kwa mfanyakazi anaposhindwa udeliver.Nafikiri imefikia wakati mawaziri apewe targets asiemeet target off he/she go...Kaaaz kweli kwel....
 
Siwezi kushangaa hata kidogo, ikiwa unamfahamu Waziri huyu, ikiwa unafahamu mizinga anayopiga kwa kweli hata hilo ni dogo. Akiwa na hao jamaa wachimbaji utaona kabisa ambavyo anaangalia mifuko yao kuliko kodi wanazostahili kutoa. Issue sio uwezo wake- issue ni wizi wanaoufanya yeye na team yake, iwe ni kwa jengo hilo ama kwa vitu vingine. Wenye uwezo wa kufuatilia wafuatilie wataona uharibifu unaopitia mikononi mwao.
 
Back
Top Bottom