Elections 2010 Werema amkubali Dr. Slaa - Gharama za uchaguzi

Kamakabuzi

JF-Expert Member
Dec 3, 2007
2,861
1,302
Nimemsikia jana Bungeni Jaji Werema akikubali kwa lugha ya kisiasa kuwa sheria ya gharama za uchaguzi inabidi ifanyiwe marekebisho. Na katika vifungu alivyotaja ni kifungu cha 7 ambacho Slaa alikuwa amekilalamikia. Japo ametumia usiasa zaidi, amekiri kuwa kwenye kamati alibanwa na kulazimika kuleta mabadiliko haya.

Kwa upande wa msemaji wa kambi ya upinzani -yeye hakuuma maneno; ni kweli vifungu viliingizwa kinyemela na sasa vijadiliwe upya.

Kwa wanaJF: Kuna mtu mmoja alituwekea hansard ya siku husika hasa mjadala wa sheria hii, lakini baadhi ya wanaJF wakaisoma kisiasa na kuona kuwa kuweka kifungu cha 7(3) ailikuwa sawa.

Silazimishi wote tuwe na maoni yanayofanana, ila kwa jambo lililokuwa wazi (hansard) tulipaswa kuwaeleza wasomoaji wetu ukweli. JF inapaswa kuwa sehemu ya wasomaji kupata hoja za ukweli.
Kwa jaji werema: Enzi za kuburuza bunge zilikwisha siku nyingi - kwenye bunge kuna serikali mbili - ile iliyo madarakani na ile inayosubiri kuingia madarakani.

Usidhani wale wanaosubiri kuingia madarakani wataacha kuwa makini; lazima wachimbue sana ili waonyeshe udhaifu wa walio madarakani ili wao wachaguliwe awamu inayofuata - be careful; otherwise u-jaji wao utakuwa questionable!
 
Tungelikuwa na akina Dr. Slaa kama hamsini hivi Bungeni, mambo yangelikuwa mazuri sana. Lakini, kila siku ni Slaa tu ndiye anayefanya homework yake kwa utimilifu!
 
ukiwa na serikali ya hovyo hovyo obvipus utakuwa na watendaji wa hovyo hovyo
 
ukiwa na serikali ya hovyo hovyo obvipus utakuwa na watendaji wa hovyo hovyo

UKIWA NA JAMII HOVYO UTAPATA SERIKALI HOVYO! Serikali inatokana na jamii na JAMII MAKINI HATAKUBALI SERIKALI HOVYO, ITAIONDOA NA KUWEKA MAKINI.
 
Werema akielewa jambo huwa sio mbishi kulifanyia kazi... Alikuwa hajaelewa tu lakini jamaa he is good yuko flexible kwa kweli.
 
Tungelikuwa na akina Dr. Slaa kama hamsini hivi Bungeni, mambo yangelikuwa mazuri sana. Lakini, kila siku ni Slaa tu ndiye anayefanya homework yake kwa utimilifu!

Hamsini wote wanini? >>>>>...Slaa + Zitoo + vichwa vitatu kama hivyo= Bungeni Ze patamus!....acha bwana,
 
Nimemsikia jana Bungeni Jaji Werema akikubali kwa lugha ya kisiasa kuwa sheria ya gharama za uchaguzi inabidi ifanyiwe marekebisho. Na katika vifungu alivyotaja ni kifungu cha 7 ambacho Slaa alikuwa amekilalamikia. Japo ametumia usiasa zaidi, amekiri kuwa kwenye kamati alibanwa na kulazimika kuleta mabadiliko haya.

Kwa upande wa msemaji wa kambi ya upinzani -yeye hakuuma maneno; ni kweli vifungu viliingizwa kinyemela na sasa vijadiliwe upya.

Kwa wanaJF: Kuna mtu mmoja alituwekea hansard ya siku husika hasa mjadala wa sheria hii, lakini baadhi ya wanaJF wakaisoma kisiasa na kuona kuwa kuweka kifungu cha 7(3) ailikuwa sawa.

Silazimishi wote tuwe na maoni yanayofanana, ila kwa jambo lililokuwa wazi (hansard) tulipaswa kuwaeleza wasomoaji wetu ukweli. JF inapaswa kuwa sehemu ya wasomaji kupata hoja za ukweli.
Kwa jaji werema: Enzi za kuburuza bunge zilikwisha siku nyingi - kwenye bunge kuna serikali mbili - ile iliyo madarakani na ile inayosubiri kuingia madarakani.

