Who influenced Nyerere: His Ujamaa Philosophy and Azimio Principles?

Mchungaji mbona umeshajijibu mwenyewe. Mawazo ya Mwalimu Nyerere ni matokeo ya kile ambacho Profesa Ali Mazrui anakiita 'Africa - A Triple Heritage', yaani 'Urithi wa Afrika Kutoka Sehemu Tatu' sehemu hizi ni Afrika-Asilia, Asia-Arabuni na Uropa-Amerika. Hivyo basi, ni sahihi kabisa kusema kuwa Mwalimu alichanganya madesa yote matatu ndio maana kale kajitabu kake kwa mwaka 1962 kanakoitwa 'Ujamaa - The Basis of African Socialism', yaani 'Ujamaa- Msingi wa Usoshalisti wa Kiafrika', kanaonesha mambo tuliyoyarithi katika jamii ya Kiafrika/Kitanzania yanavyoweza kutumia ufahamu/teknolojia kutoka ...


Nyerere alichanganya madawa tu. Vitabu na falsafa yake ilitokana na mtazamo wake bila kufanya utafiti wa kutosha.

Angefanya utafiti wa kutosha asingeandika ujamaa. Kwa sababu hakuna kitu kinachoitwa ushoshalisti wa Kiafrika. Kuna ushoshalisti tu.

Na misingi aliyotumia kuandika au kujenga ujamaa sio misingi unique kwa Afrika peke yake. Hile ni misingi ya primitive life style. Hata wazungu walipokuwa katika primitive life style walisaidiana katika masuala mengi.

Hivyo basi ukiona waafrika wanasaidiana kuombana chumvi basi isifikiriwe kuwa wanaweza kutumia ushirikiano wao wa kuombana chumvi kutengeneza space ship rocket.
 
Umesikia yanatokea Marekani leo? hujaona wamekimbilia kuomba "chumvi" kwa mfalme? Unajua majuzi marekani imetoa checks kwa walipa kodi ili kuwasaidia chumvi? Ubepari umewashinda sasa wanajaribu ujamaa ingawa hawatakubali kamwe kuwa ujamaa unamvuto wake. Ubepari ni mzuri ukiwa tajiri, lakini ukiwa na umaskini.... Ujamaa still rocks!
 
Hapa duniani hakuna cha ubepari kamili wala ujamaa kamili. Yeyote atakayefuata mifumo hii strictly (sijui kiswahili chake) lazima atalosti. Muhimu ni kuchanganya na kuchukua mazuri ya kila mfumo katika mazingira na wakati muafaka.
 
Well and okay for those who think he was a failure. Ukwlini kuwa hakuna sera hata moja hapa duniani imeweza kuwa perfect 100%! Angalia jinsi Marekani inavyochechemea sasa hivi kiuchumi pamoja na kuwa ni bepari na bingwa wa soko huria!

NInachojaribu ni kufanya tathmini kujua ni vipi tulikuwa na mtu mmoja ambaye alikuwa na mawazo shupavu ya kujenga Taifa na maono/fikra kama hizo na kutaka kujua influence na drive yake vilitoka wapi?

GM umemzungumzia Kambona, lakini what did Kambona do apart from criticising Nyerere? alipokuwa kwenye exile, alishindwa nini kuwa mwanamapinduzi wa fikra na falsafa na kuwapa Watanzania mtazamo tofauti na ule wa Nyerere?

Inaelekea wengi waliopingana na Nyerere walipingana kwenye Utendaji na si ujenzi wa Fikra au Falsafa.

Kinachotisha n kusikitisha ni swali ambalo Mwanakijiji kaniwahi kuuliza hapa, je viongozi waliomfuatia, marais Mwinyi, Mkapa na Kikwete, walikuwa na mvuto gani au ushawishi gani katika ujenzi wa nchi na uongozi wao

Kikwete alisomea Uchumi, ni influence gani zimetumika kumjenga kuwa Kiongozi na hata kukimbilia urais? ni falsafa gani, fikra gani au mtazamo upi alionao katika kujenga Taifa na kuongoza?

Nyerere alikuwa na makosa yake na mapungufu kama binadamu mwingine yeyote. Lakini at least na huo Ujamaa ambao wengine wanauona sumu, alikuwa na blue print ya kulijenga Taifa lake kwa udi na vumba.

