Waziri wa elimu simamia watu wa TCU, wanaelekea kuharibu mfumo wa elimu ya juu

Zygot

JF-Expert Member
Apr 14, 2016
2,240
2,866
Nimekuwa nikifuatilia utendaji wa TCU na hasa baada ya Magufuli (RIP) kuwapokonya kazi ya kudahili wanafunzi waliyojipachika. Kwa ufupi hapo Magufuli alishauriwa vizuri maana walishaanza kufanya biashara na vyuo vikuu na hasa vyuo binafsi (private).

Sasa yaonekana hawana mwongozo wa kazi zao za kila siku ukiacha ile ya kufungia vyuo binafsi wakati vya serikali viko hoi kwa miundombinu. Wameanza kazi ya kubadilisha muelekeo wa mitaala ya vyuo vikuu bila kuelewa wanachokifanya jambo ambalo linaleta usumbufu bila manufaa. Nitaeleza.

Kuna mkumbo wa kujidai vyuo vikuu vyote vifuate mitaala, wanaita ni competence based badala ya mpangilio uliovianzisha, yaani knowledge based. Uelekeo huu naomba niuite ni wa "Kijinga" kwa sababu hakuna nchi duniani iliyo na vyuo vikuu vyote ambavyo ni competence based.

Kila nchi ina mchanganyiko wa vyuo. Tanzania tayari tuna mchanganyiko huo. Wahitimu wa digrii ambazo ni competence based wako chini ya NACTE. Vyuo chini ya TCU vilistahili kubaki kwenye mfumo wa knowledge based na ndivyo nchi zote zinavyofanya. TCU sasa wanajidai ni wataalamu sana, wanaleta usumbufu kwa vyuo na kwa hili, nafahamu wazi vyuo binafsi vitasumbuliwa sana bila sababu.

Tuwaombe TCU wajifunze mifumo ya dunia kabla ya kutuharibia mfumo wetu wa elimu kwa uelewa wao mdogo. Kama wamepewa pesa na hawajui nini wakifanye, ni bora wakaziachia ziingie kuwasaidia vijana wanaotafuta ada za vyuo.
 
Nimekuwa nikifuatilia utendaji wa TCU na hasa baada ya Magufuli (RIP) kuwapokonya kazi ya kudahili wanafunzi waliyojipachika. Kwa ufupi hapo Magufuli alishauliwa vizuri maana walishaanza kufanya biashara na vyuo vikuu na hasa vyuo binafsi (private). Sasa yaonekana hawana mwongozo wa kazi zao za kila siku ukiacha ile ya kufungia vyuo binafsi wakati vya serikali viko hoi kwa miundombinu. Wameanza kazi ya kubadilisha muelekeo wa mitaala ya vyuo vikuu bila kuelewa wanachokifanya jambo ambalo linaleta usumbufu bila manufaa. Nitaeleza.

Kuna mkumbo wa kujidai vyuo vikuu vyote vifuate mitaala wanaita ni competence based badala ya mpangilio uliovianzisha, yaani knowledge based. Uelekeo huu naomba niuite ni wa kijinga kwa sababu hakuna nchi duniani iliyo na vyuo vikuu vyote ambavyo ni competence based. Kila nchi ina mchanganyiko wa vyuo. Tanzania tayari tuna mchanganyiko huo. Wahitimu wa digrii ambazo ni competence based wako chini ya NACTE. Vyuo chini ya TCU vilistahili kubaki kwenye mfumo wa knowledge based na ndivyo nchi zote zinavyofanya. TCU sasa wanajidai ni wataalamu sana! Wanaleta usumbufu kwa vyuo na kwa hili, nafahamu wazi vyuo binafsi vitasumbuliwa sana bila sababu.

Tuwaombe TCU wajifunze mifumo ya dunia kabla ya kutuharibia mfumo wetu wa elimu kwa uelewa wao mdogo. Kama wamepewa pesa na hawajui nini wakifanye, ni bora wakaziachia ziingie kuwasaidia vijana wanaotafuta ada za vyuo
Mleta mada ungeanza kwa kutueleza utofauti wa kimantiki baina ya mfumo wa "competence based" dhidi ya "Knowledge based". Kisha ukatueleza ni kwa vipi mabadiliko hayo yataharibu mfumo wa elimu yetu.
 
Mleta mada ungeanza kwa kutueleza utofauti wa kimantiki baina ya mfumo wa "competence based" dhidi ya "Knowledge based". Kisha ukatueleza ni kwa vipi mabadiliko hayo yataharibu mfumo wa elimu yetu.
Nijuavyo mimi, ufupi Competence-based ni elimu ya vitendo zaidi na knowledge-based ni ile ambayo inategemea sana uimarishaji na ugunduzi wa maarifa mapya na hasa kupitia tafiti.
Kama TCU wanaamini vyuo vikuu vyetu vyote viwe ni competence-based, hawana tofauti na yale yaliyoletwa na Mungai kule sekondari. yaani ujinga-jinga tu!
 
Hivi haya mambo ya elimu yakoje? Mbona tunachezewa kila siku? Leo tena nimeona eti kuna mpango mkubwa wa kuhangaika na elimu ya juu kwa ufadhili wa Benki ya Dunia. Hivi kweli Waziri huyu, profesa anaamini elimu ya juu inaweza kuwa nzuri wakati primary na sekondari hali ni hoi?

