Who influenced Nyerere: His Ujamaa Philosophy and Azimio Principles?

Sio kweli.

Kulikuwa kuna sababu kwa nini J.K. Nyerere alitaka tuimbe "Zidumu fikra za Mwenyekiti..." Maana yake fikra zingine hazikaribishwi.

Hadithi za kina Mzee Bomani ni historia potofu ambazo anaweza kuhadithia wasioelewa kilichojiri tu. Ukimuuliza Mzee Bomani maoni yake kuhusu Nyerere ni kumpelekea ngedere kesi ya nyani. Hawa wote ndio watendaji, "ndio-mzee," chinja-chinja wa kisiasa na kimatendo katika mkoba wa vifaa vya J.K. Nyerere.

Na, hata kusema J.K. Nyerere haambiliki ni kupendezesha lugha tu. J.K. Nyerere alikuwa nduli wa mawazo, kama sio nduli. Alitumia dola kushughulikia waliotofautiana nae (4). Aliyethubutu kubisha aidha alifungiwa kijijini ( Balozi Kassanga Tumbo (1) au jela (Chief Justice Wolfango Dourado ( 3 ), Abdallah Said Fundikira, Mwinyijuma Othuman Upindo, na James Mapalala (2), kufukuzishwa nchini (Waziri Kambona), kufukuzwa kazi (Rais Jumbe) na orodha inaendelea na kuendelea na kuendelea....(Kassim Hanga, Makamu wa Rais wa Zanzibar, na walinzi wake; Waziri Abdulrahman Mohamed Babu (5), na Wabunge Joseph Kasela Bantu na Mbunge Eli Anangisye, aliyekamatwa na kufungwa bila mashitaka baada ya kuchangia mjadala wa kikao cha Bajeti Bungeni, 1968 ( 6).

Kusema J.K. Nyerere alikuwa ana hoja kali sana kiasi kwamba hakukuwa na wengi wanaoweza kujadiliana nae ni kituko kwa sababu inamaanisha watu wote walikuwa watupu ila Nyerere na wachache fulani. Huku ni kupumbazika kulikotokana na kuleweshwa propaganda. Toka mdogo unaimbishwa nyimbo:

"Kambona, kaolewa!
Wapi? Huko Ulaya

Kambona, kaolewa!
Wapi? Huko Ulaya

Na nani ? Waingereza"


Ni lazima upumbazike. Hata mimi utotoni nilipumbazika. Kuja ukubwani nakuja kuambiwa eti Kambona alilazimika kuingia mitini kwa sababu alitofautiana mawazo ya mfumo wa kiuchumi. Hebu angalia hilo ndugu yangu. Sio nduli wa mawazo huyo J.K. Nyerere? Binadamu kweli unamfunga Jaji Mkuu mstaafu wa Zanzibar kwa sababu ametoa hotuba kama mgeni mwalikwa kwenye mkutano wa Tanganyika Law Society kujadili kuboresha na kubadili Katiba! (3) Huyu Muasisi Marehemu J.K. Nyerere utasema kweli sio nduli wa mawazo? Eti, "ilibidi ujenge hoja barabara." Ukipumbazwa unaweza kuamini ya ajabu!

Rev. Kishoka, kama nimetoka nje ya mada ni katika kurekebisha historia inayopotoshwa hapa. Nina marafiki mababa zao wameuawa baada ya kuugulia kwenye vyumba vya giza Oysterbay Polisi baada ya kuswekwa miaka bila mashitaka. Umenikamata nishitaki, usiniweke niugue kisukari na magonjwa ya moyo kwenye chumba cha giza polisi, nikitoka nakaa kidogo nakufa!

( 1 ) The Standard (Tanganyika), 28 Sept. 1962.

( 2 ) Chris Maina Peter; A Comparative Study of the African Human and People's Rights Charter and the New Tanzanian Bill of Rights 31 (Studies in Human Rights No. 10, Consortium on Human Rights Development, University of Denver 1990).

( 3) Ahmed Rajab, Foul Play, Afr. Events, Nov. 1985, at 28.