What happened after he left? don't we have creative thinkers, philosophers and historians who could carry the torch to move Tanzania to its destination?
 
Nyerere alichanganya madawa tu. Vitabu na falsafa yake ilitokana na mtazamo wake bila kufanya utafiti wa kutosha.

Angefanya utafiti wa kutosha asingeandika ujamaa. Kwa sababu hakuna kitu kinachoitwa ushoshalisti wa Kiafrika. Kuna ushoshalisti tu.

Na misingi aliyotumia kuandika au kujenga ujamaa sio misingi unique kwa Afrika peke yake. Hile ni misingi ya primitive life style. Hata wazungu walipokuwa katika primitive life style walisaidiana katika masuala mengi.

Hivyo basi ukiona waafrika wanasaidiana kuombana chumvi basi isifikiriwe kuwa wanaweza kutumia ushirikiano wao wa kuombana chumvi kutengeneza space ship rocket.

Zakumi,

Okay Nyerere alichanganya madawa akitaka kujenga uniqueness kwa Tanzania, je kuna kosa gani?

je kuna mfumo hata mmoja duniani wa kiuchumi au maisha ambao haunyofoi mambo kutoka sehemu mbalimbali na kujijengea taswira mpya?

Umesema dhana ya ushirikiano na umoja, je huoni kuwa mwanzo mkubwa wa jamii yenye afya na kuelewana ni kuwa na ushirikiano na kuheshimiana na ndipo kila mmoja anaweza kuwasilisha mawazo yake ya maendeleo na ni demokrasia na utashi binafsi wa kuungana kujenga hiyo space ship rocket au kukwepa umande na kushangaa matokeo ya waliohenya?

Nafikiri mtazamo wa wengi wetu ni kutaka kuona kinachopandwa leo kinavunwa juzi!

Kama kuna kitu nitampa sifa Nyerere ni kujaribu kujenga jamii na uchumi kwa kutumia falsafa, historia na masuala ya uchumi na jamii aliyojifunza maishani mwake na kutaka kuyaundia mfano wa pekee, african socialism and self reliance kinyume na wengine ambao badala ya kujenga jamii zenye nguvu, wamekimbilia kuhemea na kutegemea fikra na mawazo ya Mkoloni na mgeni kuwa mvuto wa kujenga nchi!
 
Well and okay for those who think he was a failure. Ukwlini kuwa hakuna sera hata moja hapa duniani imeweza kuwa perfect 100%! Angalia jinsi Marekani inavyochechemea sasa hivi kiuchumi pamoja na kuwa ni bepari na bingwa wa soko huria!

NInachojaribu ni kufanya tathmini kujua ni vipi tulikuwa na mtu mmoja ambaye alikuwa na mawazo shupavu ya kujenga Taifa na maono/fikra kama hizo na kutaka kujua influence na drive yake vilitoka wapi?

GM umemzungumzia Kambona, lakini what did Kambona do apart from criticising Nyerere? alipokuwa kwenye exile, alishindwa nini kuwa mwanamapinduzi wa fikra na falsafa na kuwapa Watanzania mtazamo tofauti na ule wa Nyerere?

Inaelekea wengi waliopingana na Nyerere walipingana kwenye Utendaji na si ujenzi wa Fikra au Falsafa.

Kinachotisha n kusikitisha ni swali ambalo Mwanakijiji kaniwahi kuuliza hapa, je viongozi waliomfuatia, marais Mwinyi, Mkapa na Kikwete, walikuwa na mvuto gani au ushawishi gani katika ujenzi wa nchi na uongozi wao

Kikwete alisomea Uchumi, ni influence gani zimetumika kumjenga kuwa Kiongozi na hata kukimbilia urais? ni falsafa gani, fikra gani au mtazamo upi alionao katika kujenga Taifa na kuongoza?

Nyerere alikuwa na makosa yake na mapungufu kama binadamu mwingine yeyote. Lakini at least na huo Ujamaa ambao wengine wanauona sumu, alikuwa na blue print ya kulijenga Taifa lake kwa udi na vumba.

What happened after he left? don't we have creative thinkers, philosophers and historians who could carry the torch to move Tanzania to its destination?

Hivi ni kitu gani aliandika kweli? Mwanafalsa sikuzote anaacha vitu ambavyo wengine wanachukua na kama wanashindwa kuchukua basi ulichoandika ni maoni yako tu.
 