Ifike hatua sera ya elimu isiwe ni mali ya waziri aliyeko madarakani. Wengi ktk mawaziri hawa ni hovyo kabisa na wana tabia ya kumiliki uelekeo wa elimu yetu kwa kuiharibu.
 
Nimekuwa nikifuatilia utendaji wa TCU na hasa baada ya Magufuli (RIP) kuwapokonya kazi ya kudahili wanafunzi waliyojipachika. Kwa ufupi hapo Magufuli alishauriwa vizuri maana walishaanza kufanya biashara na vyuo vikuu na hasa vyuo binafsi (private).

Sasa yaonekana hawana mwongozo wa kazi zao za kila siku ukiacha ile ya kufungia vyuo binafsi wakati vya serikali viko hoi kwa miundombinu. Wameanza kazi ya kubadilisha muelekeo wa mitaala ya vyuo vikuu bila kuelewa wanachokifanya jambo ambalo linaleta usumbufu bila manufaa. Nitaeleza.

Kuna mkumbo wa kujidai vyuo vikuu vyote vifuate mitaala, wanaita ni competence based badala ya mpangilio uliovianzisha, yaani knowledge based. Uelekeo huu naomba niuite ni wa "Kijinga" kwa sababu hakuna nchi duniani iliyo na vyuo vikuu vyote ambavyo ni competence based.

Kila nchi ina mchanganyiko wa vyuo. Tanzania tayari tuna mchanganyiko huo. Wahitimu wa digrii ambazo ni competence based wako chini ya NACTE. Vyuo chini ya TCU vilistahili kubaki kwenye mfumo wa knowledge based na ndivyo nchi zote zinavyofanya. TCU sasa wanajidai ni wataalamu sana, wanaleta usumbufu kwa vyuo na kwa hili, nafahamu wazi vyuo binafsi vitasumbuliwa sana bila sababu.

Tuwaombe TCU wajifunze mifumo ya dunia kabla ya kutuharibia mfumo wetu wa elimu kwa uelewa wao mdogo. Kama wamepewa pesa na hawajui nini wakifanye, ni bora wakaziachia ziingie kuwasaidia vijana wanaotafuta ada za vyuo.
Nimekuwa nikifuatilia utendaji wa TCU na hasa baada ya Magufuli (RIP) kuwapokonya kazi ya kudahili wanafunzi waliyojipachika. Kwa ufupi hapo Magufuli alishauriwa vizuri maana walishaanza kufanya biashara na vyuo vikuu na hasa vyuo binafsi (private).

Sasa yaonekana hawana mwongozo wa kazi zao za kila siku ukiacha ile ya kufungia vyuo binafsi wakati vya serikali viko hoi kwa miundombinu. Wameanza kazi ya kubadilisha muelekeo wa mitaala ya vyuo vikuu bila kuelewa wanachokifanya jambo ambalo linaleta usumbufu bila manufaa. Nitaeleza.

Kuna mkumbo wa kujidai vyuo vikuu vyote vifuate mitaala, wanaita ni competence based badala ya mpangilio uliovianzisha, yaani knowledge based. Uelekeo huu naomba niuite ni wa "Kijinga" kwa sababu hakuna nchi duniani iliyo na vyuo vikuu vyote ambavyo ni competence based.

Kila nchi ina mchanganyiko wa vyuo. Tanzania tayari tuna mchanganyiko huo. Wahitimu wa digrii ambazo ni competence based wako chini ya NACTE. Vyuo chini ya TCU vilistahili kubaki kwenye mfumo wa knowledge based na ndivyo nchi zote zinavyofanya. TCU sasa wanajidai ni wataalamu sana, wanaleta usumbufu kwa vyuo na kwa hili, nafahamu wazi vyuo binafsi vitasumbuliwa sana bila sababu.

Tuwaombe TCU wajifunze mifumo ya dunia kabla ya kutuharibia mfumo wetu wa elimu kwa uelewa wao mdogo. Kama wamepewa pesa na hawajui nini wakifanye, ni bora wakaziachia ziingie kuwasaidia vijana wanaotafuta ada za vyuo.
Sasa ndugu unachong'a ng'ana ni nini? maana hii tz unaweza ukasoma ukawa knowledge based ukaishia mtaani vilevile, hakuna miundombinu yakusimamia ulichosomea!
 
Mleta mada kubali mabadiliko kwenye chuo chako, elimu ya nadharia pekee imepitwa na wakati
Kama uko TCU huo ndo mwanzo wa uzembe na ushenzi. Unaposema elimu ya 'nadharia' imepitwa na wakati nani aliyeondoa vyuo vya ufundi na kuvifanya vyuo vikuu? TCU ndo waliosajili vyuo vyote na kujidai wana vyuo vikuu 40+! That is rubbish men!

Btw. unaweka mambo ya vitendo, vitendo gani? Yaani kulima kwa jembe la mkono ndo iwe vitendo? Unahangaika na vyuo vikuu wakati hadi sasa sekondari hawana maabara, hata kale ka Bunsen burner nilikofundishwa miaka ile, hawana! Another rubbish, men!

Ulaya iliyoendelea kwa sayansi na teknolojia, kwani iliingiza ujinga-jinga huu vyuo vikuu? Kwani ugunduzi gani ambao haukutokana na elimu unayodhani ni nadharia? Einstein, Newton, Arrhenius, n.k. wote walikuwa vyuo vikuu (classical), siyo kujidai kuweka vitendo mshenzi kwenye misingi ya elimu. Learn out of this rubbish, men!
 
Back
Top Bottom