(4) Chris Maina Peter; Incarcerating the Innocent: Preventive Detention in Tanzania; 1997 The Johns Hopkins University Press, Human Rights Quarterly 19.1 (1997) 113-135


(5 ) H.G. Mwakyembe, Issa G. Shivji; The Parliament and the Electoral Process, in The State and the Working People in Tanzania; 1986 Colin Leys, Tanganyika: The Realities of Independence, in Socialism in Tanzania 187 (East African Publishing House Political Studies 14, Lionel Cliffe & John S. Saul eds., 1972).

(6) Ludovick S Mwijage, The dark side of Nyerere's Legacy; Raymond F. Hopkins, The role of an MP, Swarthmore College

Hivi Nyerere aliwahi kuwataka watu kuimba zidumu fikra zake? Hilo tamko au agizo alilitoa wapi na lini na kwa njia gani i.e. hotuba, memo, sheria ya bunge...?
 
Hivi Nyerere aliwahi kuwataka watu kuimba zidumu fikra zake? Hilo tamko au agizo alilitoa wapi na lini na kwa njia gani i.e. hotuba, memo, sheria ya bunge...?
kama alikuwa hataki si angekataza watu kusema hivyo. tatizo nadhani jamaa alikuwa anapenda watu wanaomwambia "yes sir". Huitaji kuwa Rocket scientists kuelewa hilo.
 
mimi mpaka sasa bado sijaona makosa aliyoyafanya na hasa ukizingatia wakati huo nchi ilikuwa ni changa sana ila kinachonishangaza ni watu kuendelea kulaumu tu.lakini swali linakuja je wakati wa utawala wa mwalimu na utawala uliopo sasa ni upi wenye muelekeo? maana ninapotizama tanzania inakoelekea naona ni gizani?sasa nyie wana jf mnaojifanya mabingwa wa kuchambua na kukandia yale yote aliyofanya nyerere nawaona ni wenda wazimu.maana mngejiuliza kitu kimoja tu JE NI NINI SERA YA MAENDELEO YA NCHI KWA SASA? je baada ya miaka kumi tanzania itakuwaje.nafikiri baada ya miaka kumi tanzania itakuwa ni giza totoro
 
Mzee Mwanakijiji au mwana-jamii yeyote anayemfahamu Mwalimu naomba mniambie kwamba nani alikuwa anamshauri katika mambo yake? kwa sababu hata kama mtu una vision lazima uwe na washauri au kama alikuwa anakwenda na vision yake peke yake. Ni kweli ilibidi watu wam-convice na waende na strong plan ya kum-convice, what if he was hard head yaani alikuwa hamsikilizi mtu? kwa sababu hata wewe unajua kuna watu huku JF ambao hata uwaambiaje hawakubaliani na wewe!. Kwa hiyo hata ukimuambia nini at the end yeye ndiye Raisi na ndio anaamua cha mwisho kwa hiyo sijui kama alikuwa anawasikiliza hao watu au hawasikilizi, na ni kina nani aliokuwa anawasikiliza.
Na haikuwa lazima Nyerere kukubaliana na mawazo ambayo yalikuwa tofauti kabisaa, ila kama alikuwa anasikiliza hata hoja za kuboresha alichokuwa anakifanya yaani Ujamaa. Mimi naona ndio maana hata na Kwame N hawakuelewana kwa sababu ilikuwa ni vigumu sana kumshauri au kumbadili mawazo kwa sababu alikuwa sio mtu wa kubadilika (yaani anachofikiri yeye ndio uamuzi wa mwisho) haya ni mawazo yangu tu.

Sajo,

Kwa niliyoyasikia na kuyafahamu, kuna watu watatu tuu ambao walikuwa washauri wa na wasaidizi wa Nyerere (watendaji) ambao walikuwa wakiweza kusimama kidete na kubangua mada na Kifimbo. Edward Sokoine, Cleopa Msuya na John Malecela.

Wengine sijui kama walikuwa na ubavu kama Jasusi alivyoeleza kutoa hoja za msingi kwa Mwalimu.