Binafsi sidhani kama kuna mtu anayeweza kusema kwa uhakika Nyerere alipata wapi wazo la Ujamaa zaidi ya kwamba wakati huo somo kubwa lilikuwa ni kupambana na Ubepari ambao kwa kina ulikuwa ukilenga zaidi kutumia nchi maskini..

Sasa kama wewe ni mtu unayetaka mageuzi na hasa kuondokana na utumwa huo ni lazima uwe na mbinu ya kujikwamua ambayo kwanza itahitaji uwezo wako wewe kujitosheleza bila kumtegemea huyo tajiri..unajenga imani kwamba bila wewe huo Utajiri wake hauwezi kuwepo..toka hapo unaanza kujenga mbinu za kujikwamua na ni ktk kupitia elimu ndio unaweza kupata mbinu pingamizi..

Na kama tujuavyo Nyerere alikuwa mmoja kati ya wasomi wa Kiafrika wakati huo na nakumbuka zamani msomi yeyote aliweza kuwa msomi tu kwa kusoma vitabu vya kila aina. Ilikuwa ni moja ya show, umaarufu, celebrity na stunt zote zilichezwa kwa kusoma vitabu vya elimu tofauti na 70's ambapo vitabu vya crime fiction vilichukua nafasi na siku hizi vitabu vinavyouzwa zaidi ni hadithi za mapenzi..

Kwa hiyo siku hizi vijana wetu ni mahodari sana inapofikia swala la mapenzi, wanatoa stunts za Kamasutra kiasi kwamba sisi wazee inabidi tujiuliza hawa vijana elimu hiyo wameipata wapi?...Kwii... kwii.... kwii!

Mkuu Mkandara,

Tofauti kubwa ya Nyerere na wengine katika Afrika na hata dunia changa na nyumbani Tanzania ni kuwa Nyerere alikuwa mwanafunzi mzuri aliyejifunza kila kitu alichokutana nacho na kujijenga kimtazamo na kifikra na kuweza kuanzisha msukumo wa kuunda na kujenga Taifa ambalo linajitegemea na linatumia mbinu za medani kutoka sehemu mbali mbali kujijenga.

Tunajua kwenye Jeshi, tunajifunza kutoka kwa Wachina, Wamarekani, Wacanada, Waingereza, Wairaqi, Waisraeli na kwingine, swali ni kwa nini tulijifunza kutoka kwa wote hawa na si kujifunza kutoka kwa nchi na mfumo mmoja?

I think I will stand tall to state Nyerere was ahead of his time to think outside the box and piece together multiple principles, ideologies and philosophy to formulate and create one unique identity and philosophy for Tanzania.
 
Zakumi,

Okay Nyerere alichanganya madawa akitaka kujenga uniqueness kwa Tanzania, je kuna kosa gani?

je kuna mfumo hata mmoja duniani wa kiuchumi au maisha ambao haunyofoi mambo kutoka sehemu mbalimbali na kujijengea taswira mpya?

Umesema dhana ya ushirikiano na umoja, je huoni kuwa mwanzo mkubwa wa jamii yenye afya na kuelewana ni kuwa na ushirikiano na kuheshimiana na ndipo kila mmoja anaweza kuwasilisha mawazo yake ya maendeleo na ni demokrasia na utashi binafsi wa kuungana kujenga hiyo space ship rocket au kukwepa umande na kushangaa matokeo ya waliohenya?

Nafikiri mtazamo wa wengi wetu ni kutaka kuona kinachopandwa leo kinavunwa juzi!

Kama kuna kitu nitampa sifa Nyerere ni kujaribu kujenga jamii na uchumi kwa kutumia falsafa, historia na masuala ya uchumi na jamii aliyojifunza maishani mwake na kutaka kuyaundia mfano wa pekee, african socialism and self reliance kinyume na wengine ambao badala ya kujenga jamii zenye nguvu, wamekimbilia kuhemea na kutegemea fikra na mawazo ya Mkoloni na mgeni kuwa mvuto wa kujenga nchi!

Makosa makubwa yaliofanyika ni kuwa nchi nyingi za kiAfrica zilikuwa ni maeneo ya kijiografia tu. Na ndani ya nchi watu walikuwa na tofauti kubwa baina yao.