Usidhani wale wanaosubiri kuingia madarakani wataacha kuwa makini; lazima wachimbue sana ili waonyeshe udhaifu wa walio madarakani ili wao wachaguliwe awamu inayofuata - be careful; otherwise u-jaji wao utakuwa questionable!

Sisi ni akina Slaa pia. Tuwasaidie kwa kila hali. Endeleza!! Yes we can!!
 
hatuwezi kuwapata wote hao itakuwa ngumu kwani hawa jamaa waupinzani wamelenga kwenda ikulu tu.Hawataki kukimbizana na serikali ya chini kama mwenyekiti wa serikali ya mtaa na udiwani.Huko ndo wanakoanzia kupatikana kina Slaa.
Mfano mzuri eneo la kata ya mbweni DARjimbo la Kinondoni hakukuwepo na chama kingine zaidi ya CCM katika uchaguzi. Hivyo hata kura haikupiwa maana waliendelea wale wale waliopitishwa na CCM.
Sijui upinzani wa TZ unaanzia wapi?
 
Binafsi naishukuru serikali chini ya Mhe rais kukubali bila ubishi maoni na kuyafanyia kazi! Serikali sikivu huwa naikubali sana
 
UKIWA NA JAMII HOVYO UTAPATA SERIKALI HOVYO! Serikali inatokana na jamii na JAMII MAKINI HATAKUBALI SERIKALI HOVYO, ITAIONDOA NA KUWEKA MAKINI.

kumbe sisi wanajamii ndio tunasababisha serikali yetu kuwa ovyo ovyo kivip Lebabu11 bado sijaipata point yako vizuri
 
Kama huyo jaji Werema yuko 'flexible' hatufai kwani kwenye shaeria hakuna 'flexibility'. 'Flexibility' yake ndio imepelekea kuongeza hivyo vifungu.
 
Tungelikuwa na akina Dr. Slaa kama hamsini hivi Bungeni, mambo yangelikuwa mazuri sana. Lakini, kila siku ni Slaa tu ndiye anayefanya homework yake kwa utimilifu!

Mkuu Dr. Slaa hamsini wote hao wa nini! Wangekuwepo angalu watano tu kama yeye, hakika tungeshuhudia mabadiliko makubwa sana.
 
Tungelikuwa na akina Dr. Slaa kama hamsini hivi Bungeni, mambo yangelikuwa mazuri sana. Lakini, kila siku ni Slaa tu ndiye anayefanya homework yake kwa utimilifu!

Mkuu Boramaisha, bado siamini kwamba hawa jamaa ni mambumbumbu kiasi hicho yaani hata kushindwa kugundua vipengere vilivyo chomekewa ki fisadi ndani ya muswaada kabla ya Rais Kusaini kweli? hapana mi naona kinachofanyika ni uzembe / ufisadi wa makusudi wakijua fika kwamba wasaidizi wa Rais na Rais mwenyewe hapendi kupitia pitia vipengele katika makaratasi kabla ya kutia wino.

Rais kama hasomi na wasaidizi wake hawasomi basi wapuuzi wengine wanachomeka mambo ya ajabu wakijua kuna udhaifu mule - yale yale ya kukabidhi magari yanajirudia tena.

Ni kweli bila kuwa na DR. Slaa basi mambo yangekuwa zaidi ya hiyo HOVYO HOVYO tunayoisema. Cha ajabu hakuna mtu yeyote atachukuliwa hatua juu ya uhuni huu - hii nchi mimi sielewi tunakwenda wapi - na kama CCM wakiongoza nchi hii in next 20 years naapa Tanzania itakuwa jalala la takataka.

Mimi ningekuwa Rais kwanza ningeanza na wale waliochomeka upuuzi huo - pili katibu mkuu wangu na ofisi yake wote maliganyaja - lakini aaaaa nipo YUESII sina tatizo mtu wa watu.

Hongera sana Dr Slaa sisi watanzania wanaelewa sana mchango wako - nafikiri itafika hatua hata utafaa kuitwa baba mdogo wa taifa (2nd father of the Nation) - maana we ndiye umebakia mwenye uchungu na nchi yako wengine hawayaoni haya yote. Thanks once again - Mtetezi wa wanyonge - BIG UP.
 
