100 others
JF-Expert Member
- Aug 5, 2017
- 3,626
- 12,057
Stanley Kakubo ambaye ni waziri wa mambo ya nje wa Zambia amejiuzulu baada ya video inayoonyesha yeye na mfanyabiashara wa Kichina wakikabidhiana vibunda ambapo inasemekana ni US dollars na Zambian kwacha.
View: https://streamable.com/m1vwpu
Inasemekana jamaa alikuwa anapokea mlungula kutoka kwa mfanyabiashara huyo wa ki China ambae anajihusisha na biashara za madini.
Kakubo ambae inasemekana tayari alishakuwa na scandal ya kuonekana akitoka nje ya ofisi ya kampuni ya Kichina inayohusika na utengenezaji wa cement akiwa na briefcase, inasemekana jamaa alikuwa ametoka kupata mlungula.
Kakubo amejitetea kwa kusema ilikuwa ni biashara ya kifamilia ikifanyika. Lakini Mr Hichilema amekubali Kakubo kujiuzulu.
Aisee watu wanakula maisha, vile vibunda si chini ya milioni 400 Tshs. Watu wanakula maisha jamani.
Mafisadi kumbe ndivyo namna wanakula keki ya taifa namna hii.