Ukoloni ulitufanya tuungane na kushirikiana kudai uhuru lakini ushirikiano huo ulikuwa superficial tu kwa sababu makabila na jamii mbalimbali zilikuwa na interests na mazingira tofauti.

Africa ni eneo la kijiografia. Lakini waafrika wenyewe wanatofauti kubwa miongoni mwao. Na unaposema UJAMAA kuwa ushoshalisti wa Kiafrika, je umeangalia tofauti za waafrika au umeaangalia eneo la kijiografia.

Kama unaangalia eneo la kijiografia basi siasa zako zitashindwa tu kwa sababu ya diversity ya interests ya wakazi wa eneo hili. Na kama unaangalia watu basi ni lazima uangalie interests zao na siasa ziwe customized hili ziendane na interests za watu.

Kitabu kimoja kisitumike kumuongoza mmakonde na mmasai ingawaje wote wako katika eneo moja la kijiografia.
 
Hivi ni kitu gani aliandika kweli? Mwanafalsa sikuzote anaacha vitu ambavyo wengine wanachukua na kama wanashindwa kuchukua basi ulichoandika ni maoni yako tu.

Umeshajiuliza ni kwa nini Watanzania wamekunywa KoolAid ya Ujamaa na kuipenda CCM kiasi kuwa imekuwa ni vigumu kuachana na Ujamaa?

Ndio bado hatujaweza kujitegemea ambalo ni upande wa pili wa ujamaa, lakini ile dhana iliyotuletea ujamaa na hata Watanzania kunufaika na Ujamaa na makali yake kiuchumi, ni sababu tosha kusema kuwa asilimia kubwa ya Watanzania walifuata fikra na wameshika falsafa za Nyerere na inawawia vigumu kuachana nazo kwa kuwa hakuna fikra, sera au falsafa mpya hata za kumpinga Nyerere ambazo zinaonekana zinawezza kufanya kazi.

Azimio la Zanzibar na hata mfumo wa soko huria tukiuchukulia kuwa ndio mfumo mpya wa kujenga Taifa letu, bado haujaweza kuuzika machoni mwa wananchi.

Wanaonufaika na mfumo huu mpya ni wale wale viongozi ambao waliwekewa masharti ya uongozi kudhibiti utumiaji wa nafasi zao kujilimbikizia mali.

Sehemu kubwa ya wanaosadikika kuwa ni Upper na middle class wa Tanzania ni Wanasiasa na kwa nyuma wanafuata wafanyabiashara na watendaji wachache katika taasisi, mashirika na makampuni.

Asilimia kubwa ya Watanzania bado wako watika lower class, masikini mpaka masikini wa kupindukia. Na uwiano na kugawanyika kwa takwimu hizi zimeongezeka sana baada ya Azimio la Arusha kwa lile tabaka la kati (middle class0 kupoteza sura na kuegemea kwenye tabaka la chini (lower class).

Leo hii, shibe ya Ujamaa inamfanya Mtanzania aendelee kung'ang'ania apate huduma bure. Je kutoa huduma bure ilikuwa jambo sahihi? majibu ni ndiyo na hapana kwa wakati tulipoanza kutoa huduma za afya na elimu bure.

Je nyakati hizi na mfumo wetu mpya, kutoa elimu na huduma za afya bure bila Mtanzania kuchangia japo kwa kiwango fulani kunawezekana, jibu ni moja, hapana!

Mfumo wetu na falsafa za sasa hivi za jiachieni,zimesababisha Taifa kukosa dira na mwelekeo hata msukumo wa kujitegemea kiuchumi.

Uongozi wetu umekimbilia mfumo mpya wa uchumi kwa kutafuta njia rahisi kujipatia kipato kama kuomba misaada na kukwepa kuwa wachapa kazi na wabunifu kujinusuru na kufufua yaliyoharibiwa na "Ujamaa"!

Leo kila sekta inauzwa kwa mgeni mwenye pesa, leo kila hitaji mpaka chakula tunakimbilia kuagiza na si kukaa chini na kujitengezea na kujizalishia.

Kwa mtaji huo, nitakuwambis wazi tena ni heri mfumo tulioukimbia wa Ujamaa ambao japo watu walihhamasishwa na kufundishwa kujitegemea na kilichokosekana nyakati zile ni mtaji mahiri wa kulitosheleza Taifa changa kujitegemea.
 
