Wazungu bora kuliko waafrika?

Darwin

JF-Expert Member
May 14, 2008
908
56
Baba yangu mzungu, mchanganyiko Irish/dutch. Mama yangu msambaa lakini nilishangaa jana kukuta hii post kule JIACHIE.

JE NI KWELI KUWA WANAUME WAKIBONGO HAWANA MPANGO?
Salama jamani huko?

Kuna huyu dada mmoja wakiTanzania, yeye baada yakuolewa na mzungu anaona kuwa manamume wakibongo hawana mpango. Hebu soma hii blog yake. Ni kweli wajomba zangu wakiswahili ni wayeyushaji?

Im not a great writer, that is evident. Sijui kupangilia sentensi zangu, so bear with me. Sasa leo nataka tuweka wazi swala zima la wasichana wa kitanzania kuolewa au kuwa na maboyfriend wa kizungu. Mimi binafsi nime-notice kwamba wasichana wengi wa kitanzania wamekuwa wakiona kwamba kuwa na boyfriend ama mume ambae ni mzungu is actually an achievement in life. Na wengi wamekuwa hawataki kabisa hata kuwa na ma-boyfriend ambao ni waa-africa especially watanzania.

Na kuna wasichana ambao nawajua ambao wako kwenye relationships na mwanaume wa kitanzania lakini anaeleza wazi wazi kwamba anatamani apate mwanaume wa kizungu. Mdau wewe unanaoje swala hili? Je hawa wasichana ni kwamba they are shallow and stupid? Or are they very smart?

Really kabla huja-judge na kutuma comment za kuwatukana lifikirie hili swala vizuri. Mimi personally naona kuna 2 sides to this issue.kuna wale ambao watanaka kuwa na wazungu na hawataki ku-date watanzania wenzao kwasababu za kijinga na zisizo na msingi.

1st side
Kwa mfano kuna wengi facebook unaona mtu akipata boyfriend wa kizungu basi anamwaga picha zake na mzungu facebook, sasa hizo comments za marafiki nayeye mwenye mchumba ndio zinazotuharibia wengine wote..nashindwa kuelewa kabisa ni kwanini mtu akiweka picha yake na mzungu facebook basi kila mtu anamwandiki comment UKO JUU, UMEOPOA MAMA UKO JUU , KWELI MUNGU MKUBWA , RISKI ZIMEFUNGUKA MWAKA HUU, KWELI MUNGU AMEKUKUMBUKA.

Comment kama hizi na zingine za disini hii zinanisikitisha mnojamani hivi kweli kuwa na mwanaume mwenye ngozi nyeupe ni kitu cha maana kiasi hiki? alafu hivi kweli tumejishusha utu wetu kiasi cha kwamba tunafurahia in public? Kwanini msiweke comment kama u look happy ,hongera kwa kupata mchumba and so forth kuwa na mzungu sidhani kama inamaanisha uko juu or whatever. (kama moja ya comment nilizoandika hapo zipo kwenye picha yako ,please usijisikie vibaya, niliitumia tu kama mfano ili kuwapa wasomaji wangu picha kamili,its really not about you)
hivi kweli hawa wazungu wenyewe wangekuwa wanajua kusoma Kiswahili humo facebook ingekuwaje?

Wanawake wenzangu wa kitanzania, tuache kujiabisha na hili swala zima la mzungu mzungu mzungu, especially kwenye facebook, mtu akikuwekea comment ya kishamba kama hizo hapo juu usiishadadie sana, ikiwezekana i-delete akuwekee comment ya maana.

Kama wewe ni mwanamke ambae kupata mzungu is an achievement basi , I am sorry to say ,you are without a doubt a loser

Wazungu wanamatizo mengi tu, na hata ukiangalia the highest divorce rates in the world zipo western countries na sio kwetu.

na kwa wale wenzetu wanaodhani wazungu wote wanapesa na kwamba atakuhonga basi unajidanganya kabisa, mzungu sio muhongaji , kama unataka kuhongwa bora mapedeshee ya kibongo litakununulia hata gari baada ya kukujua kwa siku chache tu.hahahahha.