Mkuu Boramaisha, bado siamini kwamba hawa jamaa ni mambumbumbu kiasi hicho yaani hata kushindwa kugundua vipengere vilivyo chomekewa ki fisadi ndani ya muswaada kabla ya Rais Kusaini kweli? hapana mi naona kinachofanyika ni uzembe / ufisadi wa makusudi wakijua fika kwamba wasaidizi wa Rais na Rais mwenyewe hapendi kupitia pitia vipengele katika makaratasi kabla ya kutia wino.

Rais kama hasomi na wasaidizi wake hawasomi basi wapuuzi wengine wanachomeka mambo ya ajabu wakijua kuna udhaifu mule - yale yale ya kukabidhi magari yanajirudia tena.

Ni kweli bila kuwa na DR. Slaa basi mambo yangekuwa zaidi ya hiyo HOVYO HOVYO tunayoisema. Cha ajabu hakuna mtu yeyote atachukuliwa hatua juu ya uhuni huu - hii nchi mimi sielewi tunakwenda wapi - na kama CCM wakiongoza nchi hii in next 20 years naapa Tanzania itakuwa jalala la takataka.

Mimi ningekuwa Rais kwanza ningeanza na wale waliochomeka ujinga huo - pili katibu mkuu wangu wote maliganyaja - lakini aaaaa nipo YUESII sina tatizo mtu wa watu.

Hongera sana Dr Slaa sisi watanzania wanaelewa sana mchango wako - nafikiri itafika hatua hata utafaa kuitwa baba mdogo wa taifa (2nd father of the Nation) - maana we ndiye umebakia mwenye uchungu na nchi yako wengine hawayaoni haya yote. Thanks Mtetezi wa wanyonge - BIG UP.

Mkuu, hivi unaaamini kwamba kuongeza hivyo vifungu baada ya muswada kuwa umpetishwa bungeni na kabla Rais hajasaini ulikuwa ni uamuzi wa Werema peke yake? Tutakuwa tunajidanganya hapa. Serikali kupitia kwa Werema waliamua kufanya hivyo na Rais alijua hilo kabla ya kusaini. Cha kushukuru ni kwamba mpiganaji Dr. Slaa aliwashtukia au labda alitonywa na mtu juu ya mchezo mchafu uliochezeka kwenye huo muswada.

I stand to be corrected.

Tiba
 
Kuchomekwa kwa hivyo vifungu si kwamba rais alikuwa hafahamu lilikuwa ni deal lakini kwa vile siku zote Mkubwa huwa hakosei ikatafanywa coverup kuwa yeye hakuusoma ili kumlindia heshima yake lakini vilevile wakasahau hata kule kusaini bila kuusoma ni kashifa nyingine.
 
Werema akielewa jambo huwa sio mbishi kulifanyia kazi... Alikuwa hajaelewa tu lakini jamaa he is good yuko flexible kwa kweli.
GS ninahofu na huo uelewa wake au may be alikuwa mwelewa b4 kuwa mwanasiasa. Jaji Werema umetusikitisha sana sisi tuliokuwa tunakufahamu before. Ulimshambulia kabisa Dr. Slaa infact ulitoa mpaka press release kwenye magazeti kwa kutumia kodi zetu kupinga kitu kilichokuwa wazi hata kwetu sisi ambao hatukuwapo Bungeni. Sifahamu zilitumika pesa kiasi gani kutoa hizo adverts kwenye magazeti lakini ninafahamu watanzania wengi tu ambao mlo mmoja kwa siku kwao ni muujiza. Sasa ili tukusamehe kwenye hili ulilofanya nashauri pesa iliyotumika kutoa press release ukatwe toka kwenye mshahara wako kwani kuna watanzania kama wewe ambao wanakufa kwa njaa.
 
Sehemu kubwa ya viongozi wakuu serikalini wamekaa kiwiziwizi tu. Ni aibu kubwa kwa kiongozi wa nchi kukubali huo uchafu wa kuongezi vifungu kinyume na utaratibu/sheria. Nafikiri alifanya hivyo baada ya kuona vina maslahi kwake (CCM). Sidhani kama angekubali kusaini kama kipengele hicho kinge wasaidia wapinzani.

Kwa ufupi ni kwamba yeye mwenyewe ni fisadi ndo maana anashindwa kuwabana mafisadi.
 
UKIWA NA JAMII HOVYO UTAPATA SERIKALI HOVYO! Serikali inatokana na jamii na JAMII MAKINI HATAKUBALI SERIKALI HOVYO, ITAIONDOA NA KUWEKA MAKINI.

Laiti Watanzania wangeelewa hili mbona raha Oktoba
 
Back
Top Bottom