Makosa makubwa yaliofanyika ni kuwa nchi nyingi za kiAfrica zilikuwa ni maeneo ya kijiografia tu. Na ndani ya nchi watu walikuwa na tofauti kubwa baina yao.

Ukoloni ulitufanya tuungane na kushirikiana kudai uhuru lakini ushirikiano huo ulikuwa superficial tu kwa sababu makabila na jamii mbalimbali zilikuwa na interests na mazingira tofauti.

Africa ni eneo la kijiografia. Lakini waafrika wenyewe wanatofauti kubwa miongoni mwao. Na unaposema UJAMAA kuwa ushoshalisti wa Kiafrika, je umeangalia tofauti za waafrika au umeaangalia eneo la kijiografia.

Kama unaangalia eneo la kijiografia basi siasa zako zitashindwa tu kwa sababu ya diversity ya interests ya wakazi wa eneo hili. Na kama unaangalia watu basi ni lazima uangalie interests zao na siasa ziwe customized hili ziendane na interests za watu.

Kitabu kimoja kisitumike kumuongoza mmakonde na mmasai ingawaje wote wako katika eneo moja la kijiografia.

Mbona Wamarekani na Waingereza na mabepari wote wameweza kutumia kitabu kimoja na kushikamana na kujenga jamii moja pamoja na tofauti zao za asili, kiitikadi na kifikra?

Why is it so complex when it comes to Africa and we always run to claim traditional differences as a cause of instability intead of creating a unifying environment and share common values?
 
Umesikia yanatokea Marekani leo? hujaona wamekimbilia kuomba "chumvi" kwa mfalme? Unajua majuzi marekani imetoa checks kwa walipa kodi ili kuwasaidia chumvi? Ubepari umewashinda sasa wanajaribu ujamaa ingawa hawatakubali kamwe kuwa ujamaa unamvuto wake. Ubepari ni mzuri ukiwa tajiri, lakini ukiwa na umaskini.... Ujamaa still rocks!

Mwanakijiji:

Kuna kitu ambacho nchi nyingi zilizoendelea wamekubaliana nacho lakini hawataki kusema. Kwao sasa umuhimu zaidi ni ubora wa maisha na sio siasa za kuongoza nchi.

Kama sera za serikali zinaweza kumpa mwananchi wa chini sehemu ya kulala, chakula na vitu vingine vya lazima kwanini wa-CLING kwenye total ubepari au total ujamaa?
 
unachosema ni kuwa mfumo wowote wa maisha ambao utayainua maisha ya mtu na kumtimizia mahitaji yake muhimu unapaswa kukubaliwa na jamii hiyo. Ndiyo maana China kuna Ukomunisti na wananchi wake wanaanza kula matunda ya mfumo huo. Na Russia inaelekea huko huko, Nordic kuna socialism na wanaenda hivyo hivyo; Spaina wanatawaliwa na ujamaa, so is Venezuela, and so is Vietnam... Ujamaa haujafa na ninaamini TZ tutaurudia in one shape or form..
 
Mwanakijiji:

Kuna kitu ambacho nchi nyingi zilizoendelea wamekubaliana nacho lakini hawataki kusema. Kwao sasa umuhimu zaidi ni ubora wa maisha na sio siasa za kuongoza nchi.

Kama sera za serikali zinaweza kumpa mwananchi wa chini sehemu ya kulala, chakula na vitu vingine vya lazima kwanini wa-CLING kwenye total ubepari au total ujamaa?

Zakumi,

Nyerere alikuwa mjamaa na alisema kuwa Ujamaa ni Imani na ni watu. Alileta mfumo wa ujamaa akiamini ni njia ya kujenga taifa linalojitegemea.

Wamarekani walisema ubepari ndio njia pekee ya mafanikio na maendeleo, wakaruhusu soko huria na watu kujifanyia wanavyotaka.

Sasa common denominator hapa ni hizo unazosema, chakula, paa na afya, sisi Tanzania tulipokuwa na sera za kutoa afya na elimu bure, tulikoromewa kwa ni makosa makubwa.

Kweli ilikuwa makosa makubwa kwa kuwa hatukuwa na mtaji wa kutosha, lakini ili kuwa ni wajibu wa Serikali kuhakikisha kuwa kila mtu anapata furs ya kusoma na kuwa na afya njema.