Wazungu wanachukua muda wao kumsoma mtu na tabia zake, na kama kuna chochote atakachokufanyia ni baada ya muda mrefu na kwamba umeshakuwa mke wake au labda anahisi utaishia kuwa mke wake.

Na pia ndugu zetu wa kibongo wanaweza kuishi na mwanamke asie na income yoyote, na asiejishughulisha la lolote, asilimia kubwa ya wazungu hawawezi kabisa hii tabia.

So kabla hujarukia na kugeza watu, angalia usije kuchanika msambalol.

2nd side
Kuna wale wasichana wa kibongo wanaotaka kuolewa na wazungu for the right reasons. Hao ndio ninaowalewa mimi
Ukweli lazma tuuseme leo

Asilimia kubwa ya wanaume wa kibongo ni miyeyusho mitupu , tuseme labda 80%....sasa wewe utakuwa na bahati gani mpaka upate mmoja wa hiyo 20% ambao ni wastaarabu.

Ukweli ni kwamba, nikiangalia rafiki zangu walioolewa na wanaume watanzania na walioolewa na wanaume wazungu, walioolewa na wazungu, are way more content in their marriages, ofcourse kuna exception za rafiki zangu wachache waliiolewa na wabongo na wana-enjoy ndoa zao na ndoa zao haziwapi homa kila siku

Mie nafikiri,wanawake wengi wa kitanzania wameamua kuwa na wazungu kwasabu wanatafuta pumziko la rohoukweli ni kwamba wanaume wengi wa kitanzania wanasumbua mno tena kupita kiasa.

Mwanaume wa kitanzania amelelewa akiona baba yake ana wake wawili na nyumba ndogo kama tatu, je unadhani yeye atakuja kuwa mume wa aina gani? Mwanaume wa kitanzania anajiona ni mwanaume kamili zaidi kama anawanawake wengi, na kitu ambacho yupo proud nacho kiasi ya kwamba anaweza kukaa na rafiki zake bar akaadisia jinsi gani anawanawake wengi na wenzio wakamuona YUKO JUU.

Mwanaume wa kizungu, hajakulia kwenye mazingira haya and automatically ipo kichwani mwake kwamba anatakiwa kuwa faithfull kwa mke wake na kumtreat as an equal.hata ikitoea akawa macho juu akapata kidosho nje, atajificha, hutojua lolote na ni jambo la aibu sana kwake kiasi cha kwamba hawezi kuongelea hadharani.

Umeona tofauti hapo?

Huwa nasikitika sana, nikienda disco, unaona kabisa janamme lina mke na watoto, lipo disco na totos nyingine na anajua unamjua mke wake na labda utamueleza lakini haogopi kabisa.

Hivi kweli hapo unaweza kumlaumu mtoto wa kitanzania akianza kutafuta mzungu? Anakuwa ni kwamba ameamua hataki kuumizwa roho yake wala akili yake ana anataka kuishi maisha yake in peace.

Sio kwamba wazungu hawacheat au na wao sio washenzi wakati mwingine, tofauti ni kwamba hiki sio kitu cha kawaida kwao na hata akiwa mshenzi basi huu ni samaki mmoja mmbovu,inabidi tu awekwe kwenye kapu la pekeelol
Mwanaume wa kitanzania, kama hajatembea na rafiki zako,au mtu ambae unamjua basi haoni raha kabisa,
And whats worse, wanaume wa kitanzania haachi mke wake hata siku moja, atamtesa mke wake miaka kibao lakini hamuachi. yaani mmbongo atakufanyia vituko weeeee mpaka utaondoka mwenyewe utarudi kwenu, but mzungu akipata mtu nje, atakuja kukwambia on your face, i dont love you anymore,I love somebody else. Ofcourse inauma sana but atleast utakuwa umeachwa with respect, lakini kaka zetu atamake sure amekutoa all your dignity, kakuabisha mji mzima, amekutoa confidence yote ndio anakuachalol

Na wasichana wengine wameniambia pia wanachukia tabia za kaka zetu za kufanya nao ngono alafu wanakaa bar na kuanza kuhadithia rafiki zao, Yule demu yuko hivi yuko vile, huu mji ni mdogo sana, unaingia sehemu unadhani umevaa nguo kumbe watu wanakujua ulivyo ukiwa uchi

Basi siku hizi utawasikia wanaume wa kitanzania wanatukana hawa wanawake wetu wanatamaa sana, sijui wanawafatia nini wazungu,kila mtu mzungu,kila mtu mzungu.