Ukiangalia kwa kina wale waliokimbilia kuua Azimio la Arusha na kulikumbatia Azimio la Zanzibar na kuchangua ni wapi na kina nani walifanya kazi chini ya Mwalimu, utagundua kuwa katika CCM kwa ukubwa walikuwa ni wanafiki na ni wachache sana walikuwa wakweli na kuweza kum-face Mwalimu kwa jambo lolote.

Haya ni maoni yangu kwa mtazamo wangu na natumaini ukiongeza watu kama Kaduma, Msekwa, Sefu Hamad, Salim, Warioba na hata Kolimba, hawa wanaweza kuwa walikuwa na uwezo wa kuongea na Mwalimu bila shida.
 
kama alikuwa hataki si angekataza watu kusema hivyo. tatizo nadhani jamaa alikuwa anapenda watu wanaomwambia "yes sir". Huitaji kuwa Rocket scientists kuelewa hilo.

Ok, kuna ushahidi wa kwamba aliwataka watu? Na kuna ushahidi kwamba hakuwakataza watu? Na kama watu walijiamulia kuimba hizo nyimbo au ngonjera kwa nini alaumiwe Nyerere? Hivi ni yeye pia aliyewataka watu kumwita baba wa taifa?
 
Sajo,

Kwa niliyoyasikia na kuyafahamu, kuna watu watatu tuu ambao walikuwa washauri wa na wasaidizi wa Nyerere (watendaji) ambao walikuwa wakiweza kusimama kidete na kubangua mada na Kifimbo. Edward Sokoine, Cleopa Msuya na John Malecela.

Wengine sijui kama walikuwa na ubavu kama Jasusi alivyoeleza kutoa hoja za msingi kwa Mwalimu.

Ukiangalia kwa kina wale waliokimbilia kuua Azimio la Arusha na kulikumbatia Azimio la Zanzibar na kuchangua ni wapi na kina nani walifanya kazi chini ya Mwalimu, utagundua kuwa katika CCM kwa ukubwa walikuwa ni wanafiki na ni wachache sana walikuwa wakweli na kuweza kum-face Mwalimu kwa jambo lolote.

Haya ni maoni yangu kwa mtazamo wangu na natumaini ukiongeza watu kama Kaduma, Msekwa, Sefu Hamad, Salim, Warioba na hata Kolimba, hawa wanaweza kuwa walikuwa na uwezo wa kuongea na Mwalimu bila shida.

Kuna mengi mno tunayoyasikia kuhusu Nyerere and therein lies the "myth"......
 
Suala la mapungufu ya Nyerere sikutaka kulifanya liwe ndio msingi mkuu wa mjadala huu.

Mjadala huu ulikuwa ni kujua ni wapi Nyerere alipata mawazo na mwamko wa kutuletea Ujamaa na hata Azimio la Arusha.

Najua kuna thread nyingine ambayo ilishawahi kuanzishwa kuhusu mapungufu, basi tuende kule kulalamikia mapungufu yake.
 
Sio kweli.

Kulikuwa kuna sababu kwa nini J.K. Nyerere alitaka tuimbe "Zidumu fikra za Mwenyekiti..." Maana yake fikra zingine hazikaribishwi.

Hadithi za kina Mzee Bomani ni historia potofu ambazo anaweza kuhadithia wasioelewa kilichojiri tu. Ukimuuliza Mzee Bomani maoni yake kuhusu Nyerere ni kumpelekea ngedere kesi ya nyani. Hawa wote ndio watendaji, "ndio-mzee," chinja-chinja wa kisiasa na kimatendo katika mkoba wa vifaa vya J.K. Nyerere.

Na, hata kusema J.K. Nyerere haambiliki ni kupendezesha lugha tu. J.K. Nyerere alikuwa nduli wa mawazo, kama sio nduli. Alitumia dola kushughulikia waliotofautiana nae (4). Aliyethubutu kubisha aidha alifungiwa kijijini ( Balozi Kassanga Tumbo (1) au jela (Chief Justice Wolfango Dourado ( 3 ), Abdallah Said Fundikira, Mwinyijuma Othuman Upindo, na James Mapalala (2), kufukuzishwa nchini (Waziri Kambona), kufukuzwa kazi (Rais Jumbe) na orodha inaendelea na kuendelea na kuendelea....(Kassim Hanga, Makamu wa Rais wa Zanzibar, na walinzi wake; Waziri Abdulrahman Mohamed Babu (5), na Wabunge Joseph Kasela Bantu na Mbunge Eli Anangisye, aliyekamatwa na kufungwa bila mashitaka baada ya kuchangia mjadala wa kikao cha Bajeti Bungeni, 1968 ( 6).