Marekani, elimu ya msingi na sekondari ni bure, afya pamoja na kuwa kila mtu anahitaji bima, bado kama huna bima unaweza kwenda tibiwa hospitali bure.

Swali ni kwa nini iwe sawa kwa Marekani kuwa na elimu bure na hata huduma za afya bure lakini iwe ni sumu kwa Tanzania? tutang'ang'ania kuwa Tanzania haikuwa na mtaji wa kutosha? je kujenga nchi na taifa tukiwa na watu wenye siha bora na elimu tungefanikiwa vipi kama tungesema kila mtu alipie ili kunusuru viwanda na kujijenge utajiri?
 
Nyerere alichanganya madawa tu. Vitabu na falsafa yake ilitokana na mtazamo wake bila kufanya utafiti wa kutosha. Angefanya utafiti wa kutosha asingeandika ujamaa...

Haya madai yako ambayo sina uhakika ni kwa kiwango gani na yenyewe yamejikita katika utafiti yamenikumbusha mchango ufuatao niliowahi kuutoa kwenye mada fulani - hebu tufanye utafiti wa kina kuhusu historia yetu maana kuna Watanganyika wengi tu walikuwa Wajamaa katika miaka ya 60 tena walijiunga pamoja kuanzisha vijiji vya Ujamaa na Kujitegemea vya mfano kabla hata ya Nyerere hajawatafiti na kudesa Ujamaa wao:

...Yule mwanasiasa mahiri wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere, alilitambua hilo. Pamoja na kuwa na taaluma ya ualimu bado aliona ni vyema ampeleke msaidizi wake, Joan Wicken, katika Kijiji cha Ujamaa Litowa ili ajifunze namna ya kuendesha shule ya msingi inayojitegemea. Shule hiyo ilikuwa imeanzishwa na wanakijiji wenyewe ambao baada ya kujifunza hali na mahitaji ya mazingira yao walijiundia mfumo wao wenyewe wa elimu unaokidhi hali na mahitaji yao halisi.

Baada ya Joan Wicken kutoa mrejesho wa uzoefu wake huko, Mwalimu Nyerere aliunda sera ya ‘Elimu ya Kujitegemea’. Inasemekana kuwa kwa kiasi kikubwa sera hii ilitokana na taaluma asilia ambayo Joan aliipata katika Shule ya Msingi ya Litowa. Pamoja na mapungufu yake, hii ilikuwa ni jitihada ya aina yake ya kuoanisha maamuzi ya kisiasa na maamuzi ya kitaaluma...
 
Komredi, hivi ni watu wangapi waliuawa na simba na wanyama wakali wakati wa operesheni ya ujenzi wa vijiji vya ujamaa? Nimekuwa nikitafuta kweli mtu wa kunisaidia kujibu swali hilo, inaonekana unaweza kuwa unajua au clue ya jibu lake.
 
Mkuu Mkandara,

Tofauti kubwa ya Nyerere na wengine katika Afrika na hata dunia changa na nyumbani Tanzania ni kuwa Nyerere alikuwa mwanafunzi mzuri aliyejifunza kila kitu alichokutana nacho na kujijenga kimtazamo na kifikra na kuweza kuanzisha msukumo wa kuunda na kujenga Taifa ambalo linajitegemea na linatumia mbinu za medani kutoka sehemu mbali mbali kujijenga.
Tunajua kwenye Jeshi, tunajifunza kutoka kwa Wachina, Wamarekani, Wacanada, Waingereza, Wairaqi, Waisraeli na kwingine, swali ni kwa nini tulijifunza kutoka kwa wote hawa na si kujifunza kutoka kwa nchi na mfumo mmoja?