Kaka zetu you are the best, lakini badilisheni tabia zenu. Kuwa na wanawake wengi sio haki yako.sana sana ni kujitafutia magonjwa na kumpelekea mkeo asie na hatia.

Tunawapenda sana, lakini anzeni kutu-treat with respect ,love and humanity. Ni hayo tu wadau kwa leo ambayo nimeweza kuyaelewa ndani yah ii issue nzima ya wanawake wa kitanzania na wazungu.

wewe una yapi mdau?

ps. nitaweka comments zote ila zisiwe na matusi au majina ya watu.


18178_284054663097_624983097_4687929_1384610_n.jpg

Je Ni kweli kuwa Wanaume wa Kibongo Hawana mpango??
 
Eti huyu kichwa panzi anasema wazungu hawacheat?? Hoja zake ni za kijinga mpaka inatia hasira, kwa anataka kusema cheating is a middle name of 80% of Tz men?? Takwimu za wapi na kazipata wapi na kazilinganisha na zipi , kutoka wapi??
 
Lol hao wote wanaojibu huko juu ni wanaume mbona hakuna madada hapa ili watudhihirishie maana sie ndie tunajua kuwa km wanaume wa kibongo ni wayeyushaji au lah, nyie kina kaka wala msijitetee hapo ni sbb tu amewaponda. Ok sawa anaweza kuwa hana takwimu kudhihirisha may be aliyeyushwa sana na makaka wa kibongo.

hakuna ubishi wanaume wa kibongo ni wayeyushaji, mkiwa na uhusiano ukikuta mtu anapropose ndoa ni wachache sana na hata akifanya hivyo bado inafika wakati anakuona km we amekuweka ndani km chombo cha starehe na kumzalia watoto ila ye anatafuta wanawake nje ya ndoa, sikatai kwamba wapo wazungu wenye tabia hiyo hapo mange kakosea kweli ila sasa mwanaume wa kibongo culture yetu nayo imetuharibu, yaani ye anaona ni kitu cha kawaida kuwa na kimada na sio kosa, ila mwanamke akifanya hivyo ni kosa, naona tunahitaji kurudi beijing kwa ajili ya usawa wa wanawake kuwa na vimada nje ya ndoa pia km wafanyavyo waume.

kitu kingine wazungu wakifumaniana huwa wanaamua kuachana kbs ila sie wabongo huwa tunang'ang'ania ndoa sbb ya umasikini wetu na pengine unaona ukiachana na mmeo maisha yatakushinda ni sbb tu tunategemea wanaume sana kimapato sbb wanawake wengi Tz Africa hawana vipato sawa na wanaume, hivyo kuonekana km unaolewa ili kuinua kipato pia, ndio mana mange anatofautisha ndoa za wazungu na waafrica.

Achane wanawake tuongelee hili na nyie wanaume hamjui sbb sie nyie mnaoathirika ni wanawake, sbb tunajua na takwimu tunazo vichwani mwetu, sbb unaona kabla ya kuolewa ni wanaume wa watu wangapi ambao wameoa waliokutongoza, na wengine wanadiriki kuingilia kwa suala a nitakuoa uwe mke wa pili then akipata anaishia zake, wazungu hawafanyi hivyo, lol.
wanaume wa kibongo acheni uyeyushaji.
 
hakuna ubishi wanaume wa kibongo ni wayeyushaji, mkiwa na uhusiano ukikuta mtu anapropose ndoa ni wachache sana .

kitu kingine wazungu wakifumaniana huwa wanaamua kuachana kbs ila sie wabongo huwa tunang'ang'ania ndoa sbb ya umasikini wetu na pengine unaona ukiachana na mmeo maisha yatakushinda.