Kusema J.K. Nyerere alikuwa ana hoja kali sana kiasi kwamba hakukuwa na wengi wanaoweza kujadiliana nae ni kituko kwa sababu inamaanisha watu wote walikuwa watupu ila Nyerere na wachache fulani. Huku ni kupumbazika kulikotokana na kuleweshwa propaganda. Toka mdogo unaimbishwa nyimbo:

"Kambona, kaolewa!
Wapi? Huko Ulaya

Kambona, kaolewa!
Wapi? Huko Ulaya

Na nani ? Waingereza"


Ni lazima upumbazike. Hata mimi utotoni nilipumbazika. Kuja ukubwani nakuja kuambiwa eti Kambona alilazimika kuingia mitini kwa sababu alitofautiana mawazo ya mfumo wa kiuchumi. Hebu angalia hilo ndugu yangu. Sio nduli wa mawazo huyo J.K. Nyerere? Binadamu kweli unamfunga Jaji Mkuu mstaafu wa Zanzibar kwa sababu ametoa hotuba kama mgeni mwalikwa kwenye mkutano wa Tanganyika Law Society kujadili kuboresha na kubadili Katiba! (3) Huyu Muasisi Marehemu J.K. Nyerere utasema kweli sio nduli wa mawazo? Eti, "ilibidi ujenge hoja barabara." Ukipumbazwa unaweza kuamini ya ajabu!

Rev. Kishoka, kama nimetoka nje ya mada ni katika kurekebisha historia inayopotoshwa hapa. Nina marafiki mababa zao wameuawa baada ya kuugulia kwenye vyumba vya giza Oysterbay Polisi baada ya kuswekwa miaka bila mashitaka. Umenikamata nishitaki, usiniweke niugue kisukari na magonjwa ya moyo kwenye chumba cha giza polisi, nikitoka nakaa kidogo nakufa!

( 1 ) The Standard (Tanganyika), 28 Sept. 1962.

( 2 ) Chris Maina Peter; A Comparative Study of the African Human and People's Rights Charter and the New Tanzanian Bill of Rights 31 (Studies in Human Rights No. 10, Consortium on Human Rights Development, University of Denver 1990).

( 3) Ahmed Rajab, Foul Play, Afr. Events, Nov. 1985, at 28.

(4) Chris Maina Peter; Incarcerating the Innocent: Preventive Detention in Tanzania; 1997 The Johns Hopkins University Press, Human Rights Quarterly 19.1 (1997) 113-135


(5 ) H.G. Mwakyembe, Issa G. Shivji; The Parliament and the Electoral Process, in The State and the Working People in Tanzania; 1986 Colin Leys, Tanganyika: The Realities of Independence, in Socialism in Tanzania 187 (East African Publishing House Political Studies 14, Lionel Cliffe & John S. Saul eds., 1972).

(6) Ludovick S Mwijage, The dark side of Nyerere's Legacy; Raymond F. Hopkins, The role of an MP, Swarthmore College

hata MAO alikuwa haambiliki alipokuwa hai lakini baada ya kufa, leo wachina wote wamegeuka na kumfanya Mungu maana wanamuabudu kama sisi tunavyomuabudu Yesu tusiyemjua,Swali je ni yupi mzuri kati ya nyerere asiyeambilika na H .MWINYI au B. MKAPA AU JK wanaoambilika? 'shame on you'
 
Suala la mapungufu ya Nyerere sikutaka kulifanya liwe ndio msingi mkuu wa mjadala huu.

Mjadala huu ulikuwa ni kujua ni wapi Nyerere alipata mawazo na mwamko wa kutuletea Ujamaa na hata Azimio la Arusha.