I think I will stand tall to state Nyerere was ahead of his time to think outside the box and piece together multiple principles, ideologies and philosophy to formulate and create one unique identity and philosophy for Tanzania.
Nakubaliana na wewe alikuwa mwanafunzi mzuri na alichukua mawazo tofauti na kuweka la kwake (At least alikuwa na mwongozo ambao alitaka kuufuata tofauti na viongozi wetu wa sasa ambao ni bora liende). Lakini tatizo lake alipochukua madaraka hakutaka kusikiliza mtu, yaani ni his way or no way, yaani hakutaka kusikiliza mtu, kwa hapo hakuwa tena mwanafunzi na wakati watu hata walimu inabidi unavyoendelea kuishi unajifunza kutoka kwa watu wengine na kusikiliza mawazo ya watu wengine. Tanzania haikuendelea kama alivyotaka kwa sababu alikuwa hasikilizi mawazo ya watu waliokuwa tofauti na yeye, alipenda watu waliokuwa wanamsikiliza tuu "yes sir" na sio waliokuwa wana mawazo tofauti na yeye na hilo lilikuwa tatizo lake.
 
Nakubaliana na wewe alikuwa mwanafunzi mzuri na alichukua mawazo tofauti na kuweka la kwake (At least alikuwa na mwongozo ambao alitaka kuufuata tofauti na viongozi wetu wa sasa ambao ni bora liende). Lakini tatizo lake alipochukua madaraka hakutaka kusikiliza mtu, yaani ni his way or no way, yaani hakutaka kusikiliza mtu, kwa hapo hakuwa tena mwanafunzi na wakati watu hata walimu inabidi unavyoendelea kuishi unajifunza kutoka kwa watu wengine na kusikiliza mawazo ya watu wengine. Tanzania haikuendelea kama alivyotaka kwa sababu alikuwa hasikilizi mawazo ya watu waliokuwa tofauti na yeye, alipenda watu waliokuwa wanamsikiliza tuu "yes sir" na sio waliokuwa wana mawazo tofauti na yeye na hilo lilikuwa tatizo lake.

Najua hapa tunaongelea falsafa na influence ya kuleta Ujamaa na azimio, lakini tukiteleza na kujiuliza, je utamaduni wa "haambiliki" alijifunza kwa nani hatuoni kuwa tunaukuta kwa kila Rais wa dunia hii?

Je dhana yake ya kujenga nchi na imani ya binadamu sawa na kupiga vita ukandamizaji ilikosea njia na kusahau kufafanua dola na utawala na hivyo kumfanya ajiunge namarais waliomtangulia na walimfuata duniani kote kuwa Ma-Alfa na Omega?

Maana hata Bush na Blair walikuwa ni haambiliki, Gordon Brown na Hugo Chavez ni haambiliko, Olmert amekuwa haambiliki mpaka kashinikizwa kubwaga manyanga.

Je Kutoambilika ni kasumba ya viongozi na watawala na si Julius wa Nyerere pekee?
 
Nakubaliana na wewe alikuwa mwanafunzi mzuri na alichukua mawazo tofauti na kuweka la kwake (At least alikuwa na mwongozo ambao alitaka kuufuata tofauti na viongozi wetu wa sasa ambao ni bora liende). Lakini tatizo lake alipochukua madaraka hakutaka kusikiliza mtu, yaani ni his way or no way, yaani hakutaka kusikiliza mtu, kwa hapo hakuwa tena mwanafunzi na wakati watu hata walimu inabidi unavyoendelea kuishi unajifunza kutoka kwa watu wengine na kusikiliza mawazo ya watu wengine. Tanzania haikuendelea kama alivyotaka kwa sababu alikuwa hasikilizi mawazo ya watu waliokuwa tofauti na yeye, alipenda watu waliokuwa wanamsikiliza tuu "yes sir" na sio waliokuwa wana mawazo tofauti na yeye na hilo lilikuwa tatizo lake.

Lusajo, haitoshi mtu kuwa na mawazo tofauti tu ili asikilizwe, ni lazima awe na hoja yenye nguvu kushinda hoja iliyopo. Yeye mwenyewe alisema hivi "mtu mwenye akili akija na kukushauri kitu cha kipumbavu akijua na wewe una akili (kwamba utakiona ni cha kipumbavu) na wewe ukakubali atakudharau".

Nikiangalia baadhi ya watoa hoja humu na watu ambao tunajadiliana nao humu na kuwaweka hao kwenye utawala wa Mwalimu na kuwaambia watoea ushauri kwa Mwalimu na wakatoa jinsi wanavyotoa humu sitoshangaa kwanini ilikuwa ni vigumu kumshauri lolote.

Na kama mawazo ya namna hii ndiyo yanayotolewa kwa Kikwete sishangai kwanini tunaona hamsikilizi mtu yeyote kwa sababu kama hoja zinatolewa au zinapangwa zinavyopangwa hapa basi tuna matatizo makubwa zaidi kuliko uongozi mbaya.