Achane wanawake tuongelee hili na nyie wanaume hamjui sbb sie nyie mnaoathirika ni wanawake, sbb tunajua na takwimu tunazo vichwani mwetu, wanaume wa kibongo acheni uyeyushaji.
nimependa maneno haya kwenye post yako da LS, it shows the reality on your side
 
Kawaida wazungu wengi wanatawaliwa na wake zao.. Card ya bank, nyumba, gari etc vinakuwa chini ya mwanamke.. Hii ni moja ya sababu.. Mswahili gani atakubali ujinga huo?
 
Kawaida wazungu wengi wanatawaliwa na wake zao.. Card ya bank, nyumba, gari etc vinakuwa chini ya mwanamke.. Hii ni moja ya sababu.. Mswahili gani atakubali ujinga huo?
hakuna wa kukubali bra dreamliner, labda kama yupo atuambie ili tujifunze kutoka kwake anafanyaje,
 
Lol hao wote wanaojibu huko juu ni wanaume mbona hakuna madada hapa ili watudhihirishie maana sie ndie tunajua kuwa km wanaume wa kibongo ni wayeyushaji au lah, nyie kina kaka wala msijitetee hapo ni sbb tu amewaponda. Ok sawa anaweza kuwa hana takwimu kudhihirisha may be aliyeyushwa sana na makaka wa kibongo.
hakuna ubishi wanaume wa kibongo ni wayeyushaji, mkiwa na uhusiano ukikuta mtu anapropose ndoa ni wachache sana na hata akifanya hivyo bado inafika wakati anakuona km we amekuweka ndani km chombo cha starehe na kumzalia watoto ila ye anatafuta wanawake nje ya ndoa, sikatai kwamba wapo wazungu wenye tabia hiyo hapo mange kakosea kweli ila sasa mwanaume wa kibongo culture yetu nayo imetuharibu, yaani ye anaona ni kitu cha kawaida kuwa na kimada na sio kosa, ila mwanamke akifanya hivyo ni kosa, naona tunahitaji kurudi beijing kwa ajili ya usawa wa wanawake kuwa na vimada nje ya ndoa pia km wafanyavyo waume.

kitu kingine wazungu wakifumaniana huwa wanaamua kuachana kbs ila sie wabongo huwa tunang'ang'ania ndoa sbb ya umasikini wetu na pengine unaona ukiachana na mmeo maisha yatakushinda ni sbb tu tunategemea wanaume sana kimapato sbb wanawake wengi Tz Africa hawana vipato sawa na wanaume, hivyo kuonekana km unaolewa ili kuinua kipato pia, ndio mana mange anatofautisha ndoa za wazungu na waafrica.

Achane wanawake tuongelee hili na nyie wanaume hamjui sbb sie nyie mnaoathirika ni wanawake, sbb tunajua na takwimu tunazo vichwani mwetu, sbb unaona kabla ya kuolewa ni wanaume wa watu wangapi ambao wameoa waliokutongoza, na wengine wanadiriki kuingilia kwa suala a nitakuoa uwe mke wa pili then akipata anaishia zake, wazungu hawafanyi hivyo, lol.
wanaume wa kibongo acheni uyeyushaji.
% 80 kwangu mimi naona ni asilimia kubwa sana.

Halafu kama ni kweli hizo asilimia 80 ni wayeyushaji hio mitandao yenu inayoonyesha kitchen party, send off, sijui nini vitu ambavyo hatuvijui huku Ulaya hao wanaume wanapatikana wapi?
Ina maana waoaji wote kwenye hizo blog zenu ni Import kutoka nchi nyingine?
 
Napozidi kusoma michango ya watu humu, naanza kupata picha mbili.

Moja ni ya sour grapes.

Ya pili inanikumbusha mdada mmoja sijui kama alikuwa ni 'mpiganaji' au ndio walewale wababaikia wazungu aliyetolewa kizazi baada ya kufanyishwa ngono na mbwa na wazungu wake.

Marejeo ngamani...
 
Back
Top Bottom