johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 84,035
- 142,137
Waziri wa afya Mh. Ummy muda huu anazungumza na viongozi mbalimbali wa dini juu ya mikakati ya kudhibiti Corona.
--
ALIYOZUNGUMZA WAZIRI UMMY MWALIMU (KWA UFUPI)
Viongozi wa dini mnayo nafasi ya kipekee kutoa taarifa sahihi, kwa weledi na uwazi, hivyo kupunguza uwepo wa taarifa zisizo za kweli zinazoweza kupelekea hofu, unyanyapaa na mashaka miongoni mwa wananchi.
Tunaomba pia ibada ifanyike muda mfupi, pia wekeni utaratibu wa kupunguza msongamano wa waumini wakati wa kuingia na kutoka katika nyumba za ibada.
Nimpongeza mkuu wa mkoa wa Pwani (Everist Ndikilo) kwa kuzuia kongamano la dini lililopangwa kufanywa na madhehebu ya kidini na kuhusishwa watu 3,000 wanaotoka nchi nzima.
Ugonjwa tumeletewa kutoka nje, hivi sasa takwimu za jana, juzi na wiki iliyopita tumeanza kuambukizana wenyewe kwa wenyewe. Ili viongozi wangu wa dini naomba niliweke wazi its no longer imported cases, tumeanza local transmission.
Ndani ya siku chache tutaingia katika community transmission. Maana yake tutapata mgonjwa ambaye hajui ugonjwa ameupata wapi? Sasa hivi amekuja mtu anamuambikiza fulani ndio maana tunafanya contact (muingiliano) kujua.
Lazima niwaambia ukweli nisiwafiche soon (karibuni), tutaingia kwenye community transmission. Bado tunatakiwa kuchukua tahadhari na kuongeza juhudi za kukabiliana na ugonjwa huu
Rais amesema hatuwezi kufunga kazi, kazi lazima tufanye lakini tuweze kudumisha kutokaribiana baina yetu. Hata Baba Askofu unaweza kufanya 'Video Conference' ukiwa na jambo na waumini
Tafiti zinaonesha virusi vya corona pia vinaambukizwa kwa njia ya hewa hivyo baada siku chache Serikali itatoa mwongozo ikiwa ni pamoja na kumtaka kila mtu anapotoka nyumbani awe amevaa barakoa ili kupunguza kasi ya mambukizi.
Mwanzoni kulikuwa na hisia kwamba Afrika hatuwezi kuumwa ugonjwa huu lakini leo kwa mujibu wa takwimu za Africa CDC, tuna wagonjwa takribani 10,000 na vifo vimefikia takribani 500
WHO ilitukadiria kufikia katikati ya Aprili tutakuwa na wagojwa 1000 nchini na katikati ya Mei tutakuwa na wagonjwa 10,000, kufikia sasa tumeruka kiunzi hicho kwa sababu hatuna wagonjwa wengi tunapaswa kumshukuru Mungu
Tunashauri wananchi tujiulize, je ni lazima tusafiri kutoka mijini kwenda vijijini wakati huu wa maambukizi ya corona? Tutafakari tusije tukawapelekea wazee wetu, wazazi wetu, na walezi wetu hivi virusi vya corona.
--
ALIYOZUNGUMZA WAZIRI UMMY MWALIMU (KWA UFUPI)
Viongozi wa dini mnayo nafasi ya kipekee kutoa taarifa sahihi, kwa weledi na uwazi, hivyo kupunguza uwepo wa taarifa zisizo za kweli zinazoweza kupelekea hofu, unyanyapaa na mashaka miongoni mwa wananchi.
Tunaomba pia ibada ifanyike muda mfupi, pia wekeni utaratibu wa kupunguza msongamano wa waumini wakati wa kuingia na kutoka katika nyumba za ibada.
Nimpongeza mkuu wa mkoa wa Pwani (Everist Ndikilo) kwa kuzuia kongamano la dini lililopangwa kufanywa na madhehebu ya kidini na kuhusishwa watu 3,000 wanaotoka nchi nzima.
Ugonjwa tumeletewa kutoka nje, hivi sasa takwimu za jana, juzi na wiki iliyopita tumeanza kuambukizana wenyewe kwa wenyewe. Ili viongozi wangu wa dini naomba niliweke wazi its no longer imported cases, tumeanza local transmission.
Ndani ya siku chache tutaingia katika community transmission. Maana yake tutapata mgonjwa ambaye hajui ugonjwa ameupata wapi? Sasa hivi amekuja mtu anamuambikiza fulani ndio maana tunafanya contact (muingiliano) kujua.
Lazima niwaambia ukweli nisiwafiche soon (karibuni), tutaingia kwenye community transmission. Bado tunatakiwa kuchukua tahadhari na kuongeza juhudi za kukabiliana na ugonjwa huu
Rais amesema hatuwezi kufunga kazi, kazi lazima tufanye lakini tuweze kudumisha kutokaribiana baina yetu. Hata Baba Askofu unaweza kufanya 'Video Conference' ukiwa na jambo na waumini
Tafiti zinaonesha virusi vya corona pia vinaambukizwa kwa njia ya hewa hivyo baada siku chache Serikali itatoa mwongozo ikiwa ni pamoja na kumtaka kila mtu anapotoka nyumbani awe amevaa barakoa ili kupunguza kasi ya mambukizi.
Mwanzoni kulikuwa na hisia kwamba Afrika hatuwezi kuumwa ugonjwa huu lakini leo kwa mujibu wa takwimu za Africa CDC, tuna wagonjwa takribani 10,000 na vifo vimefikia takribani 500
WHO ilitukadiria kufikia katikati ya Aprili tutakuwa na wagojwa 1000 nchini na katikati ya Mei tutakuwa na wagonjwa 10,000, kufikia sasa tumeruka kiunzi hicho kwa sababu hatuna wagonjwa wengi tunapaswa kumshukuru Mungu
Tunashauri wananchi tujiulize, je ni lazima tusafiri kutoka mijini kwenda vijijini wakati huu wa maambukizi ya corona? Tutafakari tusije tukawapelekea wazee wetu, wazazi wetu, na walezi wetu hivi virusi vya corona.