Well, ninachotaka kusema ni kuwa Nyerere hakulazimika kukubali mawazo tofauti, alitakiwa kukubali mawazo yenye hoja tofauti na kubwa kuliko hoja zake. So far, sijasikia hoja iliyowahi kutolewa na kumshawishi Mwalimu aachane na hoja yake ya awali labda mara chache sana.
 
Nakubaliana na wewe alikuwa mwanafunzi mzuri na alichukua mawazo tofauti na kuweka la kwake (At least alikuwa na mwongozo ambao alitaka kuufuata tofauti na viongozi wetu wa sasa ambao ni bora liende). Lakini tatizo lake alipochukua madaraka hakutaka kusikiliza mtu, yaani ni his way or no way, yaani hakutaka kusikiliza mtu, kwa hapo hakuwa tena mwanafunzi na wakati watu hata walimu inabidi unavyoendelea kuishi unajifunza kutoka kwa watu wengine na kusikiliza mawazo ya watu wengine. Tanzania haikuendelea kama alivyotaka kwa sababu alikuwa hasikilizi mawazo ya watu waliokuwa tofauti na yeye, alipenda watu waliokuwa wanamsikiliza tuu "yes sir" na sio waliokuwa wana mawazo tofauti na yeye na hilo lilikuwa tatizo lake.

Lusajo, mwongozo wenyewe ulikuwa na matiki nzuri tu ambayo Watanzania wengi tuliiunga mkono.
 
Komredi, hivi ni watu wangapi waliuawa na simba na wanyama wakali wakati wa operesheni ya ujenzi wa vijiji vya ujamaa? Nimekuwa nikitafuta kweli mtu wa kunisaidia kujibu swali hilo, inaonekana unaweza kuwa unajua au clue ya jibu lake.

Mwanakijiji sidhani kama kuna utafiti wa kina ambao ulifanywa enzi hizo kuonesha ni watu wangapi waliuawa na simba na wanyama wakali. Kumbuka huo ni mwanzo wa enzi za Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 - [media]http://www.parliament.go.tz/Polis/PAMS/Docs/3-1976.pdf[/media] - ambayo ilipiga marufuku machapisho mengi tu hivyo labda watafiti wetu walihofu kwenda kutafiti hayo masuala ya vifo na mauaji. Pamoja na hayo riwaya nyingi, kama vile 'Njozi Iliyopotea' cha Claude Mung'ong'o na 'Sudi ya Yohana' cha Seti Chachage vilivyoandikwa kwenye miaka ya mwanzo ya 80, vinazungumzia sana ufisadi waliofanyiwa watu waliohamishwa kwa nguvu kwenye vijiji vya Ujamaa. Pia Tafiti zilizofanywa na wanazuoni kutoka nje, kama vile Michaela Von Freyhold (1979) katika kitabu chake cha 'Ujamaa Villages in Tanzania: Analysis of a Social Experiment' na Jean M. Due (1980) katika kitabu chake cha 'Costs, Returns and Repayment Experience of Ujamaa Villages in Tanzania, 1973-1976', vinaelezea matatizo waliyoyapata watu wakati wa operesheni sogeza hiyo ya Vijiji vya Ujamaa. Nakushauri ufanye utafiti wa mahojiano kuhusu hilo suala na ukianza unitaarifu nikupe anuani ya dada mmoja ambaye mtoto wa jirani yao alikufa kwa homa ya mapafu kwa sababu walilala/walilazwa nje wakati wanahamishiwa kwenye kijiji cha Ujamaa - yaani mambo ya kuhamishana ovyo ovyo yalikuwa kama ya kule Afrika Kusini wakati wa Utawala wa Kibaguzi wa Kikaburu! Pamoja na hayo yote daima tukumbuke kuwa Ujamaa ulianza kama jambo la hiari na watu wenyewe walianza kujumuika kabla hata Nyerere hajaanza kuwahimiza. Hakika mambo yaliharibika pale warasimu wa serikali yetu walipoamua kutufanya tukimbie na kukimbizana wakati wengine wanatembea!Kweli historia yetu bado haijaandikwa kikamilifu!Ole wao wanaoisahau historia yao!
 
Back
Top Bottom