Najua kuna thread nyingine ambayo ilishawahi kuanzishwa kuhusu mapungufu, basi tuende kule kulalamikia mapungufu yake.

You should know by now that any thread about Nyerere will take this kind of a detour....

For some reason it's hard for people to stay focused in this forum....
 
Kuna kitu kimoja ambacho Watanzania tunakifanya kwa ama ushabiki wa chuki kutokana na yaliyotusibu kwa namna moja au kwa kuishi kwenye mawazo na nchi ya kusadikika.

Nyerere tunamsema kuwa alituletea umasikini, alikuwa haambiliki, alikuwa akitesa watu na maneno mengine mengi kana kwamba Nyerere alikuwa ni Malaika mtakatifu ambaye asiye na mapungufu ya kiubinadmu kama wanadamu wengine.

Naomba kama kuna mmoja wetu mwenye ushahidi na kutupa mfano wa japo viongozi watano duniani hii ambao wamekuwa wakuu wa nchi ambao hawakuwahi kufanya maamuzi ambayo hayakuwafurahisha kila mtu, na atuletee hayo majina na mifano!
 
hata MAO alikuwa haambiliki alipokuwa hai lakini baada ya kufa, leo wachina wote wamegeuka na kumfanya Mungu maana wanamuabudu kama sisi tunavyomuabudu Yesu tusiyemjua,Swali je ni yupi mzuri kati ya nyerere asiyeambilika na H .MWINYI au B. MKAPA AU JK wanaoambilika? 'shame on you'
 
Suala la mapungufu ya Nyerere sikutaka kulifanya liwe ndio msingi mkuu wa mjadala huu.

Mjadala huu ulikuwa ni kujua ni wapi Nyerere alipata mawazo na mwamko wa kutuletea Ujamaa na hata Azimio la Arusha.

Najua kuna thread nyingine ambayo ilishawahi kuanzishwa kuhusu mapungufu, basi tuende kule kulalamikia mapungufu yake.

Mapungufu ya Nyerere sio mahala pake hapa; na mapambo ya Nyerere yasiyohusiana na Azimio la Arusha na vyanzo vya fikra zake? Hayo ni sawa, sio?

Tena mapambo ya kupotosha, ya uongo, hayo hayakataliwi? Nimeona wasifu wa uongo umejipenyeza nikapinga mapambio hayo, na nikijua ni mada nyingine, nikaeleza kwa nini nimeandika niliyoandika.

Sasa tukikataa yasiyohusika hapa tukatae yote, mapambio ya uongo na mapungufu ya Nyerere. Yote sio mahala paka.

Haya nawaacha na majadiliano yenu, al muradi yasisemwe ya uongo yasiyohusika, maana hatutaruhusu vizazi vya kesho kutwa vidhanie woooote tulikuwa bado tumepumbazika (hoodwinked ) na bunk za Nyerere, mpaka mwaka 2008.

(Kwanza nilichokiongelea hata hivyo kiko on point, kwamba Nyerere hakutaka kutofautiana na mtu. Kimewashtua kwamba nimeongelea jinsi alivyosweka watu ndani waliojaribu kutofautiana nae ? Come on guys!)
 
Hebu jaribu kufikiria kama yeye mwenyewe leo angekuwa hai na pia member humu ndani labda tungepata majibu mengi sana,lakini hayupo.
Kila mtu anakuja na tafsiri yake kuhusu mambo aliyoyafanya Mwalimu wakati wake.Lakini wengi tunakubaliana kuwa he had his countries interests in his heart,kwa sababu kama sio hivyo basi kuna mengi mengine zaidi ambayo angefanya,na sijui hapa tungekuwa tunasema nini sasa hivi.
Why Nyerere all the time? Kila siku mambo yanakwenda yanajirudia yaleyale,Nyerere kafunga watu,Nyerere fisadi,Nyerere haambiliki,Nyerere mkatili.....kweli jamani huu sio wakati wa kuweka vichwa vyetu na kuangalia matatizo ambayo tunayo sasa hivi.Fine Ujamaa failed,yeye mwenyewe ali admit,sasa ambacho tunacho sasa hivi in its stead ni bora?Watoto wanauza mali walizoachiwa na baba yao,then wanamlalamikia kuwa ni kosa lake. The country seems to have gone backwards,lakini bado tupo hapo kumlaumu mtu aliyetoka Madarakani miaka 23 iliyopita....only in Tanzania.Maana kuna watu humu wanasema hata JK katuletea Nyerere,wakati nyie wenyewe ndio mlienda kumpa 80% of the votes,na yeye mwenyewe aliwa warn kama mnapenda sura yake mkanywe nae chai.
Let the man rest in peace guys,na tujaze pages hapa with what we have infront of us for the good of our kids and theirs
 
