Mcqueenen
JF-Expert Member
- Nov 2, 2019
- 6,820
- 11,553
Ukisoma vitabu vya watu mashuhuri kama shakespeare, kuna ile unakuta mwandishi ameandika kwa ustadi wa hali ya juu...yani ametumia maneno vizuri, yani maneno ameyatumia kama rangi vile kuchora picha nzuri sana inayovutia kutazama machoni.
Bila stori nyingi au maelezo mengi, weka fungu la kitabu chako cha dini ambalo unaona limeandikwa kwa ustadi wa hali ya juu.
Naanza mimi:
Warumi 8:31
Tuseme nini basi kuhusu haya yote? Ikiwa Mungu yuko upande wetu ni nani atakayetupinga?....Ni nani atawashtaki wale ambao Mungu amewachagua? Ni nani atakayetutenganisha na upendo wa Kristo? Ni shida? Au taabu? Au mateso? Au njaa? Au umaskini? Au hatari? Au Kifo?
Hapana. Lakini katika mambo yote haya sisi ni washindi, naam, na zaidi ya washindi, tukiwa ndani yake yeye aliyetu penda. Kwa maana nina hakika kuwa, si kifo wala uzima; si malaika wala mashetani; si mambo ya sasa wala mambo yajayo au mamlaka nyingineyo yote; si mambo yaliyo juu wala yaliyo chini sana; wala hakuna kitu kingine cho chote kati ya vitu vyote alivyoumba Mungu kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu ulio ndani ya Kristo Yesu Bwana wetu.
Bila stori nyingi au maelezo mengi, weka fungu la kitabu chako cha dini ambalo unaona limeandikwa kwa ustadi wa hali ya juu.
Naanza mimi:
Warumi 8:31
Tuseme nini basi kuhusu haya yote? Ikiwa Mungu yuko upande wetu ni nani atakayetupinga?....Ni nani atawashtaki wale ambao Mungu amewachagua? Ni nani atakayetutenganisha na upendo wa Kristo? Ni shida? Au taabu? Au mateso? Au njaa? Au umaskini? Au hatari? Au Kifo?
Hapana. Lakini katika mambo yote haya sisi ni washindi, naam, na zaidi ya washindi, tukiwa ndani yake yeye aliyetu penda. Kwa maana nina hakika kuwa, si kifo wala uzima; si malaika wala mashetani; si mambo ya sasa wala mambo yajayo au mamlaka nyingineyo yote; si mambo yaliyo juu wala yaliyo chini sana; wala hakuna kitu kingine cho chote kati ya vitu vyote alivyoumba Mungu kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu ulio ndani ya Kristo Yesu Bwana wetu.