Someni yote aliyoyaandika Mwalimu; sikilizeni hotuba zake zinazoendelea kurushwa na redio yetu ya Taifa; mtagundua kwamba akili na mawazo ya Mwalimu vilikuwa vya kwake mwenyewe na aliweza kuyasimamia vizuri yale yote aliyoyaona ni sahihi na ya MSINGI kwa TAIFA letu.Angalieni mifano hapa kwa majirani zetu tu. Mtu anakuwa maarufu kwa sababu ya KABILA yake, DINI yake, UTAJIRI wake,... Rais anahutubia watu wake kupitia wakalimani...
 
Mapungufu ya Nyerere sio mahala pake hapa; na mapambo ya Nyerere yasiyohusiana na Azimio la Arusha na vyanzo vya fikra zake? Hayo ni sawa, sio?

Tena mapambo ya kupotosha, ya uongo, hayo hayakataliwi? Nimeona wasifu wa uongo umejipenyeza nikapinga mapambio hayo, na nikijua ni mada nyingine, nikaeleza kwa nini nimeandika niliyoandika.

Sasa tukikataa yasiyohusika hapa tukatae yote, mapambio ya uongo na mapungufu ya Nyerere. Yote sio mahala paka.

Haya nawaacha na majadiliano yenu, al muradi yasisemwe ya uongo yasiyohusika, maana hatutaruhusu vizazi vya kesho kutwa vidhanie woooote tulikuwa bado tumepumbazika (hoodwinked ) na bunk za Nyerere, mpaka mwaka 2008.

(Kwanza nilichokiongelea hata hivyo kiko on point, kwamba Nyerere hakutaka kutofautiana na mtu. Kimewashtua kwamba nimeongelea jinsi alivyosweka watu ndani waliojaribu kutofautiana nae ? Come on guys!)

Kuhani,

Kosa lako ni kujiona kuwa ni wewe pekee ambaye unajua watu walioathirika na utawala wa Mwalimu Nyerere. Na hii si mara ya kwanza kulifanya hili!

Je unajua ni mangapi ambayo familia yangu iliyapata au kuyapoteza kutokana na huyo huyo Nyerere? If you would have known ungekaa kimya, ila ni jambo la binafsi na sitalileta hapa!

Kuna wengi ambao walipoteza mali, marafiki hata watu kuwekwa ndani kama ulivyotuletea listi, lakini katika mada hii, hakuna hata mmoja wao aliyesema kuwa aaah Nyerere ni hive au vile isipokuwa wewe.

Imekuwa ni kawaida yako kuyasema haya, na hilo naliheshimu, lakini kama nilivyosema, mjadala haukuwa unachunguza ni nini Mwalimu alikifany aau kukosea, ni kujiulilza, chimbuko la Mwalimu Nyerere kuwa mjamaa na kutuletea siasa za Ujamaa, Kujitegemea na Azimio la Arusha.

Kwa nini usianzishe basi thread nyingine ya facts na data zako kuhusu waliofungwa, kupoteza mali au kunyanyaswa na Nyerere na tuje huko kufocus machungu yetu kuhusu Nyerere?
 
Kuhani,

Kosa lako ni kujiona kuwa ni wewe pekee ambaye unajua watu walioathirika na utawala wa Mwalimu Nyerere. Na hii si mara ya kwanza kulifanya hili!

Je unajua ni mangapi ambayo familia yangu iliyapata au kuyapoteza kutokana na huyo huyo Nyerere? If you would have known ungekaa kimya, ila ni jambo la binafsi na sitalileta hapa!

Kuna wengi ambao walipoteza mali, marafiki hata watu kuwekwa ndani kama ulivyotuletea listi, lakini katika mada hii, hakuna hata mmoja wao aliyesema kuwa aaah Nyerere ni hive au vile isipokuwa wewe.

Imekuwa ni kawaida yako kuyasema haya, na hilo naliheshimu, lakini kama nilivyosema, mjadala haukuwa unachunguza ni nini Mwalimu alikifany aau kukosea, ni kujiulilza, chimbuko la Mwalimu Nyerere kuwa mjamaa na kutuletea siasa za Ujamaa, Kujitegemea na Azimio la Arusha.

Kwa nini usianzishe basi thread nyingine ya facts na data zako kuhusu waliofungwa, kupoteza mali au kunyanyaswa na Nyerere na tuje huko kufocus machungu yetu kuhusu Nyerere?

Mchungaji!... hii inaitwa kumtolea mtu uvivu; kuna watu wanadhania kuwa ni wao peke yao wanaijua historia ya nchi yetu na wimbo wao kila wakati umekuwa ule ule kana kwamba sisi wengine tumezaliwa na kukulia Ulaya! Hapo umemkoma nyani giledi.
 
Nimewafungulieni wale wenye ugwadugwadu na Nyerere thread yenu maalum, nendeni kule mkayatoe yale ya moyoni tujadili mapungufu, ubaya na ukatili wake!
 
Mchungaji!... hii inaitwa kumtolea mtu uvivu; kuna watu wanadhania kuwa ni wao peke yao wanaijua historia ya nchi yetu na wimbo wao kila wakati umekuwa ule ule kana kwamba sisi wengine tumezaliwa na kukulia Ulaya! Hapo umemkoma nyani giledi.

Mwanakijiji,

Alichonacho Kuhani dhidi ya Nyerere ni chuki na si kukosoa mapungufu ya uongozi dhidi ya Nyerere.

Hili kaliweka wazi baada ya kuja kudai Nyerere anatia aibu kwa kwenda kufia nje uya nchi badala ya Lugalo.

Hiyo hoja nilipoisoma, nikajiuliza maswali mengi sana pamoja na Kuhani kuoneka kuwa ni mahiri, ni vipi akose utu na kuanza kudhihaki? nikagundua kuwa ni chuki na si kitu kingine na hivyo kamwe hapatakuwa na jema kuhusu Nyerere machoni pake.

Ni haki yake kutokumpenda Nyerere, lakini anapokuja na kuharibu mada alimradi hampendi Nyerere, hapo anakosea.

Nimemsaidia yeye na wenzake wasioona hata chembe ya jema alilofanya Mwalimu Nyerere kwa kuwafungulia thread waende huko wakajadili ubaya wa Nyerere!
 
Mapungufu ya Nyerere sio mahala pake hapa; na mapambo ya Nyerere yasiyohusiana na Azimio la Arusha na vyanzo vya fikra zake? Hayo ni sawa, sio?

Tena mapambo ya kupotosha, ya uongo, hayo hayakataliwi? Nimeona wasifu wa uongo umejipenyeza nikapinga mapambio hayo, na nikijua ni mada nyingine, nikaeleza kwa nini nimeandika niliyoandika.

Sasa tukikataa yasiyohusika hapa tukatae yote, mapambio ya uongo na mapungufu ya Nyerere. Yote sio mahala paka.

Haya nawaacha na majadiliano yenu, al muradi yasisemwe ya uongo yasiyohusika, maana hatutaruhusu vizazi vya kesho kutwa vidhanie woooote tulikuwa bado tumepumbazika (hoodwinked ) na bunk za Nyerere, mpaka mwaka 2008.

(Kwanza nilichokiongelea hata hivyo kiko on point, kwamba Nyerere hakutaka kutofautiana na mtu. Kimewashtua kwamba nimeongelea jinsi alivyosweka watu ndani waliojaribu kutofautiana nae ? Come on guys!)
Kuhani,
Fortunately you do not have monopoly on the truth, do you? Hii dhana ya kuita maoni ya wengine uwongo ni dhana muflisi.
 
Back
Top Bottom